Ingia

Sema Jambo 2025

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  never give up harmonize

MY FOREVER MAN 💘* __________________________________* *SEHEMU YA KWANZA*

26th Aug, 2025 Views 24



Ilikuwa majira ya saa moja jioni kamila alikuwa amekaa kwenye jumba lake la kifahari katika seble yake iliyopambwa na vitu vya thamani aliendelea na kazi zake za ofisini huku pembeni kukiwa na grass ya juice ya passion.
Akiwa anaendelea na kazi zake mara mlango Mkuu wa kuingilia ndani ulifunguliwa kwa nguvu akaingia mpenzi wake kijo.
Kijo alisimama mbele yake akawa anamuangalia huku akiyumba yumba.
" Inamaana hunioni mpenzi. Kijo aliuliza
Kamila alivua miwani yake ya macho akamuangalia vizuri alafu akasimama.
" Kijo umerudi tena ukiwa umelewa na unaweza kuniambia ulikuwa wapi kwa siku tatu?
Kijo alitoa tabasamu dogo lenye dharau.
" Yani wewe bwana hujui kabisa mahaba baada ya kunipokea kwa shangwe na furaha , unipetipeti unanipokea kwa maswali kwanza ushukuru nimerudi kama isingekuwa nimeishia na pesa nisingerudi hapa.
Sasa mpenzi naomba unipe laki tano hapo marafiki wananisubiri.
" Sikiliza kijo nimechoshwa na mambo yako najua huko uliko ulikuwa na wanawake zako sasa nasema hivi sina hela za kuchezea
" Kwahiyo hunipi au?
" Sina hela za mchezo.
" Wewe ni atm yangu huwezi kukosa hela.
" Basi atm yako leo imeishiwa hela.
" Siku hizi umekuwa jeuri sana lakini sawa tu nitajua nini cha kufanya .
Wakiwa wanaendelea kuzozana Abby gateman wa hiyo nyumba aliingia .
" Na huyu mfungua geti wako, mkaa getini ndio anakutia kiburi nina uhakika huyu mwanaume unalala nae.
Abby alisimama huku akiwa anashangaa anaingizwa vipi kwenye ugomvi wao?
" Madam mimi nimeleta hii karatasi kuna mtu kanipa pale getini.
" Naona na wanaume wa nje wanaanza kuleta vibarua wewe mwanamke malaya sana na mimi siwezi kuendelea kuwa na wewe. Na wewe gateman unaejifanya una kifua cha mazoezi unawavutia wanawake za watu siku nikikukamata nakuchinja.
" Kijo naomba uende ndani .
" Niende ndani saizi kwani mimi kuku? Au una mahamu yako unataka .... Kijo hakumaliza kuongea akaondoka huku Abby akimsindikiza kwa macho wakati huo kamila alikuwa anajisikia vibaya kwa kudhalilishwa .
" Madam mzigo wako huu.
Kamila alipokea ile karatasi.
" Samahani Abby kwa kile kilichotokea.
" Usijali ila pole.
" Asante. Abby alionekana kumuonea huruma kamila lakini hakuwa na msaada.

" Yani nina kila kitu, kazi nzuri, pesa, nyumba , magari lakini kitu kimoja tu nimekosea kupata mpenzi wa kweli. Nampenda sana kijo lakini siku zote amenifanya Chumio lake na suruhisho la matatizo yake hana mapenzi ya kweli kwangu yupo kwangu kwa sababu. Kamila aliongea kwa uchungu
" Pole madam ninaona unachopitia lakini ipo simu Mungu atakupa wa kuendana nae.
Kamila alitoa tabasamu dogo.
" Tatizo nampenda sana na sijui kama naweza ku move on.
" Basi unatakiwa kumuomba sana Mungu waweze kumbadilisha na awe kwenye mstari unaotaka wewe.
" Nahisi kukata tamaa juu yake .
" Kumbuka ni vibaya kukata tamaa na Mungu ndio kimbilio letu na suruhisho letu kwa kila kitu ,niombe sana akionyesha kipi bora kwako.
Abby alijaribu kumfariji kwa maneno baada ya hapo alirudi getini kuendelea na kazi zake.

Siku ya pili Mida ya saa mbili usiku kamila alipiga simu ya kijo ikawa haipokelewai. Alikaa na kufikiria sana badae aliamua kuchukua koti lake na kutoka nje.
Alipokuwa kwenye maeneo ya bustani alisikia sauti ya kike ukiongea kwa ukali.
" Unashangaa nini nimekuja kuchukua hela.
" Latifa mpenzi wangu hela sasa hivi nitapata wapi na unajua mwisho wa mwezi bado haujafika?
" Mimi sitaki kujua , hivi unajua kuwa mimi ni mwanamke mzuri sana?
" Ndio najua mpenzi wangu wewe ni mrembo.
"Basi kama unajua hilo ndio nahitaji huduma sitaki unifuje .
" Mbona najitahidi sana mpenzi wangu kukupa vi elfu kumi kumi...
" 😀😀😀 Ongea taratibu wewe watakucheka watu sasa elfu kumi si hela ya maandazi tu. Na nasema hivi kama huniwezi bora tuachane.....
" Usiseme hivyo mpenzi wangu .
" Basi ukitaka kuwa na mimi tafuta hela kijana kabla wenye nazo hawajapata nafasi na mwaka huu usipotimiza ninachotaka mimi na wewe byebye.
" Nionee huruma Latifa.
" Wakukuonea huruma ni mama yako mzazi mimi sicheki na wowote, eti nakosa hata hela ya kununulia chu* alafu nasema na mimi nina mpenzi.
" Basi nusu ya mshahara wangu nitakupa ukafanye mambo yako.
" Nipe hela ya nauli niondoke boda ananisubiri hapo nje.

Abby aliingiza mkono mfukoni akatoa noti ya shilingi elfu kumi akampa.
" Hii inatosha nini sasa?
" Si nauli .....
Latifa aliingiza mikono kwenye mifuko ya Suruali akachukua hela yote aliyokuwa nayo.
" Hizi una mbakishia nani?
" Hiyo ni hela yangu ya kula kesho, ukichukua mimi nitaanzia wapi kesho?
" Hizo sio shida zangu.
Latifa alichukua hela zote hakubakisha hata mia mbovu kisha akaondoka.

Kamila alitingisha kichwa.
" Nilijua ni mimi tu napitia haya kumbe tupo wengi huyu mwanamke hana tofauti na kijo.
Kamila aliingia ndani huku akiwaza haya mapenzi ni kitu gani mpaka yanaburuza watu kiasi kile.

Siku zilienda siku moja Mida ya saa kumi jioni akiwa chumbani kwake amesimama dirishani alimuona yule mwanamke wa Abby siku hiyo alikuwa na furaha walikumbatiana na Abby alionyesha upendo kwa yule mwanamke alikuwa akimtengeneza nywele.
" Leo ndio ile siku ya furaha kwako .
" Siku ya mshahara si ndio?
" Ndio yani unapenda pesa wewe.
" Hakuna asiyependa hela.
Abby waliingiza mkono mfukoni akatoa hela na kumpatia. Yule mwanamke alifurahi na kumbusu, Abby alitoa mfuko uliokuwa na zawadi akampatia furaha ilizidi kwa Latifa .

Mambo aliyokuwa anafanya Abby yalikuwa yanamvutia kamila alitamani mpenzi kwake kijo aweze kuwa kama yeye angalau awe na furaha nae ajione anaishi na mwanaume halisi na sio kivuli cha mwanaume

Full 1000
Whatsp 0784468229.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

MY FOREVER MAN 💘* __________________________________* *SEHEMU YA KWANZA*  >>> https://gonga94.com/semajambo/my-forever-man-__________________________________-sehemu-ya-kwanza

#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Maoni

You're not logged in
Click here to login and comments
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
profile
mjukuu 26 Aug 2025 15:20
MY FOREVER MAN 💘*
__________________________________*

*SEHEMU YA KWANZA*
never give up harmonize
ZETU
SIMULIZI NA SAUTI ZETU
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork

RATIBA YA SIMULI ZETU

Hakuna ratiba iliyopangwa kwa sasa.


Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest