β€οΈβ€οΈ SHEMEJI INAUMA LAKINI TAMUπ Sehemu ya pili π Mke wangu niambie maiko ni nani mbona unalia unamtaje yeye?. " Ni bwana....π
Bwanaππ.
( Ikabidi nidakie kwa kumzuga shemeji)
" Bwana ametwaa tulia dada.
" Siwezi niacheni tu.
" Mke wangu kazi ya Mungu aina makosa sasa kunywa POMBE ndio nini acha mke wangu.
" Sawa naombeni mniache nilale kwanza.
" Sawa lala mke wangu.
( Dada alilala sebuleni shemeji alikaa na yeye pembeni kumlinda dada mimi nikaenda kulala chumbani uku najiuliza dada mbona anataka kufanya mambo ya ajabu kwenye ndoa yake ivi pale alitaka kusema maiko ni bwana ake inamaana ndio mapenzi yamemzidi mpaka anashindwa kuelewa hili baya hili zuri...nikawaza nikalala asubuhi shemeji ananiambia)
" Shem wangu naomba uende na dada yako uko kwenye msiba shika laki hii.
" Sawa.
( Moyoni nasema sijui na dada wameongeaje ila acha shemeji aende kazini nitamuuliza dada...kweli akaondoka dada akaniambia)
" Mdogo wangu acha niende kwa recho Nikamwambie kwanini anakubali kuolewa na shemeji yake.
" Dada mbona utakuwa unafanya jambo la aibu wewe muache tu aolewe ndio bahati yake.
" Hapana sio bahati wanaume akuwaona mpaka amchukue maiko na anajua fika mimi moyo wangu upo pale hapa nipo kwenye ndoa kumlizisha mama.
" Ila dada badilika mpende shemeji mbona yeye anakupenda.
" Upendo aulazimishwi mimi naenda mdogo wangu sikia shemeji yako si amekupa laki moja chukua elfu 40 na wewe kazunguke zunguke mjini uko saa 12 jioni uludi mimi naenda kwa recho nikimkosa naenda kwa maiko hapo chamazi mbali.
" Ila dada samahani naomba naomba tena twende tu kwa mama kumsalimia tukae mpaka iyo jioni turudi wote ila usiende kwa maiko wala kwa recho italeta picha mbaya kwenye ndoa yako yule recho anaweza akaja uku mbezi kukuharibia na wewe.
" Aje tu kuharibu mdogo wangu ilo lisikupe tabu unajua maiko kabadilisha namba nampigia simpati hewani acha nijiandae niende.
" Dada tuliza hasira.
( Akuweza kunisikia aliingia bafuni kujiweka sawa kwa safari ya kwenda chamazi...na mimi nikaingia choo cha nje kuoga fasta nia niongozane nae dada yangu siwezi kumuacha niende mjini nikikutana na shemeji si nitaonekana na mimi ni wale wale tu...kweli wote tukawa sawa Nikamwambia)
" Dada twende wote.
" Wapi?
" Unapoenda.
" Twende Ukaone timbwiri langu wewe ujui mapenzi yanaumaje nakuombea upate bwana unayemuelewa alafu mama akuzingue ukikurupuka utamchukia mama.
" Mungu aniepushe nimchukie mama yangu kisa mapenzi sizani labla nimchukie mama mkwe sio mama yangu mzazi.
" Twende.
( Kweli tulitoka tukapanda gali za mbagara kwanza tukaenda kushuka rangi tatu tukapanda gali za m-bande...tukashuka chamazi magengeni dada akaniambia)
" Hapa nachukua pikipiki moja kwa moja kwa maiko au nianze kwa recho nishauri.
" Twende kwa maiko.
( Kweli tulipanda pikipiki mshikaki tukawa tunaenda kwa maiko anakaa sehemu moja panaitwa jengo la yatima...tunafika kwa maiko nje ya mlango wake tunaona viatu vya kike na vya kiume dada akaniambia)
" Afadhari wote wapo ivi ni viatu vya recho mwizi wa wanaume za watu.
" Subiri Basi tufike ugonge hodi.
" Mdogo wangu ujakuwa wewe nigonge hodi mlango naona umesindikwa ule ujafungwa naingia mazima yani recho atanitambua.
" Dada sio vizuri.
( Akunisikia akaongeza spead ya utembeaji mpaka mlangoni akausukuma mlango akaingia mazima ndani sijui alikuta wanafanya nini nasikia sauti ya maiko)
" Amina ujinga gani unaleta kwangu unaingia pasipo hodi kwangu.
" Wewe recho nakuita mala mbili recho recho...
ITAENDELEA
Unajua Nini dada alifanya?
Au Nini kimetokea NUNUA simulizi USOME yote mazima.
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi