ðºððððð ððððð ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð: 11
niahidi utakuwa sawa tu.â
Nilikuwa natokwa na machozi nikisema âdada unaongea kama unaniaga vile, hakuna kibaya kitatokea. Utakuwa salama, niahidi utatetea uhai wako.â
Dada alitabasamu na kusema âNakuahidi, sikia mdogo wangu. Nampigia simu shemeji yako, ila hapokei simu yangu. Nenda kwake. Mwambie hali yangu pengine atakuja.â
Nilitabasamu na kusema âUsijali, nitafanya hivyo. Sasa jiandae mimi nitakuwa nje nakuombea sitaondoka mpaka ujisikie nafuu.â
Dada yangu alitabasamu, aliniambia ânashukuru mdogo wangu nitakuwa sawa.â
Nakumbuka nilitoka katika kile chumba nikilia, hata boss wangu aliponiona alinihurumia sana, alikuja na kunikumbatia akisema âtotoo, unaweza ukaacha kulia tafadhali. Unapolia unaniweka katika wakati mgumu sana. Moyo wangu unavuja damu na jasho. Nakuomba sana kipenzi, nakuomba mno Ndeana wangu, usilie, acha kulia.â
Nilikumbatia nikisema âdada alikuwa sahihi, tungeacha kwanza baba apone. Nitawapoteza wote sasa, vipi kama wote wakiniacha.â
Aliniziba mdomo akisema âUnaongea nini Ndeana, unaongea upumbavu gani tukiwa katika wakati wa majonzi namna hii. Wote wanapata tiba kipenzi. Wote wanatakiwa kupona. Wangebaki bila matibabu ndiyo hatari zaidi.â
Nilimuuliza nikisema âdada yangu, dada yangu hatokuwa mama tena si ndiyo.â
Nakumbuka aliniambia âNdeana, yeye atashindwa kubeba watoto lakini wewe utaleta watoto na watamuita mama. Ndeana dada yako atakuwa mama kwa namna yoyote ile ila lazima ataitwa mama. Mungu anapofanya jambo fulani, anakupa na namna ya kukufanya upate amani juu ya mambo hayo. Sikia mpenzi, Unanipenda?â
Nikawa namuitikia tu kwa kichwa, na yeye aliniambia âkama unanipenda basi unatakiwa uniamini pia. Dada yako atapona, na baba pia atapona kwasasa tunatakiwa tuondoke hapa ili usishihudie ya hapa tukirudi hapa kila kitu kipo sawa.â
Nikamuuliza nikimtazama usoni âina maana hutoondoka?â
Aliniambia hivi kwa upendo ânitaondoka Ndeana ila sio sasa wala usiwe na haraka. Hata ikinibidi nikae pembeni yako usiku mzima ili wewe upo sawa nipo tayari.â
ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð: 112
Nilijikuta natabasamu machozi yakonitoka na kumkumbatia nikisema âNakupenda sana, wewe ni mwanaume wa pekee sana. Nakupenda mno. Stewart, baki na mimi, Nakupenda.â
Alinikumbatia na kuniuliza âUnaweza tena kurudia hayo maneno?â
Nikasema nikiwa nimemkumbatia kwa nguvu nikilia âNakupenda sana.â
Akaniambia kwa utani âTotoo, kwani kulia si ni haramu?â
Nikajikuta natamani kucheka ila siwezi nina huzuni sana, huku nalia nilisema âni haramu baby wangu, dini hairuhusu..â
Akaniuliza âumeniita baby!!!!â
Nikamtazama na kusema âKipenzi, unaweza kunisindikiza huko kwa mpenzi wa dada?â
Akaniambia âbila shaka, tukirudi hapa mambo saafi.â
Tukiwa tumeshikana mikono kwa pamoja tulitoka mimi na yeye tena kwa upendo mkubwa sana.
Tukiwa barabarani kiukweli sikuwa naweza hata kuzungumza. Sikuwa na utulivu, mara nisali kimoyomoyo, mara nilie, mara nifumbe macho mara nijikumbatia. Watu wangu muhimu wawili sasa wapo hospitali, siku moja, nitafanyaje mimi peke yangu. Mungu wangu!!, nachanganyikiwa.
Boss wangu yeye alikuwa ananihurumia tu, kuna muda alinishika mkono na kuniachia, kuna muda alinitazama kwa huruma lakini angefanya nini.Hakuwa na la kufanya zaidi ya kukubali tu lile ambalo linatokea mbele ya macho yake.
Nakumbuka tulifika mpaka anapoishi shemeji. Mpenzi wangu mimi yaani My boss, alishuka kwa gari ila hakusogea. Alikuwa ananitazama tu huku mimi nikiwa naenda kwa huyo shemeji, yaani mpenzi wa dada.
Nilishtuka sana baada ya kufika mlangoni, usiku ule nikawa nasikia ndani sauti za vicheko kati ya mwanamke na mwanaume. Nilishika moyo wangu shemeji asiwe ana msaliti dada yangu. Katika hali ile ya maumivu asifanye hivyo. Niligonga mlango. Aliuliza ânani?â
Kwakuwa nilitaka atoke, basi sikujibu nikagonga tena , akatoka. Aliponiona alishtuka sana. Kabla sijasema kitu mwanamke pia alitoka na upande wa kanga kwani mwanaume alikuwa na taulo tu. Nilitabasamu huku moyoni ni kama vile kisu chenye ncha kali kimenipitia. Hata boss wangu kipenzi alikuwa ameona hilo. Alianza kusogea.
ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð: 113
Nilifumba macho na nikawa naona dada yangu anavyopambana hospitali na mwanaume wake yupo na mwanamke mwingine wakati yeye mpaka dakika za mwisho anamuwaza. Nikajikuta nasema âSo, ndiyo maana hupokei simu za dada kwasababu upo na mgeni?â
Akatabasamu kuzuga akisema âNdeana karibu sana. Karibu ndani.â
Nikasema âsina haja na karibu yako, hata kitu nilichotaka kukuambia naona hapa sio sehemu sahihi. Endelea na mgeni wako.â
Yule dada akaniuliza âkwani kuna nini hapa?â
Nikamwambia kwa ukali na hasira âmuulize huyo mwanaume wako ambaye hana hata aibu, shemeji nilikuona mtu wa maana sana. Kumbe ndiyo walewale kasoro majina. Sawa ila utamkumbuka dada yangu mjinga sana wewe.â
Mpenzi wangu wangu wa moyo alinifikia. My Boss, Mr Tarick. Mbele yao aliniuliza âMy sweet person, kuna nini hapa?â
Nikalia kwa uchungu nikisema âAnamsaliti dada yangu, yaani dada yangu anampenda sana mpaka dakika za mwisho anamuwaza mwanaume ambaye yupo kifuani kwa mwanamke mwingine. Ni tabia gani hii?â
Yule mwanaume aliingia ndani akabaki yule dada, alibaki anatutazama tu. Baby wangu alinikumbatia na kusema âimekuwa vizuri hili limetokea totoo, tumejua mapema kuwa hampendi, kwahiyo huyu sio sahihi kwake. Mwanaume anayekupenda hawezi kukusaliti.
Mwanaume anayekujali hawezi kufikia hatua ya kuleta tena mwanamke mwingine ndani anapokuwaga na mpenzi wake. Huyu hana adabu wala heshima. Tuondoke hapa. Acha kulia na usimwambie dada mpaka atakapokuwa sawa.â
Nilimtazama na kusema âroho inaniuma sana, anawezaje kumfanyia hivi dada anavyompenda namna ile.â
My boss alinitazama na kunishika mkono kisha tukaingia ndani ya gari akisema âkipenzi, Ndeana wangu. Mtu akitaka kukuumiza. Hakuchagulii namna ya kuumia haswa kwenye mapenzi.
Hajali kama unampenda na kumjali. Kwasababu yeye haoni furaha kwako, haoni thamani yako wala hawezi kukufurahia kabisa. Ndiyo maana anakuumiza na hawazi lolote. Mbaya zaidi hujiona mjanja sana. Ndiyo hivyo.â
Nilimtazama tu nikafuta machozi nikisema âtupite nyumbani sasa tuchukue nguo.â
ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð: 114
Akaniambia kwa upole âsawa mumy wangu.â
Kivivu nikatabasamu.
Akatabasamu pia akisema âkwani totoo kuigiza ni haramu?â
Nikamuuliza âKuigiza tena?â
Akaniambia ândiyo tuigize kama hakuna matatizo.â
Nikamtazama na kusema âkivipi sasa?â
Akacheka akisema ânimemiss husu kwakweli?, ina maana huwezi hata kunibusu hata kidogo tu.â
Nikashusha pumzi nikisema âhuoni nina matatizo lakini?â
Alinitazama na kusema âSio mimi totoo, nikiwa na wewe nakua tu sina akili. Nimemiss busu lako kwani ni haramu?â
Nikajikuta nacheka kivivu kisha tukaendelea na safari hata tukafika nyumbani. Nilimkaribisha nikisema âkaribu sana hapa ndiyo nyumbani kwetu. Mimi, dada yangu na baba yetu. Karibu sana.â
Alitabasamu na kusema âWewe huyo wakati mdogo, tabasamu vilevile. Ndeana huyu ni nani?â
Nikatabasamu na kusema âni mama yangu.â
Akatabasamu akisema âmimi na baba ni sawa sawa kwenye kuchagua. She was so beutiful.â
Nilitabasamu na kuanza kupapasa picha ya mama nikisema âmpole na mkarimu pia. Mama alikuwa na huruma na mcheshi sana. Yeye na baba walikuwa marafiki sana. Baada ya mama kufariki, baba aliteseka sana. Ila tupo hapa kumchangamsha. â Nikavuta pumzi na kusema ânaomba nisubiri narudi sio muda.â
Nilimuacha akiendelea kushangaa ndani kwetu. Atajua yeye kama alikuwa anashangaa ile Tv ya chogo na deki yetu ambayo mlango upo wazi muda wote. Au kama alikuwa anashangaa kabati la vyombo pale sebuleni ambalo vioo vyake vyote vimetoka au sabufa yetu ya mchongo.
Sijui, labda vile viti vyetu ambavyo vitambaa vimechakaa hata godoro la ndani linaonekana au usafi wa nyumba yetu, maana kwenye usafi tupo vizuri na wala hatuna shida ndogo ndogo tunakula, tunavaa na kulala safi kabisa. Labda kama alikuwa anashangaa stuli zetu zenye miguu mipana. Sisi wala hatuna shida wacha asafishe macho.
Mimi nikiwa napanga baadhi ya nguo simu yangu iliita. Alikuwa ni Joan. Basi nikamsimulia naye alisikitika na kunipa pole nyingi sana huku akisema âSasa kipenzi naweza kuja hapo hospitali nikupe kampani maana upo peke yako.â
ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð: 115
Nilitabasamu na kusema âsipo peke yangu. Usijali kuhusu hilo Joan. Nipo na mpenzi wangu. Kwasasa wewe pumzika kesho ukiwa na nafasi utakuja.â
Aliniambia kwa upole âsawa kipenzi. Kesho asubuhi nitawahi ibadani na kisha baada ya hapo nitakupigia. Kukiwa na chochote unahitaji niambie sisi ni marafiki.â
Yaani akisema hivi naumia, unajua huyu kavuliana nguo na mwanaume wangu ila nitafanyaje sasa ndiyo tumependana kama marafiko na vile akisimulia lazima boss atajwe huwa natamani kumwambia acha kumsema Baby wangu ila nakosa nguvu kabisa. Sasa ndiyo basi tena.
Nilitoka na kukuta bado anatazama picha ukutani tena ile ambayo tupo na baba na mama. Alikuwa kama analia hivi. Nikamtazama na kusema ânimemaliza sasa, tuondoke?â
Alitabasamu na kusema âNyumbani kwenu ni pazuri sana. Najua nimefika hapa bila utambulisho rasmi ila naamini nikirudi tena hamtonifukuza si ndiyo.â
Nikasema âHata sasa umefanya mengi sana kwangu na familia yangu. Karibu sana jisikie upo nyumbani ingawa ni heshima mbaya hii wewe kuja bila utambulisho.â
Akatabasamu na kusema ânipo tayari, nijitambulishe ili nije kuona furaha za nyumba hii. Tazama hii picha. Baba Yenu ni baba mzuri sana, na mimi natamani kuja kuwa baba mzuri sana kwa watoto na mke wangu.â
Nikatabasamu na kumuuliza âbaba yako yuko wapi?â
Alinitazama na kisha alitabasamu akisema âalifariki.â
Nikamwambia âpole sana. Baby tuondoke sasa.â
Akanitazama na kusema âMpenzi wangu, najua unavyojisikia. Ila naomba nikubusu, mimi akili inatamani busu lako.â
Nikalalamika âLakini baby!!â
Akanivuta akisema âMy sweet person, usiwaze kingine chochote nataka ujisikie vizuri. Naomba midomo yako mitamu please. â
Nikamtazama yeye akanikumbatia na kunisogeza karibu yake, na kisha alianza kunibusu na ulikuwa ni usiku sana.Kidogo nilisahau maumivu, maana akili ilizingatia busu. Wakati ananibusu simu yake ikaita. Haraka aliniachia akisema âitakuwa dokta nilimwambia apige simu akimaliza.â
Nikasema kwa hamu ya kutaka kujua âanasemaje, pokea, pokea.â
ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð: 116
Ndipo alipokea na kuweka sauti ya juu ili kusudi na mimi nisikie. Nilimsikia dokta akisema âTunashukuru Mungu, watu wa upasuaji wamemaliza salama na mgonjwa wetu katoka salama. Ingawa kwa sasa bado amelala ila mnaweza kumuona.â
Nilijikuta napiga magoti nasema âAsante Mungu, Asante Mungu wangu.â
Huku mpenzi wangu anavyohangaika utafikiri yule ni dada au ndugu yake. Alipomalizana na dokta tulijikuta tunakumbatiana kwa furaha huku nikisema âtuondoke sasa, tuondoke.â
Boss alitabasamu na kusema ânipe kabusu kafuraha sasa.â
Basi nilimkumbatia na kuanza kumbusu usoni, macho, bua, shingo, mabega, kichwani, midomo, kidevu, kifuani yaani mimi nambusu kila mahali hata alianza kucheka akisema ânilikuambia atapona, sasa nikufanyie nini kingine unibusu kila sehemu yaani sehemu zote.â
Nikamtazama na kucheka nikisema âMjinga sana wewe. Sehemu zote ndiyo nini sasa.â
Tukacheka, tunaondoka tukiwa na furaha yaani sisi tumeshikana mikono hatuna habari hata tumesahau dada kasalitiwa. Hakika mapenzi ya kweli na mazuri hata katikati ya maumivu huleta furaha.
Tulifika hospitali na kweli tulienda kumuona dada yangu. Dada yangu alikuwa amelala tu bado hakuwa ameamka.
Nilimshika dada yangu nikisema âNimefurahi sana dada yangu, najua sasa utakuwa sawa kabisa. Najua Mungu atatupa namna nyingine ya kufurahi. Asante kwaajili yangu. Nakupenda sana dada, nilichanganyikiwa, nilijua sitakuona tena unajua.â
Mpenzi wangu alinitazama na kusema âtotoo, inatosha usiongee sana.â
Nilimtazama na kusema âsikuwaza siku nitakuwa na wagonjwa wawili. Twende kwa baba. Nimechoka sana.â
Alinishika mkono na nikamwambia âtangulia kwa baba mimi naenda kwa dokta nikazungumze naye.â
Taratibu nilielekea kwa dokta. Lengo nikajue gharama nianze kupunguza. Nilipofika kule dokta aliniambia âmpenzi wako amemaliza kila kitu. Kuanzia bill ya baba na ya dada. Hapa labda tutajua mpaka mwisho itakuaje ila kwasasa kila kitu safi. Huna deni hapa.â
Nilitoa macho na kuuliza âKalipia kila kitu.â
Alinitazama na kutabasamu akisema âhakika. Kila kitu tayari.â
Nikamtazama Dokta na kusema âkaribu sana.â
ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð: 117
Nilitoka nikitamani kulia kwa furaha, ni mwanaume gani anajali wazazi wangu familia yangu tena kwa mara ya kwanza. Angekuwa mwingine angeniuliza nina kiasi gani au familia iko wapi. Huyu kafanya tena bila kutaka asante yangu na hajasema kitu. Nilikuwa najiambia tu âAsante Mungu, asante Mungu.â
Nilifika mpaka chumbani kwa baba, nilikuta Boss anaongea na baba. Ila baada ya mimi kuingia aliacha akawa anacheka tu. Nikamtazama nikisema âUnamwambia nini baba yangu?â
Alitabasamu na kusema âninavyokupenda.â
Nikatabasamu na kusema ânaona hata baba sura walau sasa imechangamka. Kesho inaweza kuwa siku nzuri sana.â
Alisema âkabisa, dawa zinafanya kazi vizuri, wala usiwe na shaka atakuwa sawa.â
Baba alikuwa anatazama tu ila haongei. Nilitabasamu kwa huruma na kusema âbaba lala sasa. Mimi nipo nje hapo.â
Baba alitazama tu. Basi mimi na baby wangu tulishikana mikono na kutoka nje.
Tulikaa kwa benchi pale nje. My boss alinilaza mapajani mwake akisema âunatakiwa kupumzika kidogo. Ni usiku sana sasa na umekuwa busy mwezi mzima huu utaumwa totoo.â
Nililala mapajani nikisema ânapenda harufu ya mwili wako. Unanukia vizuri sana.â
Alitabasamu na kusema âNa wewe utapenda haya marashi.â
Nikajibu kwa upole ândiyo, yananukia vizuri.â
Akasema âsawa kipenzi, pumzika kwanza. Nakupenda sana.â
Nilijibu ânakupenda pia huku nikiwa nasinzia kwa maana nilikuwa nimechoka sana.
Asubuhi palikucha. Ila Niliamka nikiwa chumbani kwa dada pale hospitali. Na dada hakuwa ameamka. Nikiwa namsalimia dada yangu, alikuja Boss, alinisalimia akisema âMorning my sweetperson.â
Nikatabasamu. Akaniambia âAsubuhi uzuri wako unazidi. Unawaka sana mpenzi.â
Nikatabasamu tena na kusema âkwani ulinibeba?, nimefikaje hapa?â
Akacheka na kusema âbaba anakuita, ameamka vizuri leo.â
Nikasema âunasema kweli?â
Akatabasamu. Nami nikatoka pale haraka kwenda kwa baba yangu.
Nilipofika nilikuta baba yangu anafanyiwa vipimo. Nilifika na kumtazama na yeye alinitazama akitabasamu. Niliita âBaba!!â
Na yeye aliitikia kwa upole âNdeana wangu!!â
ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð: 118
Mpenzi wangu aliingia na kututazama tu. Kisha nilimkumbatia nikisema ânimefurahi sana umeamka baba. Nilikuwa nakuwaza sana.â
Baba alisema kwa huruma ânisamehe nawasumbua wanangu.â
Nikamtazama nikisema âhata hunisumbui, kwanza unakula nini baba. Utakuwa unanjaa, ule unywe dawa.â
Niliona baba akimtazama Stewart akisema âmwanangu alishaleta chakula, kanibadili nguo ina maana hunioni. Wewe ulichoka sana na sasa muda umeenda sana.â
Nikajikuta namtazama Stewart kwa upendo sana, nikamwambia âAsante sana. Mungu akubariki.â
Alinijibu kwa tabasamu âNashukuru, lakini leo nakuacha kidogo. Nina kazi nyingi ila nakuahidi nitarudi mapema.â
Nikasema kwa huruma âhapana, nenda kapumzike kidogo. Kisha baada ya hapo utakuja jana hujalala ujue na leo umewahi kuamka.â
Akatabasamu. Kisha baba aliniambia âMsindikize mwenzio mwanangu.â
Nikatabasamu.
Nakumbuka nilitoka na Stewart mpaka kule ambako gari lilikuwa limesimamishwa. Kabla hajaingia kwa gari nilimshika mkono na kusema maneno haya machozi yakishuka taratibu kwa hisia za upendo zinazowaka ndani yangu, ninayakumbuka sana âStewart mpenzi wangu. Sina neno zuri la kuelezea hisia zangu juu yako kwa haya yote ambayo umeyafanya kwangu na familia yangu. Wewe sio mpenzi tu ila ni maisha yangu pia.
Sijui bila yako peke yangu ningefanya nini. Ninakupenda kwa kiasi ambacho siwezi na sitaweza kusema nikaeleweka. Siku zote umekuwa ukisema unanipenda. Naomba sasa iwe zamu yangu.
Stewart moyo wangu ni nyumbani kwako, hisia zangu ni chakula chako. Nipende kama ninavyokupenda. Mapenzi yetu yawe yenye furaha na amani. Asante kwa kila kitu, asante kwa kufanya maisha ni marahisi pamoja na wewe, asante kwa kuwa na mimi nyakati ngumu, asante kwa kubeba familia yangu kama yako, asante kwa kunichagua na kunipenda, asante umekuwa wangu, wangu wa maisha, wangu peke yangu. Nakupenda sana Stewart.â
Alinikumbatia akisema âmimi nilishasema yote. Nakupenda kuliko mwanamke yeyote hapa duniani. Ndeana wewe ndiyo Penzo langu la kwanza na la mwisho.
ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð: 119
Sitakuja kupenda tena nasikia raha na amani kuwa kando yako. Familia yako ni yangu pia. Na yangu ni yako pia. Nataka tuwe kitu kimoja kama familia.
Nilikuambia nafsi mbili zikielewana kila kitu kinakuwa sawa. Nafsi yangu na yako, yako na yangu zimefungamana, zimeshikana, yaani zimeungana na kuwa nafsi moja.
Hakuna mimi Stewart bila Ndeana.â
Nikatabasamu nikisema âHakuna Ndeana Bila Stewart.â
Akatabasamu na kusema ânenda kwa baba sasa.â
Nikatabasamu na yeye akanifuta machozi.
Alipomaliza, nilianza kuondoka. Nilipiga hatua chache akaniita âMy sweet person!!â
Nikageuka, akaniambia âutahitaji chochote?â
Nikamwambia âno, labda wewe tu.â
Akatabasamu na kusema âdada akiamka mwambie asijali. I will make her happy.â
Nikacheka tu, kisha akaniambia kwa tabasamu âNakupenda.â
Nami nikatabasamu na kurudi kumkumbatia.
Kisha baada ya hapo alinongâona masikioni, wenzio wamekuja kukuona wanatushangaa. Nikashtuka. Kugeuka nyuma naona wasichana watatu wa kazini akiwepo na Joan. Yeye wala hakujali, aliwasalimia na wao wakamjibu kwa nidhamu tu. Kisha Stewart akasema âtotoo, see you.â
Nikatabasamu tu kwa aibu maana wenzangu walikuwa wanatazamana tu ingawa moyoni nilipata furaha kiasi ni kama sifichwifichwo tena. kisha niliwakaribisha wenzangu tukaingia ndani.
Niliwapeleka kwa baba yangu. Baba aliwasalimia nami nikawatambulisha kwa baba yangu. Baba alifurahi sana. Na kisha nikawapeleka na kwa dada yangu ambaye tayari aliamka. Bado hakuwa sawa muda mwingi machozi yanamtoka ila hakuwa na budi kuyakubali tu. Wageni waliona sio wakati mzuri kuendelea kuwepo pale. Hivyo waliniaga nami nikawasindikiza.
Tukiwa nje, Joan alinivuta pembeni nakumbuka alinitazama na kusema âmbona hukasiriki, hunichukii na una mahusiano na Boss.â
Nikamtazama na kumuuliza âsasa kwanini ninune. Yamepita ilikuwa zamani na sasa ni wakati wangu.
ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð: 120
Joan aliniambia ânisamahe sana Ndeana. Laiti ningejua wala nisingefanya hivyo. Pia hongera sana. Natamani niseme naomba namba ya mganga wako ila nitakuwa nachekesha. Yule mwanaume mwanamke hamrudii na hajawahi kuhangaika na mwanamke. Sasa mwenzetu umempa nini.â
Nilitabasamu tu, na kisha nilisema âNi Mungu tu, sijui ya Mbele ila Tunapendana sana.â
Alinitazama na kusema akitabasamu âsasa naelewa kumbe ndiyo maana alikuwa...â
Nikacheka nikisema ânendeni sitaki umbea mimi.â
Nilibaki nawatazama wakiondoka huku nikiwa na hakika kuwa habari zangu zitaenda kutapakaa kazini. Nilikuwa natabasamu tu maana penzi ni kikohozi alifichiki katu.
Nilitoka nikarudi kwa dada yangu, nilipofika akanitazama na huzuni akaniuliza âYupo hapa?â
Nikamtazama tu na kutikisa kichwa changu.Dada yangu akauliza tena âulienda?â
Nikamjibu ânilienda lakini nikamkuta..â
Kabla sijajibu alijibu yeye mwenyewe âna mwanamke, mjinga ni mimi, nimekuwa nikimfumania mara nyingi anaomba radhi namsamehe tena. Ona sasa akijua hata sina uwezo wa kuzaa atafanya nini, si ndiyo atasema kabisa hanitaki.â
Nikashangaa na kuuliza âkwani dada bado unasubiri kuambiwa hakutaki. Utabadilika lini dada ujinga gani hata kwenye mapenzi. Sikia dada wewe ni mzuri sana. Utapata tu mwanaume mzuri sana.â
Dada yangu akalia kwa uchungu sana, alilia akilalamika kuwa nani atampenda na hana uwezo huo wa kuzaa.
Haukuwa wakati mzuri kwangu kabisa. Maana tena ilinibidi nikaongee na baba. Ila tofauti pengine baba aliumia moyoni tu. Zaidi alinitazama na kusema âNipeleke kwa binti yangu nikamuone.â
Nikachukua kiti mwendo kwa maana baba bado hakuwa na nguvu vizuri. Nilimsukuma mpaka kwa dada. Nilipofika dada alianza kulia kumuona baba yake. Ilinibidi nitoke maana najua tena baba na mtoto.
Nilikaa nje peke yangu nikitia huruma tu. Hakuna kitu kigumu kama kuuguza. Yaani mimi siku ya pili ndiyo inaanza ila nipo hoi maana wagonjwa wewenyewe wana maumivu sana. Ila nitafanyaje.
Muendelezo sh 1000
Njoo WhatsApp 0743433005


Maoni