Ingia

Sema Jambo 2025

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  never give up harmonize

PENZI LA KIKOMANDO EPISODE 1

25th Aug, 2025 Views 35



Mwanzo….

Ni katika vita kali vinavyopigana majira ya usiku kati ya wanajeshi na waasi .

Wanajeshi wengi wanapoteza maisha katika vita hiyo, James ambaye ni captain wa jeshi anawaambia wenzake sita walio salia wakimbie sababu tayari walikuwa wamezidiwa nguvu na waasi .

“ Kiongozi tukimbie wote, hatuwezi kukuacha hapa pekeyako ….” Wanajeshi walikuwa wakimwita James kwa sauti ya juu lakini james anaamua kubaki kupambana peke yake .

“Hii ni amri kutokakwa mimi captain wenu kimbieni , kumbukeni familia zenu zinawahitaji msihofu kuhusu mimi “ aliongea James kwa sauti ya juu akiwa anaendelea kufyatua risasi .

Wenzake sita waliobaki wanaanza kukimbia.

James anaendelea kupambana na waasi akiwa peke yake amejibana nyuma ya

Mti .

Taratibu waasi wanaanza kumshinda nguvu james na kuanza kusogea katika ule mti aliojibana .

Kuna kumbukumbu mbaya inamjia James akiwa yupo kwenye ule mti .

Baada ya kumbukumbu hizoJames akajitokeza kwa hasira akiwa na mitutu miwili kwenye mikono yake na kuanza kumimina risasi kama kichaa .

“Haaaaaaaaaaaaa……” James alipiga kelele kwa hasira akiwa anawashambilia waasi akisuri tu umauti umfike maana waasi walikuwa ni wengi zaidi na zaidi.

Mitutu ya James aliyokuwa ameishika katika mikono yake miwili inabaki kutoa sauti tu badala ya risasi.james anaharuki na kugundua risasi zilizokuwa ndani ya silaha zake zimeisha

Waasi wengi alikuwa tayari amewaangusha lakini waliobaki ni wengi zaidi ya waliokufa .

Hapohapo waasi wanamzunguka james wakiwa na siraha kubwa ambazo zote zilielekezwa katika kichwa cha james ikisubiriwa amri ya kiongozi wafyatue risasi.

James anamtazama kiongozi kwa macho ya hasira sana akiwa katikati ya waasi .

Kiongozi anatoa amri kwa sauti kali “ uwaaaaaaaa” ghafla sauti nyingine ya kike inasikika nyuma yao.

“Subirini …” Ilikuwa ni sauti nyororo sana iliyowafanya waasi wote wageuke kutazama ni nani?

INAENDELEA……

Mambo ni moto

Je, james atapona mbele ya waasi ?

Mwanamke huyo ni nani?

Kumbukumbu gani mbaya zilizomjia james na kumpa hasira ?
.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

PENZI LA KIKOMANDO EPISODE 1  >>> https://gonga94.com/semajambo/penzi-la-kikomando-episode-1

#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Maoni

You're not logged in
Click here to login and comments
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
profile
majario 25 Aug 2025 19:06
PENZI LA KIKOMANDO

EPISODE 1
never give up harmonize
ZETU
SIMULIZI NA SAUTI ZETU
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork

RATIBA YA SIMULI ZETU

Hakuna ratiba iliyopangwa kwa sasa.


Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest