*AAAAAASH BOSS ENZO* *season two* *SEHEMU YA TANO*
"Habari za hapa?"
Aliuliza Suzy baada ya kutufikia Mimi na pili.
"Salama"
Alijibu pili na Mimi Nikabaki nikimuangalia Suzy kwa dharau sana Maana huyu msichana amejua kuninyanyasa sana NYUMBANI kwao.
"Nikusaidie nini
Nilimuuliza
Hapo pili akaniangalia na kuniuliza.
"Mnajuana ?"
"Ndio"
Baada ya kumjibu Kuwa Mimi na Suzy tunajuana, pili akageuka zake na kwenda chumbani kwake na tukabaki Mimi na Suzy tukiangaliana tu
Safari hii Bwana Suzy alionekana Kuwa mpole na Mtulivu Sanaa na tofauti na Suzy Yule ambaye namjua Mimi.
"Umepajuaje hapa ?"
Nilimuuliza Maana naona ni Kama wanaanza kupazoea NYUMBANI kwangu, wanaambizana tu na kuja muda na Saa yoyote ile wanayojisikia.
"Tunaweza kupata muda wa kuongea mawili matatu?"
Suzy aliniuliza.
"Suzy unavyoangalia unahisi Mimi Nina muda wa kuzungumza na wewe? Unajua Mimi Siwaelewi wewe na familia yako mnashida gani
na Mimi? Mbona Mimi siwafatilli Kama ambavyo
ninyi mnafanya? Mnataka nini kutoka kwangu"
Kwa SAUTI ya upole Suzy akazungumza. "Ni kuhusu Enzo"
Weeeh kitendo cha kusikia Jina la habibi wangu, kwa jazba ya hali ya juu nikauliza.
Enzo amefanya nini? Anaumwa Amepata matatizo au? Nambie Enzo Ana shida gani?"
Suzy akatabasamu na kwa upole akazungumza.
"That is love, tazama unavyopata shida kutaka kujua kuhusu yeye, ishani hatuwezi kuzungumza
tukiwa tumesimama, hapa kuna mawili, tuingie Ndani kwako au Twende kwenye gari"
Nikafikilia kwa muda kidogo kisha nikaamua kumkaribisha Ndani kwangu liwalo na liwe tu.
"Karibu"
Nilimkaribisha
"Asante, Hongera Ndani kwako pazuri sana"
Alizungumza Suzy akinisifia Assaah Walahi Ndio alizidi kunipatia wasiwasi kabisa, yaani huyu msichana huu wema ametoa wapi?R Yaani Suzy ninayemjua mimi na huyu wa Leo ni
watu saba tofauti
"Enzo Ana shida gani?"
Nilimuuliza nikiitaji kujua
"Enzo anakuitaji sana ISHANI, sana Tena Sana, lakini pia Enzo anakupenda sana Tena sana"
Nikamuangalia na kucheka kwa dharau.
"Najua uniamini na kuna Namna unashindwa kunielewa lakini huo Ndio ukweli ishani, Enzo anakuitaji sana Tena sana"
Hapo kwanza Ndio nikakumbuka Kuwa huyu
Mwenyewe alikuwa anamtaka kaka yake, na Kwakuwa Leo yuko NYUMBANI kwangu wacha nimwmbie ukweli wake
"Kwahiyo hapo Suzy Unataka Mimi niwe na mahusiano na Enzo si Ndio ?"
"Ndio"
"Vipi kuhusu Mke wake? Au achana na Mke
wake, vipi kuhusu wewe 7 Maana najua unatamani sana Kuwa Mke wa Enzo, hivi hauna akili nzuri au? Enzo si kaka yako wewe?"
Suzy akatabasamu na kujibu.
"Ooooh kweli Enzo anakupenda sana mpaka amekuambia mambo yangu Mimi na yeye, lakini
kuna kitu kasahau Labda, Ishani Mimi na Enzo sio ndugu ata kidogo, Yaani ata nusu, Enzo
amezaliwa Pekee yake Kuanzia kwa baba mpaka
kwa mama"
Hapo kwanza nilishtuka na kwa shauku nikamuuliza
"Kivipi?"
Suzy akakaa vizuri na kuendelea kunipatia uondo wa mambo ambayo sikuwa nikiyajua
kabisa.
ISHANI Mimi sio Mtoto kishua Kama unavyofahamu, Mimi ni Binti wa KIJAKAZI tu,
Yangu mzazi alikuwa ni mfanyakazi pale NYUMBANI Kwa kina Enzo, na mama yangu
mama
alikuwa ni single mama, tangu nimezaliwa
sikuwa kuonana na ndugu ata Mmoja wa mama
yangu, na Ndio Maana ata mama yangu
alipofariki bado niliendelea kubaki kwa kina
Enzo
"Suzy unanitania si Ndio Hivi uwe tu Mtoto wa mjakazi halafu Ndio madam groly akupende
kiasi iko
"ISHANI yako mengi sana ambayo uyafahamu
na huu sio wakati sahihi, sitaki Kuwa muongo
kwako nampenda sana Enzo Tena sana,
Lakini Enzo anakupenda wewe mno, na
wahenga walisema Kuwa, upendo wa kwanza kwa mtu ni kumpatia Furaha na furaha ya Enzo
ni wewe tu na sio pully, ishani, nataka kumuona
Enzo akiwa na Furaha, nataka kumuona Enzo akiwa na amani Kama hapo awali, nimechoka
kuona na kusikia SAUTI ya kilio chake kila
Siku
Nikamuangalia Suzy kwa muda na
Kuzungumza.
"Suzy umekuja kunichezea wewe si Ndio?"
"Najua sio rahisi kunielewa lakini huo Ndio ukweli, tshani, Enzo anakupenda sana Tena
sana, kwa sasa hivi anapitia kipindi kigumu
sana
"Lakini Enzo amenitamkia Kuwa aniitaji kabisa
kwenye maisha yake"
"Kwa sababu anakulinda wewe ISHANI
Kwnza nikashtuka, ule mshtuko wa herufi kubwa
na kumuuliza.
"Ananilinda?"
Kabla Suzy ajanijibu swali langu, muda huo huo simu ya Suzy ikaita na Nick Rafiki
wa Karibu sana wa Enzo Ndio alikuwa akipiga.
"Hellow kaka nick"
Alizungumza Suzy baada ya kupokea simu.
Muda huo huo ikasikika SAUTI ya Nicki akiongea kwa jazba lakini pia na wasiwasi mkubwa sana
Ndani yake.
"Suzy, Nipo hospital, nimemleta Enzo ana hali mbaya sana amekunywa sumu"
"Nini?
Nilijikuta nikidakia kwa mshtuko wa hali ya juu
na kumpokonya simu Suzy.
"Nick unasemaje? Na umempeleka hospital
gani?"
Basi Niki akatutajia hospital aliyompeleka Enzo
na pasi na kupoteza muda Mimi na Suzy tukapanda gari na kwenda kwenye hospital
husika
Walahi nilikuwa Nina wasiwasi sana, njia nzima nilikuwa niktetemeka tu na kuna muda nilikuwa
Niona Kama sifiki, Basi foleni za hapa na pale Ndio zilikuwa zikinichanganya zaidi
Hatimaye kwa uwezo wa Mungu Mimi na Suzy
tukafika hospital, nyieeeeh ndugu yenu siku subili ata gari ipaki vizuri, chap nikafungua
mlango wa gari na kushuka na moja kwa moja
nikawal mapokezi ambapo nilikutana na nick akiwa anazunguka uku na uku.
"Enzo yuko wapi?"
Nilimuuliza nick nikiwa na wasiwasi sana.
Muda huo huo pia Suzy nae akafika kwenye
enec ilo na kuuliza swali lile lile ambalo Mimi Nilimuuliza Nick.
"Yuko emergency room hawaruhusu mtu kuingia
Yaani nilijikuta mawazo yangu yakienda mbali.
sana, nilijikuta tu nikikumbuka jinsi nilivyopoteza
wazazi wangu, kuna Namna pia Nilihisi Kuwa
naenda kumpoteza na Enzo pia, Kiukweli nilishindwa kuficha wasiwasi wangu na
nikajikuta nikilia kwa uchungu sana
"Aaaah Ishani Ndio nini sasa"
Alizungumza Suzy na kunishika mkono na
akanitoa nje kabisa ya hospital na Nick akatufuata
"Nafikili pia ishani ungeondoka tu Maana madam groly akikukuta hapa hali itakuwa sio
shwari kabisa na ukizingatia yuko njiani anakuja
uku
Alizungumza Nick akionesha kumuogopa sana
madam groly
Kwa ujasili wa hali ya juu, nikafuta machozi na
kuzungumza
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni