SHAMIRA 44 kwa 45
Sehemu ya 44
Mwandishi; lissa wa huru media
Aseeee tulichoka mno na shoga yangu asa mimi jamani.nafanya nini na hili tumbo na mwanaume hanitaki. Na ameshakana kuwa hii mimba sio yake na hausiki nayo. Mh kazi ipo. Aisha wala hakuona aibu akainama akaziokota zile pesa zote . Akanambia twende shoga tuatajua tunafanya nini tukifika nyumbani.Basi shoga akaanikokota tu mpka stand. tukapanda gali la mbagala. Na tulivyofika mbagala tukapanda gari mpka kwetu saku. Aseeee sikuwa sawa kabisa . Yani nilikuwa na mawazo sana.na chengine kilichoniumiza ile kumkuta hamadi ana mwanamke mwengine.nikawa na waza yani mda uhuu mchache tu awe ameshapata mwanamke hapana itakuwa alikuwa anacheat.mbona mapema sana jamani. Nilijikuta ata sijielewi mpka machozi yakawa yananitoka sasa. Aisha akaniuliza unalia .aah shamira usiniangushe bwana usilie. Wewe ni mwanamke shipavu unayejua kupamabania changamoto zako plsss acha
Nikasema aisha yule ni mwanamke wake eeeh. ni mwanamke wake si ndio. Yani nilishachanganikiwa nafanya kumuuliza aisha wakati nilikuwa nae na hana analolijua ata. Akasema tulia kwanza nini bwana unataka kujipandisha mapresha shamira. Nikasema plssss kwanini anikatae vile ina maana anaona mimi nambambikia mtoto. Aisha si unaelewa kuwa sijawahi kutembea na mwanaume mwengine tangu niende kwake si unajua aisha. Akasema ndio naelewa tulia basi.nikasema sasa kwa nini anakataa mimba na wakati allinambia anataka tuzae. Kwa nini ananisusia sasa. Nauliza kwa nini mimi ntaishije mwenyewe jamani. Nililia hii siku kwa uchungu mkubwa na aswa wivu ilinikaba mno.ile kumuona ana mwanamke mzuri ndo alinivuruga mimi wallah .mh nikaona kabisa nitakuwa chizi
Basi aisha alinisogelea akanikumbatia akanambia tulia achana nae yule. Mshamba tu alafu shamira ww ni mzuri kama kaondoka yye wewe utapata mwengime na maisha yataenda shida nini acha kulia bwana.nikasema lakini mimi nampemda sana hamadi yani sana .namuhitaji mno asa katika iki kipindi. Aisha akanmbia upo na mimi achana nae bwana na asikupe mapresha ata.
Basi ilikuwa ngumu kumuelewa aisha .kuhusu hamadi. Mana nampemda sana uyu mwanaume.basi akanibembeleza sana shoga yangu mpka nikalala kabisa
Nikaja kustuka mchana mchana hivi nakuta shoga kapika ugari na dagaa . Nikavuta chakura nikala vizur mana njaa iΔΊikuwa inanuma sna. Nilivyomaliza kula nikaenda kuoga kisha nikaludi kitandani nikasema napumzika akanmbia powa shoga yangu lala kidogo na pole kwa majanga.nikasema ya dunianai ayo wala usijali. akanambia sawa
Basi niliamka usiku sana .nikawa chumbani peke yangu nikajua aisha kaenda dukani kwake. Mana ile pesa nilimpaga milioni tatu aisha alifungua fremu na akaweka vipodozi vya wadada na rosheni na chupi na taiti.yani urembo wa wanawake ule. Basi bwana nikavuta simu nikajalibu kupiga namba ya hamadi ikawa haipatikani bado.nikabaki nimechoka nawaza sana .nafanyaje na hii mimba mimi. Niliwaza mno ila sikufikilia kutoa kabisa. Mana maremu shangazi alishawahi kunambia usije ukajalibu kutoa mimba ata siku moja. Nikawa za au nizae na mtoto akishakua namwambia baba yako alikukataa au vp πππππππππππππππππ
πππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππππ
SHAMIRA
Sehemu ya 45
Wassap; 0742443214
Mwandishi; lissa wa huru media
Niliwaza sana .na mawazo yalikuwa mengi sana .ila nikawaza nikasema mimi shamira siwezi kushindwa na maisha mpka nikashindwa kumuhudumia mtoto. Nikaona lakini pia nimezingua ndo mana hamadi kachukia sana na kawa mkari sana kwangu. Ila ninaweza nikaenda tena nikaongee na hamadi vizuri alielewe ili suala jamani mh. Mimi sikuuwa nataka kabisa kuwa single mother jamani. Basi nikiwa pale nawanza mno aisha akanipigia simu. Akasema shost nataka nikununuliee chipsi nikubebee chipsi yai au kavu.akasema leta kavu tu na soda akasema sawa shost
Basi kweli akaniletea ila sikuwa sawa kabisa. Sio kwamba nilikuwa najisikia kichefu hapana .ila mawazo yalikuwa .engi sana kichwani nilikula kidogo sana. Sikuwa sawa kabisa. Aisha akasema shamira ebu kula basi. Unamuwazia mwanaume kiasi iko na alivyonichamaba mimi ata hamu naye sina. Ahaaa kajua kutuumbua yule kaka jamani. Alafu kwa nini ulikuwa hufuti sms shamira.mpaka naonekana mnafiki pale. nikasema aisha kwa sasa sitaki lawama. Naomba nipumzike niliona anaichanganya tu. Nikapanda kitandani nikawa navuata usingizi. Aseee nilipata usingizi kwa shida sana. Mawazo jamani kila nikimuwaza mwanaume nahisi kuumwa mimi. Nawaza nakuwaa single mama mimi daaah. Basi mawazo yalikuwa mengi mpka nikapitiwa na usingizi na sikujua ata nimelela saaa ngapi mimi.
Asubuh niliamka nimechoka mno.ila kidogo akri ilitulia nilienda kuoga nikaludi chumbani. Nikakuta aisha nae kashaamka anaaandaa chai. Akanmbia vp shoga yangu wa kuteswa na mapenzi unaendeleaje.nikatabasamu tu .nikasema wewe tena mimi nipo powa kidogo leo. Aisha akanambia aya ebu njoo kwanza apa tuongeee kitu. Badi nikasogea nikaaa kwenye sofa .nikasema aya nipe mchapo shoga nakusikiliza.akanambia kwanza naomba ujikaze shamira. Wewe ni mwanamke usiwe unalia lia bwana. Tuna biashara teali na umenipa msingi ile ni biashara yetu hatuwezi kushindwa kuendesha maisha yetu. plssss ebu acha kuwaza na kujikondea .halafu kitu kengine mwanaume ameshakataaa mimba na hii mimba ni ndogo shamira kwa nini usiitoe hii mimba. Mh moyo wangu ulifanya paaah. Kutoa tena kisa nini kwanza
Nikasema wewe aisha mbona umefika mbali sana sijaplan kutoa mimba ata kidogo. Kwa nini nitoe .akasema sikia kwiyo unataka kuwa single mama. Mana mwanaume kama ulivyomuona katuchamba atari na kasema hakutaki na kashapata mwanamke. Unazani ataa atamuwaza uyo mtoto. Ebu utazeeka shamira toa mimba tuludi sokoni maisha yaendelee. Na mimba kama iyo kuna mwanaume atakutamani sasa. Acha ushamba bwana katoe. Nikasema aisha mimi mimba sitoi kabisa na sina mpango wa kutoa mimba. Akasema unaogopa nini mimba changa iyo . Mimi apa nimeshatoa mimba 3 na mbona sijafa na nalipa sina mpango .na labda nikwambie shamira kuzaa sio kazi .ila kazi kulea mzigo utaweza kuulea mtoto. Nikasema niweze ama nisiweze mimba sitoi shoga yangu. Na ata kama kakataa sio mbaya kanipa zawadi ya mimba nitalea mwenyewe. Mwisho napaga mtoto wangu atanilea baadae ila kutoa mimba hapana
Ayaaa mzigoooo uoooo njoooni tuendleeeeeeeeee mambo ji motroooooooΓ²ooβ€οΈβ€οΈβ€οΈβ€οΈβ€οΈβ€οΈβ€οΈβ€οΈβ€οΈβ€οΈβ€οΈβ€οΈβ€οΈβ€οΈβ€οΈβ€οΈβ€οΈβ€οΈβ€οΈβ€οΈ
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni