VYOTE NDANI GONGA94
MY TRUE LOVE STORY SEHEMU YA 18
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
Naona niwaambie ukweli wa kila kitu, najua kuna baadhi ya vitu mnavijua na kuna baadhi ya vitu hamjavifahamu bado na mimi sina shida yoyote ile na maamuzi yenu wala maamuzi ya familia yenu na mapenzi yenu, na nitapambana sana kumuweka mke wangu sawa na atakubaliana na kila kitu ila ni swala ambalo litakuwa linahitaji mud asana…
Ipo hivi “ siku moja mimi na mke wangu tulikuwa tunaenda sehemu, kuna sehemu tukafika gari letu likaharibika, na ilikuwa ni usiku wa kama saa tano hivi, tukaagiza n fundi aje, na kweli baada ya muda flani fundi alifika na baada ya kufika, akatutengenezea gari kisha akaondoka zake, sasa wakati huo mke wangu alikuwa anazunguka zunguka, na hilo eneo ambalo tulikuwa tunapita ilikuwa ni karibu na mto tengeru, sijui hata ulikuwa unatokea wapi…
Tukamuona huyu kijana amezombwa na maji, mke wangu alipomuona tu akasema “ mume wangu mtoto wetu hakufa huyu hapa tumpeleke hospital…
Nilishangaa sana na nikasema niende kumuangalia huyo ambae mke wangu anamuongelea, ndio nikakutana na huyu kijana, alikuwa katika hali mbaya sana, tukampeleka hospital ila napo hakuwa amekaa sawa, mke wangu ikabidi auze mpaka vitu vyake vya thamani akaenda kutibiwa nje, na baada ya muda akakaa sawa, ila kwa kipindi kile alikuwa amepoteza kumbukumbu na tukampa jina la nabil..
Kijana wetu alifariki akiwa mdogo sana, na mke wangu hakutaka kuwaambia ndugu wala jamaa zake kuwa amefiwa na mtoto, hivyo tukamzika kinamna, na akawa kama kachanganyikiwa hivi, na akawa anasema “ kama watu wakijua nimefiwa na mtoto wataniita mgumba sitaki kuitwa mgumba mimi, hivyo akawa akiulizwa kuhusu kijana wake, akawa anasema kuwa yupo nje, na hapo mtoto alifariki akiwa na miaka nane tu, na miaka yote hio mpaka tunakutana na wewe, ni zaidi ya miaka kumi, mke wangu ana waaminisha watu kuwa mtoto wake yupo nje ya nchi anaishi na hakuna anaejua kama ana matatizo ya kiakili hivyo watu wakaamin…
Basi tukakuhudumia kwa muda flani na baada ya hapo, nikakupeleka kusoma na uzuri ulikuwa na akili sana, tukafoji vyeti vyako na ukaingia kusoma chuo cha biashara huko huko nje, na uliporudi mke wangu akawa anaamin kuwa umepoteza kumbukumbu hivyo alikuwa anataman sana kukuona haukumbuki ndugu, jamaa wala mtu yoyote yule ambae anakufahamu, hivyo akawa anaamin kuwa usipokumbuka utakuwa mtoto wake maisha yake yote, na ndio maana mali zake nyingi ameweka majina yako, akaendelea kusema Yule baba…
“ mimi najua muda mrefu sana kuwa umekumbuka kila kitu, ila nikawa naangalia sana tabia na mienendo yako, nikaja kugundua ni kijana mwenye upendo sana, na nikijana ambae unajituma sana, mke wangu alikuwa anajua kuwa ulikuwa muhuni, ila mimi nilikuwa najua unamsubiri mwanamke wako na haukuwah kuwa muhuni, ila nilichagua kukaa kimya ili nije kuona mwisho wa kila kitu ni nini…
“ na zinura, sio kwamba mke wangu anakuchukia sana, niamin mimi, hakuchukii hata kidogo ila anaogopa sana kuwa utampeleka nabil kwao, na yeye atakosa mtoto, na ameshaaminisha watu na jamii yake yote kuwa nabil ni mwanae , ndio maana unamuona kama anakuchukia kwa sababu anakuchukulia kama adui yake namba moja…
ITAENDELEA …..
Umesoma kwa utulivu · dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi my-true-love-story-sehemu-ya
