*NIMEKOMA MIMI π* *SEHEMU YA KUMI NA MOJA* Mimi sikujua lolote lililokuwa limeendelea. Baada ya kumaliza kuoga, nikajifuta, nikavaa
nguo zangu, nikaendelea na kazi kama kawaida. Siku hiyo tulikuwa hatuna chakula cha kutosha, so Tobias akanipa hela niende sokoni kununua vitu. Nilifurahi sana maana nilijua hii ndo nafasi yangu ya kumwona labubu wangu, Michael
Nikachukua nguo za kubadilisha ili nikifikia mbele nibadilishe nirudi kuwa pisikali Shege. Basi Nikapanda daladala kuelekea kwangu. Nilikuwa na furaha, yani nilihisi kama niko njiani kurudi nyumbani baada ya muda mrefu.
Nilipofika apo tayari nisha badilisha nguo, nikaenda moja kwa moja hadi kwenye chumba changu. Nilipokaribia mlangoni, nikasikia sauti ndani. Ilikuwa ni sauti ya Michael na ya mwanamke. Wote walikuwa wanacheka alafu ghafla nikasikia hawacheki tena bali wanatoa sauti za kuhema kama vile wapo busy kitandani.
Nilishtuka nikaanza Nilipanic. Nikasema labda nimekosea kusikia! Na Kwanini kuna mwanamke ndani ya chumba changu?
Uvumilivu ukanishinda nikasukuma mlango kuingia ndani bahati nzuri hawakuwa wamefunga kwa funguo.
Wapendwa nilicho kiona nilitamani kiwe ndoto. Imagine wanakulana kigodoro changu cha inch
6. Nilihisi kama damu imenipanda kichwan na Ivi Nilimpenda Michael mpaka mwisho nilitamani kunyonga mtu.
Bila kuchelewa nikaanzisha varangati, nikaanza na yule bi shosti asie na haya. Nikamrukia nikaanza kumpiga na kuvuta nywele zake kama niza kwangu vile..
Siwadanganyi, ila ukweli ni kwamba hakuna rangi ambayo hakuacha kuona siku iyo yule dasa. Michael kuona hali inakua mbaya ndo akaingilia ule ugomvi akanikamata. Ile kanikamata tu yule bi shosti akapata upenyo akatoka mwendo wa ngiri.
Kwaiyo alipokimbia Nikawa nimebaki na Michael namuangalia vibaya huku nalia na kutetemeka
kwa hasira. "Michael, ulikuwa unafanya nini juu ya godoro langu na kile kibwengo?"
"Ulitaka nifanye nini? Nilikuwa nibanwa..."
"umebanwa?? Yani niliondoka hata wiki haijaisha, tayari unaleta mwanamke ndani kwangu? We uko serious kweli Michael?"
"Kulikuwa na baridi nikazidiwa Nikaona bora nilete demu"
"Nini??? hata huonyeshi kujuta! Kwani nimekosea wapi mimi?? Mbona Nilichokifanya ni kukupenda?kwaiyo Karma ningekuacha mwaka mzima, si ningekuta umeoa tayari na una wajukuu? Umeniumiza sana, Michael"
"Pole basi, kama ningejua unakuja nisingemleta huyo mwanamke"
"Pole???? Nilipiga simu ngapi? Nilimtumia sms ngapi Hukujibu hata moja?? Kwaiyo nikisema nakuja ndo hutachiti siku iyo??"
Akanijibu kwa dharau "Nimefanya nilichotakiwa kufanya. Tangu umeanza kazi, hujanitumia hata senti. Unajua hali yangu huku ilivyo"
mwezi haujafika! Nilikwambia subiri nikilipwa "Sijakutumia hela kwa sababu bado mwisho wa nitakutumia. We uliona wapi unalipwa siku iyo iyo bila kufanya kazi??"
Akanitazama tu akasema, "Sasa ndo Ishatokea we potezea" Akaanza kuvaa nguo zake taratibu.
Hap ndo nilijua kabisa Michael hanipendi. Hana hata aibu wala huruma, Nilianza kulia lakini hata hakunibembeleza. Yani kwake ilikuwa kama kitu cha kawaida.
"Michael, umeniuumiza sana kuliko vile nilitarajia. Tafadhali toka kwenye nyumba yangu"
"Umesema nini?"
Nikajibu "Nimesema toka kwenye nyumba yangu. Sitaki kukuona tena kuonyesha niko serious Nikafungua kabati, nikatoa begi lake, nikaanza kupakia vitu vyake vyote kwa hasira.
Yeye alisimama ananiangalia akicheka tu "Najua una hasira, lakini najua pia huwezi kuishi bila mimi
"Labda siwezi, lakini nitaanza kujaribu.
Umeniumiza sana leo. Wewe hujui hata nilivyopata hii kazi, nilivyoteseka. Nilifanya yote kwa ajili yako, lakini wewe huna hata shukrani. Nimechoka bhana! Toka kwangu"
Akasema "Sawa"
Nikapaki kila kitu kwenye begi kisha akatoka bila hata kugeuka nyuma. Alijua nitamtafuta baada ya siku moja maana kuishi bila yeye ndo sikuweza.
Alipoondoka Nikafunga mlango wangu vizuri ili niondoke. Kwakua Lily alikuwa kazini mda huo nilimtumia meseji kumuambia kilicho tokea kisha Nikabadili nguo, nikavaa za kiume na kuelea sokoni kununua vitu nilivyotumwa na Tobias.
Nilitembea sokoni kama roboti sababu sikua na mood kabisa. Kuna wakati niliweka mfuko chini nikaanza kulia mwenyewe. Watu kule sokoni wakaanza kuhisi labda nimedata! Ila nyie mapenzi, shikamoosa. Kusema kweli nimekoma mimi Shege
Baada ya kumaliza manunuzi nikarudi nyumbani moja kwa moja. Nilipofika nikagundua nae Bishop alikua karudi. Sikutaka hata kujua alirudi saa ngapi na wala Sikuwa na nguvu ya kujali.
Nikaenda jikoni nikatoa vile vitu nilivyonunua nikapanga kwenye friji nikiwa kimya bila kusemeshana na mtu. Mpaka namaliza muda wa kupika ukawa umefika.
Nikapika haraka, nikawatengea chakula chao then nikarudi chumbani nilie vizuri maana hado
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi