TIPWA TIPWA NA MR MARVEL. SEHEMU YA 15
.
🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋
Iris alipoingia ofisini, Mr. Marvel alikunja uso. Alijua Iris si mtu mzuri baada ya kile alichomfanyia Noela, lakini hakutaka kuonyesha kwamba anamjua vizuri. Akaamua kuwa mtulivu na kusubiri kusikia shida yake.
Iris akatabasamu na kusema “Good morning”
Mr. Marvel akajibu “Good morning”
I“Naweza kukaa?”
“Ndiyo, kaa”
Iris akakaa kwenye kiti karibu na meza ya Mr. Marvel. Akamtazama huku moyoni akimsifia jinsi alivyo handsome. Aliona kabisa ni type yake na wanaendana. Akajiuliza kwa nini hakumuona mapema mpaka Noela akapita nae🤔?
“Ok! Ndiyo, nikusaidie nini?” Mr Marvel akauliza
“Kuna kitu nataka kuzungumza na wewe”
“kuhusu nini?”
“kuhusu Noela. Najua anaishi kwenye nyumba yako”
Mr. Marvel akatabasamu “Mimi sitaki kusikia mambo ya Noela kwa sababu kila kitu kumhusu ninakijua”
“Hujui kila kitu, Mimi ni rafiki yake namjua vizuri sana. Taarifa zake zote ninazo hapa!”
“Chochote kile kuhusu yeye sitaki kukisikia, Especially ukiwa ni wewe ndo unae niambia”
“Najua hutaki, lakini lazima unisikilize. Noela si msichana mzuri. Alimuumiza sana mwanao, mpaka Salmon akaja kwangu kutafuta msaada. Najua unajua kuwa kuna kitu kilitokea kati yangu na Salmon. Ilikuwa ni makosa na ilitokea mara moja tu. Tena Ilitokea chini ya ushawishi wa pombe, Hakuna aliyekuwa na akili timamu. Najuta sana Na yote haya yasingetokea kama si Noela. Alimuumiza sana mtoto wako”
“Sasa unanisimulia haya kwa sababu gani? Nifanye nini na taarifa hizi?”🤷♀
“Ninakuambia ili ujue mimi si mtu mbaya, Mtu mbaya hapa ni Noela na Unatakiwa uwe makini naye. Najua unatumia pesa nyingi kwake, lakini hastahili”
Mr Marvel “Asante kwa taarifa” akiwa hajali kabisa.
Iris akashangaa mbona mwamba hata hashtuki?? Vyote alivyomwambia havijamtikisa hata kidogo. Ikabidi aongeze nguvu
“Mr. Marvel, mimi ni msichana mzuri sana. Sidhani kama mwanao atapenda kukuona upo karibu na ex wake. Itakuwaje akigundua kuwa wewe na Noela mnaishi nyumba moja?”
“Kinachoendelea kati yangu, Noela na mwana wangu havikuhusu! Also Najua namna ya kumshughulikia Salmon so thanks”
“Please usimuumize mwanao hivi, Anampenda Noela ujue??? Mwache awe naye kwani shi ngapi??? Mbona Mimi nipo hapa kwa ajili yako…… Naweza kukujali na kuwa na wewe zaidi ya anavyofanya Noela. Alafu mimi ni mtamuuu” akang’ata lipsi zake kimakusudi ila Mr Marvel ndo kwanza hana time zaidi ya kutabasamu.
Mpaka pale akawa kashapata uhakika ni kitu gani kilimpeleka Iris ofisini kwake. Kwanza akawaza ilikuaje Noela akawa na rafiki kama Iris??? Alitafakari mpaka akachoka.
“Wewe una wivu sana! Kwa nini unataka kila kitu alichonacho Noela? Kwanza ulimchukua Salmon kutoka kwake, ukalala naye na sasa umeona Noela anaishi vizuri bado unataka kumharibia!Why???”
“Hapana, hapana! Nilishakuambia, kilichotokea kati yangu na Salmon kilikuwa ni bahati mbaya”
“Kulala na boyfriend wa rafiki yako kwa miezi minne mfululizo unasema ni bahati mbaya? Kama ingetokea mara moja, ningeweza kusema kweli ni bahati mbaya! Lakini nyinyi mlifanya hivyo mpaka mkawa na uhusiano wa siri! Stop that”
“Kuna mtu alikuwa ananilazimisha. Haikuwa kwa hiari yangu”🥺
“Binti, Nina kazi nyingi za kufanya. Please toka ofisini kwangu na usirudi tena hapa na mambo ya kipuuzi”
“Mr. Marvel embu……embu…nitazame vizuri. Angalia jinsi nilivyo mrembo. Mwili wangu uko vizuri, tumbo flat Naweza kukupa mambo mpaka ukapagawa. Mimi ni mzuri kuliko Noela, Nitakuridhisha kitandani”
Iris akasimama na kuanza kujinengua mbele ya Mr. Marvel, akidhani atamtega kirahisi kama alivyo mtega Salmon.
Mr Marvel akachukia akaona kama Iris anampanda kichwani. Alipiga simu moja tu, walinzi wakaja kumtoa Iris juu juu kama mwenge na kwenda kumtupa nje🤣.
Baada ya kufukuzwa Iris akaapa kwamba hatokubali. Lazima atamwambia Salmon kila kitu kuhusu baba yake na Noela ili kama kukosa basi wakose wote.
Haya, ikafika tarehe 18 Agosti, siku ya birthday ya Noela. Kwa sababu alikuwa kwenye mitihani chuoni, alikuwa busy hivyo birthday yake haikuwa jambo kubwa sana kwake.
Lakini Mr. Marvel hakuweza kuiacha siku ipite bila kumfanyia kitu maalum. Alimpenda sana Noela na kumuona akiwa na furaha ilikuwa jambo kubwa kwake.
Siku hiyo, akaandaa chakula kizuri cha usiku kwenye hoteli yake nzuri kwa ajili yake na Noela tu.
Baada ya kuandaa kila kitu, akamtumia sms Noela
“Nimekuandalia surprise nzuri kwaajili ya birthday yako. Jiandae, leo usiku tunaenda dinner❤️💕”
Noela aliposoma ujumbe huo, akatabasamu. Alipomaliza mtihani tu akatoka darasani na kutembea haraka kuelekea parking ili arudi nyumbani mapema kwaajili ya kwenda kujiandaa. Lakini njiani akakutana na Salmon, akiwa na maua pamoja na boksi.
Noela akamuuliza, “Unataka nini tena jamai??? Please niachie”
“Nataka kukupa zawadi ya birthday”
“Sihitaji chochote kutoka kwako”😒
“Ni zawadi tu hakuna kingine. Kwa nini unaumiza hisia zangu hivi?”
“Siumizi hisia zako bali unajiumiza mwenyewe. Kubali tu kwamba sitaki tena kuwa na wewe then Endelea na maisha yako. Mbona ni simple ivo”
Salmon akavuta pumzi, akamtazama Noela kisha akampisha apite sababu hata angesema kitu gani, Noela asinge zipokea zawadi zake.
Alipokuwa amesimama pale, Iris akamfuata akitaka waongee.
“Please Unaweza kuniacha peke yangu? Nina mambo mengi kichwani”
Iris akacheka “skia Sitaki chochote kutoka kwako, nataka tu tuzungumze”
“Kuhusu nini? Nimeshakuambia kaa mbali na mimi!”😡
“Najua na huna haja ya kunikumbusha kila mara. Nilikuwa nataka kukuambia, kama una nafasi tunaweza kutoka pamoja leo usiku”
“Una kichaa wewe sio bure! Unavyo niona nipo kama nina mood ya kutoka na wewe?”
“Kheee! Sikiliza vizuri, Hata mimi sitaki chochote kutoka kwako nina mipango yangu saa izi! Nataka tu kutoka na wewe ili nikuonyeshe kitu kuhusu Noela. Kama hutaki napo ni sawa ila jua tu kitakulamba mpaka uchanganyikiwe”
“Unamaanisha nini? Unataka kuniambia nini kuhusu Noela?” Salmon alikua na shauku sana ya kutaka kujua🤔
“Nitakuambia na kukuonyesha kila kitu leo usiku. Jiandae, tutaenda pamoja”Baada ya kusema hivyo, Iris akaondoka.
Salmon akabaki anajiuliza anataka kuonyeshwa nini tena kuhusu Noela??? Hakutaka kutoka na Iris, lakini hakuwa na chaguo baada ya kutishwa kiasi kile.
Basi Usiku huo, Noela alikuwa amejiandaa vizuri kutoka na Mr. Marvel. Alikuwa amevaa gauni jekundu na viatu vyeusi! Weeeh alikua kama malaika.
Sema wapendwa mbali na utipwa tipwa, Noela ni mrembo sana na kale ka uso kake ka kitoto kalimfanya avutie zaidi. Mr. Marvel hakuchoka kumtazama kila dakika😍
Walienda hotelini, wakapokelewa na maua kisha mhudumu akawapeleka kwenye meza yao juu kabisa ghorofani ambapo huko ndipo kila kitu kilitakiwa kufanyika.
Huko kulikuwa na mtu anapiga piano na wengine wachache waliokua wanapata dinner na wapendwa wao.
Noela Akamtazama Mr. Marvel na kumuuliza “Umeandaa yote haya kwa ajili yangu?”🥺
“Ndiyo, kwa ajili yako tu. Ili Kuonyesha kwamba birthday yako ni muhimu”
Noela akasema “Asante” kisha akamkumbatia🫂.
Mara Ghafla wakasikia sauti nyuma yao. Walipogeuka, wakamuona Salmon na Iris wamesimama pale🔥.
Mambo yameiva sasa… Nakuja.
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni