MY WANGU❤️ sehemu ya 71 na 72
Mama akaningalia akanmbia ni mlige uyo ndo anakuliza.nikasema mama nampenda sana niombee msamaha kwake. Mama mi naumia naumia sana . Hataki kuwa na mm. Na hana mda na mimi. Mama kosa gani lisilosameheka amapata mwanamke mwengine tayari .mama naumia sana..shule nikimpigia simu anakuwa ananijibu vibaya. Mi na moyo mama. Nililia kwa sauti. Uzuri tu mzee hakuwa karudi. Mama harkaa aknikumbatia na akaamza kunituliza. Akanmbia basi tulia farida.sawa naelewa mwanangu .tulia kabisa. Naomba utulize kichwa sawa. Nikasema ndio. akanmbia sitaki umuwaze mlige sawa..muache amalize hasira za moyo wake. .na wewe relax na uwe free na maosha yako.na ikiwezekana kesho nikupe nauli uende kukaa kwa mma yako mdogo nyakanazi ata week 2 kwanza ukatulize akirii. Nikasema sawa mama bola niende nyakanazi kwa mama mdogo. Basi maam alinibembeleza jamani. Alinituliza sana. Akanmbia relax mwanagu basi ndo nikatulia nikawa naongea na mama mambo mengine kabisaaa.
Basi mpaka mzeee akaludi tukala kwa pamoja mie nikaenda kujipumzisha . Nikasema mm uyu baba simtafuti tena kumwambia masuala ya mapenzi naona moyo wake ushagoma so sitakiwi kumfosi hapana . Basi mie nikajilalolia zangu. Asubuh mama akaniamsha nikajiandaa akanipa na nauli.ila nilikataa nilimwambia mie pesa nnayo mlige alinitumia tena na yeye nikampa laki 1. Akafurahi uyooo. Nikabeba na nguo zangu 2 tatu. Nikamuaga na baba. Na shoga yangu yusta nilimtumia sms.kuwa naenda kwa mma mdogo week 2 kumsalimia kwanza . Yusta akanambia sawa. Basi kweli mama akanisindikiza mpka stand mie uyoo mapaka nyakanazi. Kutoka kwetu mpaka nyakanazi nuli elfu 5. Basi shoga yenu mpaka kwa mama mdogo. Mama angu mdogo uyu wala hakuwa na familia. Yani single tu. Ila anafanya biasha biashara. Na amejenga kabisa. Kinyumba chake cha kawaida tu. Basi oddo alifurahi kweli mie kwenda kumtembelea. Alinikaribisha vizuri mno . Basi mie nikawa nipo tu nyakanazi kwa mama mdogo ile kubadilisha mazingira kidogoo. Basi nilikaa nyakanazi kama siku 3. Mlhhh siku iyo usiku naona mlige ananipigia.nilishngaaa nikasema leo kuna nn . Mie nikapokea ile simu nikasema haloo
Akaniuliza upo wapi? . Mh nikasema nipo nykanazi. Akaniuliza nyakanazi kufanya nn. Nikasema nimekuja kwa mama mdogo kutembea kidogo. Mlige akasema kesho ludi nyumbani . Sipaamini uko kabisa. Kwanza sikuoni. Na sijuh unafanya mambo gani ukute unakaa na bwana.alafu mm natoa pesa zangu. Mh nikamuuliza kwani kitu kidogo natowa pesa zangu. Natowa pesa zangu. Au unanaisomesha ili unisimange. Akanmbia kua na ww usomeshe mtu ambae sio mwanao wala ndugu yako ndo utajua raha yake. Nikasema sawa hesabu gharama zako nikipata kazi ntakulipa.akanmbia yani we mshenzi ungekuwa karibu yangu ningekunasa vibao ww. Mh alishapanik akaanza kupanda akanmbia unanaijibu unavyotaka sio. Unaona unanaiweza we mpumbavu si ndio we mjinga. Nikasema kwani umenipigia leo unigukane si ndio. Akanmbia sikia ww. Naomba kesho uludi nyimbani . Sitaki ukae uko nyakanazi nimemaliza sasa bishana na mm.nikasema mm siludi uku nipo na mama mdogo na nimebadilisha mazingira. Mlige akanmbia unabishana na mm sio. Mi nikaka kimya .akanmboa okey nataka usiludi kama kweli ww mwanamke. kisba akakata simu
Mh nikajua kanipigia kutafuta ugomvi. Mie nikakausha nikajipumzikia zangu. Na wala sikuwa na plan za kuludi nyumbani mm.Kesho yake saa 7 mchana anapiga. Mh niakpokea. Et umeshaludi nyumbani. Nikasema mm siludi mpakaa week 2 zipite. Akanmbia sawa tunabishana sio. Mie nikasema mlige kwaiyo mimi nisitembee kwa ndugu zangu kisa unanisomesha mbona unakuwa hivyo. Niache bwana niwe huru na mimi na ndugu zangu. Mlige akanmbia sawa . Kisha akakata simu. Apo hakunutafuta mpaka.nimamaliza week kwa mama mdogo. Na nikaongeza week ya 2. Nikatumia week 2 kwa mama mdogo ndo nikaludi nyumbani sasa . Basi mama aknmbia unajua yule mlige anakupenda sana .nikasema mh kwa nn mama.mama akasema Alipiga simu et amekutafutia tution hii likizo ukasome.mie nikamwambia umeenda kwa maam yako mdogo.ananza kusema ooh mma nyakanazi sio salama kuna wahuni wengi alafu ww mtoto wa kike. Mie nikabaki nimemshangaa ila nimeshamuelewa wivu unampelekesha .mh mie nimanyamaza mana mlige mwenyewe sie ni kugombana tu mda wote
Basi mie nikawa busy na mamabo yangu na yusta wangu. Siku iyo sasa tulikuwa nyantakara centre mie na shoga yangu yusta tunapiga story sehemu moja uku tunakunywa juice ya miwa. Basi tuliwa pale bwana.mh gari ya mlige ikapaki kwa pembeni . Kisha akapiga honi. Nikajua anajita mie .mie nikaenda akanifungulia mlango akanmbia ingia ndani. Mie nikamuuliza tunaenda wapi. Akanmbia unahisi ntaenda kukuza ama. Mh mie nikamwambia samahani kisha nikapnda. Basi kanuna uyoo kama anataka kupasuka. Basi akadrive mpaka nyamsebehi kwake makazi mpayaa. Tumefika. Akshuka akfungua geti lake .kisha akaingiza gari ndni. Kisha akafunga geti lake.akanmbia njoo ndani. Mie nikaingia mpaka.ndani .aseeeeee ni kuzuri jamani. Yani kuzuri mnoo.hii nyumba ilikuwa bomba mnooo.basi tumefika ndani akanmbia kwaiyo huwezi kununua juice ukaenda kunywia nyumbani. Unakunywa bala balani unajianika wanaume wakuone au sio. Mie nikanyamaza kimya wala sikutaka kujibu .namuheshimu tangu anipige . So nachunga mdomo wangu sana nikiwa nae karibu. Akanambka naenda kulala.nisaidie kufanya usafi ndani leo. Mie nikasema sawa.akanionesha vifaa vya usafi .kisha yeye akapanda chumbani kwake. Na kweli ndani kulikuwa na vumbi mnoo. Mtoto wakike nikaanza usfi.
Nilifanya usafi kote . Kila sehemu . Kuanzia iyo saa 7 mchana mpaka saa 10 ndo namliza nimechoka. Apo na vyombo nilishaosha mana alikuwa anatumia tu ata haoshi. Ila apa ni kuzuri jamani yani kila kitu alikinunua kipya. Baada ya kumalaiza usafi sasa ndo namuona anatoka chumbani kwake akanmbia nenda kamalizia na kwangu. Asa nakataaje ndo ananilipia ada uyu. Mie nikaingia chumbani kwake.nikapiga kazi aswaa. Nikambadilishia na mashuka pale. Iko kitanda chake woow. Yani chumba cha kisasa wallah mpka raha.basi nilipomaliza sasa nikatoka nikamkuta anacheka movue.nikasema mi naomba kuondoka sasa mda umeenda alfu sijamuoga mama kama nakuja uku. Akanmbia sawa . Akanipa pesa elfu 50 . Akanipa na funguo. Akanmbia hii ni funguo ya apa kesho asubuh uje apa kufua..nguo zangu zote chafu. Mie nikasema sawa .kisha uyo nikaondoka zangu. Nikapanda tu boda mpaka home.yani nilichoka mnoo nilifikia kujipumzisha tuuu
Kesho yake sasa niliamka alfajir nikamuaga na mama kuwa naenda kwa mlige kaniomba nikamfulie.mama akacheka aksema yani mlige anajifanya anakukazia ana lolote.aya bwana kafulianeni .mi siingili mapenzi ya watu.mie nikacheka tu. Basi bibi mie nikaakodi boda mpka kwake. Nikakuta yeye kashondoka kwa kua mie nilikuwa na funguo . Nikafungua nikaingia ndani. Basi nikaanza dobi na uzuri alikuwa na machine. Ila kusuuza ni mm na kuanika. Aliniekea mpkaa boksa zake kila kitu yani. Na nguo zilikuwa nyingi. Alikuwa anavaa yu ata hafui. Mpaka nikawa nawaza kwani uyo maraya wake hamfulii. Basi nilipomaliza kufua nilichoka sana. Mie nikaenda kujimwagia maji chooni kwake. Kisha nikaludi mpaka chumbani kwake . Nikabuta taulo lake nikajifunga kwa juu ya maziwa nikajilaza kitandani kifudi fudi. Basi usingizi wala haukunichelewsha nikapitiwa kabisaa
Nikaja kustuka namuona mlige amekaa pembeni yangu anachezea simu. Mh nikaamka nikasema heeee sory jamani nimelala kitandai kwako. Akaningalia kisha akanambia nimeleta vyakula jikoni. Kanipikie ugali nyama huu mda. Mie nikasema sawa . Kishs nikaelekea jikoni. Basi kweli shoga yenu nikaanda chakura vizuri nikatenga dining. Nikaenda kumuita mwanaume . Sasa kuwa chakura teali. Akambia sawa na kweli akaja . Mie ata sikutaka kula.nikasema nataka kwenda sasa. Akanmbia njoo ule kwanza. Mie nikasema naenda kula nyumabani akanambia sitaki tubishane nimesema njoo ule apa. Basi nikasogea nikawa nikaanza kula. Mh namuona mtu et ananilisha nyama. Mh nikala. Nikaona leo wamemtoka leo. Basi tukawa tunakula.ila uku anaiilisha nakwambia. Nikaona aka na mimi nikachukua kipande cha nyuma nikamlisha . Na yehe akala tena uku kanishika mkono wangu ule nilokuwa namlishia. Nilisika rahaa sana. Yani nilipata amani ya ajabu asee kweli mi nampemda uyu baba jamani
🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi