AFANDE MILLAN😎 Sehemu ya 44 na 45
Basi bwana tumefika kwake, ikabidi niwaache kisha nikatoka nikaenda super market kuwachukulia mahitaji, aseee nikawabebea kila kitu cha kula, sijuh unga ,mchele, kuku , nyama, maziwa ya mtoto mana bado zena maziwa yalikuwa hayatoki, nikambebea mtoto dipers ,net , nguo, sijuh sabuni za kuogea na kufulia ,na vitu kibao yani, kisha sasa baada ya maemezi ndo nikaludi kwa zena , naikamuingizia ndani vile vjtu vyote, zena wala hakuongea kitu, na wala hakuonesha utata na mimi, na wala hakuvigimea, pale sasa nikamwambia shey, kuwa shemu inabidi ukae apa ata kwa week 2 uwe unamuangalia shoga yako si unaona hali yake kwa sasa, basi naomba hwe apa na umsaidie , na mm ntakuw nakupa elfu 70 kila iku, shey akafurahi nakwambia akanmbia kweli shemu, nikasema kweli, we kaa nae kwanza mana ana mshono hawez kufanya kazi ngumu , msaidie na mtoto uyu namuona makari kweli analia sana so atakuwa anamsumbua sana, shey akanmbia limeisha hilo shemu, mi ntamsaidia kila kitu , na kweli mm nikatoa laki 7 nikampa ya siku 10,shey akafurahi nakwambia naona hakutegemea kama atapata pesa za gafra hivyo, kisha sasa nikaingia chumbani kuongea na zena ,nikakuta anambembeleza mtoto, nikamwambia nimeshaongea na shey atakuwa na wewe apa anakusaidia mroto akanmbia sawa ,nikampa laki 3 nikamwmabia hii ya matumizi ,wala hakuleta ubishi akapokea akanmbia asante , kisha nikamuaga sasa mana daaha nilikuwa na usingizi kinoma, sikuwa nimelala vizuri kule hospital , zena akanmbia sawa karibu tena, apo sasa mimi ndo nikaondoka na kurudi kwangu
Nilikuwa nimechoka kweli kweli, nilivyofika nyumbani ,nilipiga maji moja kwa moja nikajitupa kitandani, na ilikuwa jioni kama saa 10 hivi, ila niliamka kesho yake asubuh saa 1 , mpaka kwenda kazini nimechelewa, nikajiandaa haraka haraka, na nikampigia simu zena ,heee nakuta kuanitoa block na anapatikana ,nikajua basi apa kesi imeisha ila nitulize akiri kwa zena,mana daah akichukia anakuwa na hasira sana, mi nikaongea nae kuwa anaendeleaje na mtoto , akanmbia jana mtoto kawasumbua sana hawajalala ,ila sasa maziwa yameanza kutoka ananyonya kaacha kusumbua ,nikamwmabia sawa basi mi naenda job na nikiludi nakuja na nitampa jina mtoto, akanmbia sawa hakuna shidaa, nikamuuliza vp ummy, akanmbia kashaenda shule, nikasema sawa ,basi nikakata simu na nikaelekea kazini, apo ibraa ananiuliza we na zena imekuaje tenaa mmeludi pamojaa, aseee nikamsimulia sasa ibraa mroto alivyokuwa ananipelekesha ,ibraa alicheka sana akanmbia hivi kuna mwanamke ambae umetamani kuwa nae sawa kama uyu , nikasema hapana, ibraa akanmbia we unampenda zena muoe utulie sasa, ahaaa masuala ya kuoa ya nn sasa daah
Basi bwana mi jioni nilivyotoka job tu, nikaenda kwa zena , na kweli nikapewa mwanangu, mh mkari uyu, nikajua uyu atakuwa na mdomo kama mama yangu, mana mama akinipigia simu wee kinawaka, ananimbia dawa yangu ipo jikoni mi si sitaki kuoa, basi jina nikatoa nikase.a uyu ataitwa arishaina , mama yake wala hakuwa na dhida akakubali, na nilikaa sana pale mpaka nikala pale pale , na chakura lipika shemu shey, ila sio kitamu kama akipeka zena ,weee zena anajua kupika ila sasa bado hayupo sawa, mi nikaongea sana na zena, yani hakuonesha kunikasilikia kabisa na mm sikutaka kuulizia ugomvi, nikajua kanifungulia moyo, basi na kwakua nahudumia mwanangu basi mambo yasiwe mengi na ugomvi ukaanza tena
Basi bwna mi nikaanza kulea mtoto na zena na baada ya week 2 , zena akanmbia anaendelea vizuri so nimruhusu tu shey aendelee na mjukumu yake, na mm kweli nikamruhusu shey kuwa busy na mambo yake, na zena akawa busy na malezi sasa, ahaaa nilikuwa namwaga hela mwanaume , yani nilikuwa nahudumia ile serious, mtoto akiumwa namfata zena tunaenda hospital , na nikawa sichagui sassa, ummy mwanagu na aka kadogo mwanagu, na naenda kuna mda nashinda nao sana, ila sasa mimi na zena hatukuwahi kuongelea mapenzi kabisaaa yani , ata siku moja, sisi ni kuelea tu, nikienda ni habari za watoto basi, sisi kama sisi hatukuwa na chochote amabcho kilikuwa kinaendelea kati yetu,
Tukapambana na malezi mpaka mtoto uyu mdogo akafikisha miezi 3, apo nna adabu na zena wee, simjibu vibaya ata kidogo, najua kichwa chake tu , kwaiyo heshima na adabu ilinijaaa juu yake, ila sasa nilijikuta mi namuelewa sana zena, yani sawa ni tunalea ila kuna mda natamani tu kumuona na kuongea nae, najifanya naenda kuona watoto, au nampigia simu najifanya naulizaia watoto ila sio kweli nilikuwa nammis yeye, nikisafiri sasa daah moyo naona hauna amani, yani natamani mda wote niwe na zena, ata kuongea nae tu mi nafarajika, nikipiga nikikuta simu yake inatumika mi nakuwa na wivu kwamba anaongea na nani, ila nashindwa kumuuliza mana hatuna mahusiano, naweza kusema mi bwana nilijikuta nampenda sana zena, ilikuwa ni mala ya kwanza nampenda mwanamke na kumfikilia hivii, aseeeeee acheni kabisaaa mapenzi aya , nilihisi kabisa zena kaushinda moyo wangu, au kwa sababu sijatembea mda mrefu ,mh sina uwakika... HUU NDIO MWISHO WA SEASON 2 YETU USIKOSE SEASON 3 SOON INAKUWA TAYARII
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni