Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  never give up harmonize

SEHEMU YA 20--21 A STRANGER WHO STOLE IS HEARTโค๐Ÿ˜

11th Aug, 2025 Views 20


"Amepatwa na nini ?" Aliuliza Elian

" Amepata ajari "
alijibu dactari mmoja

" Amepata ajari gani mbona yupo hivi ?" Aliuliza Elian huku ameshika mkono wa Winnie

" Unaundugu na mgonjwa mbona unauliza maswali mengi tunaomba utupishe tumpeleke ndani akafanyiwe huduma laa sivyo atapoteza mtoto wake "
madactari walimuingiza Winnie ndani na muda huo riffat alifika na gari lake
" Riffat "
aliita Elian lakini riffat hakumsikiliza aliingia ndani ya hospital kujaza taarifa za mgonjwa Elian alimfuata nyuma

" Unajua ana mimba ya miezi mingapi ?"
Dactari mmoja alimuuliza riffat

" Ndiyo ni miezi mitatu Sasa kama na week mbili , tafadhali dactari naomba umuokoe Winnie na mtoto wake" riffat alimuomba sana dactari, Elian yeye alibaki kushangaa

" Tutafanya chochote tunachoweza kuwaokoa wote wawili"
alisema dactari kisha aliondoka

" Ina maana mtoto ni wa kwangu ?"
Elian alijiuliza mwenyewe

" Wewe kwanini umefanya hivi Elian nina uhakika watekaji wataKuwa walikutafuta kwanza wewe na sio mimi "
riffat alimshika shati Elian

" Sikuwa najua kama ni mtoto wangu "
machozi yalimtoka Elian

" Hata Kama sio mtoto wako Elian ulitakiwa kuwa na ubinadamu hata kidogo Nina uhakika ungeweza kumsaidia milioni 5 sio kitu kwako ,nataka uondoke Sasa hivi Winnie ni jukumu langu kwanzia leo nenda kwa mwanamke wako "
riffat alimfukuza Elian, Elian alitembea akiwa na mawazo hakujua hata amefika vipi kwenye chumba alicho pumzishwa loveness

" Elian vitu nilivyokuagiza viko wapi ?"
Aliuliza loveness

" Aaah ngoja nikanunue sijui imekuwaje sikununua "
Elian alitaka kuondoka loveness akamzuia

" Elian haupo sawa niambie nini shida ?"

" Ni Winnie yupo hapa hospital ameumia vibaya sana na ana mimba yangu , loveness sijui nafanya nini "

" Nenda ukajue Hali yake ukiendelea kukaa hapa utazidi tu kuumia na kusongwa na mawazo "

Elian alienda alikuta Winnie anatolewa chumba Cha huduma na kupelekwa wodini

" Winnie nisamehe najua nimefanya kosa kubwa sana lakini nahitaji msamaha wako "

Elian alitaka kumshika Winnie, Winnie akausukuma mkono wa Elian

" Doctor nataka kuwa mwenyewe waambie watoke "
Winnie aliongea kwa sauti ya chini sana ni wazi alikuwa na maumivu makali

" Mtoke nje Sasa ili mgonjwa aweze kupumzika "
doctor alitoka nje ya chumba akiwa na riffat na Elian

" Anaendeleaje kwa Sasa yeye na mtoto ?"
Aliuliza Elian

" Maendeleo ni mazuri kidogo kwa mama ataendelea ku recover lakini amempoteza mtoto wake ndomana anahitaji kupumzika zaidi "
doctor aliondoka

" Haya yote ni makosa yangu "
Elian alianza kulia , riffat alimkumbatia

" Sasa unalia nini na unatarajia mtoto mwingine kutoka kwa loveness"

" Loveness ni kama rafiki tu kwangu na yule mtoto sio wa kwangu riffat ni story ndefu "
Elian alimuelezea riffat kila kitu

" Ulitakiwa kusema mapema ona Sasa na mimi nikaanza kukuchukia "

" Nilitaka iwe Siri mpaka tutakapofanikiwa kumpata Collins, natamani kurudisha masaa nyuma ili nimuokoe Winnie pamoja na mtoto wetu "

" Unajua kabisa Hilo haliwezekani kwa ushauri wangu subiri apone utajaribu kuongea nae "

" Hawezi kunielewa kabisa anauchungu wa kumpoteza mtoto"

" Acha kukata tamaa mapema mimi nitakusaidia kuongea nae "
aliongea riffat huku analipiga piga bega la Elian

" Nitashukuru sana kaka "
Zilipita siku nne Winnie akiwa bado yupo hospital na siku hiyo alikuwa anaruhusiwa kwenda nyumbani akiwa anashuka ngazi alikutana na loveness pale pale hospital

"Mambo Winnie,nimesikia ulipata ajari pole "
loveness aliongea lakini Winnie hakumjibu chochote badala yake alimkaba loveness

Riffat na Elian walifika wakakuta watu wanashangaa Winnie amemkaba loveness

" Winnie acha kufanya hivyo ni hatari "
alisema Elian

" Hatari ? Unajua mimi nilinguka sehemu hatari kiasi gani hahaha " Winnie alicheka kama chizi

" Nitamsukuma kwenye ngazi mtamlipa mtoto wangu kwa mtoto wenu "
Winnie aliongea kwa kupiga makelele

" Winnie tafadhali usifanye hivyo unaweza kuniumiza mimi kama unataka lakini sio loveness Wala mtoto wake"
alisema Elian
" Wow hongera sana binti inaonekana unapendwa sana " Winnie alimsukuma pembeni loveness kisha alianza kuondoka.

" Winnie "
Elian alitaka kumfuata Winnie , riffat akamzuia

" Ana hasira sana kwa Sasa utaongea nae siku nyingine "
riffat alimfuata Winnie
Ilipita week nzima ndipo Winnie alirudi kwenye Hali yake ya kawaida

Na kwa upande wa Elian alifanikiwa kumpata Collins

" Mbona unatabasamu sana umefanikiwa kurudiana na Winnie ?" Aliuliza loveness

" Hapana ni habari njema kwako ,nimefanikiwa kujua Collins Yuko wapi " aliongea Elian huku anatabasamu

" Wow thank you so much Elian "
loveness alienda kumkumbatia Elian

" Kesho tunatakiwa kwenda London amesema anataka kukutambulisha kwa shangazi yake na mjomba ake watu pekee waliomlea na baada ya hapo atakuja Tanzania kwaajili ya ndoa "

" Yani natamani twende hata Leo "
loveness alifurahi sana

" Anza kufanya mandalizi mimi natoka kidogo Kuna mtu naenda kuonana nae "

" Tunaenda wapi riffat ?" Winnie alimuuliza riffat wakiwa kwenye gari

" Kuna sehemu nzuri sana tunaenda utajua tukifika "
walifika nje ya jumba moja kubwa sana walipaki gari na kuingia ndani

" hii nyumba ni nzuri sana afu inaonekana mpya kabisa unataka kununua nyumba kwaajili yako na Tracy mkifunga ndoa ?"
Winnie alimuuliza riffat

" Hapana utajua Sasa hivi nisubiri kidogo narudi endelea kuangalia mazingira ya nyumba " riffat alitoka nje Winnie akiwa anaendelea kuangalia mazingira ya nyumba alisikia mlango unafunguliwa

" Riffat hii nyumba Iko Bomba sana kama unataka kuiacha sikushauri kabisa ingekuwa sio huu ufukata wangu ningeinunua hii kwaajili ya wazazi wangu " Winnie aliongea bila kugeuka nyuma akijua aliyeingia ni Riffat

" Umeipenda?"
Ilisikika sauti ya Elian nyuma ya Winnie Unafanya nini hapa,?" Winnie alimuuliza Elian kwa ukali

" Nipo hapa kukuomba msamaha Winnie tafadhali misikiliza kule nitakachokwambia " Elian alitaka kumshika Winnie , Winnie alimsukuma

" Sitaki kusikia chochote kutoka kwako na kingine jiheshimu kwani wewe si una mke na unaenda kuwa baba hivi karibuni " Winnie alitaka kuondoka Elian alimvuta akamkumbatia kwa nguvu

" Nisamehe sana Winnie sikuja hapa kugombana na wewe nataka tu kuongea maneno machache na wewe "

" Niachie Elian nitakun'gata Sasa ivi " Winnie hakuwa anatania aliun'gata mkono wa Elian , Elian alimuachia alitoa karatasi na kumpatia Winnie

" Unanipa hizo karatasi za nini ?"
" Ni hati ya hii nyumba inaonyesha wewe ndo mmiliki wa hii nyumba kwanzia leo "

" kwanini unipe hati ya hii nyumba na sio loveness ?au unataka kunifanya niwe mchepuko ? Hilo sahau " Winnie alimtupia Elian ile hati ya nyumbaA

Offer offer offer
Soma yote kwa sh 600
Whatsp 0784468229.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

SEHEMU YA 20--21 A STRANGER WHO STOLE IS HEARTโค๐Ÿ˜  >>> https://gonga94.com/semajambo/sehemu-ya-20-21-a-stranger-who-stole-is-heart
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

never give up harmonize
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+

RATIBA YA SIMULI ZETU

Hakuna ratiba iliyopangwa kwa sasa.


Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest