AFANDE MILLAN😎 Sehemu ya 43
Mi sikufanya ajizi, nikamuuliza kwani apa majirani zako hawapo, akanmbia mmoja alisafiri na mwengine kaenda kwao leo, wote hawapo, nikaona kazi leo, nisingekuja sijuh ingekuajee, ni mungu tu aliniongoza nije uku, nikamuuliza vifaa vyako viko wapi, akanioneshea, yani kakataa vyangu, kabangaiza kanunua vyake ,ahaa mwanamke jeuri uyu, yani ananionesha kuwa mm sio lolote aya bwana ,nikamchukulia akanielekeza na nguo zake nimbebe nikamuekea kwenye mfuko vizuri kisha sasa , akanmbia nichukue dera nimveshe mana alivaa kitenge tu, basi mi nikamtoa kitengee, nikamvesha deraa, kisha sasa nikamchukua na ummy, mana sikuwa na jinsi na hakuna wa kumuacha nae mtoto, ummy ananiuliza tunaends wapi bab, namwambia tunampeleka mma hospital anaumwa ,akanambia sawa kweli mi nikaangaika na zena mpaka kwenye gari, nikampakia nyuma ,kisha ummy ndo nikamueka mbelee, aseee nilikimbizaa gari kweli kweli, mana zena alikuwa ananlalamika sna akuwa naumia ,nikajua uchungu ndo unazidi kumchanganya uyu
Aseee mpaka saa 4 tukafika hospita moja ya private kubwa ipo maeneo ya airport, basi nilimshusha harka na nikamuaharakisha ndani na manurse haraka wakampokea ,wakampeleka leba, mimi uku njee nikabaki na ummya sasa, apo niliomba dua, kumuonbea zena ajifungue salama ,mana mambo ya uzaizi huwa yana mambo mengi kweli kweli, aseee mpaka saa 8 tuko pale, zena hajajifungua na njia inagoma kutanuka, so nikaambiwa nitie saini afanyiwe operation ,na mm nilichanganikiwa ,ila sikujiuliza mi nikasaini ili zena afanyiwe hiyo operation, na kweli mpaka.saa 11 asubuh zena alijifungua mtoto wa kike, kwa njia ya operation, ahaaaa nilivyosikia kuwa amezaa wakike nikifurahi kinoma, mana daaah nilikuwa nimemis sana mtoto wa kike, nna watoto wa 5 ila wote wakiume, afadhali sasa uyu kaja binti daah , nilifurahi sana, na ata zena alikuwa anaendelea vizuri na alishazinduka tukaruhusiwa kwenda kumuona
Mi nikaingia sasa, ila zena alikuwa kawaida tu ,wala hakunioenesha kisirani wala hasira, sijuh na mimba ilikuwa inampelekesha , basi mimi nikawa namuuliza unaendeleaje, vip hali yako, akawa ananijibu tu kuwa anaendelea vizuri ila kidonda tumboni kinamvuta tu, nikajua ganzi ishaanz akumuisha, nikapewa mwananagua sasa nimuone, mashaallah, yani uyu dogo alifanan na mama yangu kila kitu, yani kaam mama , nikajua daaah apa nimepata mama, ila ni kakali yani kanalia mnooo, alafu sasa kwa mda huo zena maziwa yakawa hayatoki, sijuh ndo njaaa kakawa kanalia mnoo, ummy alifurahi et nimempata mdogo wangu, ntakuwa nacheza nae ,nikawa namwambia yaaa mdogo wako uyuu ,mpendane sawa, basi zena akawa anatabasamu tu, apo sasa nikampigia simu ibraa nikamwambia kuwa zena kajifungua mtoto wa kike, ibraa akanmbia kuanzi leo wewe ni baba mkwe wangu, mimi uyo mtoto akikua naoa mke wapili, nikacheka tu, na baada ya mda ibra akaja kweli kumuona zena na akaampa hongera tu, et kwa kumletea demu
Na jioni ndo shey anakuja hospital na yey kumuona shoga yake, akampa sana hongera zena , na akamwmabia hakuwa anapatikana mana simu yake kwa jana ilimzimikia kwa skku nzima , ahaa uyu nae mdangaji tu kama mimi alafu mambo mengi, basi bwanaa zena alikaa pale hospitalini siku 3 akiangaliwa, nilikuwa nipo nae bega kwa bega, full kujiongelesha ,oooh unataka nni, unajisikia kula nn zena, ana akinambia chapu naenda kumchukulia ,namjua zena akichange weeee sikutaka hizo shida, so kwa siku tulizokuwa tunakaa hospitali mm na zena tilikuwa tunaongea vizuri tu wala hakukuwa na shida kabisaa japo hakuwa amenichangamkia sana, na siku ya 4 sasa zena ndo akaruhusiwa kurudi nyumbni, na mm ndo nijamludisha sasa mpaka nyumbani kwake, japo nilikua natamani akakae kwangu, yani yule mtoto nilikuwa na raha nae kinomaa, si mnjua tena mtoto wa kike nilikuwa na hamu nae sana
🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈🦈
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni