SASA NAKUPENDA Sehemu ya 29
Mwandishi; lissa wa huru media
Basi nimefika home nimenuna kweli kweli.nikaona yule adrian kama alikuwa anataka kunitia nuksi tu. Mtu kashanikaa mbele ya wazazi . Na yeye ndo kasababisha ata shule nimefel pumbavu zake.nikaona aka ngoja bwana baraka mie. Basi nikawa binti mzuri nakwambia .yani ni mimi na nyumbani .nyumbani na mimi. Nikitoka ni dukani mala moja nimetumwa na sichelewi nishaludi home .ila sasa adrian na yeye alikuwa anakomaa kunifatilia jamani. Yani nilikuwa nikitoka nje nakutana nae sana .ila wala sikutaka upumbavu mie nikasema namngoja mpenzi wangu baraka.na kama.madihara ikakata miezi 3. Nikawa nangoja siku tu ni lini baraka analudi.
Siku iyo sasa nipo home na mama. Tukapika vizuri tulivyomaliza tukatenga mezani mana mzee alisema yupo njiani analudi muda sio mrefu. Basi sie tukaanza kula uku tunapiga story kweli kweli. Mala mzee nae akaingia . Akaingia kwanza ndani kwake .kisha ndo akatoka sasa. Akasema mke wangu nijazie chakula kingi leo nna njaa sana. Kweli mama akamjazia chakura. Kisha tukaanza kula taribu. Baba akasema leo bwana nimepokea habari nzri sana juu ya baraka. Mh nilivyosikia barkaa nikatulia kwanza mana moyo ulikuwa unapiga kweli kweli. Baraka tena kafanya nini. Baba akasema baraka alikua anatalajia kuludi leo. Ila hataludo tena.nikauliza kwa nn. Akasema amepata nafasi ya kujiunga jeshini hivyo ameona ajiunge tu na jeshi . Eeeeh nini. Nikasema kwaiyo baba hatarudi. Akasema ndio. Amenambia atakuwa huko kwa miaka 3 kwanza ya mafunzo. Aseeeee nilibaki.nimeganda kama sio mimi. Ningoje miaka 3 tena. Na mbay zaidi hanitafuti mimi anampigia mjomba ake tu .yani baba yangu. Na kuna siku nilienda kwa mjomba bakari.niliwauliza wadogo zake wakanmbia huwa anapiga kuwasalimia. Nikaona kabisa basi mimi baraka hanipendi na sina umuhimu kwake. Nilijikuta machozi yananishuka mbele ya wazazi.
Mama akauliza we mbona unalia eeeh. Aseeee nikasukuma chakura.nikanyanyuka kwa hasira nikaingia chumbani kwangu. Nikajifungia kabisa malango.nikalia mno.nilililia sana.tena kwa sauti na hasira kweli kweli. Nikasikia mama anagonga fungua. Ebu fungua . Shakira mwanangu fungua. Nikasema mama kwa nn ananifanyia makusudi.nimemvumilia miezi 3 kanambia analudi tunakuwa wote .atakuwa anakupigia ili tuongeee lakini ni muongo hajawahi kupiga ata siku moja. Bado anatakaa kuwa mbali na mimi kwa miaka 3. Naishije bila ya yeye naishije. Nampenda sana mimi. Nampenda sana baraka ananitesa mimi. Hivi mnajua nilikuwa kama chizi. Nililia uku nikilalamika sana .na wazazi wakisikia . Sikujali ata kidogo. Nilikuwa nalia tuuu. Nillia mno. Mpaka nilipojisikia kunyamaza ndo nilinyaamaza mwenyewe kisha nikalala kabisaaa. Ila usingizi ulikata usiku kama saa 7 .mama alikuwa aita shakira shakira .nikasema abeee mama akasema fungua mlango mwanangu.
Basi nikasogelea mlango kisha nikafungua mama akaingia. Akanikuta nimechoka sana. Akaa kalibu na mimi. Akanishika mkono. Akanambia pole sana. Naomba nieleze nini kinaendelea kati yako na barkaa. Mimi nilisema mama .nisameheni mimi nampenda sana baraka.mama akanmbia sawa nielezeee. Nikasema nilianzisha mahusiano naye na alinambia akiludi tutakuwa pamoja nimngoje na atanioa tu .mama akanmbia mmewahi kufanya mapenzi. Mh apo nikakakataa nikasema hapana hatujawahi. Mama akasema sawa lakini shakira si unajua baraka ni kaka yako ama umesahau mwanangu? .nikabaki kimya. Mama akanmbia sikia niwambia ata uyo baraka hakupendi.mbona akimpigia baba yako hamuulizi chochote kihusu ww. Yeye anaangalia mamabo yake tu. So plsss naomba uache kulia na uendelee na maisha yako unanielewa nikasema lakini nampenda sana mama. Mama akasema achana nae .wewe tulia upate cheti chako ukaenze kujifunza urembo upambanie mambo yako sawa. Nikasema sawa mama. Basi maa akanikumbtia kisha akawa ananituliaza kwa mamaneno mazuri.nashukuru nikapoa tu. Na nikawa kawaida tu. Temper ikashuka kabisa. Nq hii siku mama akalala na mimi kabisaaaa.
๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ๐ผ
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni