MY WANGU❤️ sehemu ya 116 na 117
Mlige akanambia sikia sio kila wanachosema wazazi wnapatia. Nooo kma mama yako amesema anakupa radhi. Ukiludiana na mm ata mm mama yangu kanambia hivyo hivyo. Lakin faridah mi bila wewe nashindwa. Unazani mi napenda kusaliti ndoa. Hapana faridah. Nashindwa kila nnaposikia habari zake. Nashindwa nnapokuona .naomba sana tusifatishe wazazi. Na naomba sana usitoe mimba yani ukitoa mimba yangu faridah .sijuh ntakufanya nn. Na safari hiii mimi wala sitakusamehe . Mh mimi nikawa nalia mana ata mimi bwana namtaka na nampenda sana tu. Ila sasa mazingira ni magumu . Nikawa nalia. Mlige akanambia kuwa makini na ujauzito wangu. Lia unavyitaka ila ikitoka iyo mimba utanibeba nakwambia. Kisha uyoo akafungua mlango akaondoka ndo na mama anaingia chumbani kwangu.
Mama akanmbia yani nakwambiaje uyo mlige wako ntampeleka polisi na ntampigia bab yako kumuelezea uhu uchafu wako mjinga ww. Mie nikawa nalia tu. Heee nashika simu nakuta matusi jamani ni yanatoka kwa mama mlige na kwa yusta . Mbona nilikoma mimi. Yani sikuwa swa kabisaaa. Nikazima na simu tu. Basi zikapita siku 3 sijawasha simu na mama kaninunia. Na hizo siku 3 zote ambazo sipatikani mlige anakuja nyumbani anaingia kinguvu . Et anakuja kuniona.yani hajali kuhusu watu kabisa. Mi mpaaka nikawa namkattaza kwamba sio sawa. Hataki kunielewa .namjua nikajua apa anapelekwa na hasira na ujeuri wake. Basi ndo ikawa hivyo. Siku iyo kaja nakwambia mama yangu kamwambia ondkka usingiiee kwa farida. Loooh kama hamsikii kaingia chumbni kwangu. Kisha kafunga mlango. Mie nilikuw nimelala.mpaka nimeamka. Namsikia mama ana bwata kweli kwi. Mlige akatoa simu akanipa. Akanmbia mi siwez kulala sijajua hali yako na ya mtoto wangu tumboni. So chukua hii simu nishaweka na laini kila kitu . Tutakuwa tunawasiliana umo. Mie nikasema sawa . Hakukaaa sana akaondoka. Nyieee mlige jeuri.sijapata kuona
Basi ayo ndo yakawa maisha yangu. Sijuh yusta akiamua kuja kutukan kwetu na mama yake . Sie tunafunga mlango ndani. Watachamba apo kwrli kweli. Et wanamuita mama yangu mwanga. Na mie mwanag tunamloga mligee. Basi mama analia tu. Mie nabaki kimya ata cha kufanya sina. Ata road nikawa siendi mana habari ni zangu tu. Mh sikuwa naenda kabisaa. Basi apo mlige yeye ananipigia simu tunaongea .japo sina raha nae sasa. Na pesa ananitumia na kashanambia . Jiwazishe jilize. Jione una matatizo sana. Ila iyo mimba ikitoka utanibeba. Mi nafanyaje sasa. Basi napambana na tumbo languu. Mpaka matusi nikawa nishazoea sasa. Nikalea mimba mpak ikafika miez 7 . Apo mlige anatka mpaka tuonane hatki kuelewa. Ni mm ndo namkatalia nilimwambia tu tuzae na tuleee basi . Ila aendelee na mkeo. Mlige wala hakunijibu. Ila siku akiamua kuja hakuna cha kuomba ruksa wala nn. Anakuja. Na yusta akaacha kuja kunifanyia fujo nyumbani sijuh alimpiga mikwara ataa sielew
Basi ikawa hivyo yani. Mi nikawa nalea sasa tumbo lake. Yani ni ndani tu . Nikienda road kwa emergency sanaa. Basi siku iyo nipo nyumbani. Mlige kaja. Mh ana ata kusema.nakuja uyu baba. Mama yangu akawa ata salamu za mlige hataki. Ila mlige hajali . Mi.nikainua nikaingia chumbani na yye akaja . Nikakaa kitandani. Nikamuuliza vp mbona leo sahizi. Mana kaja usiku. Akanmbia ahaaaa mi najisikia kulala na wewe leo. Mh uyu baba mbona ana shida lakini. Nikamuuliza wewe una nn . Huoni kama tunaandamwa na tuna majanga mlige . Ebu nenda bwana..ahaaa mi apa hunitoi yani siondoki . Kma hutaki nilale apa jiandae tukalale njeee. Khaaaa . Na mtumbo wa miez 7 . Anataka kunisumbua. Nikamwambia we huoni hali yangu mlige . Mi sitaki presha now ebu niache nipumzike. Akanambia sawa kwani mi naenda kukuchosha noo . Mi nimekumisss nataka tukalale wote . Nataka kusikia joto la mwanangu. Mh nikamwambia hapana mama hataniruhusu. Mh basi akanambia swa et kanikalisha hataki kuondoka .nyoeee uyu baba
Mi nikamwambia ondoka kwako bwana. Et usinipagie bwana. Basi kajikalisha mpka saa 7 mama ndo kaja kumfukuza ndo kalizika🤣🤣🤣🤣🙌🙌🙌. Et aya bwana naondoka watu washaanza kunifukuza. Mpaka nikawa nacheka. Ndo uyoo anaondoka. Ndo ikawa hivyo . Siku anakuja ndani anajifungia mpaka saa 8 za usiku. Mpaka afukuzwe na mama. Ndo ananiaga anaondoka. Siku iyo nipo na mama . Mama akawa ananingalia sana. Mpaka nikawa najistukia mama akaniuliza we yule baba umempa nini kwani. Mie kimya. Mama aknmbia au umemroga kweli mlige ww. Mbona unampelekesha yule baba eeeh. Mie nikasema jamni mam hadi wewe unaona mie mchawi . Sijamfanya kitu. Mama akasema hapana sio kwa kukupenda uku. Ata kama ndo tuseme we mtoto mdogo mbichi. Mbona yusta nae mbichi. Khaaa . Mi akij ap namfukuza nakwambia sitaki mabaalaa. Mie nikajinyamazia . Kwanza uyo mlige mwenyewe mnazani anakubali kufukuzika bila ya kuniona sio kweli.
Basi mie nikalea mimba mpaka miez 8. Apo nikimuona yust namkwepa naogopa kupigwa shoga yenu. Siju iyo sasa ilikuwa ni mida ya mchana . Rahul ametoka shule . Akanisalimia nikamuitikia. Akambia mama mi sitaki ugali leo nataka chipsi kuku lleo na mayai. Loooh . Nikamwambia koma usinihalibie bajeti zangu . Ugaki ule bibi kakufunikia .et sitaki mimi mama mwambi baba elly anitumie hela. Nikamwmabia nyoooi ukome kushobka na mababa wa wenzio. Toka apaa. Akanuna akajibanza pembezoni mwa mlango et kanuna.. ila nikajisikia vibaya na pesa nnayo . Kwa nn mwanagu asile alichokitaka. Nikamwambia aya nyanyuka twendeee ukale unachokitaka. Mjinga wewe. Ndo iwe mwisho leo kunipangia cha kukila. Basi mwanangu akafurahi mnooo nakwambia . Akakenua uyoooo
Bibi mie nikainuka. Kujikokota tu. Mana mtumbo ule kule. Basi nikamshika mwanagu tukaend mpka wanapouza chipsi bala balani kabisa. Akagiza anachokitaka nkwambia. Namwambia vizur yule muuza chipss. Eka mayai mengi umo🤣🤣🤣🤣🤣🤣🙌🙌🙌 mama yangu atalipa. Nyiee uyu mwarabu koko ana visaa. Aseeee tupo pale tunasubir chips nikastuka nnaitwa na sauti ambayo naijua vizuri sana. Nikageuka haraka nyieeeee nilistuka ssna namuona zayd pale . Mh nikamshika mwanangu mkono vizur haraka. Zayd akanambia woow una mimba sasa. Umependeza sana . Umekuwa mrembo kweli kweli na mimba imekupenda. Nikasema we zayd unataka nn . Ebu achana na mimi. Akanmbia unazani nimekufat wwewr. Nooo . Nimefata damu yangu ya kiarabu. Huwa haiendi mbali kabisaa. Nipe mwanangu we uendelee kufanya umaraya wako . Weeeee . Nikamwambia mpumbavu ww. Ukitaka kumchukua uyu mtoto labda kwanza mm nife ndo ntakupa uyu. Yani kwanza niue mm. Kisha nakupa mwanangu. Weeeee namjua michezo yake uyu . Akanihalibie mtoto thubutu
Weee akaanza kunivutaaa . Et amchukue mwanagu nilimbana rahuli. Yani nilisema uyu laba atoke na mkono. Ila mwili ni wangu. Rahul akawa analia si anaumia tunamvuta . Aseeee hana ata huruma. Anamvuta tu mtoto. Mi naona mwanagu anakia anambia mma mkono ananitoa naumia mama. Weee alfu mwanangu alivunjika mkono mi nikamuachia nakwambi. Uku nalia pale. Akamvuta upnde wake mtoto akanmbia hautkaaa ukamuona mwanangu tena. Naondoka nae uyu. Nikajua uyu ataenda kumfanua shiga mwananagu. Ile anataka kugeuka. Mh kakutana na mligeee. Nyieeeee mlige akamuuliza uyu mtoto unampeleka wapi zayd?
🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni