ALIMWOKOA SAMAKI MTU MJAMZITO KWENYE MTO BAADA YA SIKU 7, HIKI KILITOKEA... sehemu ya tatu
Amara alifumba macho kwa muda na kunong`ona moyoni mwake Mungu. Tafadhali tusaidie. Wasitupate hapa. Wawindaji walipokaribia kugeka nyuma ya mti wa mianzi, wawindaji mmoja ambaye alikuwa akitembe nyuma ya wengine, gafla alipiga kelele kwa nguvu, swala. Wawindaji wengine walisimama mara moja na wakageuka haraka. Iko wapi? Iko wapi? Walipiga kelele. Huko, pale, akikimbia kuelekea upande mwingine, muindaji alisema, akionyesha bunduki yake kwenye vichaka. Wawindaji walimsahau nguva huyo kwa muda, wakanza kukimbia kuelekea sehemu ambayo swala alisemekana kuwa. Huku wakinyanyua bunduki zao hewani tayari kupiga risasi. Viatu vyao vilitoa sauti kubwa kwenye majani makavu. Huku wakikimbia kuelekea upande wa swala, wakipiga kelele na kuitana.
Macho ya Amara ya limtoka kwa mshangao. Aliona hii kama nafasi yake peke. Alitoka haraka kutoka kwenye mificho yake na kurudi mbio kwa nguva. Tafadhali, tuende sasa kabla hawajarudi. Amara alimnong`oneza nguva. Mikono yake ikienda kwa kasi kuifungua ile kamba. Vidole vyake vilikuwa vikitetemeka huku akivuta fundo kali. Kamba ilikuwa ngumu na yenye nguvu na ili umiza vidole vyake lakini hakuacha. Nguva alikuwa akigugumia kwa maumivu lakini alimtazama Amara kwa matumaini macho ni pake.
Asante, asante. Nguva alinong`ona kwa unyonge. Amara hatimaya kafungua fundo wa mwisho na kamba ikaanguka chini. Mikono ya nguva ilianguka kando yake na akaegemea mti akiwa dhaifu sana asiweze kusimama vizuri. Amara alitazama huku na huku haraka. Bado aliweza kusikia sauti za wawindaji, lakini sasa walikuwa karibu na mto, wakipiga kelele na kuhitana huku wakimtafuta swala. Alijua lazima aondoke mara moja, au ange rudi na kumkuta nguva hayupo.
Meumeid alijaribu kusimama, lakini akaanguka nyuma, mkia wake wa feathers ukisuguwa kwenye majani makavu. Tafadhali, nisaidie. Alinong`onga. Amara akainama chini, akazungusha mikono yake kwenye kionjo cha nguva na kujaribu kumuinuwa. Nguva alikuwa mzito na Amara hakuwa na nguvu za kutosha, lakini alijaribu kadri awezaavyo. Aliweka mkono wa nguva juu ya bega lake na nguva akamuegemea sana Amara, uvimbe wa mtoto wake ukifanya iwe vigumu kwake kusogea kwa urahisi. Amara akapiga hatuwa mbele. Kisha nyingine, miguu yake ikitetemeka kwa uzito. Walitembea pole pole, hatuwa kwa hatuwa, wakijaribu kuepuka majani makavu ambayo yalifanya kelele chini ya miguu yao.
Nguva alikuwa akihema kwa maumivu, akipumua sana na kushika tumbo lake. Ah! Ah! Nguva aliugua kwa upole. Amara alimtazama kwa huruma. Hakujua wangechukua muda gani kufika kwenye kibanda chake, lakini hakuweza kumuacha nguva. Kila dakika tano, Amara alilazimika kusimama na kupumzika. Alikuwa akiinama chini, akimruhusu nguva kukaa chini kwa muda huku akijifuta jasho usoni mwake. Chungu chake chamaji cha udungo kilikuwa bado pale, lakini hakuweza kukibeba sasa. Aliacha nyuma, akilenga kumpeleka nguva salama.
Jua la asubuhi lilikuwa linaanza kuchomoza na ndege walikuwa wakiimba kwa sauti zaidi sasa. Kanga ya Amara ilikuwa imeloa jasho na mgongo wake ulikuwa unauma, lakini aliendelea kusonga mbele. Nguva alikuwa akilia kwa upole. Uso wake umepauka na mikono yake ikiwa imeshika tumbo lake kubwa. Tafadhali, usiniache. Sitaki kufa. Aliendelea kunong'ona. Sitakuacha. Amara alisema ingawaje mwili wake ulikuwa umechoka na miguu yake ilikuwa ikitetemeka.
Walipita kwenye vinjia vidogo vidogo vya vichakani wakikwepa sehemu ambazo watu wange waona. Amara aliogopa kwamba ikiwa wanakijiji wange muona nguva, wanaweza kuwaita wawindaji au kumletea shida. Walisimama kupumzika tena chini ya mwembe na Amara akamtazama nguva. Uko sawa? Aliuliza kwa upole. Baada ya muda, Amara kakusanya nguvu zake na kumuinuwa nguva tena. Waliendelea kusonga, kupumzika na kusonga hadi hatimae wakakifikia kibanda kidogo cha udongo cha Amara kilichokuwa pembezoni mwa kijiji.
Amara akasukuma mlango wake uangalifu na kuchungulia ndani. Watoto wake wawili walikuwa bado wamelala fofofo kwenye mkeka. Alikuwa na furaha kwamba bado walikuwa wamelala kwa hiyo hawata muona nguva bado. Amara akamsaidia nguva kuingia. Nguva aliuguwa kwa maumivu, mikono yake juu ya tumbo lake, mkia wake umelazwa kwa unyonge kwenye mkeka. Amara alimtazama kwa wasiwasi. Aliona mwili wa nguva umevimba sehemu na alama nyekundu pale kamba ilipo fungwa.
Nitapeleka maji ya moto. Amara alisema kwa upole. Haraka haraka alitoka nje, akachukua maji na kuayweka kwenye moto mdogo uliokuwa jikoni kwake. Maji alipopata joto, akayamimina kwenye bakuli ndogo na akayaingiza ndani. Akachovyesha kitambaki safi, akakikamuwa na kukiweka taratibu kwenye mikono na mabega ya nguva yaliovimba. Nguvu ali inama kwa maumivu, lakini baada ya muda akashusha pumzi laini. Amara akaendelea kusuguwa mwili wa nguvu akifuta jasho na kumkandamiza kwa nguvu nguva mgongoni kwake.
Asante. Asante. Nguvu aliendelea kunong'ona huku machozi ya kimlengalenga. Amara alihisi huruma moyoni mwake na pia alihisi hofu. Hakujua nini kingefuata na hakujua kwanini nguva alikuwa nchikavu, mjamzito na kukamatwa na wawindaji. Chumba kilikuwa kimya ispokuwa miungurumo midogo ya nguva. Amara alitazama tumbo kubwa la nguva na kujiuliza, kuna mtoto aina gani ndani yake? Atakuwa samaki au wanadamu? Hakujua lakini alijua kwamba hangeweza kumuacha nguva huyo. Nguva akafumbua macho yake kwa unyonge na kumtazama Amara. Naitwa nene, alisemakwa upole. Amara alishangaa. Nene? Hilo ni jina zuri. Jina langu ni Amara. Nene alitabasamu ka unyonge, lakini macho yake bado yalikuwa yamejaa machozi. Asante Amara, sita sahau hili, alinong`ona. Amara akatikisa kichwa kwa upole, akishikilia mkono wa nene kwa upole.
Mara wakasikia sauti za nyayo nje ya kibanda hiki, na macho ya Amara yalitoka kwa woga. Haraka akatazama mlango, kisha akamtazama nene. Nene alimtamama Amara kwa woga machoni pake, akishikilia tumbo kubwa huku wakijikunjusha mkia wake wa fedha juu yake. Ghafla mlango ulifunguliwa kwa sauti kubwa. Amara akakimbia haraka na kusukuma mlango mbele huku wakitumia mwili wake kumzuiya mtu aliye kuwa nje asione ndani ya kibanda hiki.
Kuna nani huko? Bwana unafungua mlango wangu hivyo? Amara aliuliza huku akihema sana jasho likimtoka usoni kwake. Aliyesimama mlangoni alikuwa mama njideka, mmbeya wakijiji. Kila mtu kijijini hapo alimjua kuwa ni mmbeya wakijiji. Anaependa kuingiza puwa yake kwenye biashara za watu wengine. Alikuwa ameshika kionochake kwa mkono mmoja na mkono wake mwingine ulikuwa juu ya mlango huku wakijaribu kusuka kwa upana zaidi na kunyosha shingo yake kutazama ndani ya kibanda cha Amara. Amara alizuiya mtazamo wake kama ukuta.
Ah! Ah! Amara, unatabia ya ajabu. Mama njideka alisema. Je, unaficha kitu? Au kuna mwana ume humo ndani? Macho ya Amara yalimtoka kwa mshituko. Mwana ume katika kibanda changu? Mama njideka, ni maongezi gani hayo ya asubuhi na mapema? Lakini mama njideka hakuwa tayari kuondoka. Akausogelea uso wake kwa ukaribu zaidi. Macho yake akiwa makali mithili ya mwewe akitafuta kifaranga.
Nimekuja kuazima chungu chako tu. Mama njideka alisema huku akikunja mikono kifuwani. Amara alishtuka. Ghafla akakumbuka chungu cha maji alikiacha porini alipokuwa akimuokoa nguva. Alijua hawezi kukichukua chungu kwa sababu wa windaji wanaweza kumtafuta mwenye nyumba na wakigundua kuwa yeye ndie alie mchukua nguva ingeleta shida kubwa. Amara alimeza mate kwa nguvu na kulazimisha tabasamu dogo.
Ah, mama njideka, nakitumia chungu sasa, siwezi kukitua tafadhali. Mama njideka akaziinua nyusizake juu na kuzomea. Wewe, kutumia chungu? Unatumia kwanini sasa? Unaficha kitu Amara? Nasikia harufu yake. Alisema akiinama kwa ukaribu, macho yake akiwa na mashaka. Moyo wa Amara ulikuwa ukidunda kwa hofu. Aliibuka na mlango kwa nguvu zaidi. Akaziba kila nafasi ambayo mama njideka angeweza kutumia kuona ndani.
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi