*AAAAAASH BOSS ENZO 💍❤️* *SEHEMU YA 01 & 4
ANZA NAYO……
“Wewe sikiliza umu Ndani teshachoka kukulea sasa,
Kazi utaki kufanya, unataka kukaa tu, unataka tukulishe na kukuvisha Binti akili zako Zipo Sawa au ? Sasa Basi usiku wa Leo Utakuwa wa mwisho kwenye hii Nyumba, Yaani kesho utatafuta pa kwenda Nyumbani kwangu sikuitaji Tena nimekuchoka”
“Lakini ma mdogo”
“Hakuna cha lakini, usiku huu ni wa mwisho kwenye Nyumba yangu, labda Kama utakubali kufanya kazi ambazo nakutafutia la Sivyo, njia yako nyeupeeeeh, Yaani unasepa bila Fujo”
Ooooh yaaaaaah that me, najua wote mnajiuliza nimefikaje kwenye hiyo situation, na Nipo hapa kukusimulia kila kitu pasi na kuficha ata kitu kimoja, lakini Naomba nikuambie kitu, siku zote baraka ya mtu aiwezi kutoweka, zaidi inaweza ikachelewa tu lakini sio kupotea kabisa.
Call me Ishani, Mtoto wa Pekee kwa baba na mama yangu, kwa upande wangu Nimebahatika kulelewa na wazazi wangu wote wawili, lakini waswahili usema kisichokuwa riziki Basi akiliki.
Nikiwa na miaka 13 na nikiwa Mwanafunzi wa darasa la 7 baba yangu akaugua kwa muda mfupi sana na kupoteza maisha, na kujikuta nikibaki na mama yangu tu.
Kwa rehema za Mwenyezi Mungu nikamaliza darasa la 7 na moja kwa moja nikaanza kidato cha kwanza uku mama yangu akiwa ndio sapoti kwenye kila pande ya maisha yangu,
Guys am so proud of her 😊.
🥹Naomba niseme Kuwa dunia tunapita tu maana nilipokuwa kidato cha tano, mama yangu pia akafariki na kuniacha Mimi Mwenyewe.
Hapo ndio ukawa mwanzo Mpya wa maisha yangu, hapo ndio nilijua dunia adaa ulimwengu shujaa 💔🥹.
Baada ya kifo cha mama yangu, Ishani Mimi nikatolewa Mbeya kijijini na kupelekwa mjini Dar es salaam kwa mama yangu Mdogo, Yaani Nyumbani kwa Mdogo wake mama yangu.
Mama yangu Mdogo Bwana ni mwanamke ambaye Mungu amembariki sana, anamiliki duka kubwa sana la nguo mjini sinza,
Lakini pia mume wake ni mzungu, ambaye ana Pesa sana.
Mama yangu Mdogo amebarikiwa Mtoto mmoja wa kike ambaye yeye ni mkubwa kuliko Mimi anaitwa WENDY Yaani Mimi na mtoto wa mama yangu Mdogo tumepishana miaka miwili tu.
Mume wa ma mdogo, Mara nyingi uwa anakuwa nje ya nchi na uja Tanzania Mara moja moja sana.
Kitendo cha Mimi kwenda kwa
Mama Mdogo tu ndio nikageuka na Kuwa dada Yao wa kazi za Ndani, hiyo haikuwa shida, shida ni kwamba ma amekuwa ni mtu wa kunitesa sana, kunipiga, kuninyima chakula na kila kitu.
Ma mdogo ajawai kuniruhusu kutafuta kazi zaidi amekuwa akinitafutia wanaume na kutaka nilale nao ndio nipate kulipwa.
Kitu ninachoshukuru ni kwamba, Nimekuwa mtu wa kujiamini lakini pia kujitetea na wanaume wa ma mdogo hawakuwai ata kunigusa.
Kwa Sasa ma
Mdogo aniitaji Tena na ameamua kunifukuza.
TUENDELEE.
Katika usiku huo nilijitaidi sana kujielezea na kujitetea Kwa ma Mdogo lakini ilishindikana kabisa, ni wazi Kuwa ma Mdogo alikuwa amekusudia kunifukuza Nyumbani kwake na hakusubili ata kupambazuke usiku huo huo akanifukuza NYUMBANI kwake.
Unamjua mtu hopeless 😩 wewe ? Huyo ni Mimi sasa, Ndani ya muda mfupi tu nilijikuta nikilanda landa MTAANI uku nikiwa sina msaada wowote ule, si msaada tu, sikuwa ata na Mia mbovu kwa wakati huo kwenye jiji kubwa Kama ili la Dar es salaam.
Baada ya kuzunguka uku na uku kwa muda mrefu, ndipo nikakumbuka Kuwa, Nina Namba ya Rafiki yangu ambaye nilisomaga nae kijijini, lakini kwa hapa Dar yeye ni mwenyeji sana Maana ana miaka minne tangu afike Dar.
Pasi na kupoteza Muda nikampigia na hakuchukua muda mrefu akafika na kunichukua.
“Waooooh chumba chako ni kizuri sana Tusajigwe”
Nilimwambia baada ya kufika chumbani kwake, tusajigwe akaniangalia Kwa muda na kuniambia.
“Ilo tusajigwe limeishia Uko Uko Mbeya binti Sawa ? Hapa mjini najulikana Kama Tuntu”
Nilijikuta nikicheka na kumwambia.
“Sasa tuntu Ndio Jina gani ? “
“Ukikua utaacha, eeeh nambie na mabegi usiku huu Kama taraka nginja nginja ni nini binti ?”
Hapo nilijikuta nikianza kulia Walahi Maana kuna Namna ni Kama nilianza kusahau Kuwa nilipotoka nimefikuzwa 😂, hivyo tusajigwe ni Kama Ndio kanikumbusha.
“Ma Mdogo amenifukuza NYUMBANI kwake “
Tuntu akashusha pumzi nzito kisha akakaa kwenye kochi na kuniuliza.
“Shida nini ? Au umeanza jeuri nawe ?”
Nikaka kwenye kochi na kuanza kumsimulia Kila kitu ambacho kilikuwa kinaendelea nyumbani Kwa mama Yangu Mdogo.
“Kwahiyo Unataka kuniambia Kuwa mama yako Mdogo anauza wasichana pale nyumbani kwake isipokuwa binti yake tu ?”
“Ndio, na Mimi sitaki kabisa kufanya hiyo kazi, tusajigwe Rafiki yangu Naomba sana unistili hapa nyumbani kwangu”
Tusa akaniangalia kisha akakunja nne na kwa SAUTI ya kujiamini akanijibu.
“Kukaa NYUMBANI kwangu ni uongo mkubwa sana binti, Yaani uwezi kuishi hapa “
Kwanza nilishtuka sana na kumuangalia Tuntu kwa mshangao wa hali ya juu, uku akili yangu ikiniambia Kuwa Tuntu ni ananitania tu, hivyo nikaishia kucheka.
“Unahisi nakuchekesha eeeh! ? Sina huo muda wa kukuchesha, Ishani kitu usichokijua ni kwamba, hiyo kazi ambayo wewe unaikataa kwa herufi kubwa, Mimi mwenzio Ndio inaniweka mjini “
Alizungumza Tuntu uku akiwa amenikazia macho akisisitiza Maneno yake.
“Tuntu unajiuza ?”
“Na huyo mama yako Mdogo Ndio madam wangu, Ishani, Mimi bila huyo mama yako Mdogo Saa Hizi Sijui ningekuwa wapi, mama yako Mdogo amenisaidia sana Tena kupitia kazi hiyo hiyo ambayo wewe uitaki”
“Tuntu umeuza utu wako “
“Lakini nalala Ndani kwenye chumba kizuri, naishi na nakula ninachokitaka sio Kama wewe unayelandalanda usiku huu na mabegi”
Alizungumza Tuntu Tena kwa dharau ya hali ya juu.
“Sasa sikia, msaada wangu kwako, ni kukuacha ulale kwa usiku huu na kukipambazuka tu tafuta pa kwenda Maana nikikuacha wewe tu nitagombana na
Tajiri yangu aliyenionesha mji ukoje”
Walahi nilibaki sura ndogo Kama kidonge cha piliton.
Hatimaye asubuhi ikashika nafasi uku nikiwa sijapata ata lepe la usingizi usiku kucha.
Kweli cha kuazima si chako,
Majila ya sa MBILI asubuhi Tuntu akaniamsha na kuniambia niondoke msaada wake umeisha.
*******
Week nzima ilipita nikiwa nalanda landa tu mtaani, kwa wakati huo ata BEGI la nguo sikuwa nalo wahuni wa Dar walipita nalo kitambo sana. 😂🙌
Baada ya kuangaika sana mtaani, Ishani Mimi nikaamua kurudisha mpira kwa kipa, Yaani niliamua kurudi nyumbani kwa ma Mdogo na kukubaliana na sheria zake zote.
Ma Mdogo aalitumia mwezi mzima kunitengeneza na kuniandaa uku akihakikisha Kuwa nakuwa na muonekano mzuri sana, aaaah nisiwe Muongo Bwana, Mimi Mungu ameumba halafu mama akazaa, Niko vizuri kinyama.
“Kazi yako inaanza Leo Mteja wako atakuja Saa 3 usiku jiandae na usiniangushe “
Alizungumza ma Mdogo kisha akanipatia nguo Mpya na akaondoka zake.
“Huyu atogusa ata mwili wangu, na akinigusa tu napandissha mashetani”
Nilizungumza kimoyomoyo uku nikimuangalia kwenye kioo.
Hatimaye muda ulifika na moja kwa moja nikapelekwa kwenye chumba cha kazi, mtumeeeeh uso kwa uso nikakutana na……….
unataka kujua ni Nani ? Tukutane kwenye sehemu ya Pili
ITAENDELEA
SEHEMU YA 02
SONGA NAYO………
💍❤️💍❤️💍❤️💍❤️💍❤️
USO kwa uso ni kakutakana na mkaka ambaye si mgeni kwenye macho yangu na Nina mkumbuka vizuri sana, Yaani namkumbuka vizuri.
Iko hivi, Huyu kaka alishawai kuja Mara ya kwanza na nikamuigizia Kuwa Nina mashetani na sikuishia hapo Yaani hadi ku mng’ata nilimng’ata mbwa Huyu, halafu Leo amerudi Tena kwa Mara ya Pili.
“Mmmmh Huyu nikimuigizia Tena si atagundua ? Au anikumbuki sura ? Maana sasa hivi nimenawili sio Kama Mara ya kwanza alivyonikuta”
Nilijiuliza kimoyomoyo uku nikimuangalia kwa macho ya wasiwasi na nikiwa nimeshikilia mlango Sijui ni ufunge au niuache wazi.
Kwa Mwendo wa polepole kaka Yule akanisogelea na kisha akanipita na kwenda kufunga mlango, alikuwa akiniangalia kwa macho ya kunitamani sana ni Kama alikuwa bado ana hasira na Mimi hivi tangu siku ile nilipoweza kumng’ata.
“Vipi Leo mashetani yako mbali ? “
Mkaka huyo aliniuliza kwa SAUTI yenye kejeli sana Ndani yake.
Kiukweli mkaka alikuwa mzuri sana, handsome kuliko maelezo, ananukia vizuri na Pesa anaonekana Kuwa anayo, lakini Saa matendo yake Wala hayaendani na mambo yake anayoyafanya, Yaani anaishi maisha ya kihuni na hanasa.
Mkaka huyo akatembea taratibu na kwenda kukaa kwenye kitanda kisha akaniuliza.
“Kwahiyo Unataka nikufundishe Kila kitu ? “
Nikamuangalia kwa huzuni nikitaka anionee huruma lakini Ndio kwanza Kama nilijichomea utambi tu, kwa SAUTI ya kibabe akaniambia.
“Njoo uanze kazi yako binti sijaja kupiga Picha hapa “
Hapo nikashtuka na kumuuliza.
“Nani Mimi ?”
“Hapana naongea na hayo mashetani yako ya kuigiza, unajua siku ile kwajili ya ujinga wako nimepoteza Pesa kiasi gani ? Unajua nimeharibu Pesa ngapi ? Leo sitaki ujinga, sitaki upuuzi wa aina yoyote ile”
Nilimuangalia na kuzungumza kimoyomoyo.
“Muone kwanza, mkaka mzuri lakini ni msherati”
“Unataka nikufate Uko ulikosimama ?”
Akaniuliza kwa hasira sana.
“Aaaah, aaaah Hapana, am mkojo umenibana sana”
Nilianza kuzungumza Maneno ambayo ata Mimi sikuwa najua nazungumza kuhusu nini, Yaani nilikuwa Kama nimechanganyikiwa hivi 😂🙌.
“Sasa naelewa, wewe na Huyu madam wako, mnaniona Mimi Kama bwege na Ndio Maana mnanichezea hii michezo yenu ya kijinga Saa subili uone,
Leo maji utaita mma na hakuna mtu ataweza kuja kukusaidia “
Akanyanyuka pale kitandani haraka na kuja kunifata, hapo sasa
Ukaanza mchezo wa kuku na jogoo 😂🙌 Yaani tulijikuta tukikimbizana Ndani ya chumba Kama watoto wadogo 😂.
Mwanaume ni mwanaume tu jamani, kaka alinikamata akiwa na hasira ya hali ya juu kutokana na jinsi ambayo Nimekuwa nikimfanyia.
Kwanza nikashangaa sana akianza kuachana nguo zangu kwa hasira sana na sio kuzivua, baada ya muda nikajikuta nikiwa mtupu tu, Nikabaki kijitaidi kujificha kwa mikono yangu.
Kwa mwendo wa haraka akasogea na kuwashasabufa na akaweka SAUTI ya juu kabisa, SAUTI ambayo ata sisi ilikuwa tukioongea hatuelewani hao wa nje Ndio kabisa hawakuweza kusikia chochote zaidi ya mziki.
“Boss, subili kwanza, subili sasa nikuambie kitu”
Nililalamika baada ya mkaka huyo kunisukumia kitandani na kuanza kunifuata.
“We msichana wewe, wewe nitakupiga nikuchakaze Sawa? Me sio babu yako Sijui unanielewa ? Acha fujo zako me sina muda wa kupoteza”
Alizungumza kwa ukali sana kisha akanivamia mwilini.
“Polepole sijawai “
Nililopoka ikiwa ni sehemu ya kujitetea lakini pia Ndio ulikuwa ukweli wa mambo.
Mkaka huyo akacheka sana kisha akaniambia.
“Kahaba mzoefu na bikra ni vitu 9 tofauti”
Baada ya muda kaka akafanikiwa kufanya Jambo lake na kuna Namna nilimuona akiwa Mtulivu na mpole kuliko alivyokuwa mwanzo.
Kwa upande wangu nilibaki nikiwa nimekikunyata kwenye kona ya kitanda nikiugulia maumivu ya mwili wangu, lakini pia maumivu ya moyo baada ya kupoteza usichana wangu kwa njia ya hovyo sana baada ya kuitunza kwa muda mrefu.
“Am sorry”😔
Alizungumza mkaka huyo kwa sauti ya chini sana na yenye majuto Ndani yake.
“Can you just leave ?”
Nilimuomba aweze kuondoka tu, mkaka huyo akaniangalia kisha akavaa mavazi yake na kuondoka.
Kwa upande wangu Walahi ni Kama Chizi aliachiwa jalala vile, nilijikuta nikilia kwa SAUTI kubwa sana, SAUTI yenye maumivu ya hali ya juu, nilijikuta nikikumbuka mpaka wazazi wangu kutokana na haya maisha ambayo nayapitia kwakuwa tu wao Hawapo kwenye uso wa dunia.
Baada ya muda ma
Mdogo akaingia.
“Kwani wewe utoki umu Ndani au ? Ebu nyanyuka tuweke chumba Sawa msichana mwenzio aingie na Mteja wake”
Alizungumza ma Mdogo uku akionesha kutokujali kuhusu Mimi ata kidogo.
Nilinyanyuka kwa kujivuta vuta uku nikitoa na mashuka ambayo yalichafuka kwa damu.
“Eeeeeeeh Makubwa haya, Ishani usiniambie Kuwa wewe ulikuwa bado mbichi ?”
Alizungumza ma Mdogo kwa mshangao uku akinikejeli.
“Sasa ulikuwa unamtunzia Nani ? Kwani ulikuwa na ndoto za Kuwa sister mtawa au kuolewa ? Yaani umeharibu mambo Mwanangu, Yaani ungeniambia mapema Kuwa ujawai, Huyu mbwa ningemuongezea bei jamani khaaah”
Imagine anayezungumza hivyo ni mama yangu Mdogo kabisa Tena amelelewa na mama yangu Mimi baba ya mama Yao kufariki hey akiwa na miezi mine tu, halafu Leo hii ananifanyia Mimi ujinga Kama huu 🥹.
Basi nikajizoa zoa pale kwenda chumbani kwangu.
**********
Siku zikaendelea kwenda na kazi yangu Ndio ikawa ni hiyo, Yaani Leo Niko na mwanaume Huyu kesho Nina Huyu, Kiukweli nilijikuta nikiwa mzoefu sana Tena sana, niliacha kulalamika na kuamini Kuwa hayo Ndio
Maisha yangu sasa.
Hatimaye miezi 3 ikapita nikiwa Bize na kazi yangu Hiyo, Yaani Sijui niwambie nini lakini Ishani wenu Nimekuwa mbobezi kwenye hii kazi siogopi Dudu Wala Mende.
Ikiwa ni siku ya jumamosi jioni, siku hiyo madam akaniambia Kuwa Nina Mteja wa muhimu sana hivyo nikupatie huduma ya kueleweka Maana yeye ni VIP, Kama
Kawaida muda upofika tu nikaenda kwenye chumba cha kazi, na kwa Mara nyingine Tena nikakutana na mkaka ambaye Ndio alifungua fungua njia, siku hiyo nilikuwa wa tofauti sana, nilikuwa Nina tabasamu pana sana usoni mwangu, halafu nimechachuka Kama samaki aliyewelewa ndimu na Ka chumvi.
Polepole nikasogelea sabufa na kuliwasha ingawa sikuweka SAUTI ya juu sana lakini mtu wa nje ilikuwa sio rahisi kusikia.
Kwa mwendo wa madaha na mahaba mazito nikamsogelea mkaka huyo na kuanza kazi yangu.
“Sijajia Ilo Kwahiyo acha”
Alizungumza mkaka huyo muda ambao Ndio nilikuwa nataka kumtoa nguo zake.
“Umekuja kupiga Picha au kunishanga ?”
Nilimuuliza nikiwa nimemkazia macho.
“Hapana Nimekuja kuzungumza na wewe, by the way am ENZO Sijui mwenzangu unaitwa Nani ?”
Nikamuangalia kwa kumpandisha na kumshusha kisha nikamuuliza.
“Unatengeneza nida au vyeti vya kuzaliwa ?”
“Please nitaji kukujua lakini pia kukusaidia, ni wazi Kuwa hii sehemu sio kwajili yako, imani yangu inaniambia Kuwa unaitaji kuaidika”
Nikamuangalia na kumwambia.
“Broh si Umelipia Pesa kule ? Sasa Basi tusichoshane fanya kilichokuleta na uwende “
Nilizungumza kisha nikamvamia mwilini mwake, kak huyo akanisukuma na Kwa mwendo wa haraka akafungua mlango na kuondoka ?
JE NI KWELI ENZO ANATAKA KUNISAIDIA ?
ITAENDELEA
SEHEMU YA 03
ANZA NAYO………
💍❤️💍❤️💍❤️💍❤️💍❤️
Kwanza nilibaki nikishangaa uku nikiwa siamini kabisa Kama Kweli Huyu kaka amelipia Pesa nyingi sana lakini ata kunigusa ajanigusa zaidi ameondoka akiwa na hasira tu, Tena hasira ya Mimi kukataa kuzungumza nae.
“Atajua Mwenyewe”
Nilizungumza na kunyanyuka kwaajili ya kutandika kitanda vizuri, muda huo huo ma Mdogo akaingia akiwa na hasira sana.
“Mteja wangu umemfanya nini ? Mbona ameondoka kwa hasira sana?”
Nilimuangalia ma Mdogo kwa muda kisha nikamdanganya.
“Amepokea simu ya msiba, me sijamfanya chochote”
“Una Bahati Yaani leo Sijui ningekufanya kitu gani we binti wewe”
Ma Mdogo alimaliza kuzungumza Maneno yake kisha akatoka nje.
“Ila huyu mwanamke kuna siku nitamuonesha show moja hiyo atokuja kuamini kwenye maisha yake”
Nilizungumza nikiwa na hasira sana.
Baada ya kuweka chumba vizuri, polepole nikarudi chumbani kwangu, Ile Naingia tu chumbani kwangu nikakutana na Wendy, Yaani Mtoto wa mama yangu Mdogo.
Huyu msichana na mimi hatukuwai kuelewana ata siku moja, Ka binti kanajisikia sana aka, hivyo baada ya kumkuta chumbani kwani Wala sikuwa na muda nae, moja kwa moja nikasogelea kabati na kutoa taulo yangu nikiwa nataka kwenda kuoga.
“Ina Maana ujaniona au ?”
Wendy aliniuliza uku akiniangalia kwa dharau.
“Kwahiyo baada ya kukuona ulitaka nije kukubeba au ?”
Nilimuuliza.
“Ishani umekuwa jeuri sana sasa hivi, naona Uko kupendeza kwako Saa hivi kunakupatia jeuri ya hali ya juu, anyway sijajia hayo, nguo zangu chafu zinakuwa nyingi sana hivyo Basi nataka ukafue sasa hivi”
Alizungumza Wendy.
My zangu ni Kweli nilikuwa namfulia Wendy lakini Saa hivi Walahi atanitafuta kwa tochi.
Nilimuangalia Wendy kwa muda kisha nikamuuliza.
“Ulikuwa unavaa na Mimi hizo nguo au ? Nitolee upuuzi wako hapa”
Nilijibu kisha huyo nikaenda zangu bafuni kuoga.
Nilioga na nilipotoka tu nikakutana uso kwa uso na ma mdogo akiwa na binti yake wananiangalia Kama wanataka kunimeza vile.
“Kwahiyo Ishani umefikia hatua ya kumpiga binti yangu ?”
Ma Mdogo aliniuliza, kwa haraka nikamgeukia Wendy na kumuuliza.
“Nimekupiga ? “
Kuna Namna Wendy aliona kabisa Huyu sasa hivi aogopi mtu, kwa upole akaangalia chini na kuzungumza.
“Ajanipiga ila ataki kunifulia nguo zangu”
“Usijali kesho nitamuita dobi aje kukufulia”
Alizungumza ma mdogo, kisha Wendy akatoka nje na mama yake akanigeukia Mimi.
“Jiandae kuna Mteja chumbani, halafu ukitoka Uko njoo Nina mazungumzo na wewe”
Sikumjibu kitu chochote zaidi nikajianda kwaajili ya kwenda kumuhudumia huyo Mteja.
Lahaulaaaaaaaah!!😳 ata Kama Ndio Mteja Huyu Hapana kwakweli 😏 Yaani sio MZEE Ila ni kababu 😂🙌 kwanza niliganda nikimshangaa tu.
“Ooooh you are so beautiful 😍 “
Alizungumza MZEE huyo baada ya kuniona.
Mtumeeeeeeeeh ata meno hana Huyu MZEE jamani 😂 Nikamuangalia na kumuuliza.
“Umeshaacha barua ya milasi nyumbani kwako ?”
MZEE huyo akashtuka na kuniuliza.
“Unamaanisha nini unavyosema hivyo ?”
“Wewe MZEE Wewe Unataka kunipa dhambi tu, umri huo Unataka kucheza hii michezo si unafia hapa wewe, sikia me siwezi kukuhudumia, changanya hiyo miguu yako, nenda kadai Pesa yako na uende”
Nilizungumza kisha moja kwa
Moja nikatoka zangu nje, ata Kama Ndio kazi, siwezi kulala na MZEE ambaye mama yangu anaweza kumuita babu na sio baba.
Baada ya muda Kama Kawaida moto ukawaka, ma Mdogo alichukia sana baada ya MZEE Yule kwenda kudai Pesa zake na kuondoka akiwa amechukia sana.
“Ishani Unataka kunipanda kichwani si Ndio ?”
Ma Mdogo aliniuliza akiwa na hasira sana baada ya kumpotezea Mteja wake wa kizee.
“Aaah ma Mdogo hivi hii ni roho gani mbaya ambayo unayo ? Nafanya kazi kubwa halafu unipatii Pesa ata kidogo kwakuwa tu nakaa nyumbani kwako halafu Leo hii unaniletea kizee ambacho kimeshajifia kitambo kabisa, Hapana kwakweli , Kama ni rahisi Kwanini usiende wewe au Wendy ?”
Weeeeh hapo ma Mdogo akachukia sana na akanyanyua mkono wake na kunipiga kibao.
Yaani katika siku ma Mdogo amejichanganya basi ni Leo 😏 Yaani Leo amekanyaga waya wa umeme akiwa peku.
Nilishachoshwa na Kila kitu hivyo, si kufikilia Mara MBILI MBILI, nilijikuta nikimvamia ma Mdogo na tukaanza kupigana, mkubwa ni mkubwa tu, kuna Namna ma
Mdogo alinishinda nguvu, na kwaajili ya kujitetea Mimi Mwenyewe, nikaokota chupa ya soda na kumtandika nayo kichwani mwake.
Ma mdogo hakuchukua muda mrefu akadondoka chini na kupoteza fahamu uku damu zikimtililika tu.
“Huu msala huu “
Nilizungumza kimoyomoyo uku nikiwa na wasiwasi sana, haraka nikachukua BEGI la nguo na kupakia nguo zangu, sikuishia hapo, nikamsachi ma Mdogo na kuchukua Pesa ambayo alikuwa nayo kisha nikaondoka uku Lengo langu likiwa ni kurudi tu Mbeya Maana yooooh huu ni msala mkubwa sana Kwa upande wangu.
Sasa katika hekaheka za kukimbia na ile wasiwasi ambayo nilikuwa nayo, nilijikuta nikivuka barabara pasi na kuangalia, ata Sijui gari lilitokea upande gani lakini lilinigonga kwa nguvu sana.
Chapter 4
ANZA NAYO
Baada ya hapo Wala sikujua ni kitu gani kilitokea Maana nilikuja kuamka nikiwa kwenye chumba cha hospital, kichwani nikiwa na bandage, na dripu ya maji iliendelea kushuka mwilini mwangu
kwa kupita kwenye mkono wangu.
Lakini pia pembeni yangu, alikuwako mwanamama wa umri wa makamo, alikuwa amevalia nguo na vito vya thamani sana, mwanamama huyo, kwa wakati huo alikuwa amepitiwa na usingizi kiasi.
"Ashih"
Nililalamika baada ya kusikia maumivu makali sana ya kichwa.
Polepole na kwa uchovu wa hali ya juu, mama yule akafungua macho yake, ni wazi Kuwa aliweza kusikia SAUTI yangu kwa wakati huo
"Ooh thanks God umeamka"
Aizungumza mwanamama huyo akiwa amefungamanisha mikono yake, baada ya kuniona Kuwa nimeamka.
Nilibaki nilimuangalia tu mwisho nikataka kunyanyuka ili niweze kukaa kitako.
"Usinyanyuke Tulia kwanza nimuite Dokta Alizungumza mama huyo
Kisha akanyanyuka na kutoka nje.
Kwa upande wangu nilibaki nikishangaa na kujiuliza ilikuwaje? Nimefikaje na vipi kuhusu vitu vyangu, Maana nilijitaldi kuangaza macho
yangu uku na uku na sikuweza kuona ata BEGI yangu ya nguo Wala ata viatu tu ambavyo nilikuwa nimevaa.
Baada ya muda mwanamama Yule akarudi akiwa ameongozana na daktari.
"Ah kwa Sasa anaendelea vizuri kabisa, Nafikill kwa Leo tutabaki tukitazamia hali yake na kesho
tunaweza tukaruhusu uweze kwenda nae"
Alizungumza Dokta baada ya kuniangalia vizuri.
"Asante sana Dokta
Alijibu mama Yule akionekana Kuwa ni Mwenye
Furaha sana
Baada ya muda Dokta akatoka nje na kuniacha
Mimi nikiwa na mwanamke huyo ambaye sikuwa nikimfahamu kabisa, lakini alionesha kujali Sana kuhusu Mimi.
"Hellow, naitwa madam Glory Sijul wewe unaitwa Nani?"
Aliniuliza mwanamke huyo
"Haya sasa mambo ya madam yameanza Yaani Dar kila mtu mzima ni madam"
Nilizungumza kimoyomoyo nikiwa nimemkazia macho
"Umenisikia?"
Aliniuliza madam glory baada ya kuona Kuwa
nipo Kimya.
"Nimekusikia naitwa Ishani, hapa nimefikaje ?
Nilimuuliza.
"Aaah Mimi Ndio nilikuleta hapa hospital, baada ya kukukuta barabarani ukiwa umetelekezwa na mtu ambaye alikusababishia
njali
Kwanza Nikamuangalia kwa muda uku nikiwa siamini kabisa Maneno yake Maana ni Kama. alikuwa akinidanganya kwa kiasi chake.
"Asante sana kwa kunisaidia
Nilimshukuru tu ingawaje moyo wangu bado ulikuwa hauja kubaliana kabisa na maelezo
yake
"Eeeeh Una Namba ya ndugu zako tunaweza
kuwasiliana nao wakaja?"
"Sina ndugu
Nilijibu nikiwa serious sana.
"Unataka kusema Kuwa hapa jijini hauna ndugu
kabisa?"
Nikamuangalia na kumjibu.
"Ndio na sio tu jijiji ata Uko nilikotoka sina ndugu
Mmama wa watu akashusha Pumzi Ndefu na kuzungumza.
"Ni siku nne Saa naangaika na wewe hapa hospital mambo yangu yote yamesimama, Ishanii unaishi wapi?"
Nikawa za na kuwazua kwa haraka Sana kisha
niliamua kumdanganya.
"Siku ambayo nilipata ajali Ndio siku ambayo niliingia Dar es salaam kwaajili ya kutafuta
maisha
Mama
watu akahisi kuchoka kabisa na pasi
na kuzungumza kitu chochote kile, akatoka nje na kuniacha nikiwa Mwenyewe pale wodini.
Siku iliyofuata, niliweza kutuhusiwa kutoka
hospital na moja kwa moja huyo mama akonichukua akiwa ajaniambia kitu chochote
kile
Kiukweli moyo wangu ulijikuta ukiwa na wasiwasi sana, kuna Namna nilikosa amani kabisa.
"Samahani madam Groly Tunaenda wapi?"
Nilimuuliza tu, muda huo Mimi na madam Groly
tulikuwa kwenye gari moja Kali sana, na ilikuwa Ikiendeshwa na pande la mtu, Yaani kaka alijazia
kila kona
"Nakupeleka NYUMBANI kwangu, since umesema Kuwa hauna ndugu na hauna sehemu
ya kukaa
"Asante sana Mungu akubariki
Nilimahukuru Tu uku moyo wangu bado ukiendelea kujiuliza je huyu ni mtu Mwema kweli
au Ndio yaleyale ya ma Mdogo, kujifanya Mwema kumbe ana matumizi na wewe.
My zangu, kuna watu wanaishi halafu kuna sisi
hapa tunaishia, nyieeeh huu mjumba wa huyu mmama ni hatari na nusu woililih,
"Hii Nyumba au ikulu Mungu wangu si unachunwa ngozi na hakuna mtu anasikia"
Nilijisemesha Mwenyewe tu kimoyormaya, kutokana na wasiwasi mkubwa sana ambao
nilikuwa nao, Nilijiuliza hayo, kipindi ambacho gar Ndio ilikuwa inaingia kwenye geti
"Karibu sana Ishani jisikie Uko NYUMBANI"
"Asante sana ma"
Baada ya muda tukashuka kwenye gari tayali
kwaajili ya kuingia Ndani, nilibaki nikishangaa mazingira mazuri na magari ya kifahari ambayo
yalikuwa yamepangwa kwenye Nyumba hiyo.
Hivi mwanzo Nilimwambia Kuwa ma Mdogo Ana maisha mazuri ? Ebu futeni Bwana nilikoses,
madam Groly ni mwamba na nusu Ebu kwa pamoja tuseme igweeeha kwajili ya utajili anaomiliki madam glory woiiiih.
Ishan
Aliniita madam glory baada ya kuniona nikiwa nimeganda nikishangaa ukubwa na uzuri wa
Nyumba yake
"Twende Ndani
Hapo nikajishtukia na kwa aibu ya hali ya juu nikaingia Ndani, Ndani nako Ndio usisene nyie watu wanamiliki vitu vya thamani kubwa sana.
"Ma Zena, ma zena"
Mama aliita kwa Sauti ya juu wakati huo Mimi na yeye tulikuwa tumesimama tu sebuleni.
Baada ya muda akaingia mwanamke Fulani hivi ambaye kwa makadilio alikuwa anafikia miaka
40 hivi
"Karibu madam"
Alizungumza mwanamke
Huyu niliyemfahamu kwa Jina la mama zena.
"
Asante, Huyu anaitwa ishanii ni mgeni wetu, kwa sasa mpeleke kwenye chumba cha juu
apate kupumzika, wakati Ana Pumzika utamuandalia smooth na mtoli wa ndizi
Alizungumza madam Groly kisha akaondoka pasi na kusubili jibu kutoka kwa mama zena.
"Nifuate"
Alizungumza mama zena kisha akashika njia
Nami nikamfuata.
Kiukweli nilikuwa Nina uchovu wa hali ya juu hivyo. Nilijikuta nikilala Sana Tena ukizingatia chumba chenyewe ni full kiyoyozi Ndio kabisa.
Nilikuja kuamka muda ambao Giza lilikuwa
limeshaingia na sikuwa najua ni Saa ngapi, kwa utulivu kabisa nikanyanyuka na kutoka nje lengo langu likiwa ni kwenda kupata maji ya kunywa.
Katika pitapita zangu za uku na uku, kwenye
moja ya chumba, niliweza kusikia maongezi
ambayo yalikuwa ya Siri sana, lakini maongezi
hayo yalinilenga sana Mimi.
JE NINI KITAENDELEAAA!! "
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni