THE SECRET MESSAGE 3 to 4
Sina sababu ya kukuficha lolote. Lazima nikuambie ukweli. Rashid wewe Mungu anakupenda sana, mwenyezi Mungu anakupenda mno. Unafanya kazi zako vizuri kabisa mwanangu, lakini cha ajabu mwanangu kila nguo mpya unataka, kila kiatu toleo jipya unataka, mwanangu utaona wapi pesa kama unashindana na watu wa mitindo?.
Kwenye utafutaji, ndiyo kuna wakati unatakiwa kufurahia unachapata lakini sio kuishi juu ya kipato chako. Rashid wewe una matumizi mabaya sana ya pesa, pombe na wanawake, nikuambie tu kitu hata ukeshe bar mwanangu, hata usilale unywe siku nzima huwezi kumaliza hizo pombe, hata usimamie kucha huwezi kumaliza wanawake wotee kwasababu kila siku anazaliwa mpya mwanangu.
Muda haurudi nyuma. Dunia ina matatizo mengi sana, magonjwa, mikosi na laana. Nimemaliza mwanangu, asiyesikia la mkuu huvunjika guu, na asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu.โ
Nilishusha pumzi na kusema โmama maneno yote hayo wakati nimekuomba pesa kidogo tu.โ
Mama yangu alisema โungekuwa unapofanya kazi unatukumbuka, kwamba hii ni ya mama na baba ningehangaika mwanangu. Nilihangaika na wewe ukiwa chini yetu. Sasa una maisha yako. Sina pesa ya kukupa mimi.โ
Nilijilalamisha na kukata simu huku nikiona mama ananionea sana. Nikiwa kwenye hali kama hiyo nilisikia hodi mlangoni. Alikuwa ni mama mwenye nyumba. Nilishangaa kwa maana sidaiwi mimi. Hivyo nilisalimia tu. Huyu mama alinijibu. Ni mama ambaye anaishi nyumba kubwa upande wake na sisi wapangaji tuna upande wetu.
Haikuwa siku nzuri kwangu, nakumbuka huyu mama alisema kwa kunitazama โChiddy mwanangu, inatosha sasa. Nilikupangisha hapa kwasababu Nilikuamini na kuona kijana mstaarabu na mchapakazi.
Lakini badala yake umegeuza nyumba yangu Danguro. Kitu ambacho mimi sikifurahii kabisa. Nakuomba sana sana, tafuta mwanamke mmoja tu anatosha hapa. Kama huwezi tumia nyumba za wageni au hama.
THE SECRET MESSAGE ๐ฌ04
Mimi ninajiheshimu sana. Hapa kuna watoto wamekuzunguka na watu wa heshima. Unajisikiaje kuvua nguo zako kwa kila mwanamke, sasa hayo ni maisha gani?, wazazi wako wakijua huu uchafu hawatapenda kabisa. Nilipangisha chumba sio danguro. Nafikiri umenielewa.โ
Niliona kweli nina siku mbaya mno, nilikuwa nimetoka kufokewa na mama mzazi sasa mama mwenye nyumba. Nilimtazama kwa upole na kusema โsamahani sana mama, nimekuelewa vizuri tu. Nashukuru mama.โ
Mama mwenye nyumba alinitazama na kushusha pumzi kisha alianza kuondoka. Basi ile anaondoka mimi moyoni nasema โbimkubwa kanielewa anashindwa kusema nini?, kama amenielewa aseme tu mimi napita naye.โ
Halafu niliingia ndani, ni kweli, mimi wamama, watu wazima sio shida zangu. Nawashughulikia haswa.Sijui hata niseme nini juu ya maisha yangu. Maisha yangu yanatafunwa sana na dhambi ya uzinzi. Sijui kama umewahi kukutana na mtu kama mimi, au kuwa mimi, ni hatari sana.
Niliporudi ndani tu, simu yangu iliita, nilipokea na alikuwa ni mteja tena mteja wa maana. Nilianza kujiandaa haraka haraka. Nikapendeza, unyunyu sikusahau , kijana ukiniangalia hivi nimependeza balaa. Nilitoka na kumfuata huyo mteja. Aliponiona tu alinisalimia vizuri akisema โninachokupendea Chiddy usafi tu upo vizuri.โ
Nilitabasamu nikisema โnashukuru sana Sister. Najitajidi hili wateja wangu mfurahie safari na mimi sitaki kuwapa taabu ya harufu mbaya.โ
Alitabasamu na kusema โhongera sana Chiddy.โ
Alipanda pikipiki na kisha nikamuuliza โtajiri, leo gari ipo wapi?โ
Alitabasamu na kusema โshemeji yako alitoka nayo, ndiyo naifuata mahali.โ
Nilitabasamu tu. Basi mwanaume nikamchukua huyu dada. Dada mzuri mno, sisi hao mpaka sehemu gari yake ipo. Wakati anashuka aliniita kwa sauti ya madeko โChiddy!!โ
Nami kwa heshima niliitika โNaam dada yangu!!โ
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni