SASA NAKUPENDA Sehemu ya 19 na 20.
๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ
Mwandishi; lissa wa huru media
Mama akasema mungu wangu hajafanikiwa eewh hajafanikiwa. Nikasema ndio mama. Baraka akasema sio kweli shangazi . Mimi siwez kumfanyia hivyo shakira. Apo mimi najiliza atari . Mama yangu akamsogelea baraka akampiga vibao vya nguvu. Akawa bado anataka kumpiga baba ndo akaingia sasa. Akasema muache baraka namuamini sana hawezi kufanya hivi ila uyu mwanao ana hila sana juu ya baraka. Nikasema baba kweli. Kaja kuniita kule chumbani kwangu . Kanambia anaumwa nimletee dawa . Nimemletea dawa ndo akawa anataka.kunibaka bba. Baraka akasema mjomba sio kweli sio kweli kabisa. Mama akasema kellele wewe mbakaji mkubwa na kwangu unaondoka mpumbavu wewe. Huna akiri mshenzi kabisaaaa. Baba akasema ebu vaaa kwanza. Mana apo naongea nimejifunika kishuka tu. Basi mama akaniokotea gauni langu akaniveshea kwa juu. Kisha baba akasema baraka na shakira nawaomba sebeleni. Kisha baba yeye ndo akawa wa kwanza kutoka chumbani kwa baraka. Mama akaniinua uku nalia. Baraka mbona hakuamini macho yake. Basi tukafika mpaka seblen . Apo na baraka alishavaa sasa mana kule chumbani alibaki na kiboxa tu. Basi baada ya mdaa mzeee akatoka kashika msaaahafu( kitqbu cha mwenyezi mungu cha waislamu). Baba akasema baraka shika kitabu iki uape kwa mungu.kuwa haujafanya iki kitu na kama umefanya basi udhulike apa apa. Ata upate kichaaa.
Baraka akakipokea. Akakishika vizuri. Akasema mimi baraka . Kama nimefanya tukio la kutaka kumbaka dada shakira nizulike apa apa . Ata niwe chizi mimi. Apo anaongea mpaka analia .mh nikajua leo baraka nimemshika pabaya mpaka analia. Mana tunamfanyiaga mengi ila sijawahi kuona chozi lake uyu kaka ata siku mojaaa. Ila leo mpaka alilia. Bada ya kiapo baba akanipa mimi sasa. Weeee kwanza kukishika tu kila kitabu nikawa natetemeka. Baba akanmbia apa na wewe. Na kama unamsingizia mwenzako shakira kesho tunakuzika. Weeee kusikia habari za kufa tena. Nikasema.baba mimi simpendi baraka nataka aondoke kwetu. Baba akanmbia ooooh kumbe kwaiyo wala hajataka kukubaka si ndio. Nikatikiisa kichwa kuashiria ndio. Aseeee mzeee akanikamata aliniweka mingumi. Yani mingumi ya maaana.nilisikia mwili wangu kama unavunjwa vunjwa nakwambieni.
Baba akasema wewe mtoto ni shetani. Shakira wewe ni shetani.hizi tabia umepata wapi. Uyu ni baraka ni kaka yako. Kwani mnamuonaje. Naona sana kwa jinsi mnanyanypaa. Ana wakwaza nini. Uyu baraka anakula kilo ngapi. Nani anafanya kazi zaidi yangu umu ndani. Mimi ndo natafuta kwaiyo uyu baraka anakula nguvu yangu. Kama mama yako kakutuma naomba mkome. Na kama hamtaki baraka aseme nimpe tarka yake. Akuchukue na ww mwanae musepe. Wapumbavu nyinyi. Uyu baraka ana shida gani. Kwanza ni mpole sana na mwnye adabu. Anafanya kazi zote kama mtoto wa kike . Bado hamukioni hilo. Leo mnapanga njama za kutaka kumuangamiza wauaji nyinyi. Sasa si hamumtaki baraka mimi mama shakir anakupa taraka uondoke na mwanao. Nyie mbona nilichochea ya kuchochea nyie. Mama yangu akapiga magoti haraka akasema mume wangu mimi sijamtuma shakira kitu kama hicho mume wangu. Na siwez kufanha hivyo ata kidogo. Nisamehe jamni mume wangu. Baba akasema hapana wewe unayafuga aya. Mimi najua sana kama wewe na mwanao hamumpendi baraka ila sikuzani ni kwa kiasi iki mpaka mnamsingia ubaya kama huu. Mimi siwez .mzimu wa marehemu dada utanitesa kwa kumtesea mwanae. Nasemaje nakupa taraka a oyaaaaa mbona nilijuta mimi. Yani familia inafalakana kweli kweli kwa sababu yangu.daah
Aseee mama aliloa jamni uku anaomba msamah. Mpaka baraka ndo akaingialia akasema mjomba mimi sina kinyongo tena.cha muhimu imejulikana sijatka kufanya hivyo.msamehe shangazi . Hausiki bila ya shaka mjomba. Sisi ni familia. Tutakaa na shakira na kumuelewesha .usipanic mjomba na usifanye maamuzi kama ayo . Mama anasema baraka mueleweshe mjomba yako jamni. Yani mama mwenyewe anamlilia barka aongee na mzee. Na hii siku mzeeee alichafukwa alikuwa yupo serious. Basi barka akamsogelea baba akamshika mkono akaanza kumtuliza akamwambia mjomba tulia .aya yashaisha mjomba. Yani baraka aliongea mno ndo baba akaelewa sasa. Akaamchukua mkewe wakaingia chumbani .aseeee mama leo alikuwa anaachwa jamni. Nikabaki mimi na baraka apo ishafika saa 11 alfajir.
Baraka akanambia nenda kapumzike. Tutaongea kesho. Yaan aliongea normal kama hakuna kitu ambacho nimemkosea .nilijisikia aibu sana jamnai. Niliona hayaaa mno. Yani haya kweli kweli .yani uwiiii.basi akaniacha pale kisha yeye akaingia ndani kwake. Mh na mimi tu nikaenda chumbani kwangu. Nikiwa hoi. Na miaibu yangu shuuu
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni