ACHA NIKUPENDE ❤️ 2
MTUNZI uhuru media
Nicky alishusha pumzi Kama ametua mzigo mzito alipokuwa kaubeba Kisha akasema .
" Wewe Tena , umefuata Nini hapa nyumbani kwangu?
" Hili swali natakiwa nimuulize wewe Mr. Maana Mimi mwenyewe sijui kwanini nipo hapa?
" Siamini Kama nimekuona kwa Mara nyingine Tena nyumbani kwangu, kwahiyo wewe ndio binti uliewekwa rehani na Zuri? Alisema Nicky Kisha akamkonyeza na kumfanya pink ainamishe macho yake chini.
Pink alizidi kuogopa maana Nicky alikuwa anamuangalia Sana na alihisi anaweza kumfanyia chochote. Aliendelea kumuomba Mungu kimnya kimnya. Baada ya Nicky kumuangalia kwa muda akasema .
" Acha nikuache upumzike Sina haraka na wewe. Alivyosema hivyo alitoka na wale wanaume wawili.
Pink alienda kukaa kitandani huku akiwa Ni mwingi wa mawazo alikuwa anafikiria afanye Nini ili atoke Ile sehemu maana alihisi sio salama kwake.
" Eee Mungu nakuomba umsaidie dada Zuri apate pesa kwaajili ya kunitia hii sehemu sitaki kukaa hapa.
Nicky alikaa sehemu akawa anakumbuka tulia alilofanyiwana pink .
Siku moja pink alikuwa yupo barabarani na rafiki zake wa mitaani wakiwa wanakula ice cream Mara wakapishana na Nicky akiwa anaendesha gari lake akawapita na kuwamwagia maji machafu kwa hasira pink alisema
" Mjinga uliekosa akili kwani huoni macho yako Yapo kisogoni? Nicky alipofika mbele kidogo akamsimamisha gari Kisha akarudisha gari mpaka walipo akashuka .
" Nyie Malaya mnasenaje?
" Wewe sisi sio Malaya, Malaya wewe na ukoo wako. Pink na wenzake waliendelea kutukanana na Nicky. Pink alimsogelea na kumpaka ice cream kwenye shati lake jeupe kile kitendo kilinikera Sana Nicky kwasababu alikuwa anaenda sehemu muhimu Sana hivyo ilimbidi aahirishe hiyo safari akarudi nyumbani .
" Sasa huu Ni wakati wa kulipiza kusasi changu maana ameungua mwenyewe kwenye 18 zangu.
Siku hiyo ilipita pink alihudumia kwa kila kitu na ilipofika usiku alilala akiwa salama kabisa.
Kesho yake asubuhi Nicky alienda chumbani kwa pink akamkuta bado kalala fofofo. Nicky alichukua saa iliyotegesha alam na kuiweka sikuoni kwa pink, saa ikaanza kupiga kelele kwa sauti kubwa na kusababisha pink akurupuke na kuangukia upande wa pili. Nicky alicheka Sana mpaka pink akaona aibu.
" Hey, habu toa uvivu wako hapa unalala mpaka saizi una Raha gani?
" Samahani.
" Unafikiri upo hapa kwaajili ya kulala, huko nje Kuna kazi nyingi za kufanya habu nifuate.
Pink alimfuata nyuma mpaka walipofika nje kwenye bustani ya mauwa Nicky akasimama na pink nae akasimama. Nicky aliagizia kwanja kwa kijana wake wa bustani Kisha akamtupia , pink akakwepa.
" Okota Hilo kwanja na uanze kukata huo ukoka akikisha unasawazisha na kuwa sawa.
" Nini, Mimi sijawahi kufanya kazi Kama hizi.
" Hebu acha ujinga uliwezaje kunipaka ice cream na ushindwe kufyeka, huwa najua wababe huwa hawashindwi kazi nataka kazi ifanyike. Pink aliokota kwanja na kujaribu kufyeka masikini ya Mungu hakujua hata kulishika Hilo kwanja lakini Nicky hakujali aliondoka na kuingia ndani huku akisema
" Huu Ni mwanzo wa mateso yako pink utakuwa mtumwa wangu mpaka nitakapotosheka maana najua Zuri hawezi kuleta pesa zangu mapema.
Nicky alienda kukaa kwenye dirisha la chumbani kwake akawa anamuangalia pink anavyohangaika kufyeka.
Pink aliendelea kufyeka. Mpaka akahisi kuchoka na bustani hakufika hata nusu. Alienda kutegemea kwenye mti huku tumbo likiwa linamsokota kwa njaa. Baada ya masaa matano alikuwa kamaliza na mikono ilijaa malengelenge.
Aliingia ndani akamkuta yupo sebleni anaangalia movie, alimpita akiwa anaelekea kwenye chumba chake. Mara akaitwa
" Pink . Pink alisimama akaitika
" Abee
" Nenda jikoni ukaniandalie chakula.
Pink alingata meno kwa hasira alitamani kwenda kumrukia amkabe Ile shingo yake.
" Lakini ungeniacha nipumzike kidogo nimechoka.
Nick alimgeukia na kumuangalia huku akiwa kakunja sura yake .
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni