Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  gonga94 official track

Simulizi: CHEUSI MANGALA (Sara Ugandan Queen) LA!: Sehemu 01 -02

16th Jul, 2025 Views 33



Dar es salaam bandarini wanashuka watu kwenye boti wanaelekea kituo cha mabasi ya mwendo kasi abiria wanasubiri basi kuelekea mwembe chai

Abiria wanashuka muembe chai wengine wanaelekea katika mabasi kwa ajili ya safari ya Kampala Uganda

Kuna wanaonunua vyakula maji kwa ajili ya hakiba ya safari

Mizigo inatiwa sehemu maalum Wanafunzi wanaingia ndani ya basi kila moja anakaa kutokana namba yake ya kiti safari inaanza kuelekea Uganda

Tunapita mkoa hadi mkoa baadhi ya vituo Tunasimama kwa ajili ya kuchimba dawa na kupata chochote kwa ajili ya kula

Tukimaliza safari inaendelea... muda wa siku mbili ndio tunawasili mpakani tunashuka kwenye basi tunaingia uhamiaji mizigo inakaguliwa

Nasisi tunagongewa muhuri katika hati ya kusafiria kuna Mtanzania pia tunakaguliwa na Mganda

Tunachenjisha pesa palepale mpakani zoezi linamaliza tunaanza safari ya kuelekea Kampala Uganda

Chuo kikuu cha Kampala

Tunafika jioni tunashuka na mizigo yetu tunaingia ndani katika mabweni wanaume yao na wanawake yao yametenganishwa na barabara

Kila mtu anapandisha mizigo yake juu katika vyumba Tunaenda kufatia godoro

Kutoa uchovu naingia chooni kujitia maji navaa nguo yangu natoka nje saa kumi na mbili tayari wakati wa kugaiwa chakula unapanga foleni kama tupo loliondo kwa babu kikombe

Waganda wana foleni yao na Sisi watanzania tuna foleni yetu

Inafika zamu yangu natiliwa chakula kila kitu umoumo kama bata wali sembe maharage utajijua 🀣

Narudi zangu bwenini kwetu chumbani tunakula na wenzangu mapishi tafauti na kwetu chakula hakina samaki

Siku nyengine tunapikiwa matoke ndizi zinachemshwa zinapondwa 😁

Siku za skukuu ndio mnapikiwa supu ya nyama na kuku

Asubuhi mnapikiwa chai au uji kitafunwa mtajijua wenyewe

Nje kunauzwa mihogo apo ndio kijiweni tunakutana watanzania ndio hoteli yetu ya nyota tano😁

Bweni letu la wanaume horofa ya juu ukisimama unaona wanapofua na kuanika nguo wanawake

Natupa jicho kama masihara nataka kuligeuza linagoma moyo unanishawishi muangalie vizuri

Toto la kiganda amevaa taula yakufutia maji imeanza kifuani imeishia kwenye mapaja

Mrefu kiasi ana nywele za Kiafrika nyingi nyeusi refu uso wa mviringo

Shingo refu kama twiga kasiringana kiuno na hipsi miguu minene ana rangi nyeusi ya kungara

Kila nikitaka kugeuza shingo moyo unakataa
Mtoto kavaa taula anafua na kuanika nguo mapigo ya moyo yanapiga kwa kasi

Usiku wakati wakujipumzisha taswira yake inanijia kila nikifumba jicho

Kumekucha anaamka usingizini la kwanza kukumbuka taswira yake sitamani kuamka kitandani lakini imenilazimu kuamka

Tunanaanza pirika za kufanya usajili kulipa ada pamoja na kukutana na walimu mimi nachukua stashahada ya IR (international relations) uhusiano wa kimataifa

Tunaanza masomo rasmin mchakamchaka
Chuo tulichofikia cha manesi na Daktari walikuwa ni kipindi cha kufanya mitihani

Mnajua penzi likeshaingia kwenye moyo linahangaisha nikaanza kuhaha natamani kumuona mganda kila wakati

Asubuhi kabla ya mtihani wanakaa paredi jicho linamsaka kila kona linatulia ninapomuona mtoto katulia kuanzia kichwa hadi unyayo

Chuoni kuna bustani watu wanakaa kusoma mkufunzi anatusomesha upo mwili akili haipo jicho lote kwa toto la kiganda mpaka mdomo nimeachama denda linanitoka🀣

Nashtuka wenzangu wananiita oya vipi mwamba najibabaisha mkufunzi ananitizama kwa mashaka

Tunamaliza kusomeshwa uzalendo unanishinda namfata bonge la dada 😁

Samahani naomba tuzungumze mtoto ananiangalia jicho regerege la kike hasa mimi hoi msela

Analeta pozi namshika mkono tafadhali anautoa mkono mbio unamhisi kama mtu alopata shoti ya umeme

Ananitolea macho anajitahidi kukaza lakini unaona kabisa hali siyake

Anataka kunyanyuka nakaa kwenye kiti naibana mikono yake kwenye meza asinyanyuke

Uganda Queen anaangalia kila upande kama watu wanatuona au hawatuoni mimi ata sijali nijili moja maulidi ya bwana mtume🀣

Sauti yangu naiyona imebadilika hafla inanguruma kama simba yupo mawindoni macho yetu yanakutana Uganda Queen anatulia ananisikiliza kidume natema nyongo

Tafadhali nisikilize mtu hakatai wito anakataa analoitiwa tangu nikuone sijui kimeniingia nini katika moyo wangu Ugandan Queen

Natamani nikuone kila wakati inanijia taswira yako unaitwa nani ananitumbulia macho hajibu kitu

Mara anakuja mwanafunzi mwenziwe anamuita Sara twende tukasome napata kufahamu jina lake anaitwa Sara

Sara ananyanyuka anaongozana na mwenziwe namimi namsindikiza kwa macho najipa moyo kama kavutika namimi nitaona ishara

Sara wanafika mbali kidogo karibu wanataka kupinda anageuza uso ananitizama anatabasamu

Sara meno yake yamepangika vizuri meupe akicheka anabonyea mashavu. Ananiacha hoi mtanzania mimi😁

Sara anataka kujikwaa mwamba nanyanyuka haraka naita Sara watu wanageuka wananitizama

Sipepesi macho Sara anasaidiwa na rafiki yake ananyanyuka anajiweka sawa anageuka tena ananitizama anatabasamu

Nahisi amani ya moyo namimi namrejeshea tabasamu

Tunapokutana sehemu huwa tunaanzisha marafiki wapya, chuoni kuna mshkaji tunasoma kada moja tunazoena anakuwa ndio rafiki yangu

Nje ya chuo kuna muuza matunda pia anakuwa rafiki yangu nikienda kununua matunda tunapiga stori mbili tatu siku zinaenda

Kila nikimfukuzia sara ananiringia lakini mwamba sikati tamaa

Nimekaa bwenini Sara anapita chini barabarani bahati nzuri nimekaa kwenye dirisha naona mtu anaangalia juu nilipo

Namimi jicho lote kwake kwenye nafsi yangu ipo siku nitakutia mikononi Sara utakuwa wangu mama watoto

Rafiki yangu ibra anakuja karibu yangu oya Vipi nakuona hujijui kwa yule demu unamjua mtoto wa kizito baba yake ndio mwenye chuo hichi vituo vyote anamiliki yeye

Najikuta nacheka sana rafiki yangu watoto wa kizito hawana moyo hawapendi

Ibra anasema kwa msisitizo mimi nakutahadharisha anae kwambia anakupenda tafuta vinuka mkojo wenzio kina mwajuma machupi🀣

Sawa nimekusikia ila nitahakikisha mpaka anakuwa mama watoto hata kama mtoto wa raisi

Mimi nimempenda kwa nia safi kuamini nguzo marufuku kukata tamaa

Ibra umekuwa sharukhan na filamu ya koila kila la kheri ukikumbana na Amrishpuri mimi simo nakukana kabla jogoo halijawika

Sawa mkuu niachie mimi nimelianza namaliza mwenyewe mchezo mzima

Ibra anaguna hmm jifanye shujaa legendari uambulie Asante kama majeshi enzi izo

Manzi kama wale tunakula kwa macho basi tunawamezea maji funda la mate tunawaachia wanaomiliki nchi

Wewe unajifanya ukawa mkaidi ohoo kita kukuta kitu

Sawa tulale nimechoka risala gaazeti kubwa fupisha nakesho nayo siku

Watu wote washalala mimi sijapata hata lepe la usingizi nawaza maneno alonambia mshkaji mazito

Namimi nishajiingiza kwenye mtumbwi wa vibwengo

Najipa moyo hakuna kurudi nyuma CCM mbele kwa mbele😁

Naamka nachungulia dirishani naona upande wa jengo la wanawake chumba anacholala Sara na wenziwe taa haijazimwa

Sara anatoka mpaka varanda kavaa nguo ya kulalia kibukta na topu juu jicho limenitoka pima natamani nimfate lakini naanzaje kwa mfano

Sara anageuka ananiona tunatazamana anashtuka anabetua midomo anaingia chumbani mbio

Narudi kitandani nahisi hisia mchanganyiko nawaza uzuri wa sara nawaza maneno ya muhuni 😁 kanambia ukweli mtupu kanipiga mabapa ya mapanga kisawasawa

Asubuhi mapema naenda kuchukua chai tunakutana na Sara tunagongana Sara anakasirika angomba ukienda huangalii mbele

Mimi sina la kusema nakuwa kimya naangalia tu uumbaji wa mungu mtoto anamidomo mizuri unatamani umpige busu

Sara anachukua chai anaondoka nimetulia namtizama anavyotembea mpaka anapotea machoni

Nachukua chai napasha uchango kwa maji ya moto tayari kupiga kitabu

Tunafanya kazi za vikundi majadiliano tunawasilisha mada mtu moja moja mbele imefika zamu yangu unajua uwoga wakusimama mbele ya hadhira ya watu

Nasimama naanza kuwasilisha mada tulopewa katika kikundi chetu Sara anatokezea napata ujasiri sijawahi kuwa nao

Nawasilisha mada jicho lote lipo kwa Sara nahisi kama hapana mtu tupo mimi na yeye tu

Mpaka namaliza namuona Sara anapiga makofi natabasamu nasikia kofi za wengine ndio nahisi uwepo wao

Mapenzi yana nguvu sana unaweza kufanya vitu ambavyo hajawahi kufanya maishani inategemea uko upande upi wa mapenzi hasi au chanya

Ukiwa katika mapenzi chanya unakuwa na furaha kila wakati

Katika kazi za maendelo unakuwa mstari wa mbele kwenye masomo utafanya vizuri

Una utulivu na amani unaweza kushiba bila ya kula unanawiri unaridhika na vitu vidogo

Unajitoa sana kwa watu unakuwa mwenye kutatua changamoto za wengine

Unajali unathamini umpendae pamoja na watu waliokuzunguka

Unanguvu ya ndani na nje inayokusukuma kuwa na ubinaadamu kwa sababu ya kupata unachokipenda

Mapenzi yakiwa hasi unayempenda hakupendi au umependa sehemu sio sahihi

Unakosa kujiamini unajiona mkosefu unaanza kujitoa kasoro unakuwa na huzuni

Inaathiri ufanisi wa kazi unyong'onyevu wa mwili na akili

Hasira unajichukia wengine huenda mbali huona hawana sababu ya kuishi na kuondoa uhai wao jambo ambalo sio sahihi

Kukataliwa sio mwisho wa maisha kuna vitu tunavipenda lakini havina kheri nasi

Tujifunze kuto kuendekeza nafsi isitupelekeshe

Kusubiri muhimu pindi unapopata jawabu lahapana

Using'ang'anie usipopendwa unapoteza wakati

Hamisha ufanisi kwenye kazi wekeza nguvu zako kwa anaekupenda ili umsahau unaempenda

Kuna mtu tayari yupo kwa ajili yako Anasubiri utupe mshipi anase mazima.

Penda unapopendwa ridhiya utafurahia maisha

Sara wanamaliza mitihani wanataka kuondoka situlii nawaza akiondoka itakuaje sijazungumza nae

Napata wazo namtumia rafiki yake, nampa barua utafikiria tupo shule ya msingi 9100 😁

Habari yako Sara

Natumai umzima wa afya

Sara naandika barua hii matumaini yangu utaisoma na kuzingatia

Ugandan Queen naomba tuonane nina jambo muhimu nataka nikwambie

Tafadhali usikatae wito kataa utachoambiwa

pia zingatia kama kitakuwa hakina dhara na chenye kuleta faida usikatae

Mimi Omar

0778955701

Sara anamaliza kusoma barua anatabasamu anatafuta sehemu iliyojificha ametulia anaingiza namba anapiga simu

Nimekaa najisomea chumbani nasikia mlio wa simu natizama namba ngeni naipokea mbio

Upande wa pili nasikia sauti ya kike Assalam Alaykum warahmatullah wabarakatuh

Naitikia Waalaykum Ssalam warahmatullah wabarakatuh

Sara anajichekesha nimeitikia wito Omar

Najipa moyo naamini kama mtoto kakubali kuzungumza nami ishara tosha kuwa kashaanza kunielewa kilichobaki kugongomelea misumari vizuri

Nazungumza kwa hisia Sara naomba tukutane juu ya mlima tafadhali saa kumi jioni

Sara anaitikia sawa Omar anakata simu

Nahisi furaha mpaka natetemeka mara nikae mara nisimame naisevu namba ya Sara Ugandan Queen

Je! Sara atakwenda juu ya Milima?

Hii simulizi mpya nitakuwa natuma kwenye ukurasa wangu tu

muendelezo followπŸ‘‡πŸ‘‡

Simulizi Za Mpemba OG

0778955701
...............
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

Simulizi: CHEUSI MANGALA (Sara Ugandan Queen) LA!: Sehemu 01 -02  >>> https://gonga94.com/semajambo/simulizi-cheusi-mangala-sara-ugandan-queen-la-sehemu-01-02
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
karibu msagala furniture
karibu msagala furniture

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

Simulizi: MAPEPE **

majario rewards 100 Comments 0
 

NDOA YA MKEKA 03

majario rewards 100 Comments 0
 

.BABAMKWE epsd 19.

majario rewards 100 Comments 0
 

ALINIINGIA BILA IDHINI

majario rewards 100 Comments 0
 

BABAMKWE..17..18

msagala rewards 100 Comments 0
 

bei sawa na bule

majario rewards 100 Comments 0
 

BABAMKWE epsd 16

majario rewards 100 Comments 0
 

BABAMKWE epsd 14...15

majario rewards 100 Comments 0
 

MDOLI MPENDA UTAMU...1

majario rewards 100 Comments 0
 

HUYU KAKAπŸ™ˆ3~4

majario rewards 100 Comments 0
 

BABAMKWE epsd 11.

majario rewards 100 Comments 0
 

GIGY MONEY DAH😭

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest