*AAAAAASH BOSS ENZO* *season two* *SEHEMU YA TATU*
Pully alishtuka sana baada ya kuniona akabaki akinitolea macho akiwa na wasiwasi sana, macho yake tu yaliweza kueleza Kuwa kuna kitu akiko Sawa kabisa.
"ISHANI umemuona amina wangu?"
Mama amina aliniuliza kwa bashasha ya hali ya Juu
Nikawaangalia kwa muda na kweli walikuwa wamefanana sana kisha nikauliza.
"Kwahiyo huyu Ndio Binti yako Amina ambaye anaishi Dodoma ?"
Yaani niliuliza makusudi nikitaka kupata Uhakika.
wa mambo husika.
"We uoni tulivyofanana jamani, Yaani huyu Ndio kifungua mimba wangu, jamani amina wangu Karibu Mwanangu niikumisi sana Binti yangu
Alizungumza mama amina na kumshika mkono Binti yake kisha wakaenda kukaa kwenye viti, muda huo macho ya Amina ambaye Mimi namjua kwa Jina la pully, yalikuwa yakiniangalia Mimi tu.
Kwanza Nikacheka na nikagonganisha mikono yangu kwa upashukuna ambao nilikuwa nao kwa wakati huo.
"Pole na safari Mwanangu"
Mama amina alimwambia Binti yake.
Mimi sasa Binti yenu nisiyekuwa na uvumilivu rikadakia
"Safari kutoka masaki au ?"
Amina akashtuka sana na kubaki akiniangalia, mama amina akaniuliza.
"Umesemaje?"
"Nimesema Amina ni Mrembo sana Kama Mtoto wa masaki
Muda huo huo Simu ya mama Amina ikaita, akapokea na akazungumza kidogo kisha akasimama na kuniambia
"ISHANI, endelea kumpa kampani mrembo wangu hapa kuna Mzigo naenda kuuchukia hapo magomeni Mara moja
"Sawa mama
Nilijibu kwa Furaha sana Maana nilikuwa nikitamani sana muda kukaa na huyu pully
wa mchongo,
Kwa muda huo wa jioni, hakukuwa na wateja wengi hivyo ata muda wa kupiga umbea unapatikana
Nikanawa mikono yangu kisha nikamsogelea Pully na kuzungumza.
"Kwahiyo Jina lako ni lipi kati ya Amina na pully
Pully akaniangalia tu kisha akageukia upande wa pili akiwa hana majibu sahihi ya kunipatia.
Kwakuwa nilipanga kumnyoosha nikaendelea. kumtibua
"Kwahiyo Enzo anajua Kama huyu Ndio mama yako mzazi na Jina lako ni Amina na sio pully?"
Pully akanigeukia kwa hasira sana na kutaka
kuzungumza lakini nikamuwal.
"Aaaah Twende polepole Bwana, nimpigie aje
hapa au? Lazima ajue Majina yote mawili ya Mke wake au sio? Sasa, nikuulize, Yule mama
Tajiri ni Nani yako ikiwa huyu mama anayechomeka na moto kila siku Ndio mama
yako mzazi
Pully akaniangalia kwa SAUTI ya hasira
akanifokea
"ISHANI, kimya na kwenye maisha yangu hakuna
kitu kinakuhusu
Nikatabasamu na kumuuliza.
"Kwahiyo mama amina anajua Kuwa wewe ni
Mke wa mtu Sasa hivi?"
"Ishani ishani, achana na Mimi nimekuambia
Sawa, sitaki na Tena sitaki endelea kuangaika na maisha yako ya kimasikini na kutangatanga
Weeeeh hapo nilijikuta nikipata hasira zaidi, nikasimama na kuzungumza.
"Labda Kama nitakufa lakini nikiendelea kuishi
hakuna rangi utaacha kuona"
Kisha huyo nikaondoka zangu na kwenda
kusafisha vyombo vichafu ambavyo vilikuwa vikigalagala kwa wakati huo
Muda wangu wa kuondoka ulipofika nikaondoka
zangu NYUMBANI
Kiukweli nilikuwa Nina maswali mengi sana Kwa
wakati huo, niliwaza pully ni ana Lengo gani na Enzo wangu Nyleeeh ninavyompenda Enzo halafu mjinga mmoja tu anajitokeza na ujinga
ujinga wake.
Kiukweli siku hiyo nilikosa usingizi kabis nilibaki
nikiwa sina amani kabisa.
Asubuhi na mapema nikamka na Kama kawaida nikaingia zangu kibaruani, siku hiyo nilimkuta
pully ambaye kwa Jina lingine ni amina akiendelea kumsaidia kazi mama yake.
"Leo umechelewa sana Ishani
Mama amina aliniambia pale tu aliponiona.
"Nisamehe mama yangu Leo kulikuwa na foleni
sana
Nilijibu kwa utulivu wa hali ya juu.
"Jitaidi kuamka mapema Bwana, Yaani Leo nimshukuru amina Mwanangu amekuja
kunisaidia
"Haitajirudia Tena"
Nilijibu kisha nikaenda kwenye sehemu ya kubadili nguo nikavaa nguo za kazi na kwenda kuendelea na majukumu yangu ya kila
Siku
Katika siku niliunia Basi ni hit, siku hiyo mama amina muda wote alikuwa bize na Binti yake,
katika siku nilifanya kazi Kama mbwa ni hil
jamani muda wote mama amina alikuwa
bize akipiga story na amina wake, siku hii
nilifokewa bila sababu nilitumwa uku na uku
pasi na kuonewa huruma Wala kupumzika
"Ishani umefata vile vyombo ulivyowapelekea wale mafundi au?"
Mama amina aliniuliza kwa SAUTI ya juu kabisa.
"Hapana namalizia kuosha vyombo tu halafu
naenda kuchukua
Nilijibu kwa upole kabisa.
"Yaani unafanya kazi polepole Kama jongoo Kama utaki kazi si uache au ? Na vyombo
vyangu vikipotea tu unaenda kuninunulla au nakukata mshahara wako sitaki uzembe kwenye
kazi yangu
Kwanza nilibaki nikishangaa tu Maana huyu mama hakuwai kuzungumza na Mimi hivi ata siku moja, Yaani muda wote alinifanya Mimi
Kama Binti yake yake lakini Leo cha moto
nakiona Walahi
Basi nikaosha vyombo vyangu haraka haraka kisha nikaenda kufata vyombo vingine mitaani.
Siku zote uwa naondokaga pale Saa 2 lakini siku hii ilikuwa tofauti kabisa, mpaka inafika Saa 4
usiku hakukuwa ata na dalili ya Mimi kuondoka Maana nilikuwa nikipewa kazi juu ya kazi
"Mama nimemaliza kila kitu
Nilimwambia mama amina.
"Haya kwaheri
Alijibu kisha akaendelea kupiga story na Binti
yake.
"Kwani unasubili nini Binti?"
Amina ambaye ni pully aliniuliza baada ya kuona nikiwa nimesimama tu BADALA ya kuondoka.
"Nasubili Pesa yangu
Nilijibu kwani Mimi na mama Amina uwa
tunalipana kila siku elfu 7.
Mama amina akaniangalia na kujibu.
"Nitakupa kesho bado sijapiga mahesabu"
Kisha mama amina na Binti yake wakanyanyuka na kuondoka zao na kuniacha Mimi nikishangaa
shangaa tu.
Kwa wakati huo Nilihisi kuchanganyikiwa kabisa,
Maana sikuwa ata na Pesa ya nauli Mara
nyingi uwa nategemea Pesa ambayo nalipwa Ndio niturnie nauli ya kurudia NYUMBANI
Basi ISHANI Mimi nikashika njia na kwenda
dukani kwa mangi na kumkopa Pesa na mangi.
alinipa pasi na wasiwasi kwani Mara nyingi
bidhaa za mapishi uwa tunanunua kwake..
Nikiwa nimesimama kwenye kituo cha daladala,
ikaja gari moja nyeusi na kusimama pembeni yangu, na polepole vioo vikashushwa nikajikuta
nikakutana uso kwa uso na Enzo
Kwnza moyo wangu ukalipuka kwa furaha ya hali ya juu, lakini sikutaka kuonesha ilo kwa Enzo, ha
kwakumuonesha Kuwa sijali lolote nikasogea sehemu nyingine,
"ISHANI, Ishant, we ishani"
Enzo aliendelea kuniita akitaka nipande kwenye
gari yake
"Dada unaitwa
Akzungumza Mdada ambaye alisimama pembeni yangu na alikuwa akisubilia daladala.
"Me sio ISHANI"
Nilijibu uku nikitamani ata kucheka..
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni