Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94

NIPE YOTE DADYπŸ’žπŸ’žπŸ’‘28~29

30th Jul, 2025 Views 28

NIPE YOTE DADYπŸ’žπŸ’žπŸ’‘28~29

Baada ya kusoma msg ya Zuuh nilijibu sawa kisha nikainuka na kumsaidia ma mkwe kuandaa meza, baadaya kuandaa tulikaa na kumsubiri baba mkwe
hakuchukua mda alikuja na kuvuta kiti akaketi..

Tulikula chakula baada ya chakula nilitoka na kwenda mjini kwa rafiki yangu, tulipiga story kadhaa wa kadhaa kisha nikaaga na kuondoka moja kwa moja hadi ofisini kwa Selim

nikamwambia inshu iliyotokea asubuhi ili ajue kwamba tayari Aunt anajua ukweli kuhusu mimi.
Tukiwa tunaongea sm ya mezani iliita Selim
akapokea na kusema mruhusu aingie baada ya
sekunde kadhaa mlango uligongwa akaruhusu
mara akaingia Nasra kheee😳😳

Nilishangaa Nasra amefuata nini ofisini kwa Selim ?.Selim Aliniangalia kana kwamba anatamani kuniuliza kitu ila akashindwa tulimkaribisha akakaa ila alikuwa na wasi wasi sana hata ongea yake ilikuwa na kakigugumizi,

baada ya kukaa ikabidi nimwambie Norah karibu sana sikujua kama unafahamu ofisi hii " nilimuita Norah kwasababu hajui kama Selim anajua ukweli
alitabasamu na kujitahidi kuongea kama mimi
aliweza kiasi.

"Aam sikuwa najua ila kuna rafiki yangu
nilikuwa nimekuja kuonana nae hapa nilipoona
jina la kampuni nikauliza maana nilihisi kama
ndio sehemu ambayo shem anafanyia kazi
nilivyoambiwa nikaomba kumuona Maana
sikuona sawa kuondoka bila kumsalimia."

"OH nivizur aam Selim sisi tunaondoka je
kuna neno lolote unalotaka kuongea?"""No sina chochote kikubwa namshukuru shem
kwakuja kuniangalia,asante sana kwa ukarimu
wako.

" Nasra alitabasamu na kumjibu "Usijali ni
jukumu langu " Nilimuangalia Nasra kisha
nikasimama na kuweka kiti vizuri Nasra nae
aliinuka tukatoka nje mda wote nilikuwa
namuangalia hakuwa sawa kama alivyoingia.

Tulishuka hadi chini kisha nikamwambia
nimpeleke kula ice cream alikataa kitu
ambacho sio kawaida yake yani katika vitu
ambavyo Nasra hawezi kukataa ni ice cream
anapenda kuliko vitu vyote sasa leo amekataa
Bila Shaka yuko disappointed -

nikaona nimchokoze Sio kawaida yako kukataa ice cream vp zinakukumbusha nyakati zako na mpnzi wako"

"Hahahahaha haiwezekani bwana na
nilishakwambia mimi na Rajabu hatukuwahi
kuwa na mahusiano yoyote sawa"

"Mmh hamkuwahi kuwa na mahusiano yoyote
na mibinduko mkawa nayo"

"Norah bwana mi najua we nimtoto wa kitaa
unajua si kila unaelala nae basi lazima uwe na
mahusiano nae, so ilikuwa hivyo kwangu na
Rajabu "

"Kwa hiyo ulikuwa unaona kawaida kumpa
mwanaume mwili wako ilihali si mpnzi wako?? Akakaa kimya akasema mi naondoka"

Aliondoka nami nikarudi ofisin kwa selim Vp mbona umerudi?" Aliongea Selim baada ya
kuona nimerudi ofisini kwake, nilivuta kiti
nakukaa kisha nikasema.

"Selim kuna kitu nahisi hakiko sawa na mda si
mrefu kinaweza kunuka "
"Unamaana gani?"
"Nasra ni pacha wangu akili yake naijua vizuri
nauhakika kunakitu kinaendela ndani ya akili
yake"
"Umeanza umbea ee?"
"Selim niko serious ujue
""Wewe kuwa serious sijui anyway nataka
kuondoka kunasehemu ninayotaka kwenda na
ukiulizwa nyumbani sema ninakikao "
"Unaenda wapi?"
"Ni siri "
"Mmh sawa "niliinuka na kuchukua pochi yangu
kisha nikarudi nyumbani.

Nilifika nyumbani na kuingia jikoni (unajua
pamoja na kwamba mama mkwe ametaka kuwa anapika mwenyewe haina maana kukaa tu )au nakosea jamani?.

Basi niliangalia ratiba inasemaje kisha nikatoa
viungo na kuanza kuandaa haukupita mda
akaingia mama mkwe na kunikwapua viungo
akamwaga kwenye dustbin na kusema

"nilisema nini na unafanya nini?"kihele hele
nikome nilivua epron na kuchukua sim yangu
nikatoka bila hata kuongea neno alibaki
anafoka kama kawaida yake.

Wakati nikiwa ndo nimetoka nikakutana na
Jabir akiwa anakuja upande wangu nilisimama
tukasalimiana kisha akanivuta pembeni na
kusema "oya Binam sikia naomba unisaidie kitu
""Kitu gani?"
"Nataka kwenda party na unajua leo mjomba
yupo so nilikuwa nakata nichomoke kisiri siri
alafu wakiniulizia utawadanganya" party jamani
party niliposikia neno party moyo ulisimama
kwa sekunde kwanza aisee ninakaribia mwezi
sijaenda party sasa hii ni nafasi acha niruke
nayo.

Nilimvuta sehemu ambayo watu hawawezi
kutuona kisha nikamwambia "Sasa sikia Jabir
mimi mwenyewe nataka kwenda kwenye hiyo
party"
"Eeeee!"
"Achana na eee ndio nataka kwenda na nafasi
yakutoka ipo kwasababu leo Selim hayupo na atarudi mda umeenda sana kwa hiyo tunaweza
kutoka alafu tukadanganya kwamba tumetoka
pamoja na Selim."

"Unataka kuniiingiza kwenye mtego au
unamaanisha kweli""
"We mpuzi namaanisha kweli, we nenda
kajiandae naenda kumtafuta Selim hapa nijue
anarudi sangap kisha tuchomoke" nilimaliza
kuongea nikaondoka na kumuacha Jabir
akinishangaa naona hakuamini kama ni mimi
nimeongea hivyo.

Niliingia chumbani fasta nikampigia sim Selim
na kumuuliza bila hata kufikilia mara mbili
akajibu mda anaorudi, baada ya kujua niliingia
bafuni nikajiandaa vizuri kisha nikatoka
nakukuta Jabir tayar kashajiandaa kuhusu kuaga haikuwa shida tulisema tunaenda dinner
na Selim wote sawa sisi haoo

Hakukuwa na folen hivyo tulifika kwa wakati,
dakika za mwanzo Jabir alikuwa kama na uoga
ila alivyoona nimechangamka akajiachia
tukaanza kujivinjali

Tuli-enjoy hadi mda ambao Selim alisema
anarudi ulipokaribia niliingia bafuni
nikabadilisha mavazi kisha tukatoka na kuingia
kwenye gari safari ya kurudi ikaanza.

Baada ya masaa mawili tulifika sasa cha ajabu
tunafika getin tunakutana na Gari la Selim
akisubiri kufunguliwa,Jabir alitamani kupaa
maana kiasi flani anamuogopa Selim sasa na
hii inshu ya kutoka wote usiku ilimtoa jasho..

Nilimtuliza Selim aliingia nasis tukaingia kisha
tukapack,kwakuwa lilikuwa gari la Aunt alijua tu
atakuwa ni Jabir ila nilivyofungua mlango tu
alisimama na aligeuka (maana alikuwa
anatembea kuelekea ndani).

Alishangaa na kubaki akitutolea macho,
tulisogea na kumsalimia aliitika na kutuuliza
tumetoka wapi jamani katika watu ambao
siwezi kuwadanganya ni Selim sijui kwasababu
simuogopi au nini ila nilimwambia tumetoka
party.

Hakutaka kuongea sana alijibu sawa kisha
akaingia ndani na sisi tukafata nyuma, tulifika
Seblen na kumkuta aunt akatuuliza dinner
imeendaje tukajibu ilikuwa vizuri kisha tukaaga
na kuingia chumbani huko ndiko moto uliendwa
kuwashwa mr kukwida kama kawaida yake akanikwida hapo kaweka sura kavu wee nilihisi
mtoa roho yuko jirani yangu.

Akaniuliza "Nikitu gani kinaendelea kati yako
wewe na Jabir na mlienda wapi?""
"Se se selim unaniumiza" niliongea kwa
kulalamika akaniachia na kufunga mlango kisha
akaniridia tena "Norah nimekuuliza nikitu gani
kinaendelea kati yako na Jabir?"

"Hakuna kitu chochote ila tulikuwa party basi"
"Party kwanzia lini mkawa na ukaribu hadi
kupelekana party bila hata ruhusa yangu""Oh please Selim unataka kila ninachofanya
nikwambie we mbona umeenda kuonana na
Jeni uliniambia?"

"Sikukwambia wakati ulipokuwa ofisini kwangu
au sio wewe?"
"Uliniambia unatoka na sikwenda kwa Jeni"
"Kwahiyo kwasababu nimeenda kwa Jeni ndio
umeona utoke na Jabir? Na kwann usinge
eenda mwenyewe?"
"Selim siko kwenye mood ya ugomvi sawa we
nimekwambia nilienda party basi kikubwa
sijarudi usiku sana""Kwa hiyo umeachana na Skyler umeamua kuhamia kwa ndugu yangu kweli Norah?"

"Selim unawaza nini wewe nimekwambia
tumeenda party just party unaelewa baba mi
sinaga mambo ya kipuzi namna hiyo"

Aliniangalia na kukaa kimya nilikaa na kuvua
viatu (hivi mnajua nimejuaje kama huyu mtu
katoka kwa Jeni? Nimesikia manukato ya Jeni
hivyo nikajua moja kwa moja alikuwa nae) basi
niliingia bafuni nikaoga na kuvaa night dress
kisha nikapanda kitandani na kulala.

Usiku wa siku hiyo tulilala tukiwa tumenuniana
hata asubuhi aliamka akiwa kanuna
sikumsemesha maana na mimi nilikuwa kama
na hasira nae hivi alafu ukiniuliza hasira zanini
mi mwenyewe sijui.

Basi aliondoka kwenda kazin bila hata kuniaga
alivyoondoka nikatoka na kwenda kufanya
baadhi ya shughuli za ndani kisha nikafua nguo
zangu na za Selim zilivyokauka nikakunja za
nikapasi na kuweka sehemu husika.

Jabir alivyorudi kutoka kwenye mambo yake
akaniuliza kuhusu jana nikamwambia
hatujagombana basi tukaanza kupiga story za
jana kwenye party kidogo nikapata furaha
maana siku nzima nilikuwa nimenuna.

Wakati tukiwa tumekaa alikuja Selim kutoka
Kazin akatusalimia vizuri tu nikainuka na
kumpokea vitu (unajua moja ya vitu
tulivyonavyo mimi na Selim ni kuigiza kuwa
sawa mbele za watu) basi niliongozana nae
hadi chumbani kisha nikaweka vitu sehemu
husika na kutaka kutoka nje akasema."Asante kwa kunifulia nguo"nilimuangalia tu
haikuwa mara ya kwanza kumfulia nguo au
kumfanyia usafi ila leo kwa mara ya kwanza
kunishukuru

niliona sawa kisha nikataka kurudi
zangu kuongea na Jabir ila aliniwahi na
kunishika mkono kisha akanambia.
"Sorry tunaweza kuongea japo kiufupi"
Sikuongea nikasogea na kukaa kwenye sofa na
yeye akakaa na kusema"aama nisamehe kwa
kile nilichokifanya jana,..
"No huna haja ya kuomba msamaha so kuwa
huru"

Niliinuka na kutaka kutoka akanizuia aliniambia naomba unisamehe norah nikamwambia sawaa..alifurahi akasema fungua hizo ni zawadi zako nimekuletea..mmmhh leo selim kaniletea zawadi??alileta zawadi kadhaa zikiwemo heleni

Tulikumbatiana kwa sekunde kadhaa kisha
tukaachiana nilisogea kioo kilipo nikatoa ushungi
wangu kisha nikatoa heleni kwenye kibox nikaanza kuvaa..

Selim alikuja na kunishika mikono
na kuomba anivalishe mwenyewe sikubisha
nikamruhusu..

Alisogeza nywele zangu ambazo zilikuwa
zimefunguka na kufika mgongoni sasa wakati
anasogeza nywele kwa bahati mbaya selim alinigusa mgongoni nyieee..

Nilihisi msisimko wa ajabu mpaka nikajikuta nimetoa sauti ya ajabu "aaaaaaaaaaaaaaa"selim mwenyewe alikuwa kama mtu aliepigwa shoti nini hiki kinatokea mungu wangu mbona sijielewi..

Itaendeleaaaaaa

Full 1000

WhatsApp 0742133100.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

NIPE YOTE DADYπŸ’žπŸ’žπŸ’‘28~29  >>> https://gonga94.com/semajambo/nipe-yote-dady-28-29
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

NDOA YA MIE ... 8...

majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

majario rewards 100 Comments 0
 

A.J.A.D SE03 EP02

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest