Chombezo : Jamani Kaka Cheni … Ndiyo Nini Sasa?! Sehemu Ya- 2 Nilimwona kaka Cheni akishtuka sana. Hata mimi nilishtuka kwani nilijua baba
“Shikamoo baba,” kaka Cheni aliamkia huku wasiwasi wake ukiwa umegundulika na baba.
“Marhaba.”
Baba yetu alikuwa na tabia hiyo ya ajabu, ukimwamkia akiitikia hana cha kusema umeamkaje wala habari za leo! Hilo hata mama alikuwa akimshangaa.
Mwenyewe msimamo wake ni kwamba, kumuuliza aliyekuamkia shikamoo umeamkaje ni kupoteza sauti kwani angekuwa ameamka vibaya asingeamkia shikamoo angeeleza ugonjwa wake au tatizo lake.
Nilianza kutetemeka mimi badala ya kaka Cheni licha ya kwamba naye kaka Cheni hakuwa sawasawa hata kidogo.
Ishu ilikuwa lile jimwanamke kutoka chooni. Kwani ilikuwa lazima kaka Cheni amfuate akamstopishe au aache atoke mwenyewe akumbane na baba, mzee wa Kingoni, mkali kama nini! Ukimwangalia tu hivi unajua mkali maana amefuga msitachi mrefuuu! Mpaka amekuwa kama yule mtu wa kwenye dawa ya kuchulia misuli.
Ghafla kaka Cheni alikwenda chooni, akachukua kama dakika mbili, akatoka. Nilimwona akitoka jasho jembamba la woga. Nikajua leo kazi ipo. Wasiwasi wangu ulizidi zaidi pale nilipowaza itakuaje kama baba angeamua kwenda chooni baada ya kaka Cheni kutoka.
Mara, nilisikia kitu kimeanguka sebuleni, baba akashtuka na kuingia ndani. Kaka Cheni akatoka mbio hadi chooni akatoka na jimwanamke lake akiwa amemshika mkono.
Mbona ilikuwa kichekesho, mdada anavyokimbia na kaka Cheni anavyomkimbiza, miye mbavu sina!
Walitokomea huko, baba alipotoka akakuta hakuna kitu!
“Mwite kaka yako,” aliniamuru baba…
“Katoka…”
“Kaenda wapi?”
“Nadhani yuko nyuma ya nyumba.”
“Kamwite.”
Nilizunguka nyuma ya nyumba lakini sikumwona kaka Cheni, nikampigia simu…
“Baba anakuita.”
Kaka Cheni alikata simu. Iliashiria kwamba, alielewa kwamba baba anamuita. Baada ya sekunde tu alitokea akiwa mbio.
Cha ajabu ni kwamba, mambo aliyokuwa akiyafanya kaka Cheni pale nyumbani na ukali wa baba ni vitu viwili tofauti kabisa!
“Naam baba…”
“Wewe usiku huwa unakuaga na nani chumbani kwako?”
“Marafiki zangu baba…”
“Mbona mchana siwaoni?”
“Ha! Baba…mbona mchana pia wanakuja sana, muulize sista,” alisema kaka Cheni huku akinitupia macho mimi…
“Ni kweli baba, marafiki zake huwa wanakuja hata mchana. Ila kwa usiku mimi sijawahi kuwaona.”
“Mh! Huyu mara kwa mara usiku nikitoka kwenda chooni nawasikia wakiongea na wenzake.”
“Ni marafiki zangu baba.”
Moyoni nilisema baba ungejua wala usingeuliza. Huyo mwanao kazi yake kubwa ni wanawake kila siku.
Basi, baba alionekana kukubaliana na maelezo ya kaka Cheni, akanyamaza. Mara akatokea mama akiwa na ndoo ya maji…
“We Cheni,” mama aliita hata kabla ya kutua ndoo chini…
“Naam…”
“Yule mwanamke ulikuwa unampiga busu pale kwenye kona ni nani?”
Nilimwona kaka Cheni akikunja sura na macho yakisinzia kama anayesema ‘ohooo! Kimenuka sasa!’
“Namjua mama.”
“Unamjulia wapi? Anakaa wapi?”
“Mama yule anakaa kule kwa mzee Masumbuko…”
“Wewe mtoto wewe! Usije ukaniletea wajukuu wasiokuwa na mpangilio hapa kwangu,” alisema mama kwa uso wenye hasira za kweli…
“Kwani kumjua ndiyo kulikufanya umbusu?” hapo sasa aliingilia baba mwenyewe. Ilibidi kaka Cheni akae…
“Kwanza ni mwanamke mtu mzima au?” aliuliza baba…
“Ah! Anaonekana ni binti tu lakini ana mwili mkubwa sana. Mimi mwenyewe nilishangaa, nikaogopa maana walivyosimama utasema ni mtu na mtoto wake wa kiume,” mama alikoleza.
Ajabu sana! Nilimwona baba akiachia tabasamu ambalo sijawahi kuliona hata siku moja. Nilivyomjua baba yangu, pale kaka Cheni asingekaa. Lakini pia moyoni nilisema kama baba angejua mwanamke anayesemwa alikuwa chooni wakati yeye amekaa kwenye kiti cha nje, pangechimbika kama siyo kufumka!
Kutabasamu kwa baba, kulimpa nguvu kaka Cheni, naye akatabasamu lakini mama aliendelea kuwa siriasi. Akaingia ndani na kuendelea na mambo mengine…
“Hodi,” sauti ya msichana ilisikika kutoka nje ya geti dogo la uani ambalo lilikuwa wazi…
“Nani? Pita,” nilisema mimi huku nikiwa nimetumbulia macho pale kwenye geti…
Msichana wa umri wa kama miaka saba aliingia, anaitwa Mai…
“Karibu Mai,” nilimkaribisha…
“Asante…shikamoo babu,” yaani baba…
“Shikamoo anko,” yaani kaka Cheni…
“Anko, Mwanamaua anasema amesahau kitambaa chake cha kichwani chumbani kwako kitandani, kasema nipe nimpelekee ataulizwa na mama yake asiporudi nacho…halafu kasema hujamwambia usiku wa leo aje au asije maana simu yake ina matatizo ya chaja.”
##
𝐊𝐢𝐭𝐮 𝐠𝐚𝐧𝐢 𝐤𝐢𝐥𝐢𝐜𝐡𝐨𝐞𝐧𝐝𝐞𝐥𝐞𝐚….
𝐔𝐬𝐢𝐤𝐨𝐬𝐞 𝐬𝐞𝐡𝐞𝐦𝐮 𝐢𝐧𝐚𝐲𝐨𝐟𝐮𝐚𝐭𝐚
𝐉𝐚𝐦𝐚𝐧𝐢 𝐭𝐰𝐞𝐧𝐝𝐞 𝐜𝐡𝐚𝐩𝐮 🙌, 𝐋𝐈𝐊𝐄-150 𝐬𝐚𝐬𝐚 𝐡𝐢𝐯𝐢 𝐢𝐥𝐢 𝐧𝐢𝐩𝐨𝐬𝐭 𝐧𝐲𝐢𝐧𝐠𝐢𝐧𝐞 𝐜𝐡𝐚𝐩𝐮 𝐜𝐡𝐚𝐩𝐮 🚀🔥.” Naomba like ziwe zakutosha isichelewe
Akikisha una follow page yetu tukipost inakufika mojakwamoja
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi