ACHA NIKUPENDE ❤️1
MTUNZI uhuru media
" Pink ujue hapa Ni mjini na maisha ni magumu Sana pesa zinapatikana kwa shida hivyo unatakiwa kujiongeza sio Ila siku Mimi ni nikeshe huko nje nipigwe na baridi alafu wewe kwa Raha zako unavuta shuka unasubiri kuletewa. Alisema zuri huku akiwa anakunywa supu aliyotengewa na pink muda mfupi uliopita.
" Dada zuri hiyo kazi unayofanya Mimi siwezi .
" Unafikiri Mimi napenda kuuza mwili wangu hii yote Ni kwasababu ya shida tu.
" Kwani siwezi kufanya kazi nyingine.
" Kazi gani ambayo unaweza kufanya shule hujasoma , siku hizi hadi ma house girl wanaotakiwa waliosima ukienda kuomba unaulizwa cheti hii ya kujiuza haina masharti yoyote.
Pink alisimama pembeni akiwa kajiinamia maana kazi aliyokuwa anaambiwa afanye ilikuwa Ni mtihani mkubwa Sana kwake . Alikumbuka wazazi wake walinifariki na ndugu wakamdhurumi kila kitu na kumfukuza nyumbani kwao kwakuwa hakuweza kupambana nao aliamua kuondoka na kwenda kuishi na dada yake zuri.
Zuri na pink hawakuwa ndugu wa kuzaliwa Ila wazazi wao walikuwa Marafiki Sana na kwa bahati mbaya wote walitangulia mbele za haki. Wazazi wa zuri walifariki akiwa kidogo anaejitambua lakini kwa upande wa pink walimuacha akiwa kidato Cha pili baada ya hapo hakuweza kuendelea na masomo. Zuri alimchukua na kuishi nae Kama mdogo wake mtaani watu wote walijua pink na zuri Ni ndugu wa damu. Pink baada ya kujitambua zuri alitaka aungane nae kwenye biashara ya kujiuza ili waweze kujikimu kimaisha.
"Hauna haja ya kulia pink kwasababu hapa tulipo wote Ni mayatima hatuna wa kumlilia Wala kuomba msaada kumbuka yatima hadeki
Pink aliondoka akaenda kukaa nje huku akiwa anafikiria afanye Nini ilinkujikomboa kwenye haya maisha maana kila alipofikiria swala la kufanya biashara ya mwili wake haikumuigia akilini.
Siku hiyo ilipita hatimae mwezi bila zuri kumwambia kitu chochote kuhusu kwenda kujiuza , hiyo ilimfanya pink apotezee.
Siku moja usiku Wanaume wawili Walienda nyumbani kwao ktafita zuri.
" Tumemkuta zuri?
" Dada zuri hayupo. Pink alipowajibu hivyo wale wanaume walimuangalia Kisha wakasema
" Sawa tutakuja kesho. Walipoondoka pink alifungua mlango akaenda kulala.
Kesho yake asubuhi na mapema zuri alirudi nyumbani akiwa kaongozana na wale wanaume wawili lakini pink alipowaangalia alihisi Kuna kitu hakipo sawa maana Zuri alikuwa Kavita mdomo na wale watu walikuwa wanamuamrisha afanye kitu.
Zuri alimshika mkono pink wakaingia chumbani .
" Kusanya kila kilicho chako kunasehemu unatakiwa kwenda.
Pink alishituka
" Dada umeamua kujifukiza nyumbani kwako.
" Hapana mdogo wangu unaenda sehemu salama baada ya muda utarudi tutakaa pamoja.
Pink aliogopa lakini Zuri alimbembeleza afanye hivyo.
" Niamini utakuwa salama kipenzi.
Pink alichukua begi lake akakunja nguo na kunywe mabegi.
" Tayari
" Ndio.
" Haya nifuate. Walitoka wote mpaka sebleni wakawakuta wale wanaume bado wamesimama.
" Haya twende.alisema moja wa wale wanaume huku alichukua begi Pink.
" Dada niambie naenda wapi?
Aliuliza pink huku machozi yakitoka. Zuri alimkumbatia na kumwambia
" Pink kipindi kile ulivyoumwa Sana sikuwa na pesa ya kukutibia hivyo ilinibidi nikaazime pesa sehemu nikaahidi baada ya muda nitarudisha lakini kutokana na Hali ngumu ya maisha na kipato changu kidogo nimeshindwa kulipa deni huyo mtu amesema ukakae kwake mpaka nitakapolipa Hilo Deni. Naomba unisamehe mdogo wangu sikuwa na njia Ila nakuahidi kutafuta pesa Kisha nitakuja kukuchukua.
" kwani Ni kiasi gani Cha pesa ulichokopa ambacho kunathamani ya utu wangu. Aliuliza pink kinyonge.
" Sio nyingi kipenzi Ni milioni moja tu. Pink alishindwa kuongea kitu ilibidi akubali kuondoka na wale wanaume akiwa kajitoa sadaka maana hakujua hao watu wanaenda kumfanya Nini.
Walipanda kwenye gari huku pink akiwa kakaa siti ya nyuma peke yake alikuwa anajishauri aruke akimbie lakini aliona wazo lake ni lakijinga.
" Acha nikubaliane na kinachoenda kunikuta sijui huyo mbaba anaenda kunifanya Nini.
Hatimae walifika kwenye jumba moja la kifahari, wakashuka na kuingia ndani walipofika sebleni walimkuta Kaka mmoja mwenye makadirio ya miaka 29 au 30 akiwa kasimama anaangalia mlangoni na mkononi akiwa kashika grass ya mvinyo. Walipofika karibu
Pink alionekana kushituka Sana pia Nicky alishangaa kuona sura ya pink. Water walibaki wamesimama waliangaliana lakini Nicky alionyesha kuwa na chuki.
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni