πππ’ π‘π π π₯ππ ππ’ πͺπ π§πππ§π’π SEHEMU YA 16 ENDELEA..... "Ni wakati wa wewe kufurahia uboss pia, sielewi ni kwanini unapoteza kujiamini β" Zara aliongea.
"Hujanijibu swali langu, Bryant Kobe ameniachia kiti kwa hiari yake au umemuomba?"
"Bila kumuomba unadhani angeachia nafasi kwa hiari yake, unajua siku zote huwa unaamini Bryant Kobe anakupenda lakini upendo wake ni wa kinafiki.... tabasamu analo kuonyeshaga huwa ni danganya toto tu ili usije kwenda kinyume naye ....ni wakati wa wewe kuitwa boss pia. Kila Mama ana tamaa ya kumuona mtoto wake matawi ya juu. Naomba sana usije kukuza maneno utaniumiza moyo wangu " Zara alijihami kwa kuporomosha machozi.
"Hapana, kuna kitu utakuwa umemuambia Bryant Kobe ana tabia ya kukusikiliza kwa kila kitu, acha kudondosha machozi yako kwa sababu sitakubembeleza " Philips Kobe alitaka kuondoka lakini Zara alimdaka mkono.
"Ukiwa na miaka 10, nilimfuma Baba yako akimuambia maneno ya ajabu Bryant Kobe,.... nilijua ipo siku nitahitaji kukukumbusha sehemu yako " Zara aliongea kisha akaichia rekodi aliyoitunza kwa muda mrefu ikasikika.
π΅ Naamini katika akili yako, tafadhali sana naomba usije kuliacha Kampuni likaongozwa na mtu mwingine tofauti na yeye.π΅
π΅Baba kumbe humpendi Philips Kobe π΅
π΅Nampenda na ndio maana nimekuchagua wewe kuwa msimamizi wa Kampuni la Danone π΅
π΅Kwanini hutaki Philips Kobe awe msimamizi wa Kampuni ya Danone π΅
π΅Ingawa ni mdogo bado lakini kila napo mtazama naona anafaa kuizungukia dunia na si kutulia ofisini. Endapo itatokea ametulia ofisini nahofia kusema huenda Kampuni ya Danone ikasambaratika π΅
"Baba yako kabisa wa damu alizungumza haya maneno akiwa katika akili timamu, siku zote alikuona unafaa kuizungukia dunia na si kukaa kwenye Kampuni lake, ni kama alitaka upoteze maisha ukiwa safarini β....na ndio maana sikusita kumuangamiza, na kuambia ukweli kwa sababu wewe ni damu yangu halali.... Baba yako hakufa bahati bahati mbaya. Nilikitengeneza kifo chake, presha inatengenezwa. Presha inanunuliwa pia π " Zara alizungumza kwa kujiamini kupita kiasi.
Philips Kobe alimtazama kwa kumhurumia tu kisha akaondoka.
"Nini kwani ndio nishamwambia ukweli, pumbavu zake " Zara alijitia ujasiri wa kinafiki ila ukweli ni kwamba alikuwa anatetemeka hata yeye mwenyewe alishindwa kuelewa ni kwanini anatetemeka.
Philips Kobe baada ya kuingia chumbani kwake alidondosha chozi, siyo kwamba ile rekodi haikumuumiza, hapana ilimuumiza sana siyo kidogo.
Alibadilisha nguo zake chapu chapu kisha akapitia mlango wa nyuma. Kuna mahali alihitaji kwenda.
Kama angechukua gari basi Mama yake angejua kaondoka. Alihitaji kufanya vitu kimya kimya.
Alichukua usafiri kisha akatoka nje kidogo ya mji.
Alihitaji kuonana na Dada wa kazi ambaye kafanya kazi kwa muda mrefu sana. Kwa kifupi uzee ndio ulimuondoa.
"Nilijua ipo siku utakuja kunisalimia, nafurahi kuona umekuwa Kijana mzuri.... Watoto wako watakuwa warembo sana " Dada wa kazi mstaafu aliongea.
"Naomba kujua Kwanini Baba yangu hakutaka Mimi ni kae kwenye Kampuni la Danone kama CEO naomba uniambie kila kitu hata kama kitakuwa ni cha kuumiza"
"Philips Kobe macho yako yanaonesha umekuwa mtu mzima sasa lakini akili yako haipo tayari kusikia ukweli. Endapo nitakuambia ukweli huenda ukachanganyikiwa maisha yako yote...nenda sitakuambia chochote zaidi ya kusema Kampuni la Danone litakuwa salama zaidi kama litasalia mikononi mwa Bryant Kobe "
Philips Kobe alichoka kumbembeleza, alivuta bastola akaiweka usawa wa kichwa cha Dada wa kazi mstaafu.
"Nitakuambia....hakika nitakuambia ukweli "
Philips Kobe alifungua masikio yake kwa umakini kusikiliza kitu anachotaka kuambiwa.
ITAENDELEA......
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi