πππ’ π‘π π π₯ππ ππ’ πͺπ π§πππ§π’π SEHEMU YA 7 ENDELEA...... "Una mfahamu mbona umeshtuka namna hiyo, kama humjui mchukue
"Bryant Kobe aliangalia huku na kule, moyo wa kumkanyaga Tasha afe ulimuijia π
Kama si watu kuanza kujazana basi angemaliza kabisa.
Walishirikiana na Mdogo wake kumuweka kwenye gari.
Safari ya kwenda hospitali ilianza, ni mtu mwenye pesa nyingi hivyo isingemletea shida kuhusu taarifa kutoka kwa Polisi.
"Natamani nimlipe Daktari amchome hata sindano ya sumu afe, msumbufu sana huyu huko mtandaoni.... nadhani nimewahi kukuambia kuhusu Binti anaye fundisha Wanawake tabia mbaya huko mtandaoni "
"Ungeniambia mapema ningemkaba ndani ya gari, yaani ningemleta hapa akiwa mfu kabisa "
"Okay tuondoke zetu,....sisi ni wasamaria wema tuliomleta hapa hatujahusika kwa lolote " Bryant Kobe aliongea kisha akamshika mkono mdogo wake wakasepa.
Basi Madaktari walichangamka baada ya kupigiwa simu na Baba yake Tasha,
"Mtoto wa kishua huyu tufanye vitu kwa umakini pesa ipo nje nje " Daktari mpenda pesa aliongea.
Basi Philips na Bryant Kobe baada ya kufika nyumbani walishangazwa na namna Mama yao alivyokuwa bize kuandaa chakula.
"Mama, Philips Kobe huyu hapa karejea...." Bryant Kobe aliongea baada ya kuona Zara yupo bize kuonja chumvi.
"Kwahiyo nifanyeje mb....wa nyie kasoro kubweka ....shikeni kikapu mpeleke chakula hospitali, gari lenu limeonekana kwenye camera. Sitaki mniharibie undugu na hao watu....hasa wewe Philips Kobe hutakiwi kuwa na kiburi beba hilo kapu " Zara alifoka hadi mishipa ikamsimama.
Philips Kobe huwa hateteleshwi na hasira za Mama yake.
Kama si Bryant Kobe kuwahi kubeba kapu huenda Zara angezimia kwa kupuuzwa.
"Bryant.... peleka chakula wewe, huyu Mpuuzi anayenuka mkojo atakaa jikoni kuosha vyombo endapo atanipuuza nitaenda kulia kwenye kaburi la Mume wangu" Zara alisisitiza.
Bryant Kobe alimpa ishara mdogo wake aache kiburi kisha yeye akaondoka.
Baada ya kufika Hospitali wazazi wa Tasha walifarijika sana.
"Kisheria haka kapanya kadogo kakipona kanatakiwa kupelekewa Mahakamani kawalipe lakini kwa upendo mlionao kwetu mmefunika kombe mwana haramu apite" Mama Tasha alizungumza.
"Ni jambo la kawaida tu wala huna haja ya kushukuru sana β....chakula hiki hapa nimeleta kwa ajili yake. Pindi atakapo amka naomba umhimize kula..." Bryant Kobe aliongea akataka kuondoka lakini haikuwezekana baada ya Zara kuingia.
"Unaenda wapi subiri aamke umbembeleze kula."
"Aah sawa " Bryant Kobe aliongea kisha akakaa.
"Mwanaume hawezi kudeki ndani kisa kaoa nani kasema huu upuuzi?... hebu naomba watu wanaoungana na hii hoja wanyooshe mikono juu" Tasha aliongea haya maneno baada ya kukurupuka usingizini.
Watu wote walicheka isipokuwa Bryant Kobe.
Hakutaka kupoteza muda, alitoa chakula kwenye hotpot kisha akamtaka Tasha aachame mdomo wake.
Vile Tasha alikuwa na njaa aliachama kama mtoto anaye kaguliwa kimeo.
"Hebu tuwapishe kidogo π€" Mama Tasha alizungumza akijitia anajambo la kujadili.
"Sifanyi huu ujinga jilishe mwenyewe" Bryant Kobe alimbadilikia Tasha.
"Nimewahi kuzungumza siku moja huko Tiktok kuwa Wanaume wengi wenye hasira za mara kwa mara ni wale ambao hawafiki kilele kile kinacho kusudiwa, bro tafuta Mwanamke atakaye kufanya umwage mpaka ubongo.... hizi hasira za kijinga jinga hautakuwa nazo tena " Tasha aliongea.
"Fanya kunijaribu sasa nikuwekee kidogo " Bryant Kobe aliongea.
Tasha alivurugika kwa maneno aliyoambiwa.
ITAENDELEA.......
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi