TIPWA TIPWA NA MR MARVEL SEHEMU YA 16
🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋
Salmon alisimama pale akimtazama Noela na baba yake kwa macho yaliyojaa hasira na maumivu. Hakutegemea kabisa kumuona Noela akiwa kwenye dinner ya kimapenzi na baba yake mwenyewe.
Iris yeye alisimama pembeni, akitabasamu kwa dharau. Ndani ya moyo wake alifurahia sana kuona Noela akiwa amefumwa😔.
Salmon akasema kwa sauti ya juu “Huyu ndiye mwanaume anae kupa kiburi Noela? Baba yangu?”🗣️
Noela akakunja uso maana Hakupenda kabisa kumuona Salmon pale, tena kwenye usiku wa birthday yake. Ukizingatia yeye na Mr Marvel walikuwa hawapo bado kwenye mahusiano.
“Salmon hii si sehemu ya kuleta kelele please ondoka”
Salmon akacheka kwa uchungu “Niondoke? Unataka niondoke baada ya kugundua kuwa unatembea na baba yangu?”🗣️
Watu waliokuwa karibu wakaanza kuangalia upande wao si unajua wabongo kwa umbea🤣!
Ikabidi Mr. Marvel amtazame Salmon kwa macho makali “Hey Salmon, tulia. Hii si sehemu ya kufanya drama”
Lakini Salmon hakuwa tayari kumsikiliza hata baba yake. Alikuwa amechanganyikiwa kabisa.
“Why Dad??? Yani Wanawake wote duniani hawakufai mpaka uchague ex wangu? Whhhy”🥺
“Unalalamika nini wakati wewe ndo mwenye makosa??? Alafu Mimi sina mahusiano na baba yako kama unavyo fikiria” Noela alijitetea
“Ndiyo nilikosea Lakini sikutegemea wewe utafika hatua ya kuwa na baba yangu”😡
Mr. Marvel akasema kwa sauti nzito “Noela si mali yako! Mliachana na kila mmoja ana haki ya kuendelea na maisha yake”
Iris akadakia “Unaona sasa Salmon? Huyu ndiye Noela wako. Anatembea na baba yako bila hata aibu! Heri yangu mimi”😒
Noela akamgeukia Iris kwa hasira “tena Wewe kaa kimya maana Yote haya yalianza kwa sababu yako”
“Kwa sababu yangu? Mimi nilifanya kosa lakini wewe sasa umeamua kulipiza kisasi kwa kulala na baba yake sio?”
Salmon akapandwa na hasira zaidi “Iris, nyamaza!”🗣️
Iris alinyamaza Lakini tayari watu wengi walikuwa wanawatazama mpaka aibu. Mr Marvel akamshika Salmon begani “Go home, tuliza hasira then tutazungumza kesho nyumbani!”
Salmon akageuka nyuma macho yake yakiwa mekundu akaondoka bila kusema lolote huku Iris akimfuata.
Mpaka pale birthday dinner ikawa imesha haribika kabisa. Mr. Marvel akamwangalia Noela kwa upole “Kama unataka, tunaweza kuondoka”😔
Noela akatikisa kichwa “Hapana, Leo ni birthday yangu Sitaki mtu yeyote aharibu siku yangu”
“Utakuwa comfortable kuendelea kula hapa na watu wakitushangaa kiasi hiki??”
“Yes! Gharama zote hizi ni kwaajili yangu alafu tubadilishe hoteli kisa Salmon! No! Tule hapa hapa” Noela akavuta kiti akakaa
Mr. Marvel akatabasamu kidogo “thats my girl”
Basi Muziki wa taratibu ukaendelea pale, wakaletewa chakula chao wakala, na mwisho Mhudumu akaleta keki mezani na kuanza kumuimbia
“Happy birthday to youuu! Happy birthday dear Noela, happy Birthday to you”🎂
Noela akatabasamu kisha akakata keki na kumlisha Mr Marvel baada ya pale wakarudi nyumbani sababu mood yote ya birthday iliisha.
Upande wa Salmon hakuweza kabisa kukubali kumuona Noela akiwa karibu na baba yake. Picha ile ya dinner iliendelea kumtesa kichwani. Alikuwa na hasira, wivu na maumivu kwa wakati mmoja💔.
Akaamua kumpigia mama yake ambaye alikuwa Mwanza. Simu iliita weeh na ilipo pokelewa Mama Salmon akauliza
“Salmon, kuna nini? Mbona unanipigia usiku hivi?”
Salmon akajibu kwa sauti ya huzuni “Mama, please uje nyumbani, Nahitaji uwe hapa”
Mama yake akashangaa “Kuna nini kimekutokea?”
“Dad anaharibu mambo. Ana uhusiano na Noela, ex wangu na mimi Siwezi kuvumilia hilo. Please njoo ili urudiane naye hata kama ni kwa muda Itasaidia kuwatenganisha”
Mama yake akanyamaza kwa sekunde chache coz Hakutarajia kusikia kitu kama hicho.
“Hayo mambo ya baba yako na mimi si rahisi hivyo, Salmon! Kamwe baba yako hawezi kubali kurudiana na mimi”
“Mom nakuomba Hata kama itashindikana kuwa pamoja ila please njoo kwanza. Nisaidie hili”🥺
Mama yake akavuta pumzi “Sawa, nitafikiria then Nitakujulisha”
“Asante mom!” Kisha akakata simu.
Upande wa Iris, alikuwa bado na hasira. Alitaka kuhakikisha maisha ya Noela yanaharibika kabisa.
Alichukua baadhi ya picha zake kisha akaanza kuzisambaza kwenye magroup ya chuo Akaandika kuwa Noela ana mahusiano na Salmon pamoja na Baba yake.
Hapo msisahau kuwa Salmon ni kipenzi cha wadada wote wa chuo, kwaiyo Ndani ya muda mfupi zile taarifa zikaanza kusambaa huku wakimsema vibaya Noela.
“Huyu tipwa tipwa kiboko! Kuanzia baba mpaka mtoto Duuuuh!!!! Ila mijitu minene”
Iyo ilikua moja kati ya meseji za kwenye magroup ya chuo. Yani meseji zilikua nyingi tena chafu kiasi kwamba siwezi hata kuwaandikia hapa!
Je nini kitaendelea?
Nakuja………
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni