MIRANDA (Binti Yangu) SEHEMU YA 11
SONGA NAYO...
Pale nje tulibaki wawili tu mimi na madam hao wengine waliingia ndani. Madam aliponiita nilimuangalia tu bila kumuitikia, huyu mama nikimuona nahisi kichefuchefu kabisa
"Mira achana na hizi nguo, kesho tutaenda kununua nguo nyingine lakini pia ningependa kukuuliza ile simu uliipenda..??"
Nilinyanyua uso na kumuangalia kwa mshangao, akilini mwangu nilijua labda swatii ndio atakuwa kaniletea lakini nakuja kujua aliyeninunulia ndio huyu mbwa
Aah nilichoka, nikamtazamaaa kwa muda kisha nikamwambia
"Kwahiyo ulishindwa kunikabizi kwa mikono yako ukaamua kuiweka chumbani, ukute umenitegeshea bom wewe.."
"Aah Mira usifike huko, me siwezi kufanya hivyo nilikuwekea huko kwa sababu jana nilipokuita ulikataa kuongea na mimi ndio maana nikaipeleka chumbani kwako, kwanza me siwezi kukuua maana nakupenda sana binti ya..."
"We koma, yani nimekuwa binti yako au mama wa binti yako..??"
"Nini kinaendelea hapa..?"
Sauti kutokea nyuma yetu ilizungumza, haraka madm akageuka akiwa na wasiwasi sana kwa upande wangu nilikuwa kawaida kabisa yani nilikuwa nafurahi kimoyo moyo
"Aaah anfrey kumbe bado upo hapa..??
Madam alimuuliza mwanae huku akiwa anatetemeka sana
"Ndio nimefika saivi baada ya kusahau simu yangu hapo kwenye bench.."
Anfrey aliongea akasogea mpaka kwenye benchi na kuchukua simu yake kisha akatutazama kama amehisi kitu kisha akataka kuondoka mama yake akamzuia
"Aaah nilikuwa namwammbia Mira kesho aongozane na wewe muende mukanunue nguo za mtoto lakini pia na mahitaji mengine madogo madogo.."
Alizungumza madam
"Sawa.."
Alijibu Anfrey kisha akaondoka zake huku akimuacha mama yake akimtazama kwa wasiwasi sana, nami bila kupoteza muda nilishika njia ili kuingia ndani lakini madam akanisimamisha nikamgeukia
"Mira nakuomba sana hii siri ibaki kati yetu.."
Aliniambia, me nikabaki kimya sina cha kumjibu kisha nikashika njia na kuingia ndani, kama kawaida yangu huwa sipendi kukaa sebleni
Yani mida mwingi nautymia nikiwa chumbani na binti yangu, basi bwana Mira mie moja kwa moja nikaelekea chumbani nikiwa nakaribia kufika kilipo chumba changu nilipishana na Ellice
"Mchezo umeuanzisha wewe, nakwambia utaona yani nitahakikisha unaondoka kwenye hii nyumba.."
Elilice alizungumza huku akiniangalia kwa zarau na kuondoka maeneo hayo, nikabaki namshangaa huyu binti dah ana roho mbaya sijawahi ona
Na sijui amekuja lini maana wakati anakuja hapa sikumuona, basi mimi huwa sina tabia ya kuweka vitu rohoni kwa mfano nikiambiwa kitu nikae nacho makini huwa napotezea au wakati mwingine nasahau kabisa
Shoga enu nikasahau kabisa maneno ya Ellice so nikaingia chumbani kwangu na kulala....
Kesho yake niliamka kama kawaida nafuata ratiba zote za kumuhudumia mtoto, majira ya saa tatu nilikuwa nimeshamaliza kila kitu so nilikuwa free kabisa
"Mira.."
Nikiwa nimejipumzisha chumbani kwangu madam aliingia na kuniita jina langu, nikanyanyuka na kukaa kitako huku nikimtazama azungumze
"Jiandae muda ndio huu.."
Alisema na bula kusubiri neno lolote kutoka kwangu akaondoka, basi mimi ninavyopenda mitoko aweee chapu nikawa tayari kwenye gari nikiwasubiri wao wamalize kujiandaa
Baada ya muda kidogo nilimuona madam akiwa ameongozana na Anfrey mpaka pale nilipokuwa, Andrey akafungua mlango wa gari alishangaa kunikuta nikiwa nimemsubiri ๐
"Umeingia mda gani..??"
Aliniuliza
"Kitambo sana mbona.."
"Mira hakikisha unakuwa huru kuchagua yani chochote urakachokipenda we unachukua sawa..??"
Madam aliniuliza
"Sawa madam.."
Bas Anfrey aliwasha gari na kuondoka mahali pale, njia nzima tulikuwa kimya sijui kwa sababu hatujazoeana ๐ ila kusema ukweli huyu kaka namuogopa mno
Maana sipendi wanaume weupe na wazuri maana nitakuwa mtu wa kulia kila siku, ukweli au uongo ?? Nawauliza nyie akina dada ambao mnawanaume weupe na wazuri
Hivi hamjawahi kulia kweli ๐ anyway mahusiano ya watu hayanihusu ikiwa me sina hata mwanaume wa kusingiziwa tu...
ITAENDELEA........
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni