*KIJIJINI KWA BIBI* Na Mwaisa Story Sehemu Ya 2 ______________ ILIPOISHIA. _______________ "Inatakiwa nijue ili nipange ratiba zangu za matumizi vizuri" Stellah
alijibu kwa upole,
"We panga unavyojua wewe, maana
mimi nije peke yangu au na wenzangu hayo hayakuhusu na gharama zangu au wenzangu pia
hazitokuhusu" Kayoza aliongea
macho yakiwa makavu,
"Basi baba, hatugombani hapa"
Stellah aliongea huku akitabasamu,
"Haya nenda nje mimi nivae" Kayoza
alimwambia stellah,
"Kwani ukivaa mbele yangu kuna
ubaya gani?" Stellah aliuliza kwa
utani,
"Wewe mpumbavu nini?" Kayoza aliongea huku akimsukumia Stellah
nje na kubaki ndani peke yake huku akisonya kwa hasira huku akiufikiria mualiko aliopewa na Stellah..
Ila angejua ambacho kitamtokea,
basi asingekubali ule mwaliko.......
_____________
ENDELEA.
_____________
"Mpuuzi kweli huyu manzi" Kayoza aliendelea kuongea peke yake huku akivaa kaptula kabla hajashtuliwa na mtu aliyekuwa anasukuma mlango ili aingie ila alishindwa kutokana na ule mlango kufungwa kwa ndani,
"Bado hujaondoka tu?" Kayoza aliuliza kwa hasira,
"Fungua bwana" Sauti nene ya kiume iliongea kutoka nje na ndipo Kayoza akauendea mlango na kuufungua na wakaingia rafiki zake wawili, mmoja aliitwa Omary na mwingine alitambulika kwa jina la Denis,
"Vipi wewe unajifungia fungia mchana, au ulikuwa na Stellah?" Denis alimuuliza Kayoza,
"Umejuaje?, alikuwepo hapa muda si mrefu" Kayoza alijibu huku akij i tupa kitandani,
"Kwa hiyo mlikuwa mnafanya mambo flani nini?" Omari aliuliza huku akicheka,
"Muda wote unawaza ujinga tu, hivi ni lini utakuwa wewe?" Kayoza alimuuliza Omary kwa hasira,
"Huyu sio bure, zile tetesi hata mimi naanza kuziamini" Omary aliongea huku akimgeukia Denis,
"Tetesi gani?" Kayoza aliuliza kwa hamaki huku nae akimgeukia Denis,
"Maneno tu ya watu" Denis alijibu huku akionekana hataki kulizungumzia hilo,
"Maneno gani sasa, si uniambie" Kayoza aliongea huku akiwa bado anamuangalia Denis,
"Mchane, usiogope, huyu ni rafiki yetu na ni lazima chochote kinachosemwa juu yake tumwambie" Omary alimsisitizia Denis,
"Niambie hata wewe kama Denis hataki kuniambia" Kayoza aliongea huku akimgeukia Omary,
"Bwana mimi sipendi kuficha, uko nje habari zimeenea kuwa wewe ni shoga, eti haiwezekani tokea uanze kusoma hapa mwaka wa tatu huu haujawahi kuonekana na mwanamke sehemu yoyote ile" Omary aliongea huku akitazama chini na kumfanya Kayoza nae ainame chini huku akiwa na huzuni sana,
"Mimi siamini kama wewe unaweza kuwa shoga, ila nahisi labda una tatizo jingine, tueleze rafiki yetu, usiogope" Denis aliongea kwa lengo la kumfariji Kayoza ambaye bado alikuwa kichwa chini huku akiwaza,
"Tunasaidiana mambo mengi. Sisi ni ndugu sasa na sio marafiki tena, tatizo lako ndio tatizo letu, kwa hiyo Sema kama una tatizo tuone kama tutaweza kukusaidia" Omary nae alimsihi Kayoza awaeleze,
"Sina hamu ya kuwa na mwanamke wala kufanya mapenzi na sijui ni kwa nini?" Kayoza aliongea kwa huzuni huku akiwa bado kichwa chini,
"Ila ulishawahi kufanya mapenzi kipindi cha nyuma?" Omary alimuuliza,
"Tokea napata akili sijawahi na wala sina hamu kabisa" Kayoza alijibu,
"Umeshawahi kwenda hospitali?" Denis alimuuliza,
"Nimeenda mara nyingi sana na naonekana sina tatizo" Kayoza alijibu,
"Na kwa waganga wa kienyeji umeshawahi kujaribu?" Omary aliuliza,
"Kila nikipanga Mipango ya kwenda kwa waganga, uwa siku ikifika najikuta napuuza au kinaweza kutokea kitu kingine kitachoharibu huo mpango" Kayoza aliwaeleza wenzake,
"Basi ilo jambo tutalifuatilia vizuri, sio bure" Denis aliongea huku akisikitika,
"Stellah alikuwa anasemaje?" Omary aliamua kubadilisha maada,
"Alafu nilishasahau, amesema jioni tuonane mjini" Kayoza alijibu,
"Kwa hiyo leo unatuacha, utalala huko huko au utarudi?" Omary aliuliza,
"Amesema tuende wote watatu" Kayoza alijibu,
"Aisee mimi leo sina hela, kwa hiyo sitoenda, si unajua leo wikiendi so ukienda mjini inabidi ujipange" Denis aliongea huku akitabasamu,
"Amesema gharama zote zake, sisi tuende kama tulivyo" Kayoza aliongea na kufanya wenzie wafurahi,
"Basi poa, ngoja nilale kidogo ili chakula kishuke" Denis aliongea huku akijilaza kitandani,
"Ila usiku tutarudi, hatutalala mjini" kayoza alisema,
"Mimi sitorudi, nitaunganisha clab moja kwa moja, leo wikiendi bwana. Au wewe Denis nawe utarudi?" Omary aliuliza huku nae akipanda katika kitanda chake cha juu,
"Tutajua uko uko" Denis alijibu kivivu huku akiwa amesinzia.
********************
Mida ya saa moja kasoro jioni, Kayoza,
Omary na Denis walikua maeneo ya
mjini katika foleni ya ATM. Ilipofka
zamu yao kayoza akaingia ndani,
akatoa pesa, kama elfu hamsini
akatoka na kuungana na wenzake,
"oya wakubwa, mi naona twendeni
kwanza tukale kwa sababu huyu
demu mimi simuamin amini,
anaweza kuwa katenga bajeti ya
kunywa tu, akijua sisi tumekula", Kayoza alikua anawaambia wenzake,
"acha uboya we mtoto wa mama, alipokwambia uje saa moja alitaka tuje tupige nae msosi wa jioni, huyo du si
anajua ratiba zetu za msosi wa
usiku, kuwa tunakula saa tatu, kwa hiyo alijua saa moja tutakuwa bado hatujala" Omary aliongea huku akiwa anatafuna karanga.
Mara simu ya kayoza ikaanza kuita mfukoni,
akaitoa mfukoni kisha akaiangalia
kwenye kioo cha simu, jina lililoonekana wakati huo lilisomeka KICHECHE.
'huyo Stellah anapiga" Kayoza aliwaambia
wenzake ambao walikuwa
wanamuangalia,
"usilembe bishoo wewe, pokea simu uongee na mtoto mzuri", Omary
alimsisitiza Kayoza baada ya kuona anajishauri kupokea simu.
Kayoza akaipokea ile simu, kisha
akaweka sura ya umakini,
"Mambo..",Kayoza alimsalimia Stellah,
"poa, mko wapi?",Stellah alimuuliza Kayoza kupitia simu,
"tupo hapa benk, tunakuja",Kayoza
alijibu,
"mbona simu ilikuwa inaita muda mrefu hivyo?",Stellah alianza
kulalamika namna hyo,
"nimeiweka sauti ndogo mno, alafu
hapa ATM kuna utulivu sana na watu wako wengi sana, kwa hiyo ilinibid nisogee mbali kidogo ili niipokee simu yako" Kayoza
akamdanganya Stellah,
"ok.. poa, sisi tumeshafika
tunawasubir nyinyi" Stellah
akamtaharifu Kayoza,
"sisi tutachelewa kidogo kwa sababu tunaenda kula kwanza", Kayoza
akatoa udhulu,
"mambo gani sasa, nyie njooni tu, hivyo vyote nimevitayarisha",Stellah akawaka,
"poa, ndani ya dakika kumi tutakuwepo hapo" Kayoza akaongea kisha akakata simu.
"Haya waungwana twendeni
tukawachune hao vicheche, mida ya
saa nne tuwateme tukajiachie clab
mpaka kuche" Kayoza akawaambia wenzake,
"Vicheche? Kwani yuko nani?" Omary aliuliza,
"Yuko na Tausi" kayoza alijibu,
"Basi twendeni tukakae nao alafu baadae tunaenda zetu clab" Omary aliongea,
'nyie nendeni tu uko club mimi lazma nikalale
na mmoja wao" Denis aliongea na wenzake wakacheka.
"Jamaa mroho kweli" Omary alimtania Denis huku akiendelea kucheka,
"Wamekwambia wapo wapi?" Denis alimuuliza kayoza,
"Wapo Nyerere squarre" kayoza alijibu huku wakivuka barabara inayoelekea wanapokwenda.
Walipofika nyerere square,
wakamuona kwa mbali stellah na rafiki yake aitwae Tausi,
"Leo kazi ipo" sauti nzito ilipita kwenye masikio ya Kayoza na kushindwa kuelewa inatokea wapi, na cha ajabu Denis na Omary hawakuweza kuisikia sauti hiyo....
******ITAENDELEA******
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi