THE SECRET MESSAGE ๐ฌ 1,2
Ninatamani kama isiwe ni kweli kwenye hili ambalo mimi leo hii nataka niwaweke wazi. Lakini hii sio ndoto, sijaota mimi, ni kweli nimeyaishi na yamenitokea kwenye maisha yangu. Maisha yangu yaligeuka hadithi kwa kila aliyenifahamu vizuri, maisha yangu yaligeuka funzo kwa vijana wengi wenye tabia kama ambazo nilikuwa nazo mimi. Mwisho wa yote mimi kama mimi nilijifunza kuwa hatima ya mtu haibadiliki kwa vyovyote vile.
Naitwa Rashid, hilo ndiyo jina langu nililipewa na mama yangu, na baba yangu. Jina ambalo nimelitumia vizuri tu shule, nikasoma vizuri na kumalizia elimu yangu ya chuo kikuu vizuri tu kama Rashid. Rashid jina zuri tu ambalo wazazi walipendezwa nalo ila mimi nikaona wamekosea sana ni vyema zaidi kama wangeniita Chiddy Bwooooy.
Kwasasa ndiyo wanaitwa vijana wa ovyo, sasa ndiyo mimi wa enzi hizo. Mimi nilikuwa ni kijana wa ovyo, tena ovyo mnoooo haswa kwenye masuala haya ya wanawake. Aaah, mimi kwenye masuala hayo sifai, ni ovyo kuliko ovyo yenyewe. Sijui ni ujinga gani huo mimi sijafanya kwenye masuala ya wanawake, mapenzi kwa ujumla. Nimefanya mengi sana, machafu ya sharehe na ya kuumiza hisia zangu, zao hao wanawake na hata jamii kwa ujumla.
Baada ya kuona mambo sio mambo sasa, maisha magumu sana na mimi kama kijana natakiwa kupata mtoto mkali, pamba kali, vitu vizuri vya kutambia ndiyo nilijiingiza kwenye biashara ya bodaboda.
Sikuwa najua hata nu kiasi gani nakosea. Nafanya kazi kwa bidii ila pesa haionekani. Inaishia kuvaa, kuhonga na kutafuta sehemu nzuri za kulala na watoto wakali, sehemu nzuri za kutamba, sehemu nzuri za kufurahia huku nikitaka kunogesha penzi Chiddy mimi ni lazima pesa itimike. Mtoto mzuri akiniita kwa madeko ty โChiddy lakini kwanini, mimi sipendi unajua.โ
Basi huyo tayari anakula hela yangu.
Wazazi wangu walijua wamepata kijana mzuri kumbe mimi muonekano wangu na uanaume wangu mzuri natumia vibaya sana ili tu kuchanganya mambo hapa duniani. Yaani kwangu burudani.
THE SECRET MESSAGE ๐ฌ02
Nani asiyemjua Chiddy, Chiddy mwenye jina langu kubwa. Umaarufu wangu sio kwasababu ya kusababishiwa na wengine. Mimi ni smart, mimi nina mvuto, nina ulimi mtamu yaani hata uwe kauzu vipi, nikikutaka kama hunijui unaingia kingi, labda uwe unanijua na kusikia sifa zangu.
Ninajua sana kubembeleza, ulimi mtamu wenye maneno mazuri na matamu, kijana mpole na mstaarabu ila ndani yangu kuna shetani mkubwa wa uzinzi na kuniachilia hataki.
Yaani mapenzi ndiyo starehe yangu tena sio na mwanamke mmoja, leo Fatumq, kesho Aisha, kesho kutwa Asha, Jesca, Gina, Prisca, Anna, Maimuna na majina mengine mengi ongezea hapo.
Siku moja nikiwa kwangu, asubuhi sasa ile nimeamka sina hata mia. Nimepanga sio sehemu mbaya. Ni pazuri tu. Ndani kwangu nimetengeneza vizuri hatari. Ila wanawake wanavyopishana sio poa. Mpaka muda mwingine ni aibu kwa wapangaji wengine na sitaki hata mara moja hawa wapangaji wengine wakutane na wageni wangu kwa maana mimi sio poa. Najua watapewa tu habari zangu.
Sasa hii siku nimelala na mwanamke , asubuhi kaondoka zake nimebaki mweupeeee, sina senti shilingi tano. Sina kitu. Ilinibidi nichukue simu yangu, nimpigie mama yangu. Mama yangu alipokea ile simu nami nilimsalimia โshikamoo mama.โ
Mama yangu alinijibu โmarahaba Rashid, hujambo mwanangu.โ
Mama yangu anavyosema Rashid naona kama ananiua yaani, naona anapunguza utamu wa jina langu natamani hata kupasuka.
Nilisema kwa sauti ya unyonge โmama, biashara mbaya sana. Sina hata pesa ya kula leo. Najua mna hali mbaya pia ila niokoe mama, elfu kumi elfu 20 sio mbaya.โ
Mama yangu aliguna na kusema โRashid mwanangu, naomba nisikilize mwanangu. Mimi ni mama yako, mama yako ambaye nimekubeba, kiuno changu kimekutunza miezi 9 ukiwa tumboni mwangu na miaka miwili umelinyonya hili ziwa langu.
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni