*NIKUMBATIE NIPONE PLZ* *1 ---------- 5* *SEHEMU YA KWANZA* Ukipata nafasi ya kupendana na mtu mpende kwa moyo wako wote
*********
Gari ya la wagonjwa lilifika kwa kasi ndani ya hospitali ya taifa, kitanda cha wagonjwa kililetwa, mama aliwekwa juu ya kitanda hiko na kuanza kukimbizwa kupelekwa kwenye chumba maalumu cha matibabu, wakati wote uso wangu haukutamanika kwa machozi kwani nilikua nalia sana, nilipoona ameingizwa ndani.
Nilisogea karibu na ukuta mmoja na kupiga magoti hapo, nilianza kulia huku nikimwomba Mungu amponye mama angu, mama pekee ndie mzazi niliekua nae kwenye maisha yangu, sikutaka ampore mama angu.
"Mungu najua unanisikia niwewe ndie uliemuumba mama angu najua una uwezo wa kuuchukua uhai wake wakati wowote utakao ila umesema tuombe lolote utatupatia namimi kwa jina lako nakuomba Mungu usimchukue mama angu mapema, sitoyaweza maisha bila mama mimi aaaaah aaaaah" niliomba huku nikilia sana, maombi yangu yalikua marefu hapo ndipo niliamini kwenye msemo kwamba kuta za hospitalini zimebeba maombi mengi na yenye uzito huenda kuliko yale ya nyumba za ibada.
Nilitulia na kungojea majibu kutoka chumba cha matibabu.
"Hali ya mgonjwa bado haijatengamaa bado anahitaji kufanyiwa upasuaji kuziba matundu kwenye moyo wake, gharama ni kubwa sana ni millioni ishirini bila hizo gharama utatusamehe hatuna namna nyingine ya kufanya"
"Dokta dokta naomba mtibie mama angu mimi nitaleta hizo fedha"
"Utaratibu wa hospitali yetu unalipa nusu ya gharama kwanza kabla ya upasuaji na nyingine utalipa baada ya kukamilisha zoezi la upasuaji" Dokta aliniambia kwamba inahitajika millioni kumi za mwanzo ni pesa nyingi sana.
Kibaya zaidi pesa hizo sijawahi zishika katika maisha yangu yote zikiwa katika umiliki wangu. Hivyo nilihisi kuishiwa nguvu.
"Fanya hizo pesa zipatikane leo na leo hii hii tuanze matibabu ili tuweze kumuokoa mama" Dokta alishindilia msumari wa moto.
"Woiiiiiii" nilijikuta napiga ukelele, nilihisi masikio yangu hayajasikia vizuri.
"Mwende mkanze hayo matibabu mimi nalipia hizo gharama zote" sauti ya kiume ilisikika nyuma yetu ikiingilia mada ya kile tulichokua tukikiongea, niligeuka na kumtazama alikua mwanaume mmoja mrefu, uso maji ya kunde alivalia koti la suti kwa nje ndani tisheti, chini suruali ya jinsi na raba mtindo huu hujulikana kama casual yaani ile simple lakini umependeza.
"Oooh sawa tuongozane bhasi kwa mhasibu ili ulipie hizo gharama" daktari aliongea na kijana alitii kufanya hivyo nilimwona ni malaika alietumwa na Mungu kuja kuniokoa.
"Ahsante kaka angu kwa wema wako Mungu akubariki sana" niliongea maneno mengi ya shukrani.
"Kawaida potezea" Mwanaume huyo alinijibu kwa kifupi yaani kama jambo alilolitenda kwangu ni dogo sana au jepesi.
Tulienda mpaka ofisini kwa mhasibu wa hospitalini. Mwanaume alilipa millioni ishirini kwa kutumia kadi yake ya benki, mimi nilisaini pia kwenye mkataba wa kuanza matibabu kwa mama angu nilikua mwenye kufurahi lakini pia moyo wa shukrani haukua mbali nami.
Tulitoka nje bado niliendelea kumshukuru huyo mtu.
"Kaka angu yaani wewe Mungu akufungulie mbingu uende moja kwa moja, ahsante kwa kila kitu Mungu akuzidishie ila naomba siku nikipata hii pesa niweze kukurudishia pesa yako ili utumie kwenye mambo mengine"
"Usiwaze potezea haina haja naomba nioneshe wodi za wanawake ni wapi"
"Naomba nikusindikize tu hapo"
"Sawa" tulitembea kwa ukimya mkubwa hakua ananiongelesha kabisa kweli alionesha kuwa mtu serious sana nami sikutaka kumsumbua nilipofika hapo nilimwonesha.
"Ahsante" alishukuru na kuanza kuondoka.
"Samahani kaka naweza nikapata namba yako kama hutojali" hakunijibu bali alinipa kikadi cha namba na kuondoka zake alikua kauzu kweli kweli.
Kuipata tu hiyo namba mimi nilishukuru sana maana hakuonesha kuwa mchangamfu, nilisoma kikadi kiliandikwa
Jonathan Senkure nilijua hilo ndo jina la huyo mwanaume alienisaidia.
Nilirudi nilipokua mwanzo jopo la madaktari waliingia kwenye chumba chs upasuaji na kufanya matibabu stahiki kwaajili ya mama angu nikiwa nje bado niliendelea kumwomba Mungu afanye jambo la kumsaidia mama, baada ya masaa nane, madaktari walitoka na kunipa taarifa kwamba upasuaji umekamilika vyema hivyo nitulie nikiwa na imani kwamba mama angu atapona.
Siku hiyo nililala hospitalini japo sikuruhusiwa kwenda kumwona mama ila nilihitaji kupumzika hapo hapo.
Majira ya saa sita usiku niliamua kutembea tembea kunyoosha miguu nilimwona yule mwanaume alienisaidia matibabu ya mama angu yaani Jonathan alikua mahali kasimama anavuta sigara taratibu, ilikua mita kadhaa kutokea hospitalini ilibidi nimfuate alipokua kasimama. Aliponiona alipiga hatua kuondoka zake. Nikamwita aligeuka na kunitazama kwa macho yenye maswali mengi, nilijikaza kisha nikaongea.
Itaendelea......
*SEHEMU YA PILI*
"Mbona unanikwepa na nimekuja kuzungumza na wewe angalau nivushe vushe muda kidogo"
"Huwa unavuta sigara?" Aliniuliza swali ambalo lilinishangaza kidogo.
"Hapana sivuti kwanini umeuliza"
"Mimi navuta ndio maana nimeamua kusogea pembeni ili moshi usikuumize"
Sasa nilimuelewa vyema.
"Boss gari lipo tayari tunaweza kuondoka sasa" kijana aliefika alimwambia Jonathan nae aliitikia kwa kichwa.
"Hapa sio salama ungerudi hospitalini, usiku mwema" Jonathan aliongea na kuondoka akiwa na kijana wake wa kazi. Kuna namna nilimwona ni mtu wa kujisikia.
"Ila angekua wa aina hiyo asingenisaidia au angetaka kupata chochote kutoka kwangu, dunia imeharibika hii jamani wenye moyo wa kusaidia bila kuhitaji shukrani ni wachache sana, nimwelewe ndo alivyo hataki mazoea zoea" nilimwelewa namna alivyo.
Nilirudi hospitalini nilikaa hapo mpaka palipopambazuka nilimwomba daktari nafasi ya kwenda kumwona mama angu, daktari aliniruhusu ila alinitahadharisha kwamba bado hajazinduka hivyo nikienda nisifanye jambo lolote nimtazame tu nsmi nilikubali nilivaa mavazi maalumu nikaenda mahali alipokua amelala mama angu.
Machozi yalinitiririka mashavuni kila nikikumbuka namna mama angu alivyonilea kwa shida na tabu nyingi kwani baba alipofariki jukumu la kunilea mimi lilibaki juu yake alipigwa na jua akitembeza mboga mboga ili mimi nipate kula na kupata mahitaji muhimu ya shuleni.
Nilimwomba Mungu mama angu aweze kupona ili angalau ayapate matunda ya kile ambacho alikipambania kwangu kwa miaka mingi sana. Kwa neema ya Mungu mama alipona kabisa ndani ya week mbili alikua katika utimamu wa mwili wake na madaktari walimruhusu ili tuweze kurejea nyumbani tulipofika nyumbani kwanza nilimpikia chakula chake cha asili akipendacho eti alimiss sana kula mrenda hivyo nilimpikia huo kwakua mrenda hauna virutubisho mwilini ikabidi nikaange na nyama, matunda pamoja na mboga nyingine za majani nyingine ili mama angu aweze kujenga shavu kidogo.
Mama alikula kwa furaha sana kwa namna alivyokua anafuraha nilizidi kumfurahia mama angu tabasamu lake kwangu ndio ilikua kila kitu.
"Ahsante binti yangu kwa kunijali sana Mungu kanipa uzima kwa mara ya pili ili niweze kushuhudia upendo wako wa dhati kwangu nakubariki mwanangu kila utakachogusa katika maisha yako kikawe chenye baraka, ufanikiwe utokapo na uingiapo atakaetaka kuyagusa maisha yako hata kidogo akakutane na kibano kikali kutoka kwa Mungu wangu wa mbinguni" mama aliongea maneno mengi ya kunibaraki, kama umewahi barikiwa na mzazi au mlezi wako unaweza kuelewa namna nilivyokua najisikia mpaka machozi mepesi yalikua yananitoka, nilimkumbatia mama angu kwani sikuona kama kuna neno lingine ambalo litatoshea kwake zaidi ya kumshukuru kwa kumbatio.
"Natamani nimbariki na kumshukuru huyo kijana ambae amenilipia pesa ya matibabu" mama aliniambia nsmi nikachukua simu kumpigia Jonathan, namba yake iliita kwa muda mrefu pasipo kupokelewa.
"Sawa nitaongea nae wakati mwingine ila nna ombi lingine binti angu"
"Niambie mama nakusikiliza, lisiwe ombi bali ufanye kuniambia tu"
"Nataka nirudi kijijini kule nilipozaliwa unajua ni miaka mingi sijaenda kule kama ningefariki katika huu ugonjwa bhasi ningekufa pasipo hata kuyatazama makaburi ya wazazi wangu katika kipindi chote hiko nataka nikakae kwa mdogo angu kule kijijini hata mwaka mmoja huko mbeleni nitarudi tena"
"Mama jamani maisha ya kijijini utayaweza kweli pia kwa hali yako natamani nikuuguze mwenyewe"
"Oooh binti yangu mimi nilizaliwa kule siwezi kushindwa kuishi mahali nilipokua nimezaliwa hivyo nitakaa vizuri tu pia mdogo angu hawezi shindwa kunielea tumebaki wawili tu hivyo hawezi kunitupa nataka nikupe nafasi uyatafute maisha yako kwa nguvu zote huko mbeleni ukifanikiwa zaidi bhasi nitarejea" mama aliendelea kushikiria msimamo wake mpaka nikakubali nilimwomba akae siku mbili ndipo aondoke nae alikubali.
Siku ya safari nilimsindikiza mpaka stendi asubuhi na mapema nilipotoka huko nikaunganisha moja kwa moja kazini, nilikua nafanya kazi kwenye kampuni moja inayojihusisha na utoaji wa huduma ya kutibu saikolojia za watu, watu wanaopitia changamoto mbalimbali hasa msongo wa mawazo tulikua tunakutana nao na kuwaweka sawa ili waendelee na maisha yao kama kawaida.
Nilipofika secretary alinipa ujumbe wangu.
"Doreen boss alikuulizia sana kama umemaliza likizo yako hivyo ni kheri uende ukamwone" Nilipitiliza moja kwa moja ofisini kwa mkurugenzi wa kampuni yetu.
"Ooh Dee huyo pole na kuuguliwa na mama vipi anaendeleaje?"
"Anaendelea vizuri kabisa namshukuru Mungu kwa hilo vipi shughuli za ofisini hapa"
"Zinaenda vizuri ila zitaenda safi zaidi kwakua umerejea kuna kazi nono imekuja ofisini kwetu na hakuna mtu mwingine ambae anaweza kuifanya zaidi yako wewe, kuna tajiri amelipia millioni thelathini kwaajili ya kutibu saikolojia ya kijana wake ambae ametoka vitani mwaka jana lakini mpaka leo hii bado saikolojia yake haijatulia kabisa, wataalamu wa jeshi wameshindwa kumrejesha kwenye hali yake ya kawaida mpaka wamempa likizo isiyokua na kikomo ndipo familia imeingilia kati katika kupambana na hali ya kijana wao.
Ukiweza kukamilisha hii kazi kwanza utaitangaza kampuni yetu maana yule tajiri ni mtu mkubwa sana nchini hivyo kupitia yeye tutapata madili mengi pili kati ya millioni thelathini atakazozilipa millioni ishirini utazichukua wewe hizi ziko nje ya mshahara wako ila utachukua pale utakapo mtibu kijana, je uko tayari?" Boss aliuliza majibu badala ya swali kwani nilikua tayari kwa kazi hiyo kabla hata hajasema mimi na pesa ni dam dam.
"Ila kazi yenyewe ina utaratibu wa tofauti kidogo katika kuifanya unapaswa kufungua moyo ili kuifanya vizuri" Boss aliongea na kunywa maji kidogo, nilikua tayari kusikia huo utaratibu wa kazi ya mamilioni.
*NIKUMBATIE NIPONE PLEASE*
*3-10*
*________________________________________*
*SEHEMU YA TATU*
"Itabidi umfanyie hiyo huduma nyumbani kwake kwa maana kituo chako cha kazi kitakua nyumbani kwake, utafanya kazi huko mpaka apone kabisa hakikisha ni kazi tu, ishi kwenye misingi ya kazi kwa wakati wote"
"Ni sawa boss hakuna shida niko tayari kwaajili ya kazi"
"Poa bhasi twende nikupeleke huko alipo ili uanze kazi yako leo leo nilitoka na boss mpaka kwenye gari hapo wafanyakazi wengine wananiangalia tu katika nyuso zenye maswali mengi hawakujua tunakwenda wapi na boss, nilijua tu hasira zao zinazidi kupanda mioyoni mwao maana sio kwa namna walivyokua wananionea wivu mara nyingi kwa kuona boss ananipendelea mimi zaidi, mambo kama hayo. makazini yapo sana nafikiria unayaelewa vyema mpendwa msomaji.
Kabla gari haijaondoka eneo la ofisini ziliingia gari aina ya V8 tatu, zote nyeusi ni mpyaa, boss alifungua mlango na kutoka nje alitembea mpaka kwenye hizo gari.
Baada ya dakika tano za kuongea na mtu aliekua ndani ya gari kwani yeye hakushuka chini, boss alinirudia na kunambia niende nikaongee na huyo mzee ambae ndie baba wa kijana. Nilipofika nilisalimia kwa heshima zote.
"Kama umeaminiwa na hii kampuni bhasi na mimi nakuamini binti angu nenda kaifanye kazi yako kwa usahihi ukifanikiwa kunsaidia kijana angu bhasi nitakupa zawadi nyingine ambayo naamini utaipenda sana, kwasasa siwezi kwambia ni zawadi gani ila jiandae kwa mambo mazuri kama kutakua na shida yoyote usisite kunieleza, sawa binti angu" mzee huyo mwenye mwonekano wa fedha alikazia umuhimu wa kazi hiyo niliona fahari sikujua kazi itakua na ugumu kiasi gani ila niliamini nitaiweza tu.
Gari hizo tatu zilipoondoka nasi tuliondoka kwa gari la boss mpaka nyumbani kwa huyo kijana kwakua boss alipewa location na mzee hivyo haikua na tatizo lolote lile kufika mahali hapo.
Tulifunguliwa geti na mlinzi akatupeleka mpaka sebleni, jumba lilikua na uzuri wa aina yake, nililitazama vizuri kwa dakika kadhaa sikuamini kama jumba hilo lipo bongo maana lilikua na vitu vya nakshi nakshi ya dhahabu, ukimya ulitawala ndani ya nyumba hiyo.
"Boss yupo ndani ngoja nikawaitie ila kabla ya kuwaitia mngetumia kinywaji gani?"
"Haina haja kwa sasa tunaomba tuitie boss wako tupate mazungumzo nae hilo ndo muhimu boss wangu aliongea kisha mlinzi alienda mpaka alipokua huyo boss.
"Kasema msubiri kidogo anakuja mlinzi alitoka nje na kutuacha hapo tulikaa masaa mawili pasipo kijana kutokea mpaka boss wangu uvumilivu ulimshinda alimwita mlinzi aende akamwite tena boss wake, alienda huko chumbani na awamu hii walitoka wameongozana kwa pamoja.
Macho yangu yalipotua kwa huyo kijana ambae nilitakiwa kumfanyia huduma ya saikolojia sura yake haikua ngeni sana kwangu kwani ndio yule Jonathan alienisaidia kule hospitalini kulipia matibabu ya mama angu, nilijisikia vizuri sana kumwona ila nilijisikia vibaya kwaajili yake kwamba ana tatizo la saikolojia, sikutaka kuleta kujuana nilijituliza tu kwenye kochi.
"Uhali gani kijana, naitwa Mr Singano ni mkurugenzi wa kampuni ya tiba ya saikolojia nimeongozana na mtaalamu na mbobezi wa mambo ya saikolojia anaitwa Doreen, tulipewa ujumbe na mzee wako kutokana na changamoto unayo pitia hivyo pole sana na huyu mtaalamu atakusaidia kurudi katika hali yako ya kawaida boss alidadavua kila kitu wakati huo Jonathan ndo kwanza alikua anavuta sigara yake taratibu.
"Mzee miyeyusho sina hiyo shida mnaweza kwenda"
"Aah kijana nakuelewa katika hali uliyopo huyu binti atakusaidia sana" "Weeee nendeni nikifumba macho na kufumbua nisiwaone hapa" Jonathan aliwaka kweli kweli.
Boss alinipa ishara kwamba tuondoke ila mimi nilimkatalia kwamba nabaki hapo hapo, boss akaamua kuondoka zake ila akinitumia meseji kwamba niwe makini na huyo mtu. Jonathan alipofumbua macho yake na kuniona bado nipo hapo hapo kwanza alitabasamu kwa sekunde kisha alirudisha sura yake yenye hasira nyingi sana.
Itaendelea.
Chapter 4
Alinipiga hilo jicho moja kali sana bila kusema
neno alinyanyuka na kwenda mpaka chumba kilichopo upande wa kushoto. Mimi niliendelea kutulia hapo nikiwaza namna ya kupambana na huo msalaba, nikaanza kusikia kushindo cha kitu kupigwa. Nikasogea mpaka mlangoni mwa hiko chumba nilisikia kishindo zaidi huku Jonathan. alipiga makelele ya moja kwa moja. Kupitia upenyo mdogo wa mlangoni nilimwona Jonathan anapiga ngumi nyingi sana kwenye punching bag.
Niligundua chumba hiko kilikua gym ya kufanyia mazoezi, alikua anaipiga bag hiyo kwa nguvu sana kama anampiga mtu alitumia mbinu hiyo kupunguza hasira alizokua nazo, nikajua kabisa hizo hasira zilikua juu yangu nikafungua mlango na kuingia huko huko ndani.
Kuniona aliachana na kupiga bag akaanza kupiga ukuta kwa hasira sana. "Bhasi bhas Jona unajiumiza, wewe ni mtu mzuri
hupaswi kujitesa namna hii nilipambana kumtuliza.
"Aaaaah aaaaaaaah aaaaaaaaah Jona aliendelea kupiga ukuta, aliishiwa nguvu na kuanguka chini.
"Mamaa weeee" nilikimbia kuchukua khanga kwenye pochi yangu nikaanza kumpepea kwa nguvu hapo, pepeaa weeh lakini jamaa bado haamki tu, nikachukua maji kumwagia bado jamaa alibaki vile vile nikaamua kufanya zoezi la mwisho kabisa, nilipiga magoti na kumsogezea mdomo wangu karibu na wake ili nimpe pumzi, nilifanya hivyo huku nikijitahidi.
Nilishangaa nimebanwa mdomo haikua pumzi tena nilinyonywa mdomo kwa busu la kikubwa nilipotaka kujitoa akanikumbatia kwa nguvu zaidi katika namna ambayo siwezi kuchomoka ikabidi nikubali tu kudendeka nae kwa dakika mbili ndipo aliniachia.
"Ahsante sana nilihisi maumivu ya kichwal angalau umenisaidia yametulia kidogo" Jonathan aliniambia kisha kuniachia
Alisimama kwa kuegesha mikono yake ukutani, alitembea lakini alionesha kutokua na nguvu kabisa ikabidi nimuwahi na kumwekea mkono mmoja begani mwangu..
"Unaelekea wapi chumbani au sebleni?" "Chumbani" Jonathan alijibu kwa kifupi nilimsindikiza mpaka huko chumbani kwake. Chumba kilikua hovyo hovyo tofauti na mpangilio wa kule tulipotoka.
Nilimweka kitandani taratibu bado alionesha kuwa na maumivu ya kichwa maana alikua anafumba fumba macho yake. "Vipi nikupeleke hospitali na hiyo hali?"
"Hapana kuna dawa zangu pale mezani naziomba hizo
Nilisogea mezani na kuchukua dawa, nilimwekea vidonge viwili mkononi na kopo la maji alimeza na kushushia na maji akajilaza kitandani na kujikumbata kama kifaranga.
Muda huo ikabidi nimsaidie kumwekea chumba chake vizuri, nilipangilia kila kitu kwa matazamio yangu niliona kimekaa kwa usahihi. Nilipomtazama Jonathan alikua amesweat sana Ikabidi niongeze speed ya feni kisha nikatoka nje kabisa mpaka alipo mlinzi.
"Ni chakula gani boss wako huwa anapenda kula mara kwa mara"
"Mmh huyo kwenye kula ni changamoto yake kubwa vitu huwa vinaharibika kwenye friji mimi navichukua naenda navyo nyumbani kwangu ila kula yake yeye haieleweki kabisa, mara nyingi anakunywa kahawa au kula atoke aende sehemu na huko sijui huwa anakula nini
"Duuu kwahiyo kwenye friji huenda hakuna vitu?" "Hapana vitu vipo sababu kila baada ya wiki mbili huwa naweka vitu vipya na kutoa vile vya zamani hayo ni maagizo ya wazazi wake" "Ahsante nimejua cha kufanya" nilimshukuru mlinzi na kurejea ndani, nilitazama kwenye friji nilikuta nyama, viungo, mboga za majani, matunda, kila kitu muhimu kilikuwepo.
"Nikachukua nyama nikaitengeneza vizuri na kuibandika jikoni" nilichagua kuichemsha hiyo,
nikachanganya na viazi nilitengeneza kasupu flani hivi ambapo hata mimi nilivyoonja nilikubali kweli nimepika kitu. Niliweka kwenye bakuli nikabeba mpaka chumbani kwa Jonathan nilimkuta ameshaamka. "Nimekutengenezea kitu hapa kidogo unaweza
kunywa ili upate nguvu" niliweka kwenye kimbao flani kisha nilimsogezea kitandani ili anywe lakini aliendelea kuangalia tu bila kusema neno.
"Unajisikiaje Jonah ungekunywa hiyo supu
kidogo"
"Sina nguvu naomba nilishe"
"Mmmmh mgonjwa kwa kudeka niliongea kimoyo moyo ila ikabidi nisogee kwa kukaa pembeni yake, nilichukua bakuri nikapooza kijiko na kuanza kumlisha taratibu.
Alikunywa mpaka bakuri yote ikaisha, nilifanya hivyo kwaajili ya kutengeneza ukaribu nae, niliamini kwamba ili nimsaidie ni muhimu kwanza kuwa nae karibu, aniamini na anichukulie mimi sio mtu wa kumsaidia pekee bali mimi ni rafiki ake.
"Nikupikie chakula gani mchana?" Nilimuuliza. "Chochote"
"Mmh sema unataka kula nini?"
"Chochote nitakula, nichagulie wewe" namna
alivyokua anajibu ilinifurahisha kidogo nikaenda huko jikoni, nikawaza waza pale nikaona nipike kaugali na maini rosti, nilipika na mboga za majani hapo, nikamfata chumbani nilimwomba atoke nje ili tuweze kula mezani, alikubali.
Tukakaa mezani na kuanza kula taratibu hapo alikula kidogo na kusema ameshiba nilimbembeleza kidogo ili ale ila alisisitiza kwamba ameshiba hata kula hiyo tu kwangu ilikua mafanikio makubwa sana.
Jioni ilipofika nilimuaga kwamba naondoka.. "Samahani unaweza kubaki na mimi?" Jonah aliniuliza huku akinitazama kwa macho ya kunishawishi kwamba nibaki.
Itaendelea.........
Chapter 5
'Wewe ni jukumu langu kwasasa nitarejea tena kesho, kuna mazingira sijayaacha vizuri huko nyumbani hivyo naomba niende tu boss wangu" nilimwomba Jonah nae alitikisa kichwa kukubali japo macho na mwili wake mzima vilionesha hali ya kuupokea upweke ambao nilimwacha nao.
Nikaondoka baada ya kumuaga mlinzi nae, nilipofika nyumbani jambo la kwanza ni kumpigia boss wangu simu ili kumpa ripoti. "Enhee kumeendaje huko, maana jamaa aliwaka kama simba"
"Nimeenda nae sambamba tu zile hasira zilipoa nikampikia pia alinipa nafasi ya kupiga nae stori kawaida
"Kazi utaiweza kwa unavyoona au ni ngumu turudishe pesa za watu"
Haina haja ya kurudisha pesa boss, kazi
nitaiweza tu kwa uwezo wa Mungu" "Sawa nakuombea pia nikutakie kila la kheri kwenye jambo lako hilo tuliagana na boss wangu kwakua nilishiba chakula nilichokula mchana kwa Jonah hivyo nilinumua matunda tu wakati nakula ndipo nikakumbuka kumbe sikua nimempikia chakula cha usiku Jonah, nikachukua simu na kumpigia.
Simu iliita kidogo kisha alipokea. "Unaendeleaje?"
"Niko poa"
"Nilisahau kukupikia chakula cha usiku hivyo jitahidi ule hata ukimuagiza mlinzi chakula
akanununulie hapo ila muhimu kula usiku "Sawa" Jonah alijibu kwa kifupi kisha alikata simu yake. Nilijaribu kuipiga kwa mara nyingine haikua ikipatikana nilihisi huenda kaizima au imeisha chaji, sikutaka kujisumbua zaidi akili.
Nilisali nikaperuzi peruzi mtandaoni kidogo usingizi ukanipitia kama kawaida saa kumi na moja niliamka usingizini ilikua kawaida yangu hata nichelewe au niwahi kulala ni lazima saa kumi na moja nitaamka tu, mara nyingi nilipendelea kulanza siku yangu kabla jua halijachomoza, kuna siri kubwa ya kuiweza siku kwa kuamka mapema zaidi.
Nilimshukuru Mungu kwa kuniamsha mapema, pia nilimwomba kwa siku hiyo mambo mema yawe upande wangu aniepushie na kila baya, niliweka imani nikaingia kwenye kujiandaa siku hiyo nikataka niwahi zaidi kwenda kwa Jonah ili niendelee na kazi yangu kumrejesha Jonah katika hali yake ya kawaida.
Mvua ikaanza kunyesha tena ile kubwa sana ilinyesha mpaka saa nne asubuhi ndipo ilikata kabisa, nikatoka nikachukua usafiri wa kuelekea kwa Jonah nikiwa njiani mvua ikaanza kunyesha upya kwakua ilikua bajaji ya kukodi hivyo ilinipeleka mpaka getini kwa Jonah.
Nililipa kisha nilichomoka kama mshale mlinzi alinifungulia geti nikaingia ndani macho yangu yalistaajabu kumwona Jonah kasimama kwenye mvua haoneshi dalilia ya kuondoka wakati mvua ilikua kali sana inapiga.
"Mvua ni kall sana Jonah utaumwa tafadhall twende ndani" nilimwambia Jonah baada ya kumfikia alinitazama tu bila kunijibu, nilimshika mkono ili nimwongoze kuondoka hapo.
Alinivuta na kunikumbatia kwa nguvu kwa nyuma, nilijaribu kujitoa mwilini mwake ila aliendelea kunikumbatia.
'Usijiondoe tafadhali kwakua hilo halitawezekana alininong'oneza kwa sauti yake nzito sikioni mwangu, sauti ilijua kunisisimua, ilibidi nitulie tu, mvua iliendelea kutupiga pale huku nimekumbatiwa mwenzenu sina pa kwenda.
Nilibebwa na mwamba mpaka ndani nilijua ataniacha sebleni ndio kwanza alinipeleka mpaka chumbani kwake.
'Nguo zako zimelowana sana ziondoe zitakupa homa" "Heeeeeee" niliguna kwa nguvu.
Alinisogelea na kuanza kunitoa ya juu ikabidi nimsukume huko akaangukia kitandani.
"Umenibadilisha kwa kiasi fulani, sikuwahi fikiria naweza kupona kwa hatua hii niliyofikia mpaka sasa, ouuuuh kweli wewe ni mtaalamu ila sasa bado sijapona vizuri"
'Utapona kwa uwezo wa Mungu na mimi nikiwa hapa utapona kabisa
'Ila jambo moja dawa yangu nimeanza kuijua "Ni dawa gani hiyo?"
'Nikumbatie siku zote, ukinikumbatia mara nyingi kwa siku nitapona wewe ndio dawa yangu naomba unikumbatie ili nipone, Nikumbatie nipone plz" Jonah aliongea mfululizo hali ambayo sikumuona nayo tangu siku ya kwanza nilianza kusadiki kwenye maneno yake kwamba ameanza kupata nafuu.
Nikiwa natafakari alinifikia mwilini mwangu na kunikumbatia kwa nguvu sana.
'Nakupenda nakupenda mno Doreen'
"Uu unasema?"
"Nakupenda daktari wangu" "La lakini"
Hakunipa nafasi ya kuendelea kuongea zaidi alinidaka mdomo hapo nikajikuta nalegea maana kwenye denda palikua udhaifu wangu mkubwa, mwili ulizidi kusisimka nikajikuta namimi namkumbatia kwa nguvu huku namtomasa. Akanibeba mpaka kitandani, mchezo ukaendelea wa kutomasana, akanipunguza sweta na tisheti ya juu akafakamia kifua changu hapo akawa kama mtoto mdogo mwenye kiu ya maziwa, alikinyonya kwa ustadi mkubwa alikua anavitekenya vichuchu vya kwa kutumia ulimi wake, yaani anavisugua.
Nikajikuta namvuta mkanda wa suruali sijui nilikua natafuta nini huko jamani, ila nilichokitafuta nilikua karibu kukipata
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi