Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94

hivi ule msimu wakati Benki ya CRDB inaingia kudhamini michuano ya Kombe la Shirikisho

31st Jul, 2025 Views 16

Mtu anielekeze kwa upole kabisa na mniwie radhi kama nitakuwa β€œNahamisha Mada” hivi ule msimu wakati Benki ya CRDB inaingia kudhamini michuano ya Kombe la Shirikisho walianzia hatua ya Mtoano wakati awali ilikuwa inatambulika kama Azam Sports Federation Cup, ambapo Azam ndie alikuwa Mdhamini Mkuu, tunakubaliana?

Sasa Mkataba wa Azam kama Mdhamini ukatakamatika halafu CRDB akachukua kama Mdhamini Mkuu halafu Azam akabaki kuwa Broadcaster (Mrusha Matangazo) hapa si tunakubaliana? Je tulipewa status ya Azam baada ya kutamatisha mkataba wake? Maana Premier League yupo NBC anatoa hela na yupo Azam kama Broadcaster anatoa fedha tena nyingi saaana ambazo zote zinafahamika.

Sasa kwa faida ya sisi Wakulima na Back Bencher mtuelekeze mnaofahamu kwa lugha rahisi tu, Azam kama Mrusha matangazo na CRDB kama Mdhamini Mkuu maana yake thamani ya kombe la FA imepanda, sasa kiufundi hapo nilikuwa nataka kujua Azam anatoa kiasi gani (kwa nia njema tu ya kujifunza) na CRDB inafahamika anachotoa, hivyo jumla hapo mzigo ni kiasi gani kwenye michuano ya FA?

Kwa sauti ya upole tu na taratibu, kama Azam alikuwepo na amebaki kama Broadcaster, sasa yupo CRDB tunaweza kuambizana thamani ya michuano ipoje na bingwa sasa hivi anachukua kiasi gani huko? Nikiri hili silifahamu ningependa Instagram kitengo cha Taarifa mnisaidie Wakuu.

Na kwa Watu wa Masoko hivi Mdhamini anapoongeza zawadi za Mshindi na bakshishi za Washiriki zinabaki zile zile? Nauliza tu maana hizi ni taarifa nzuri ambazo ni nzuri kufahamishana, kama mikataba inaingiliana kote kote basi tunaambizana kwa sauti ya upole, lengo ni kujifunza tu.
.
.
AMEANDIKA FARHAN JR..
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

hivi ule msimu wakati Benki ya CRDB inaingia kudhamini michuano ya Kombe la Shirikisho   >>> https://gonga94.com/semajambo/hivi-ule-msimu-wakati-benki-ya-crdb-inaingia-kudhamini-michuano-ya-kombe-la-shirikisho
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

MTOTO WA MAMA LISHE

majario rewards 100 Comments 0
 

MY LUNA SEHEMU YA : 06

majario rewards 100 Comments 0
 

NDOA YA MIE ... 8...

majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

majario rewards 100 Comments 0
 

A.J.A.D SE03 EP02

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest