πππ’ π‘π π π₯ππ ππ’ πͺπ π§πππ§π’π ___________________________________ SEHEMU YA 15 ENDELEA......... "Nilikuja kufuatilia malipo yangu " Tasha alijikoroga hakuwa akilidai Kampuni.
"Malipo?.... nadhani hutudai ..." Secretary Annie aliongea huku akipitia kumbukumbu zote za malipo chapu chapu.
"Oh nadhani nimesahau kwanini nilikuwa hapa " Tasha alibeba pochi yake kisha akaondoka ilihali machozi yana mlenga lenga.
Secretary Annie aliachia kicheko cha chini chini.
"Inaonekana Tasha alikuwa anamtaka sana Bryant Kobe sasa kaondoka bila kumuaga ni aibu tupu katika moyo wake. Natarajia kuona somo Tiktok very soon kuhusu hiki kitukio " Alizidi kujichekesha, ile anainua kichwa chake alikutana na macho ya Philips Kobe yakiwa yamekaza.
"Unajua ukimfuatilia Tasha mtandaoni utagundua ni binti ambaye hababaishwi na Wanaume, yaani kuna wakati utahisi yeye ndio anaoa....kanifurahisha sana kwa namna alivyo huzunika kisa Bryant Kobe"
"Niletee taarifa ya miezi sita za nyuma kuhusiana na vitengo vyote " Philips Kobe alimjibu tofauti kabisa.
"Sa...sa... sawa "
"Hilo vazi ulilovaa si sare ya Secretary kabla hujaniletea taarifa niliyo kuagiza naomba ubadilishe "
"Bryant Kobe alikuwa ananisifia sana ni kivaa hii nguo, suti anasemaga hazinipendezei kabisa " Secretary Annie aljichekesha, lakni jicho moja la Philips Kobe lilitosha kumkimbiza kwenda kubadilisha nguo.
Alijikuta akimkumbuka Bryant Kobe kupita kiasi hakusita kumwaga machozi.
Upande wa Tasha baada ya kufika kwenye ofisi yake nyingine inayo jihusisha na mapambo ya majumbani alijifungia kisha akajitupa kwenye kiti.
Akili yake ilizunguka huku na kule asijue ni kitu gani anapaswa kuongea kuhusu Wanaume siku ya leo.
"Hao Mb...wa hao β....hapana huyo mbwa aliyejitia kuondoka bila kuniaga hata hajanikomoa.... kwenye ufahamu wake bila shaka anahisi alikuwa ananitumia eh anajidanganya kwa sababu tulitumiana tena Mimi hapa ndio nilikuwa nampelekea moto kuliko kawaida...." Basi Tasha alianza vizuri lakini dakika ya mwisho aliishia kulia...
wacha Yolanda Mdogo wake wa kufikia aangue kicheko.
"Weee kipanya sitaki kuamini ulilala chini ya uvungu" Tasha aliongea huku akimvuta.
"Bryant Kobe kajua kukuweza....kubali kataa ila huwezi kuchomoka kwake, kila iitwayo leo utakuwa una fikiria kuhusu yeye"
"Kwahiyo unanilaani "
"Nakueleza ukweli tu kwa sababu macho yako yanaonesha kuchanganywa na penzi la Bryant Kobe "
"Penzi? wakati tunapelekeana moto ulikuepo? una uhakika gani kama Mimi na huyu mtu tulitumiana "
"Nimekusikia ukiongea "
"Nilikuchagua kuwa mdogo wangu wa hiari nikijua una uwezo wa kuvunga mambo yasiyo kuhusu sioni tabu kuuvunja undugu wetu" Tasha alitishia baada ya kuguswa kunako.
Kabla Yolanda hajajibu chochote simu yake iliita, ilikuwa ni namba mpya
Aliingiwa na uvivu wa kuipokea hivyo aliiacha ikaita mpaka ikakata.
Mpigaji hakuchoka, aliendelea kupiga simu tena.
Tasha aliipokea akiwa mwingi wa hasira lakini sauti ya Bryant Kobe ilimpoza
"Kwanini umeondoka bila kuniaga ulipaswa unisubirie kwanza nizione siku zangu, vipi kama nitakuwa mjamzito na wewe uko mbali? Hakika umenikosea sana " Aliongea bila kupumzika.
"Nimekumiss ...." Neno moja kutoka kwa Bryant Kobe lilitosha kumpoza moyo wake.
"Umenimiss ilihali umesafiri?"
"Endapo utanihitaji nitarudi... nitarudi hata kwa kukimbia "
"Kukimbia? kwanini ukimbie"
"Kwa sababu najali kuhusu wewe..... nakupenda, nipo tayari kuosha vyombo na kudeki endapo utaniagiza "
"Kama kweli una maanisha maneno yako naomba urudi na kamwe usije kuondoka bila ruhusa yangu " Tasha aliongea kisha akakata simu mapigo ya moyo wake yalikuwa yakidunda kupita kiasi, hakuamini kama ametangaziwa upendo.
Upande mwingine Zara akiwa chumbani kwake, mlango wake uligongwa
Alisimama akaenda kufungua, anaachia tabasamu baada ya kumuona Philips Kobe.
"Mvulana mkubwa (Bryant Kobe) aliachia Kampuni kwa hiari yake au ulimuomba wewe afanye hivyo"
Zara alimkumbatia Kijana wake kwanza, baada ya kuridhika alimkalisha kitandani.
Philips Kobe alifungua masikio yake kwa umakini kusikia ni kitu gani anataka kuambiwa.
ITAENDELEA.......
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni