TIPWA TIPWA NA MR MARVEL 19 to 20 final
SEHEMU YA 19
π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦
Asubuhi Mr Marvel alipoenda chumbani kwa Noela kama kawaida yake ili kumuamsha, anakuta chumba kipo kimya, hakuna mtu wala baadhi ya vitu vya Noela havipoπ³.
Anadhani labda ameenda chuo mapema, Anamuita dereva wake na kumuuliza kama amempeleka Noela chuoni. Ila Dereva anamjibu hajamuona hata kidogo, wala hajampeleka popote.
Moyo wa Mr Marvel unaanza kwenda mbio. Anatoa simu yake haraka na kuanza kumpigia Noela. Simu haipatikani. Anajaribu mara kadhaa lakini ni vilevile.
Baada ya muda mfupi, simu yake inatoa taarifa ya meseji mpya. Ni kutoka kwa Noela. Meseji yenyewe inasema:
βNimeondoka sababu sitaki kuwa chanzo cha baba na mwana kugombana. Badala ya kuchagua kati yangu na Salmon, ni bora mimi niondoke ili ubaki na mtoto wako kwa amani. Najua imenichukua muda mrefu kusema hili, lakini nakupenda sana Mr Marvel na ninakutakia kila la heri kwenye maisha yakoβ
Baada ya kusoma, mikono yake inaanza kutetemeka. Uso wake unabadilika, Anahisi kama dunia imesimama. Anajaribu kumpigia tena, lakini simu bado haipatikani.
Anatoka nje kwa haraka, anaanza kumtafuta kila sehemu. Anauliza walinzi, majirani, hata marafiki wa Noela. lakini hakuna anayejua alipoπ.
Siku zinapita, Wiki mbili zinaisha tangu Noela aondoke. Ndani ya muda huo, Mr Marvel hajaenda kazini hata siku moja. Anakaa nyumbani tu, hana hamu ya kula wala kuongea. Mwili wake unaanza kudhoofika.
Mama Salmon ambaye amekuwa akimtembelea mara kwa mara anaona hali ile. Mwanzoni alidhani huenda atapata nafasi ya kurudiana na Mr Marvel, lakini sasa anaelewa ukweli kuwa, Mr Marvel anampenda sana Noela kuliko alivyowahi kufikiria.
Anamuonea huruma maana Mapenzi yanamtesa waziwazi. Basi Siku moja, anamuita Salmon nyumbani.
Salmon anapofika, anamuona baba yake amekaa sebuleni kimya, Uso umechoka, macho yamezama ndani ndo Anashtukaπ³.
βMom, Dad ana nini?β anauliza kwa sauti ya chini.
βAnampenda sana Noela kuliko kawaida. Tangu aondoke, hana amani kabisaβπ
Salmon anamtazama baba yake kwa muda mrefu. Ndani ya moyo wake, anajua ni kweli Baba yake anampenda Noela sana, hata kuliko yeye mwenyewe alivyowahi kumpenda.
Ingawa moyo wake unauma, anaamua kufanya uamuzi mgumu. Kama baba yake anampenda Noela kiasi hiki, basi ni bora amrudishe ili apate furaha.
Siku chache baadaye, Salmon anasafiri kwenda Arusha. Anaamini Noela atakuwa amerudi nyumbani kwao. Baada ya kuulizia, anafanikiwa kufika kwenye nyumba ya kina Noela. Anagonga mlango na kuomba kuongea naye.
Mwanzoni Noela anakataa, Hataki kabisa kumuona. Lakini baada ya Salmon kumsihi sana, mwishoni anakubali kuonana naye.
Wanakaa nje ya nyumba, kwenye benchi ili waweze kuongea
Salmon anaanza βNaomba unisamehe kwa yote yaliyotokeaβ
βNimeshakusameheβπ
βDad yuko kwenye hali mbaya sana. Tangu uondoke, amedhoofika na Wewe ndio dawa yakeβ
Noela anakunja uso βUna maana gani?β
βNaomba urudi, Dad atakufa kwa mapenziβ
βSiwezi! Sitaki kuwa sababu ya nyinyi kugombanaβ
Salmon anamtazama βNiko tayari ninyi muwe pamoja. Mimi Sina tatizo tenaβπ
Noela anashangaa βUnamaanisha kweli?β
βNdio! Ivi kweli Unampenda Dad?β
Noela anajibu kwa sauti ya chini βNdiyoβ
Maneno yale yanamuumiza Salmon, lakini anajikaza. Ameamua kujitoa kwa ajili ya baba yake.
βNajua nilikuumiza sana Noela na nilikua mjinga kukupoteza wewe! Nataka ujue sikukuchiti kwasababu wewe ni kibonge au sababu ya mwili wako, No! Ni tamaa za mwili na vishawishi vya Iris ndo vimenifanya nifike hapa leo! Ila jua, siku zote utabaki kuwa moyoni mwangu and please mpe Dad wangu nafasiβπ₯Ή
Anamsihi sana na Baada ya mazungumzo marefu, Noela anakubali kurudi.
SEHEMU YA 20
Siku inayofuata, Salmon na Noela wanasafiri kurudi Dar. Wanapofika, Salmon anampeleka moja kwa moja kwa baba yake.
Mr Marvel anapomuona Noela, anasimama haraka, Anamkimbilia na kumkumbatia kwa nguvu. Uso wake unaonyesha furaha na mshangao kwa pamoja.
Salmon na Mama yake wanakubaliana kuwa Mr Marvel na Noela wawe pamoja. Baada ya hapo, Mama Marvel anarudi Mwanza, na Salmon anaanza maandalizi ya kwenda kusoma nje ya nchi.
Baadaye, Salmon anafanikiwa kwenda Sweden kwaajili ya masomo. Na akiwa huko anajitaidi mno kumsahau Noela na pia anaanzisha mahusiano na binti mrembo kwajina la Prisca. Japo wanapenda ila nafasi ya Noela moyoni mwa Salmon haiwezi kufutika.
Upande wa Mr Marvel na Noela, penzi lao linaendelea vizuri. Mr Marvel anachukua jukumu la kumsomesha Noela hadi anamaliza masomo yake.
Kisha baada ya hapo wanafunga ndoa kubwa mno inayo hudhuriwa na watu wengi mno. Na toka Noela Aolewe na Mr Marvel hajawai kutoa chozi hata kidogo. Yeye kila siku ni furaha na raha hasa pale anapo dekezwa na mumeweπ₯°.
Tukiachana na hayo kuna huyu binadamu anaitwa Iris! Kwa bahati mbaya baba yake alifariki kwaiyo ikawa ngumu kwake kuendelea na chuo.
Na apo ana wadogo zake kama watano wa kuwalea na mfukoni hana hata mia. Alidhani atapata msaada toka kwa Salmon ila ndo ivyo Salmon yupo Sweden.
Kwaiyo akabaki bila mpenzi, bila rafiki na bila chochote hata marafiki wachache wa chuo aliokua nao walimtenga baada ya kuzidi kuwaomba hela kila siku.
Mwishoni Iris akarudi Mtwara kuwalea wadogo zake na ivi karibuni nimepokea Taarifa kuwa aliolewa na mmakonde mmoja ivii na sasa wana watoto watatu. Maisha yake ni magumu na huwa anajilaumu sana kwa kile alicho mfanyia Noela. Ndo maana napenda kusema, malipo ni hapa hapa duniani!π
Asante kwa kuisoma simulizi hii na kwaheriππ»
~MWISHO~
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi


Maoni