πππ’ π‘π π π₯ππ ππ’ πͺπ π§πππ§π’π ___________________________________ SEHEMU YA 20 ENDELEA....... "Twende tukale hotelini....
"Mume wangu mtarajiwa jiandae kuhudhuria hotelini nadhani unajua Mimi ni mtu wa mishemishe sijui hata imeku...." Kabla hata Tasha hajamaliza maneno yake alidakwa kwa romance lililobeba hisia.
Kila alipo furukuta ajitoe haikuwezekana, mwisho wa siku alitulia tuli.
Basi Yolanda akiwa anakuja zake jikoni aangalie chakula kilicho salia alishtuka baada ya kuwafuma watu wakibadilishana mate.
Bila kupoteza muda aliwapiga picha kisha akatupia mtandaoni.
"Hatimaye Mrembo wa Tiktok kapata Mume atakaye saidiana naye kuosha vyombo "
Picha ilisambaa kwa haraka sana mtandaoni, yaani ilikuwa ni mwendo wa kufowadiana tu.
Secretary Annie alimtumia Zara, alipoona hajibiwi na huku yuko online alipiga simu kabisa.
"Boss mwenyewe umejionea au nirudie kukutumia tena"
"Kuanzia sasa na kuendelea fanya kazi yako kama Secretary, iwe mwanzo na mwisho kunipigia simu na kunieleza umbeya wa aina yoyote ile. Kwa kipindi chote hicho nilikuwa tu na kuchunguza sijawahi kuwa mshirika wako na wala sitakuja kuwa mshirika wako " Zara alimjibu makavu kisha akakata simu.
Secretary Annie hakuamini kabisa majibu aliyopatiwa, kuna kitu aliamini hakipo sawa aligeuka huku na kule aone kama kuna watu. Baada ya kujipata yuko pekee yake alihisi amani ndani ya moyo wake.
Tasha na Bryant Kobe walijikuta wakiongea vitu serious kuhusu mahusiano yao.
Walikubaliana kuoana haraka iwezekanavyo, kuhusu mapungufu madogo dogo waliafikiana kuya sahihisha tararibu.
"Pindi harusi yako itakapoisha nitaenda zake Newyork nimekaa kule kwa muda mrefu sasa hivyo nazielewa kona zote" Philips Kobe aliongea akiwa ana mpunguza nywele Kaka yake.
"Kwanini unaondoka ghafla namna hiyo "
"Natamani kuitwa Mume wa mtu pia...nadhani unaelewa napendelea watu wenye tabia za kizungu, itapendeza zaidi kama nitaenda kuwafuata huko huko " Philips Kobe aliongea.
"Nimewahi kuiona namba yako kwenye simu ya Tasha, vipi umewahi kumpenda pia "
"Nilitaka kumuweka karibu kwa ajili yako, sikuwa na nia nyingine...nyie wawili mnaendana sana tofauti yenu ni kidogo tu kama mtakaa pamoja naamini mtaenda zaidi " Philips Kobe aliruka mita mia.
Kwa kipindi chote hiki Zara alikuwa mpole sana...... watoto wake hawakuta kumuuliza chochote kwa sababu waliamini kama watafanya hivi basi wangemchanganya zaidi.
Harusi ya Bryant Kobe na Tasha ilikuwa ya kawaida sana tofauti na watu walivyokuwa wanafikiria.
Watu wengi walihisi Bryant Kobe atakuwa Mtumwa wa ndoa yake lakini haikuwa hivyo Tasha hakuwa akipenda uchafu hivyo mara kwa mara alifua, alideki na aliiosha vyombo. Bryant Kobe si mlaji sana ukilinganisha na mkewe hivyo muda wote Tasha alikaa jikoni yaani njaa ndio zilimfanya ashike usukani.
Hatimaye wakati wa kujifungua ulifika, alifanikiwa kupata Mtoto wa kike.
Sia alikuwa kilizi asikuambie mtu....
"Ni jukumu lako kuhakikisha mtoto halii pia....kama hautanisaidia leo nitamuacha alie kashiba huyu, yaani kama ni kunyonyesha nimempa nyonyo mpaka nasikia chuchu zinauma"
"Basi kama kashiba muache alie atakuwa sawa nimechoka eh "
Basi Tasha alikausha pia Mtoto aliendelea kulia wee, siku zote huwa ni mtihani kwake kulala kama kuna kelele. Tofauti na Bryant Kobe yeye alikoroma kelele huwa hazimnyimi usingizi hata kidogo.
"Nimepatikana Mwanaume huyu ni ji....bwa lenye kiburi " Tasha alimchukua mtoto kisha akaanza kubembeleza
Basi kwenye akaunti yake Tiktok watu wengi walimpa hongera ya kuolewa. Lakini mara kwa mara waliuliza kama Mumewe anamsaidia kufanya usafi na kupika.
Mume wangu Mimi ni Mzungu, anafanya kazi zote kwa sababu anajua Mwanamke si mtumwa wa ndoa.
Tasha alijibu hivi mtandaoni lakini kiuhalisia Bryant Kobe hakuwa akifanya chochote.
Asubuhi moja aliamka akiwa kachoka kupita kiasi, aliachia tabasamu baada ya kukuta kazi zote zimefanyika.
Tabasamu lilitoweka usoni mwake baada ya kugundua Zara ndio kafanya kazi zote.
"Vipi Wanaume wanafanya kazi au kazi zina kufanya wewe " Zara aliuliza.
"Hiyo comment yako nitumie kwenye mafundisho yangu "
"Philips Kobe anawasalimia nadhani tutasherekea naye mwaka mpya, huna haja ya kumueleza Bryant Kobe kama nilikuwa hapa " Zara aliongea kisha akaondoka.
Basi mwaka mpya ulipowadia, familia ya Tasha pamoja na Bryant Kobe walikusanyika kipamoja. Vinywaji viliwekwa mezani pamoja na chakula.
Philips Kobe alikuwa kapendeza sana pamoja na mchumba wake.
Secretary Annie akiwa pia na mchumba wake walipendeza. Yolanda pekee ndio hakuwa na mahusiano hivyo alikuwa na kazi ya kulea mtoto.
Kwa pamoja waligonga cheers huku wakitakiana mema.
Huu ndio mwisho wa CEO na Mrembo wa Tiktok π₯.......
.............MWISHO π............
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni