*GENERAL SILI SILALI JUU YAKO* *16--20* *
*SEHEMU YA 16*
Kisha shangazi slimpigia simu mjomba na kumpa taarifa:
"Mumewangu hapa nyumbani kunamgeni, mgeni mwenyewe ni mama yake na Laura hivyo nimeona nikupe taarifa, anataka kumuona mwanae"
"Mkewangu subili kwanza, Laura yupo hapo nyumbani?
"Ndio yupo Mumewangu"
"Subili nakuja hapo sio muda, sitaki aumie Laura wangu"
"Sawa japo ameomba amuone wakati nakupa taarifa kama yeye yupo"
"Hapana nakuja hapo"
Mjomba alitoka na kuanza safari ya kurudi nyumbani, ili kuja kuzuia nisiumie kabisa, kwani nimuda mrefu sana usema ukweli hata sura ya mamaangu siijui kabisa, ninajuaga mama mzazi hayupo duniani yaani amefariki, kwani haji hata kuniona, na ndio maana mjomba hataki niumie kabisa, nikiwa chumbani kwangu sina hili wala lile nilipigiwa simu na General Ethane akaniambia:
"Naomba nikuone, kwani ninazawadi yako kipenzi changu"
"Ethane bwana!, unajua sipo sawa, na nawezaje kuja huko sasa, eeh!?
"Nakutumia usafili, utafika hapo sio muda mrefu jiandae mpenzi wangu "
"Baby!"
"Please baby"
"Ok"
Kisha nilianza kujiandaa, muda sio mrefu mjomba aliingia nae, baada ya hapo alitumwa dada wa kazi na kuja kuniita, bila kusita nikatoka na kwenda hadi sebreni, nilipo muoma mjomba yupo hapo nilifurahi na kumfuata nikamkumbatia na kumuambia"
"Mjomba umesahau kitu gani nyumbani, ungeniagiza mimi mwanajeshi wako faster ningekuletea"
"Nimerudi kwasababu nimekukumbuka wewe kipenzi changu"
"Mjomba bwana haya umeniona sasa umefurahi, nataka baadae nitoke naenda kukutana na rafiki yangu, ambaye niliekuwa nae kambini anaitwa Nancy"
"Mimi siutumii mudawako wote kipenzi changu utaenda tu"
"Ok sawa"
Unamuona huyu hapa mgeni?
"Ndio nimemuona mjomba"
"Huyu ni dadaangu ambaye ni mamayako wewe"
"Mh! Mjomba bwana acha basi masihara yako, nilikuwa najiandaa mimi utanichelewesha nitamfanya Nancy anisubili sana"
"Laura siku danganyi na ndio kikubwa kimenirudisha hapa nyumbani japokuwa hakuja kwa utaratibu amezuka kama mvua tu sijui kakumbuka nini?
Nilishtuka sana na nikasimama huku nikimtizama kisha nikamuambia shangazi:
"Wewe ndio mama yangu mimi ninaekujua na huyu ndio baba kwangu, hao wengine naomba mkiwajua nyie inatosha, naomba mnisamehe"
Nilipoongea hivyo kisha nilisimama na kutoka mbio nikaenda chumbani kwangu na kujifungia mlango nilijisikia vibaya sana kisha nilianza kujiandaa ilinitoke, huku mama alianza kulia na mjomba alibaki akimtizama tuu kisha alimuambia:
"Lakini dada mimi nilijua tuu tangu umenikabizi mtoto ni muda gani sasa hadi leo hii, ana haki yakufanya hivyo, hata ningekuwa mimi pia ningefanya hivyo, kwani unataka nini hasa ulivyokuja, eeh! Umuone kisha ufanyeje, hukuja siku zote uje leo, nibora hata usingekuja bwana"
Mama alizidi kulia na shangazi nae akamuambia:
"Nilijua tuu hichi ndicho kinakuja kutokea, wifi kama kweli unampenda ungekuwa unakuja kumuona hata baada ya miezi miwili unakuja mala moja, lakini tangu umetukabidhi mtoto akiwa na miaka miwili, leo hii katoka jeshini anamiaka ishirini, nimtu mzima kabisa anajua mimi ni mama na mjombaake ndio baba, alafu leo hii tumuambie wewe ndio mzazi wake, kweli hatakama niwewe unaweza kuvumilia maumivu yake, jibu ni hapana, haya sasa muache mwanangu na uondoke tafadhari nakuomba sitaki kumuona hana raha"
Nilitoka chumbani na kupita sebreni nikiwa nimekasirika, huku ninatokwa machozi kwa hasira, niliubamiza mlango na kutoka nje nilienda hadi nje ya geti kabisa, nikakuta usafili niliotumiwa na General ukiwa unanisubili, kisha nikaingia na kuondoka zangu, nae mama alipoona kachafua hali ya hewa aliamua kuondoka zake, kilamutu alikuwa kavurugwa kabisa, nilienda hadi kwa General alipomuelekeza dereva anipeleke, nilimkuta kasimama ananisubili, nilipofika nilishuka na kumkimbilia kisha nikamkumbatia huku nikiwa nalia, alishangaa kuniona nipo kwenye hali hiyo, akanishika mkono na kunipeleka kwenye kiti nikae, kisha alinianza kuniuliza:
"Nini tatizo mpenzi wangu?
Nilishindwa hata kumuambia nilikuwa bado nalia, kwani nilikuwa na hasira sana, kisha General alienda kunichukulia maji yakunywa, kisha akanipa na kunituliza kidogo, akaendelea kuniuliza:
"Nini tatizo hembu niambie, kitu gani kimekupata Laura?
Kisha nianza kumsimulia:
"General leo kuna mmama kaja nyumbani kwetu, na mjomba akanitambulisha kuwa yule nimamaangu mimi, yaani nidadaake nilishindwa kumuelewa kiukweli, kwani mimi siku zote nimekuwa nikijua hao ninao kaa nao ndio wazazi wangu mimi, sitaki mtu yeyote mimi wote niwaogo tuu kwangu"
"Haya basi tulia nipo hapa mimi mpenzi wangu, hakuna atakae kudanganya tena sawa"
"Sawa"
Je unavyodhani Laura atamuelewa mamaake mzazi au ndio hataki kabisa kudanganywa tena ili kujua endelea kufuatilia.................
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi