πππ’ π‘π π π₯ππ ππ’ πͺπ π§πππ§π’π SEHEMU YA 18 ENDELEA..... "Inakuaje unaanguka na huku umekunywa chai
"Ni ujinga kuwaza hivyo, hebu niletee pochi yangu. Nilipaswa nizione siku zangu siku iliyopita sielewi ni kitu gani kinaendelea " Tasha aliongea huku akitetemeka ni muoga kwenye swala zima la mimba.
"Sasa una tetemeka nini " Yolanda aliuliza huku akitafuta kipimo cha mimba kwenye pochi ya Tasha.
"Kwanini unatembea na vipimo namna hii kama vile una jukumu la kupima watu huko mtaani...."
"Huu si muda wa kufuatilia kuhusu hivyo vipimo, hebu niletee hiyo glass nayotumia kunywea maji...nitalimwaga humo kojo "
Yolanda alitaka kuongea lakini jicho moja la Tasha lilimfunga mdomo.
Basi mrembo wa Tiktok akiwa ni mwenye kujiamini alikojoa kwenye glass kisha akashika kipimo cha mimba. Alikiweka kwa umakini mkubwa kisha akakaa pembeni kusikilizia majibu.
Mapigo ya moyo wake yalivurugika mbaya mbovu baada ya kuona mistari miwili πππ.
"Nini mbona umepoteza amani ya moyo "
"Nina mimba π"
"Pumzika ukiwa sawa utaniita tuzungumze.... Yolanda aliongea kisha akaondoka hakuwa tayari kumaliziwa hasira.
Basi wacha Tasha alie π, alilia style zote anazo zifahamu. Baada ya kuchoka alipanda kitandani kulala. Kama utani hivi lakini usingizi ulimpitia.
Upande wa Bryant Kobe aliingia jikoni kuandaa supu kwa ajili ya mdogo wake.
Alitia viungo vya kila aina kiasi kwamba alikunja sura yake kwa ladha aliyokutana nayo baada ya kuionja.
"Unataka kuniua siyo hii ladha haifahamiki ni chungu au tamu" Philips Kobe alilalamika huku akiendelea kula.
"Ni ahidi hautarudia tena kunywa pombe kupita kiasi ..."
"Na kuahidi .."
"Nguvu za kuoga unazo au na nikuogesha!"
"Mwili wangu hauna nguvu, nitafurahi kama utaniogesha " Philips Kobe aliongea bila aibu, wawili hawa wanapendana sana hivyo Bryant Kobe hakupata tabu kumuogesha mdogo wake....baada ya kumaliza aliondoka. Moyo wake ulikuwa na tamaa ya kumuona Tasha na si kingine.
Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kufika nyumbani kwao Tasha.
Aligonga geti kisha akajielezea, kabla Mlinzi hajatoa maelekezo yoyote Mama yake Tasha alifika.
"Ka...karibu " Aliongea akiwa haamini.
"Ahsante, heshima yako...."
"Marahaba..... karibu ndani" Mama Tasha aliongea huku akionesha tabasamu.
Basi Bryant Kobe hakuwa na namna zaidi kukaribia ndani...
"Wala hata usikae sebuleni nifuate huku....sijui unajua tena nataka kutoka pia sitafurahi kukuacha hapo pekee yako njoo huku kwa Kijana mwenzio mzungumze " Mama Tasha aliongea kisha akagonga mlango wa binti yake baada ya kuona hajibiwi aliusukuma mlango.
"Pita ukae kwenye kochi umsubirie, anapenda sana kulala" Mama Tasha aliongea kisha akaondoka.
Bryant Kobe alikaa kwenye kochi, akiwa anamsubiria Tasha aamke alishtuka baada ya kuona mkojo kwenye glass kwa chini kulikuwa na kipimo cha mimba.
"Positive .... kwahiyo hapo ana ujauzito, pengine ndio sababu iliyompelekea achoke. Kuwa Mama si kitu cha mchezo hasa mtu ukiwa hujajipanga" Bryant Kobe alijisemea kisha akarudisha vitu kama vilivyokuwa.
Tasha akiwa kanogewa na usingizi alianza kujigeuza huku na kule kama samaki, kama si Bryant Kobe kuwahi kumdaka basi angedondoka chini.
Tasha alipiga kelele baada ya kukutana uso kwa uso na Bryant Kobe.
Alishindwa kuelewa huyu Mwanaume kapitia wapi..
"Mama yako kanikaribisha, kwa kuwa ulikuwa umelala hatukutaka kukuamsha.
"Unanioa lini Mimi " Tasha aliachia swali.
"Kukuoa wewe?...kuna nini hadi ni kuoe "
"Nina ujauzito wako "
Bryant Kobe alishtuka ndani ya moyo wake na hata akajikuta anakosa neno la kuzungumza.
"Vipi unataka kunitelekeza na huu ujauzito ".
"Sijamaanisha hivyo....nipo hapa kukusalimia. Kuhusu ujauzito naomba tuzungumze baadae baada ya kusalimiana ": Bryant Kobe aliongea huku akiachia tabasamu, hii ilimpa Tasha amani ya moyo.
Upande mwingine Zara anafika kwenye nyumba ya Dada wa kazi mstaafu. Kwa jinsi alivyokuwa na hasira hakuona hata sababu ya kugonga hodi.
ITAENDELEA.....
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi