MY WANGU❤️ sehemu ya 66 na 67
Aseeee nilikuwa na maumivu kwa kila sehemu ya mwili wangu. Nilikuwa na maumivu makali mnoo. Asa mkono . Yani sikuwa sawa kabisa. Namsikia mlige akiwa ndani .anasema yani nikitoka njeee nakumalizia we mpumbavu nyanyuka usepe apo. Yani nikitoka nikakukuta faridah nakuua nakwambia. Mh kiukweli nilijikokota mnoo. Nilinyanyuka kwa kupepesuka. Nilitembea na ukuta .mpaka nikatoka njee ya geti. Njlivyotoka sasa kama bahati boda inapita . Mh nikaisimamisha kwanza .nikamwambia nipeleke nyantakara. Yule boda akaniuliza kwani unaumwa dada .nikasema.hapana. sikuwa sawa kabisa. Yule boda aliniangakia sana akanmbia panda. Yani kupanda boda tu ata siwez. Ikabidi anisaidie. Ila mh akaona sitafika.mana ata kujishikilia tu siwez. Ikanipeleka hospital apo runzewe . Inaitwa chares kurwa hospital. Ni ya private ila sio kubwa . Ni ya kawaoda tu . Basi akaniacha pale. Nilikuwa na hali mbaya mnoo. Ila tu nilipata akiri ya kumuomba simu yule boda na nikampigia simu mama. Nikamwmabia tu mama mi nipo hospital runzewe
Nyieeee sikuweza tena kuongea. Nikaona nguvu zinaisha. Nikawa sijajitambua tena. Nikalazwa pale. Kiukweli akiri ilikudi usiku saa 8 pembeni namuona mama yangu pale anafuta machozi. Akaningalia akanmbia unaendeleaje mwanangu. Nikasema naendelea sawa mama. Niko sawa kabisa. Mama akanambia ulienda kwa uyo mwana haramu kufanya nn. Eeeh umeenda kufanya nn. Anakupiga kama hivi ww ni mkewe . Au kisa kukulipia iyo ada yake. Uhai wako ni muhimu kuliko chochote . Nimeshaongea nae na nishamwambia kama ni shule nitakuludisha ile ile uliyofaulia na utasoma tu. Sitaki tena msaada wake. Kupiga gani uku eeeh . Ni kupiga gani uku. Sitaki nasema .apo mama alikuwa anaongea uku analia. Aseee na mlige alinipiga. Ahaaa hii siku alinipiga. Basi mama alikaaa pale mpaka asubhh. Ndo tukaruhusiwa. Nikaambiwa tu wala mkono sijavunjika ila umestuka tu. Basi gharama zote mama akalipia ndo tukalidi nyumbani.
Nyie nilijiuguza nyumbani kalibia week. Mlige hakunipigia wala hakuniulizia hali. Na mama alinambia marufuku kwenda kwake kujiombesha msamaha. Sasa nenda akakumalizie uo mkono. Basi mie niliona mh kwa kunipiga kule .ataniua kweli. Alafu anajua kaniumiza mpka mama kamsema . Lakini ata sms ya samahani yule bwana hakunitumia .nikajua aya bwana . Alompata sa hivi kamshikilia. Basi mie na mlige tukakaushiana hivyo. Na wala hakuja nyumbani kabisa. Wala hakumpigia tena simu mama. Na kuna jinsi mma alichukia sana ile mlige kunipiga. Ata kumuongelea akawa hamuongelei. Nazani si mnawaelewa wazazi. Hawezi kufurahi kupigiwa mwanae ata kama kakosea ndo ipo hivyo. Basi shoga yenu nilikaaa mno nyumbani . Mpaka wenzangu wa kuludi rikizo wakanikuta nyumbani nimejaa tele. Niliposikia yusta kaludi nilifurahi sana. Nilienda kwao kumuona kwa shangwe. Na alinifurahia sana. Basi akawa anazani na mm ndo nimeludi kumbe mie nyumbani nna mwez naaaaa.
Sikutaka kumficha shoga yangu. Nilimueleza yote .kuanzia upumbavu nilofanya shule . Kila kitu mpaka kupigwa na mlige nusu aniue. Na mpaka mama kugombana na mlige yote nilimueleza .mh yusta alinionea huruma sana . Akanmbia pole sana. Nikasema nishapoa. Ata shule mama kanmbia zinavyofunguliwa . Ananiludsha shule ile ile niliyopangiwa mwanzo. Mh yusta kanambia na mlige akikasilika anabadilika anakuwa chui kabisa. Nikasema ndo hivyo. Na ana madame ana tembea nae . Anaitwa madame milia nasikia ndo mwanamke wake. Hawezi kunikumbuka mie . Mtoto mdogo. Yusta akanmbia basi kuwa na amani na maisha yaende. Kila kitu kitakaa sawa. Nikasema powa
Apo kidogo nikwa na rahaa .na vile yusta karudi .rafiki yangu nimemzoea sana. Mala tukazulule uku. Mala kesho kule. Yani nilichangamka sana. Kuna siku tunapita mpaka kwenye iyo nyumba mpya ya mlige. Nyieee uko nyamsebehi aliachia nyumba. Yani mpaka roho inauma ..na wivu unakuja. Kuwa apa atakuwa anakuja na mwanamke wake mwengine .wakati ningekua naletwa mimi. Ila ndo hivyo . Rohoo inauma sana ila haina jinsi. Yusta akawa ananitia ngivu sana. Kuna mda nilikuwa namuona sana center pale dukani kwake kwa jamila. Ila sikuwa nataka kuwa karibu nae tena..yani nakata zangu kona kabisa.
Ikawa hivyo. Na yeye wala hakuwa ananitafuta ata pesa hakuna. Yani nilikiwa natumia viakiba vyangu tu. Sikuwa na pesa kama mwanzo mpaka.rikizo ikakata. Wenzangu wakaanza kufanya mchakato wa kuludi shule mie nikamuuliza mama akanambia ningoje . Mwanza mpaka tuvune kwa sasa yeye hana pesa. Rohoo inauma unazani nafanyeje. Basi wenzangu wakaondoka mie wakaniacha.nikajuta ata kwenda kusoma shule ya private.bola ningeenda zangu ya serikali tu. Basi ikavuka week mie nipo nyumbani. Apo baba bado hajaludi. Na mama hakumueleza shida zangu. Alinionea aibu na aliona kama atanidhalilisha tu kwa baba. So hakumuambia kabisa. Basi siku uyo. Mie nimetoka zangu kijiji cha pili mama alinituma nipeleke mchele kwa shoga yake uko. Nimeludi nafika pale .namkuta mama anambia mlige kaja apa. Mh moyo ukafanya paaah
Mama akanmbia amesema ujiandae kesho unaludi shule. Mh nikasema mama we umekubali tena. Si ningojee tu unipeleke kule kwa mwanzo mama . Mama akanmbia nenda ukasome mwanangu. Usingoje ambayo ata hatuyajuhi yatakuaje. Naona kasafisha moyo wake. Na kajiludisha nyuma na kaomba msamaha apa. Kuwa zilikuwa hasira. Ila nenda tu ukasome. Nikasema sawa mama . Basi nikaingia ndani nikaanza kujiandaa. Mama akanmbia kasema usibebe hivi vya zamani. Kama fomu mana anakuhamisha shule..mh nikasema ananihamisha. Mama kasema ndio. Anakupeleka shule nyengine ipo kahama apo . Nikasema sawa mama. Basi mie nikaingia ndani kwangu. Ndo nakuta hii siku ndo kanitumia sms
Kanmbia tu vitu ambavyo natakiwa kubeba na vpi niache. Haina ata mambo .sms ni kavu. Mie nikamjibu sawa. Hakunijibu tena.nikapanga tu vitu vyangu. Mama akaja chumbani akaongea sana na mm. Alinambia uyu mwanaume msome. Ni mtu amabea ana hasira sana .ila anakupenda so kuwa nae makini sana. Alafu ela inauma mwanangu .si unaona anakuhamisha shule so kule katupa milion 7 . Anakuhamisha anakupeleka kwengine. Akikukuta na kosa lazima atake kukua. Kuwa makini sana mwanangu shuleni . Naomba ukasome.mie nikasema sawa ntasoma mama. Hakuna shida. Yani hatukalala mama anaongea na mie mpka asubuh kunakucha. Basi mlige aknitumia sms. Nakufata saa 4 asubuh. Mie nikasema sawa. Nikajiandaa tu vizuri. Na saa 4 asubuh mlige akaingia na gari yake
🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi