Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Pyar Ho Jane Dushman

SIMULIZI : DADA POWA WA USIKU MMOJA MTUNZI; NURU HALISI SEHEMU 06

1st Aug, 2025 Views 15



ENDELEA.......
"Ondoa hii sahani..." Sabrina aliongea.

Anjeli alinyoosha mikono yake akachukua sahanj, sijui ni nini kilimpata lakini mikono yake ilimsaliti sahani ikadondoka chini.

"Sa...sa... samahani!" Aliongea akiwa anatetemeka.

"Kama samahani yako inaweza kuirudishia uhai hiyo sahani umesamehewa, tofauti na hapo naomba uondoke" Sabrina aliongea akiwa kashikiria moyo wake.

Victor aliwahi kumnyanyua akampeleka chumbani kwake.
Mshtuko alioupata ulikuwa ni mkubwa sana kiasi kwamba alishindwa kula.

"Ondoka nitavitoa hivyo vipande vya sahani..." Hilda aliongea baada kuona Anjeli ana churuzika damu.

Anjeli alielekea chumbani kwake akiwa mwenye hofu kubwa.
Alishindwa kuelewa kwanini Osman yupo hapa.

Ila baada ya kuitafakari vizuri sura ya Sabrina, aligundua watu hawa wana uhusiano wa damu.

Usiku wake ulikuwa mgumu sana, alipoteza kujiamini hasa akifikiria ajali ya moyo aliyomsababishia Sabrina.

"Vipi kama atakufa!...." Anjeli aliwaza mbali.
Hakuwa tayari kupandishwa kizimbani kwa kosa la mauaji.

Akili ya kutoroka ilimuijia, baada ya kuhakikisha nyumba yote imepoa. Alifungua dirisha akaanza kupambana kujipenyeza mpaka akafanikiwa.

Alianza kutembea kwa kunyata, lakini ghafla alihisi kuna mtu nyuma yake.

"Unaenda wapi usiku huu..." Osman aliongea.

"Naomba unisaidie kuondoka hapa, nyota yangu na yako haziendani endapo tutakaa kwenye eneo moja hivi nahofia kusema nitakuwa ni mtu wa mikosi tu" Anjeli aliongea.

"Naelewa umezoea kutembea na Wanaume wa kila rangi, ni ngumu kwako kuishi kama Mfanyakazi mahali hapa....kuliko utoroke subiria kupambazuke uondoke kwa kuaga" Osman aliongea huku macho yake yakiwa kwenye lips za Anjeli.

Anjeli anashindwa kuelewa ni kitu gani huyu mtu anashangaa, aligeuka nyuma lakini hakukuwa na kitu

"Una lips nzuri sana, kwanini usizitumie kuonja sukari au chumvi huko jikoni na si kubadilishana mate na kila Mwanaume anayekuja kwako!" Osman alishauri.

"Una zungumza vitu gani wewe Mpuuzi! hivi hujui ile sahani imepasuka kwa sababu yako!...wewe ni mtu wa mikosi sana ni vile hujijui tu" Anjeli aliongea.

"Rudi ndani ukalale, huwezi kupita hapo getini pengine kama utampa Mlinzi Lushwa ya ngono lakini kwa jinsi navyomjua atakutumia kisha atakurudisha ndani..." Osman aliongea.

Anjeli alibakia kukodoa macho asijue ni kitu gani aseme, baada ya akili yake kufikiria vizuri alimshika mkono Osman akiwa katika sura ya kipole

"Naomba unisaidie kuniombea msamaha kwa Sabrina....tafadhali sana" Anjeli aliongea.

Mkono wake ulikuwa unampa raha fulani hivi Osman...mwili wake wote ulianza kusisimka.... maumbile yake yalianza kufurukuta kisa na maana kashikwa tu mkono.

Taratibu alianza kuusogeza mdomo wake ambusu Anjeli, ubongo wake haukuwa ukifanya kazi hata kidogo zaidi ya kufikiria ngono.

Hakuwaza kama yupo eneo la hatari, Anjeli aliachia sonyo baada ya kuyasoma mawazo ya Osman.
Alimuachia mkono kisha akarudi ndani.

Wakati yote haya yanaendelea Hilda alikuwa juu ya kibaraza akiwatazama.
Hakutarajia kama Mume wake ni mshenzi kiasi hiki.

Alirudi chumbani kwake akiwa mwenye hasira.

"Sahani haikuvunjika bahati mbaya, wawili hawa watakuwa wana fahamiana" Alijisemea kisha akakaa kwenye kiti akaanza kusoma kitabu.

Osman anashtuka baada ya kumkuta mkewe amekaa.

"Nilitoka nje kuzungumza na Victor, siku ya kesho nitakuwa na ratiba ngumu sana" Osman aliongea huku akijitahidi kuficha umbile lake lililosimama sababu ya kushikwa tu mkono na Anjeli.

Hilda aliachia tabasamu kisha akaendelea kusoma kitabu.

Asubuhi na mapema sana Asha anafika nyumbani kwa Sabrina Kutoka Dodoma.

Alitembea kwa haraka sababu alikuwa na shauku ya kumuona Osman.

"Sitaki kuamini mpaka sasa hivi kalala!...kuna muda sielewi kazi ya Victor ni nini" Asha alijisemea huku akiangalia saa yake.

Alipitiliza ndani bila kuvua viatu vyake, Anjeli anasikia hasira baada ya kuona tope na wakati amemaliza kudeki.

Kwa hasira alianza kudeki huku akimtukana mtu aliyemrudisha nyuma.
Wakati anamalizia kudeki alishtukia akigeuzwa kwa nguvu.

Macho yake na ya Asha yalikutana,
Anjeli hakuwa akimfahamu Asha hivyo alijikuta akimkodolea tu macho.

"Zimesalia dakika 20 kikao kianze, nenda kawashe gari..." Sauti ya Osman ilisikika akiwa na Victor.

Asha aliondoka, kwa mara nyingine aliacha tope tena

"Ondokeni nirudie kudekiiiii!" Alijikuta akizungumza kwa jazba, sauti yake ilitapakaa nyumba yote kiasi cha Sabrina kushtuka usingizini................FULL STORY 1000. STORY NI NZURI SANA NA NDEFU.

NAMBA YA MALIPO 0743770612 JINA JOFREY.

UKISHALIPIA NICHEKI WHATSAPP KWA NAMBA HII 0683009150..
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

SIMULIZI : DADA POWA WA USIKU MMOJA MTUNZI; NURU HALISI SEHEMU 06  >>> https://gonga94.com/semajambo/simulizi-dada-powa-wa-usiku-mmoja-mtunzi-nuru-halisi-sehemu-06
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Pyar Ho Jane Dushman
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CHANZO NI BOSS 03

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CHANZO NI BOSS 02

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CHANZO NI BOSS 01

majario rewards 100 Comments 0
 

MTOTO WA MAMA LISHE

majario rewards 100 Comments 0
 

MY LUNA SEHEMU YA : 06

majario rewards 100 Comments 0
 

NDOA YA MIE ... 8...

majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest