*AAAAAASH BOSS ENZO* *season two* *SEHEMU YA NNE*
Nilipanda kwenye gari ya Enzo, nikiwa na hasira ya usoni tu lakini nilikuwa Nina Furaha sana moyoni kwangu, my zangu huyu kaka nampenda na sio utani, Yaani nampenda kutoka moyoni, imagine, kitendo cha kumuona tu najikuta nasahau shida zangu zote.
"Funga mkanda"
Alizungumza Enzo pale tu alipoanza kuendesha gart
"Sitaki
Nilijibu kwa SAUTI ya kudeka uku nikijifanya Kuwa bize sana, masikini Enzo wa watu, akasimamisha gari na kunisaidia kufunga
mkanda na safari ikaanza.
Kiukweli safari ilikuwa ni yenye ukimya sana, Enzo hakuwa akiongea kitu chochote kile na Mimi nilikuwa kimya nikimuangalia kwa kuibia
Ibla tu
Ila Nyleeeh Enzo amepungua sana, uso wake haukuwa na Nuru Kama ambavyo alikuwa mwanzo, Yaani Sijui niseme kitu gani lakini
daaaah Enzo wangu hayuko Sawa kabisa.
Enzo akaniangalia kwa muda uku akifocus na kuendesha gari kisha akavunja ukimya na
kuniuliza.
"Uku umetoka wapi San Hizi 7"
"Ndio Maana nilikuwa sitaki kupanda hii gari yako Walahi, kwani nilipotoka Mimi wewe panakuhusu nini?"
Nilimuuliza nikionesha Kuwa sitaki kabis shobo
na yeye.
"ISHANI Saa hivi ni usiku sana, Angalia muda vizuri ni Saa 5 inaenda Saa Sita, usisahau Kuwa wewe ni Mtoto wa kike"
Nikamuangalia na kumjibu.
"Usisahau Kuwa nilikuwa nikilala nje kila siku na sikuwai kudhurika na kitu chochote, by the way. Unaendeleaje wewe na Mke wako ?"
Hapo kwanza Enzo akashusha Pumzika nzito kisha akajibu.
"Sijui amesafiri ameenda Kenya na mama yake, ishani usitake kubadilisha mada nataka kujua umetoka wapi muda huu?"
"Kwani wewe nikitembea usiku huu unaumia nini Matembezi yangu yanakuhusu nini kwa mfano
? Enzo nishushe hapa panatosha"
Nilijifanya kuwa na hasira sana lakini moyoni kulikuwa na Furaha isiyokuwa na kifani.
Baada ya mwendo wa Kama nusu Saa hivi, Hatimaye nikafika NYUMBANI kwangu, haraka nikafungua mlango wa gari na kushuka.
"Ooooh Asante Mungu umerudi
Alizungumza pili ambaye nilimkuta hapo nje akizunguka zunguka tu
"Pili kuna nini Mbona Kama umepaniki?"
Nilimuuliza
"Nakupigia simu upatikani na muda unayoyoma tu ndugu yangu umenipa wasiwasi sana ujawai kuchelewa kurudi Kama hivi
Alizungumza pili akionesha kujali sana kuhusu Mimi, Yaani Kama ni Rafiki tu, Walahi Mungu amenibariki na huyu pili, huyu msichana ananijali na kunipenda sana sana
"Simu yangu imekufa chaji, lakini pia kulikuwa na kazi nyingi sana Leo na foleni Basi weeh"
Nilimjibu pili wangu kwajili ya kumtoa wasiwasi
tu
Pili sasa kwa umbea, akasimama na kuangalia gari kisha akaniuliza.
"Ushapata Bwana mwingine tena Mwenye gari 7"
Nikacheka na kumjibu.
"Amna Bwana, huyu ni kaka wa boss wangu tu kwakuwa tumechelewa kutoka Ndio ameambiwa.anilete NYUMBANI
Niliamua tu kumdanganya pili mama akili yake naijua vizuri sana, Yaani angejua Kuwa ni Enzo angemuwashia moto wa hatari sana.
Kwa hatua za haraka haraka nikasogea mpaka kwenye gari ya Enzo na kufungua mlango.
"Kwahiyo ulitaka niondoke ikiwa ujaniaga ?"
Enzo aliniuliza
"Wewe sikiliza Ebu nendaga Uko"
Nilijibu kisha kwa hasira nikabamiza mlango wa gari na moja kwa moja Mimi na shoga yangu tukaingia Ndani na Enzo nae akaondoka.
Siku iliyofuata Kiukweli nilikuwa ninauchovu wa kutosha, lakini pia miwili uliniuma sana kutokana na kufanya kazi mfululizo pasi na kupumzika.
Nikajikongoja zangu na kwenda kazini, kwa
Mara nyingine Tena nikachelewa kazini na kumkuta mama amina akiwa na Binti yake wanaendelea na kazi zao
"Naona sasa ofisi umeifanya Kama ya baba yako
Alizungumza mama amina pale tu nilipofika kazini.
Nikamuangalia kisha kwa SAUTI ya upole na
utulivu nikajibu.
"Kwa Leo sijusikii vizuri kabisa na nilikuwa naitaji kwenda hospital"
"Kwahiyo hapa Ndio hospital au Mimi ni ness?"
Mama amina aliniuliza akiwa amenishikia kiuno.
"Hapana mama, Nimekuja kukuomba ruhusa
lakini pia kuchukua Pesa ya Jana, na nilijaribu kukupigia simu lakini ujapokea
Mama amina akasimama kidedea na kuanza
kunifokea mbele ya wateja, na ukizingatia ni asubuhi, wateja wa chai na supu uwa ni wengi
sana kwakwell.
"We Binti sikia, Nafikili Mimi na wewe tumefika mwisho sasa Sawa, kila siku unakisingizio kipya
Binti yangu yupo atanisaidia kazi zangu"
Gafla pully au kwa Jina lingine amina akadakia.
"Weeeh mama akuuuuh Mimi na Hizi kazi wapi na wapi? Unataka nikomae na kubabuka na huu
moto au ?"
Hapo mama amina akanywea Kuwa mpole sana, kisha akanigeukia Mimi na kunifokea.
"Ebu kabadilishe nguo zako upeleke chai kule site
Kwakuwa Nina shida na kazi naitaka, nikajikaza na kwenda kubadilisha mavazi yangu na moja Ka moja nikaanza kuhudumia wateja uku na uku.
KI AFYA sikua vizuri kabisa na ile zunguka ya uku na uku, nikajikuta nikianguka chini Kamal Mzigo kutokana na kizumguzungu kikali ambacho nilikipata.
"Ndio nini kuanguka kwenye biashara yangu? Unataka ufie hapa niambiwe nimekutoa kafara si Ndio
Yaani mama amina amebadilika sana, Yaani amekuwa na Mdomo mchafu sana dhidi yangu
na ameanza hivi baada ya Binti yake kuja na vile
Ndio Binti yake ana hela Basi weeeeeh, walala hoi Kama Mimi ni kunyanyasika tu
Kwakuwa nilionekana Kuwa mgonjwa sana, nikapatiwa muda wa kupumzika na nilipokaa Sawa tu nikaruhusiwa kwenda NYUMBANI
Kama kawaida, Rafiki yangu pilli Ndio alikuwa
kila kitu, pili alinisaidia kwenye kila hatua Yaani mpaka kuniogesha alliniogesha shoga yangu.
"Asante sana pili Mungu akubariki mno Nilimwambia pili nikiwa Namaanisha, waswahili usema akufahaye kwa dhiki ndiye Rafiki.
Siku hiyo pili alilala na Mimi hakutaka kuniacha ata kidogo.
Hatimaye siku MBILI zilipita nikiwa bado naendelea kujiuguza
Ikiwa ni Majila ya jioni nikiwa nimekaa nje
napigwa na jua la kuzama, muda huo huo ikaja gari nyingine nzuri sana na kupaki mbele ya
Nyumba hiyo, Mimi na shoga yangu pili tukabaki tuklishangaa tu, kisha baada ya muda mfupi tu akashuka Suzy, huyu Suzy Bwana Sijui Kama
mnamkumbuka, huyo ni Mtoto wa mwisho wa madan groly, na Kama mnakumbuka vizuri, huyu Ndio alikuwa ataki kuniona pale NYUMBANI kwao.
"Huyu Nani Tena?"
Aliuliza pili kisha Mimi na yeye tukasimama na kubaki tukimtazama Suzy, ambaye aliposhuka tu
kwenye gari akaanza kutusogelea.
Je Suzy amekuja kufanya nini? Amekuja kwa wema au Shari? Tukutane sehemu
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni