Ingia

Sema Jambo 2025

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  gonga94 official track

KICHAA NA MIMBA YA BOSS❀ SEHEMU YA TISA*

11th Sep, 2025 Views 40



Siku zilizidi kusogea na miezi lilizidi kwenda mbele. Siku moja majira ya saa saba mchana jua kali lilikuwa linawaka, Shahid alikuwa kwenye gari na Aisha walikuwa wanaenda sehemu mara ghafla Shahid alihisi kama kumuona Shania. Aliangalia kwa makini aligundua kwa ni yeye na wakazi huo Shania alikuwa na tumbo kubwa, alikuwa kachoka alitembea huku akiwa anavuta

miguu na mdoli wake alikuwa kuning'iniza.

Shania. Shahid alijikuta kuongea kwa mshangao huku macho yake yakiwa yanaangukia nje kupitia dirishani na huku akiendesha gari kwa mwendo mdogo mdogo. Aisha alikuwa amesikia na akawa makini

kuangalia kule alikokuwa anaangalia Shahid

aligundua kuwa huyo Shania ni yule mwanamke

kichaa.

"Shahidi huyo Shania ni yule kichaa? Shahidi alitaka kumuangalia na hakuona haja ya kumficha.

"Ndio.

"Kuna kitu gani au kuna siri gani unaendelea kati yako na huyo mwanamke kichaa? "Alijitolea sana na nilikuwa nampa chakula mara

kwa mara. Aisha alijikuta moyo wake unatilia na kucheka

kidogo. Alseee kumbe sikuwa na haja ya kulibeba hili kumbe mtu mwenyewe ni kichaa. Shahid alimkata jicho kisha akaendelea

kuendesha gari lakini akili yake haikuwa sawa kumuona Shania akiwa kwenye hali ile kulizua maswali mengi kichwani kwake..

Kuanzia siku hiyo shahidi alitamani kuwa mwenyewe alimwambia Aisha aende kwao kwanza anataka kusafiri kikazi. Siku iliyofuata Aisha aliondoka akarudi kwao na

shahid alipata muda mzuri wa kutafakari mambo yake bila kuchanganywa na maneno. Alianza kufuatilia kuhusu Shania

Siku moja akiwa sehemu alimuona Shania anagombana huku akimtishia mawe kijana mmoja. Ilibidi shahidi aende kujua nini kimetokea Shania alipomuona alianza kulia akamfuata na kumkumbatia "Nini kinaendelea hapa? Shahidi aliuliza watu

waliokuwepo karibu huku Shania akiwa bado kamkumbatia. Yule kijana alikuwa anamtania anakuita

mchumba. "Huyu kichaa huwa hapendi utani na wanaume. Shahid alimbembeleza baada ya hapo

alimchukua wakaenda kukaa sehemu. Shahidi Alimuangalia jinsi alivyokuwa kachoka na lile tumbo lake

Mungu wangu hii mimba inaweza kuwa ni mimba yangu. Alijisemea shahidi Shania alikuwa anamuangalia tu.

"Nataka embe.

"Sawa naenda kukununulia.

Nataka na juice. Shahidi alimuangalia na kuachia tabasamu.

"Njaa ina kuuma? Alimuuliza na Shania akitikisa kwa kichwa. "Sawa subiri kidogo utakula.

Shahidi aliemuacha pale akaenda kutafuta chakula na baada ya dakika chache alirudi akampatia chakula na Shania akaanza kula. Shahidi alikuwa akimuangalia mpaka alipimaliza kula alimshika mkono wakafika upande wa pili wa barabara wakaenda sehemu wanayouza matunda akamnunulia matunda akawekwa kwenye mfuko. Shania sasa nenda nyumbani ulale haya matunda.

"Haya. Shania aliitikia kisha akaondoka huku shahidi akiwa kasimama akimsindikiza kwa macho.

"Kweli damu zenu zinaendana huyu binti hana

ukaribu na mwanaume yoyote na huwa anakuwa mkali sana yani na watu wanajiuliza hiyo mimba kaipataje na huyo mwanaume alimshawishi vipi mpaka akafanikiwa kumvua chup. Mama muuza matunda aliongea, shahidi alinyamaza kimnywa, Shahidi akilipa hela ya matunda kisha akaondoka kwenda kupanda kwenye gari lake.

Kumbe wakati akiwa amekaa na Shania akiwa anakula Rashidi alikuwa amewaona mpaka walipovuka barabara na kunukia matunda pia aliona.

Shahidi alipokuwa anaendesha gari kuelekea nyumbani kwake Rashidi nae alikuwa akiendesha gari kumfuata nyuma.

Shahidi alipoingia tu ndani na Rashidi nae alifika. "Vipi? "Safi, nataka tuongee.

"Sawa,

"Shahid unahusiana vipi na mimba ya yule kichaa? "Unasemaje?

"Nauliza wewe ndio muhusika wa ile mimba ya yule kichaa?

Hili swali lilikuwa gumu kwa shahidi kujibu moja kwa moja alisimama na kumtolea macho Rashidi.

"Ukimnya wako ni jibu Shahid, unamaana ni kweli yake nilivyosikia? Bado Shahid alikuwa kimnya.

Unaleta albu gani kwenye familia? Hujui kama hii ni kadhia mbaya sana na vipi kama Aisha mpenzi wako akijua unaenda kuwa na mtoto na

kichaa?

Anaitwa Shania na usimuhukumu kutokana na matatizo yake. Yule ni mwanamke na anahaki ya kupendwa kama wanawake wengine. "MUNGU WANGU hiki ninachokisikia kutoka kwako ni kweli ama naota ndoto za mchana?

"Kama unaota basi amka, amka kaka yangu Rashidi na usikie ukiwa unajielewa. "Daaaah hii kali ya mwaka aiseee sikutegemea

kusikia hili kutoka kwako yani kwa jinsi ulivyo wala hauendani na matendo umayofanya kwanza ulianzaje kulala na mtu wa aina ile? "Ni kama wewe unavyofanya tu. "Hahahaha huna kinyaa wewe?

Wakuona kinyaa. ni wewe ambae unawabadilisha ila kwangu ilikuwa burudani tu na tamu kupita maelezo.

Shahidi walimaliza kuongea kisha akaelekea chumbani kwake. Rashidi alibaki kasimama na kusema.

"Hii ni aibu ya mwaka bora kunyamaza

nimuachie mwenyewe. Ila nae anatakiwa kupimwa akili yake huenda kaambukizwa uchizi au ndio tuchukulie ule msemo ukikaa na waridi lazima unukle sasa yeye anapata uchizi.

Full 1000
Whatsp 0784468229.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

KICHAA NA MIMBA YA BOSS❀ SEHEMU YA TISA*  >>> https://gonga94.com/semajambo/kichaa-na-mimba-ya-boss-sehemu-ya-tisa

#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Maoni

You're not logged in
Click here to login and comments
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
gonga94 official track
ZETU
SIMULIZI NA SAUTI ZETU
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Tangazo - Kama wewe hujatimiza miaka 18+ usije nasema usije kabisa ni wakubwa tu
Kama wewe hujatimiza miaka 18+ usije nasema usije kabisa ni wakubwa tu
Kama wewe hujatimiza miaka 18+ usije nasema usije kabisa ni wakubwa tu

RATIBA YA SIMULI ZETU

Hakuna ratiba iliyopangwa kwa sasa.


Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest