MY WANGU❤️ sehemu ya 63
Basi bwna tumefika nyumbani . Mama akaja akasema eeh baba jamani pole kwa usumbufu wote. Mlige akasema usijali mma kuwa na amani kabisa mma akauliza shida nn wamesema.. mlige akasema mama atakusimulia tu mwenyewe. Mi naomba niwaache niwahi kazini. Majukumu yananihitaji. Mh yani usiku mzima kadrive na anahitajika kazini hii asubuh nilimuonea huruma sana mlige wangu. Basi akashuka akaja akanishushia vitu vyangu vyote.kisha akaingia kwenye gari yake akaondoka.mama aliningalia sana. Akanmbia ingiza vitu vyako ndani. Basi kweli mie nikingiza vitu ndani . Nikajitupa kitandani. Nilikuwa na stress sana mtoto mdogo kama mie. Na nilikuwa nimechoka sana . Nilijikuta usingizi unanipitia kabisa.nikaja kustuka saa 7. Nikaenda kuoga. Nilipotoka sasa .nikamkuta mama chumbani kwangu ananisubur kwa hamu . Akanmbia vaa uje apa kitandani. Nikasema sawa mama.
Basi nikavaa kisha nikasogea alipo mama. Mama akaniuliza umefanya nn shule mpka umesimamishwa kwa mwez mzima.nikasema mama samahani kuna mkaka anaitwa zayd alinikiss kwa ngivu ndo mwalimu akatukuta. Ase mama aliniinukia na mkonde wa mgongo. Akanmbia ulilazimishwa ww. Ulilazimwashwa nn . Hivi faridah una akiri ww. Unachanganikiwa na aya matako eeh. Nakuuliza wwm farida akiri zako zina nn. Una nn wewe mtoto. Shule umefata mapenzi au kusoma..eeeeh unamfikilia mlige ww. Bba wa watu kakulipia ada milion 7. Baba ako anayo hiyo pesa?. Leo unafanya upumbavu we mtoto una akiri ww. Mie nikaanza kulia nikasema samahani mama nimekosea nisamehe. Mama akanmbia ngoja nikuoneshe. Akachukua kuni. Ndo alinitandika nayo. Alinipiga kisawa saw. Yani nililia mnooo. Mama alinibana kwa nguvu alinitandika na ile kuni sitaki kuwaambia. Akanmbia utajutia sana katika maisha yako siku ukimpoteza yule mlige. Nakwambia ukweli we mpumbavu. Nyie nilibaki nalia tu.. yani sanaa.
Mchana wala.sikula na jana yake sijuwa nimekukal . Na usiku mama akanmbia sikupi chakura. Alafu baba alikuwa hayupo. Sikuwa nimeelwa kaenda wapi kwa uo mdaa. Basi shoga yenu nikalala na njaaa. Na kesho yake ndo mama akanipa chakura si unajua wazazi hasira zao huwa zinaisha kuna mda.asa kwa sie watoto zao. Basi iyo asubuh ndo nilikunywa chai ila mama kaninunia kabisaa. Nyie si nna kisimu changu kile kidogo.nilimtumia sms nyingi mlige kumuomba msamahe na kumuelezea ile kujitetea ila wapi hakunijibu na nikampigia hakupokea. Alinikaushia mpaka ikakata week 1 nipo tu nyumbani ata kutembea siendi mana wenzangu wote wapo shule likizo bado ata yusta alikuwa shule .mie kwenda miez 4 tu nishaalibu daah. Apo mda wote huo mzee alikuwa hayipo. Ila nilijua kaenda kwa babu geita. Nilikuwa nasikia anaongea na mama na babu anaumwa ndo kaenda kumsikilizia.
Basi shoga yenu nilikaa nyumbani tu. Uku mwanaume kaninunia mnoo. Mama akawa ananmboa aya nipeleke shamba si hutaki kusoma .na ngoja agahiri kukusomesha kwa usenge wako. Yani unapatikna na kesi ya kukiss na mwanaume yani unamsaliti mana yake yani we mtoto hamnazo kabisa .nilikuwa nasemwa mno .mama akingia akitoka ana mimi tu. Tena nikiwa karibu yake na mgumi ananisindikiza nao. Ayo ndo yakawa maisha yangu shoga yenu. Kiukweli nilikuwa natamani sana kwenda kumuomba msamaha mlige ila naogopa naogopa mno. Nahisi ata atanipiga yani. Ila siku iyo nilijikaza mnoo . Nikaenda kwake runzewe ililikuwa j pili nikajua lazima namkuta. Basi nilipofika.nikagonga mlango .mlige akaja kufungua aliponiona. Akaniuliza umefata nn nyumbani kwangu. Mh yani kanikazia sula yuko serious.nikasema mlige plss nisikilize nikapiga na magoti apo apo kibarazani. Mlige akasema.ntakuja kukupiga mpkaa nikuue alafu nifungwe naomba unyayuke mwenyewe na uludi kwenu .mimi na wewe basi. We si unataka wasenge wenzio. Mie si unanaichukulia powa. Sasa fresh kacheweze na wasemge wenzio. Mi nilisema plsss baba usiseme hivyo. Mlige akanmbia ntakupiga ntakupiga nikuue faridah ondoka .mh nikanyanyuka nikaaanza kuondoka.uku nageuka nikihisi nitaitwa aah wapi.ndo kabamiza mlango wake kwa nguvu. Nikajua basi nishaachwa na sitakiwi mimi. Niliumia jamani. Moyo unauma kweli kweli.yani nimeludo nyumbani sula imevimba kwa kulia. Hii siku ata mama hakunipiga wala.kunisema tena akiniangalia kwa huruma tu.
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi