EPS 1 SIMULIZI;MCHEPUKO WA RAIS
SIMULIZI;MCHEPUKO WA RAIS
________________________________
CHAMA HURU MEDIA
**
UTANGULIZI
Saa tatu na dakika ishirini usiku,ndani ya Chumba cha hoteli namba 45 yenye hadhi ya nyota tano,alionekana mwanaume (37) akiwa amesimama pembeni ya kitanda huku mikono yake na suti nyeusi aliyovaa imetapakaa damu,mwanaume huyu anafahamika kwa jina la Grayson Mwailubi,kifua na mwili wake umejengeka kwa mazoezi,macho yake yalikuwa yanatazama juu ya kitanda kilichopo ndani ya hiki chumba.
Mbele ya mboni za macho ya Gray alionekana mwanamke mrembo akiwa amelala chali huku damu zinamtoka tumboni ,mwanamke yule alikuwa amevalia shela nyeupe ya harusi ambayo nayo ililowana damu zinazotoka tumboni kwake.
Gray akaitazama mikono yake kwa hofu kubwa kisha akasema
"Leyla nisamehe,hakuna mwanaume ambaye angelivumilia upuuzi ulioufanya,utanisamehe" (akavuta pumzi na kuishusha)
Leyla (30) alikuwa amepoteza maisha baada ya kuchomwa kisu mara nane tumboni na mume wake Gray, tukio hili limetokea masaa machache baada ya wawili hawa kufunga ndoa na kuwa mwili mmoja.
Wakati Gray akiwa anautazama mwili wa marehemu mke wake Leyla, mlango wa chumba alichopo ukaanza kugongwa,Gray akayatoa macho mithili ya mjusi aliyebanwa na mlango.
{"Ngo.. Ngo...ngo"}ร3
Gray akautazama mwili wa mke wake uliolala kitandani, akautazama mlango huku akihema kwa hofu kubwa,akajitazama suti yake akaziona damu nyingi zikiwa zimetapakaa,Gray akashusha pumzi halafu akajikaza kupaza sauti.
"We nani?"
Sauti ya kiume ikasikika upande wa pili
"Mimi ni Mohamed rafiki yako,njoeni basi ukumbini tunawasubiri tumalizie sherehe yetu"
Gray akageuka tena kuutazama mwili wa marehemu mke wake,akavuta pumzi na kuishusha ili Kupunguza hofu.
"Sawa mohamed nakuja"
"OK,mwambie na shemeji awahi"
"Poa"
Sauti ya hatua za miguu ya mohamed ikasikika,bila Shaka alikuwa anaondoka eneo hili,Gray akashusha pumzi baada ya mohamed kuondoka nje ya mlango wa chumba alichopo ,Gray akasogea haraka kitandani alipolala marehemu mke wake,akakichukua kisu kilichotumika kufanyia mauaji,kisu kile kilikuwa kando na mwili wa Leyla,Gray akakitupa kisu uvunguni Mwa kitanda halafu akaanza kukusanya nguo zake ili akimbie.
Akiwa anajiandaa kutoroka eneo hili mara ghafla ving'ora vya magari ya askari polisi vikaanza kusikika kwa nje,Gray akapatwa na mshituko mkubwa maana amefanya tukio la mauaji ya mke wake dakika chache zilizopita,kabla hajakimbia, ving'ora vya askari vimeanza kusikika nje ya hoteli aliyopo.
**
TUANZE SASA........
Magari ya askari polisi yapatayo sita yalifika hotelini,askari polisi wakashuka ndani ya Gari wakiwa wamebeba silaha zao,Mkuu wa hii operesheni, Inpekta Alexander Dickson (40) akatoa amri kwa askari polisi wazunguke hoteli na wengine waingie ndani ya hoteli.
Hoteli hii ilikuwa ya kifahari na imejengwa kwa ghorofa nne kwenda juu ,ghorofa ya kwanza ni Mapokezi,ya pili ni Sehemu ya kupata Chakula,ghorofa ya Tatu ni ukumbi wa mkutano pamoja na sherehe, kwenye hii ghorofa ya Tatu ndio kulikuwa na sherehe inayoendelea ya Gray na Leyla.
Wageni waalikwa hawakuwa wanafahamu kilichotokea ghorofa ya Tatu kwa Bwana na Bibi harusi,wao walikuwa bize kuucheza muziki huku wakiwasubiri Bwana na Bibi harusi wafike ukumbini kwa ajili ya kuendelea na sherehe,Meza kuu ilipambwa kwa Maua mazuri pamoja na picha za Gray na Leyla wakiwa wamevalia mavazi ya Harusi tena katika 'pozi' la Mahaba.
Askari polisi walikuwa wamefika ghorofa ya pili ambapo kulikuwa na watu mbalimbali wakipata Chakula na vinywaji.Inspekta Alexander Dickson aliwaondoa hofu wateja maana wameogopa baada ya kuona askari polisi wametapakaa kila kona.
"Naitwa Inspekta Alexander Dickson, ni mkuu wa kitengo cha upelelezi wa mauaji,niwaondoe hofu lakini hakuna mtu anayeruhusiwa kutoka nje mpaka pale uchunguzi wetu ukikamilika,Asanteni" Inspekta Alexander Dickson akaelekea zilipo ngazi,akapanda kuelekea juu,wateja walipigwa na butwaa, kila mmoja alikuwa na maswali mengi imekuwaje Inspekta Alexander Dickson afike hapa,jina la Alexander Dickson ni miongoni Mwa majina mashuhuri nchini Tanzania kutokana na utendaji kazi wake.
Alexander Dickson akafika ghorofa ya Tatu ambapo kulikuwa na sherehe inayoendelea,akakuta askari polisi wenzie wameshafika muda mrefu na wamewaambia wageni waalikwa watulie,muziki ulizimwa Kama disko linavyoingiliwa na Masai.
Inspekta Alexander hakutaka kupoteza muda ,akapanda ngazi haraka Sana kuelekea ghorofa ya nne ambayo inavyumba vya wageni maalumu (V.I.P),na kwenye moja ya chumba yupo Gray na mwili wa marehemu mke wake Leyla.
Alexander akafika mpaka kilipo chumba namba 45,chumba ambacho muda si mrefu kuna mauaji yametokea,Alexander Dickson aliwakuta askari polisi wenzake wapatao nane wakiwa wamesimama pembeni ya mlango huku wamezielekeza silaha zao kwenye mlango wa chumba namba 45.
Alexander akapaza sauti.
""Tumekuzingira. Tafadhali toka nje kwa mikono juu na usalimishe silaha yoyote uliyonayo,tunataka kumaliza jambo hili kwa amani,nakupatia sekunde 30."
Ukimya ndani ya chumba ukaendelea kutawala,Alexander Dickson akatoa amri ya ishara kwa askari wenzake waingie ndani maana sekunde 30 zimepita,Askari polisi watatu wakausogelea mlango kisha wakaupamia,Mlango ulipofunguka askari polisi wakaingia ndani ya chumba namba 45,cha ajabu hawakumkuta Grayson bali walikuta mwili wa Leyla ukiwa umelala kitandani.
SEHEM
"inaonekana kapita dirishani" (sauti ya askari polisi mmoja wakati akichungulia nje ya dirisha)
Ghorofa ya nne,haikuwa rahisi kwa Grayson kuruka kutoka juu asipoteze Maisha.
Alexander Dickson akatoa simu (Redio za mkononi),akasema
"BOLO" (Be on the lookout) ikiwa na maana ya kutoa taarifa kwa askari polisi wote waliopo eneo la tukio kuwa makini na kumtafuta mhalifu,kitu ama Gari alilotumia kutorokea.
Askari polisi wakawaamru watu wote wakae chini ili wafanye uchunguzi wao,watu wote wakatii agizo liliotolewa na askari polisi.
Alexander Dickson akashuka haraka mpaka ukumbini,akakuta watu wote wamekaa chini,wengine wakiwa wamelala kifudi fudi kwa uoga,Alexander akapaza sauti akisema
"Naomba wazazi wa Bwana harusi wasimame"
Alexander akawa anatazama huku na kule,Bibi mmoja mwenye umri wa miaka karibia sitini na tatu akasimama kwa hofu,alikuwa ameshona nguo zake kwa kitenge, kwa mwonekano anafanana fika na Bwana harusi Gray.
Alexander akamuona Bibi yule
"Wewe ndiye mzazi wa Bwana harusi?"
"Ndi...ndiyo" (Bibi alijibu kwa sauti iliyojaa wasiwasi)
Alexander akashusha pumzi,akamsogelea mama Gray.
"Mwanao anatuhumiwa kwa kesi ya mauaji"
"Mauaji...?mwanangu ni Bwana harusi,tena yupo huko juu tuna..." (Kabla mama Gray hajamalizia sentensi yake Insp.Alexander akasema)
"Mama sisi siyo vichaa,mwanao amemuua Bibi harusi tunaomba utuambie sehemu gani tunaweza kumpata" Kauli ya Alexander ikaibua minong'ono ya sintofahamu kwa wageni waalikwa pamoja na wazazi wa Leyla,hakuna ambaye aliamini anachokisikia kutoka kwa Alexander Dickson.
"...hey,naombeni mkae kimya"
Baba mmoja mwenye asili ya kiarabu akiwa amevaa kanzu yenye rangi ya dhahabu na baraghashia kichwani akasimama kwa ghadhabu,
"Unataka kusema mwanangu ameuawa..!!"
Alexander akajibu
"Ndiyo,na mtuhumiwa wetu ni Bwana harusi, askari polisi wamezunguka hoteli yote naimani watampata,ushirikiano wenu tunauhitaji"
"Uwiii.... Mwanangu weeee" (Mama yake na Leyla akaanza kulia maana leyla ni mtoto wake wa pekee)
Mama yake Leyla ana asili ya kitanzania,ile aliolewa na Muarabu ndio wakampata Leyla,sherehe imebadilika na kuwa msiba ndani ya dakika moja tu.
Alexander Dickson akaacha maagizo kwa askari wake wampeleke Baba Leyla ndani ya chumba alichopo mwanae kwa ajili ya utambuzi wa mwili,hawakutaka kumpeleka Mama Leyla maana angelizidi kuumia,Alexander Dickson akashuka ghorofa ya chini kwenda kuongea na meneja wa hoteli,lengo lake ni kupata picha za CCTV kamera ambazo zitawasaidia kufahamu alipo Gray.
Ingawaje mauaji yametokea ndani ya chumba alichokuwa Gray,lakini maswali mengi Sana yanaibuka miongoni mwa watu waliokuwa hapa,imekuwaje tukio litokee ndani ya dakika chache halafu askari polisi wafike haraka.?,na kwa nini walipita moja kwa moja mpaka kwenye chumba namba 45 alichokuwepo Gray na Leyla bila ya kuuliza kwa wenyeji..!.
**
Askari polisi waliokuwa nje ya hoteli wakakaa chonjo endapo Gray akionekana wamkamate,cha ajabu Gray haonekani ilihali ni dakika chache tu zimepita tangu askari polisi wafike hotelini.
Mageti yote mawili ya hotelini yakafungwa,waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari hawakutaka kupitwa na jambo,kila mmoja aliparangana kupata maudhui ambayo angeliweza kuyachapisha.
Upande wa pili kwa inspekta Alexander Dickson alikuwa amefika kwa meneja wa hoteli,bahati nzuri meneja alikuwepo usiku wa Leo tofauti na siku nyingine ambazo huwa anaenda kupumzika kila usiku na kumuachia msaidizi wake.
Meneja wa hoteli hii anafahamika Kama Musa,wengi hupenda kumuita 'BIG'(mkubwa) kutokana na umbo lake la unene na kitambi alichonacho,Meneja Musa aliongozana na inspekta Alexander pamoja na askari wawili mpaka ndani ya chumba kinachotunza kumbukumbu zote za CCTV, ndani ya kile chumba kulikuwa na kompyuta kubwa tatu ambazo zilionesha mbashara matukio yote yanayoendelea ndani ya hoteli,vilevile kompyuta hizi hutunza kumbukumbu za matukio yaliyopita.
Inspekta Alexander akamgeukia askari wake mmoja.
"Hebu pekua Kama tunaweza kumuona huyu mpuuzi"
"Sawa kamanda" Askari polisi akasogea kwenye kompyuta zile,akaanza kutazama kamera moja baada ya nyingine kuangalia Kama wanaweza kumnasa Gray.
Wakati askari anaendelea kupekua kompyuta,Inspekta Alexander akamuuliza meneja Musa.
"Leo ni siku ya jumapili,siyo rahisi Sana kumuona meneja akiwa eneo la kazi tena usiku,kulikoni..?" (Akamtazama kwa kumkazia macho)
Meneja 'BIG' akapatwa na kigugumizi.
"Aah..aa..unajua eeh..Leo nime..nimepata mwaliko kwenye sherehe iliyokuwa inaendelea ghorofa ya tatu"
"Ok,mchango ulikuwa shingapi?"
Swali la inspekta Alexander Dickson likamfanya meneja 'BIG' akae kimya maana hafahamu mchango wa harusi na wakati amedai kwamba alikuwa na mwaliko.
Askari polisi aliyekuwa anapekua pekua CCTV kamera akakatiza maongezi ya inspekta Alexander na meneja 'BIG'(Musa)
"Mkuu ,matukio yote ya nyuma yamefutwa,inaonekana muuaji alikuwa amejipanga kulifanya tukio hili"
Inspekta Alexander akatikisa kichwa
"Sasa kwanini amuue mke wake.! Tena siku ya Furaha Kama hii..! Kwanini asingemuua kabla ya ndoa yao kufungwa!!" (Inspekta Alexander alikuwa na maswali mengi Sana kichwani kwake)
"...Twendeni nje tukaendeleze msako,huenda tukafanikiwa kumpata muuaji" Alexander na askari wengine wawili wakatoka ndani ya chumba kinachotunza kumbukumbu za CCTV kamera, wakamuacha meneja BIG akiwa anakuja kwa nyuma.
Baba Leyla aliumia Sana baada ya kumuona mwanae akiwa ameuawa,machozi ya huzuni yakamtoka.
"Mwanangu..., mwanangu" Baba Leyla alizidi kuumia kila alipomtazama mwanae.Madaktari na wahudumu wa msalaba mwekundu wakaingia chumbani kwa ajili ya kuandika mambo ya kitabibu na kuuandaa mwili kwenda mochwali.
Baba Leyla akavuta pumzi ,macho yakamtoka kwa ghadhabu, akatoka nje ya chumba kwa hasira na kuwaacha askari polisi na wahudumu wa afya wakiwa wanakamilisha taratibu zao,moja kwa moja Baba Leyla akashuka ngazi Mpaka alipowaacha wageni waalikwa,akakuta wameruhusiwa kukaa kwenye viti vyao na askari, Baba Leyla akatupa macho kwa mama Gray ambaye alikuwa amesimama karibu na askari polisi aliyeshika kalamu na karatasi,Mama Gray alikuwa anaulizwa maswali kadha wa kadhaa na askari polisi kumhusu mwanae.
Baba Leyla hakufikiria mara mbili,machungu ya kumpoteza mwanae yakamfanya asiamue maamuzi mazuri,Baba Leyla akakunja ngumi Mpaka misuli yake ikakakamaa,akaanza kupiga hatua kusogea eneo alilopo mama Gray.
Baba Leyla anataka kwenda kumpiga makonde(ngumi) Mama yake na Gray kwa sababu mtoto wake Gray amesababisha kifo cha mwanae Leyla.
Itaendelea.....
????KWANINI GRAY KAMUUA MKE WAKE SIKU YA HARUSI..?KUNA SHIDA GANI?
????BABA LEYLA ANATAKA KUMSHUSHIA MAKONDE MAMA GRAY AMBAYE UMRI WAKE UMEENDA????
????WATAFANIKIWA KUMPATA GRAY(BWANA HARUSI)?
Muendelezo mpaka mwisho sh 1000
Unaweza ukaipata kupitia WhatsApp 0781858056
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

















Maoni