πΊπππππ πππππ ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ: 90
Namna ambavyo alikuwa anatembea, niliogopa sana. Alikuwa anaonekana amekasirika. Hata ofisini hatukufika kwakweli, alinivuta kwenye moja ya kona ambazo zipo ndani ya ile hotel.
Kisha alinitazama usoni. Macho yake tayari yamebadilika. Nilikuwa nataka nimuulize kuna nini, ila aliniwahi yeye ndiye aliyeniuliza kwa sauti yenye maumivu aliuliza βAlikuwa anasemaje?β
Nikamtazama na kumuuliza βNani tena?β
Akaniambia βacha kunidanganya, nimeona kila kitu akakupa na kadi yake. Niambie alikuwa anataka nini?β
Nikajikuta nimecheka. Yeye hata hakucheka badala yake akasema βunaona sasa unanicheka, unaniona mimi mpumbavu sina akili. Ndeana acha masihara mimi naumia roho.β
Akaniachia na kwenda kuegemeza kichwa ukutani hivi. Nilicheka kidogo ndani yangu. Kumbe jamaa mbali na upendo wote huu anao wivu. Basi taratibu nilitembea na kwenda kumkumbatia kwa nyuma.
Nilimkumbatia kwa nyuma tena kwa nguvu na kichwa changu nikalaza mgongoni kwake. Niliona na yeye akiinuka na kushika mikono yangu.
Nikiwa mgongoni kwake nikamuuliza β Unafikiri kuna mtu anaweza kuja kuchukua au kuiba upendo wangu kwako?. Anaanza vipi sasa, hakuna, haiwezekani.
Kwasababu nafasi iliyopo ndani ya moyo wangu ni moja tu, ni moja pekee nayo ni ya kwako wewe tu. Hakuna mwingine anayestahili nafasi hii zaidi ya kwako wewe.
Stewart labda hukunielewa, nilisema Nakupenda, na nasema tena Nakupenda na nitaendelea kusema na kuimba neno hili mpaka utakaponielewa.
Hutakiwi kunikumbusha kukupenda tayari nakumbuka mwenye kuwa nakupenda sana, wala hutakiwi kunifundisha kukupenda wewe, tayari nimefaulu somo hilo. Nakupenda sana.β
ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ: 91
Nilitabasamu nikisema βIna maana hujui tu. Labda ni ngumu sana kuelewa. Ila tambua ninachokuambia. Ninachokipenda kutoka kwako ni moyo wako.
Naupenda sana moyo wako. Napenda jinsi unavyojua kupenda na kunijali. Napenda sana. Vipi na wewe kwani akitokea mwanamke mzuri kunizidi utanisaliti?β
Akatoa macho akisema βmimi nikusaliti wewe?, haiwezekani. Hata hivyo Ndeana mpenzi wangu labda hujui tu. Mimi nikikusaliti basi ujue sikupendi. Hakuna bahati mbaya, kwa maana usaliti ni hatua.
Watu wanaanzisha mazoea. Wanazoeana na wanakusaliti. Ina maana katika hatua zote hizo hakuwa anajua. Huu ndiyo ukweli ninaojua mimi na nimejifunza kutoka kwa yale niliyopitia.
Mtu anaposaliti mahusiano yake ina maana kuna kitu hakijatimia ndani ndiyo anakitafuta kwa mwanamke au mwanaume mwingine. Mtu anayekusaliti hajakupenda vizuri bado. Anayekupenda kamwe hawezi kukusaliti.
Mtu anayekupenda daima atakuwa na wewe, atakutetea, atakujali, na mengine mengi haijalishi ana pesa au hana. Mimi nakupenda na Mungu anisaidie nitakupenda milele, sisi ni timu hatupaswi kusalitiana.
Tupendane, tutoshelezane na tujaliane. Tazama mahusiano mengi ya mwanamke au mwanaume waliosalitiana. Mkisamehana tu mapenzi yanakosa nuru na amani na furaha.
Na hii hufanya mtu kwa siri asaliti tena na tena. Nikikusaliti tu baby, na ukathibitisha hilo ujue Sikupendi. Hivyo haitajkuja tokea mimi niache kukupenda.Nakupenda sana Ndeana. Sijawahi kuwa hivi ndiyo nakuwa kwako. Nakupenda.β
Nilimsikiliza kwa makini na kumkumbatia. Hata ilinifanya nikumbuke baadhi ya mahusiano yangu ya nyuma. Ni kweli nilikuwa na mpenzi. Lakini tangu nimekuwa naye, anaweza kulia hapa akiomba msamaha. Kiroho ngumu unasemehe kwamba harudii kosa ila baada ya muda anarudia tena. Nikajikuta naumia kuona kumbe sikuwa napendwa, yaani mimi nilikuwa najiona ndiyo mwenyewe kumbe sivyo.
Akaniuliza βTotoo mbona kama unalia?, vipi umemkumbuka kijana wako wa zamani?β
Nikamtazama na kujikuta kama nataka nianze kusimulia kutoka na yale maelezo yake. Akaniziba mdomo na kusema
ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ: 92
βusiniambie kitu, wala sitaki kusikia chochote. Ninachojua mimi ndiyo mwanaume wako wa kwanza unanipenda sana tofauti na kwingine. Si ndiyo toto.β
Nilimtazama na kutabasamu kisha alisema βsio kwangu tu Ndeana. Nataka nikuambie kitu cha maana. Wanaume asilimia kubwa ni wakorofi. Muogope sana mwanaume ambaye upo naye kwa mahusiano anaanza kukuuuliza habari zako za zamani kuhusu mapenzi na kukuchimba mara kwa mara.
Samahani sikutaka kukukumbusha. Ila unakumbuka nilivyokuelezea mimi habari zangu nikiomba msamaha. Sasa yeye mwanaume anapenda kujihesabia haki sana. Ukimuelezea habari kuhusu wanaume wako hata watatu tu.
Anaingia kinyongo, anaanza kukushusha thamani na kukudharau. Anaanza kukulinganisha na malaya. Hajui hata ulikuwa unakutana na wanaume gani. Ni kweli haijakaa poa mwanamke kuwa na idadi kubwa ya wanaume nyuma.
Ila mimi huwa nawasifu kwa kuacha mahusiano ambayo hayana afya na kuhamia mengine kutafuta furaha. Ila wanaume wengi wakorofi na hao ni walewale wabinafsi na hawana heshima wala adabh anaweza kuwa mkubwa akili za kitoto.
Ninachojua ukimchunguza sana bata huwezi kumla. Ninachojua ukimpenda mtu anzia ulipomkuta na hata ukijua kuhusu jana yake basi jipongeze umemtuliza. Baby waambie na wanawake wengine.
Wasione raha kusimulia mambo yao yaliyowaumiza sana kwa wanaumr mbalimbali wakihisi kuwa ndiyo wataonekana wazuri na wakweli. Sisi wanaume hatueleweki.
Bora aje kujua yeye mwenyewe akikuuliza mwambie akikuwa na maana ndiyo maana sikuwa na haja ya kusema kwasababu mimi na wewe ni wapya na safari yetu ni nzuri kuliko unayoulizia. Usije kufanya kosa hilo.β
Nikatabasamu tu, kisha alisema βtunaweza kukutwa hapa.β
Nikacheka akasema βkadi ya yule mwanaume, kwanza hata sio handsome atakuchosha tu baby wangu.β
Nikacheka na kusema βupoje lakini, mbona unatabia mbaya. Muone wivu tu.β
ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ: 93
Akanikumbatia akisema βWivu lazima totoo, ona ulivyo chombo. Nisijisikie wivu naumwa. Kwanza roho yanvu ilitoka ujue. Nilitamani nimzibue. Ndiyo vile tena mteja.β
Nikasema βSi unajua sasa, mteja yeyote ni mpenzi, mpenzi. Kwahiyo usiniingilie kazini kwangu.β
Akacheka akisema βusinitanie totoo, wewe nuna tu ila mimi kulinda mali yangu siachi.β
Nikacheka nikisema βyaani wewe?
Akatabasamu akisema βunajua kushuka kule ni kukumbuka tu. I real miss you.β
Nikamtazama na kusema βhata
mimi, ila nimechoka sana tumesimama tangu asubuhi natakiwa nikalale kwanza.β
Akaniambia kwa upole βsawa kipenzi sawa, ila ndiyo hata busu kweli.β
Akanishika kiuno kisha mikono ikashuka mpake kwenye makalio yaani kuna namna nzuri alinishika. Nilimtazama usoni kisha akawa anataka kunibusu. Si tunasikia hatua mtu akiwa anakuja upande wetu. Haraka tukakimbia na kujificha chini ya ngazi. Tulijibanza huko tukicheka. Yule mtu alipita na Boss alisema βila totoo, mimi ni wakucheza michezo hii. Kweli nimekatamatika.β
Sikutaka kupoteza muda, mimi ndiyo nilianza kumbusu. Haukupita muda sana, simu yake ikaita. Alipokea na alipomaliza aliniambia βNatakiwa ofisini haraka. Baadaye kipenzi changu. Baadaye.β
Nikambusu akaanza kuondoka nikabaki tu natabasamu. Hakika siku hii nilikuwa nimepata somo kuhusu mapenzi. Hata mimi nakubali. Kwanini mtu akusaliti?, kama wewe humsaliti kwanini yeye ameweza. Ukianza usaliti tu mapenzi yameisha. Sasa hapo zipo sababu mbalimbali. Huenda huna kosa lolote mtu tu ameamua kukusaliti. Au kuna matatizo humo ndani kisha usaliti ndiyo kama suluhu. Hii sio sawa. Mahusiano yakifika hapa ni hatari zaidi. Na ukizoea kusamehe usaliti basi jiandae kusamehe maisha yako yote. Hiyo ndiyo akili ya wazi na haraka haraka.
Nilitabasamu na taratibu nilitembea mpaka mahali nikakutana na sehemu ya kuweka uchafu. Sikutaka kumkaribisha shetani karibu maana Mr Tarick alivyokuwa ananitazama hapana. Niliitupa ile kadi nikisema βnataka mpenzi mmoja mzuri mwenye moyo mzuri na yeye ni Stewart peke yake.β
ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ: 94
Taratibu nilitembea na kurudi ukumbini. Nilikuta wageni wametawanyika na wasaidiizi wanapanga kwaajili ya kesho. Tulipiga zoga kidogo na Joan naye akaja akisema βnilikuwa nakutafuta wewe rafiki yangu. Twende tukale nimechukua chakula.β
Nikasema kwa upole βasante sana kipenzi.β
Wakati tunatembea tulipita mahali, basi wakati tunapita kuna wasichana walikuwa wamekaa wanazungumza walipotuona wote wakageuka kututazama. Nakumbuka sana walicheka kicheko cha ajabu. Moyo wangu uliumia, niliumia sana.β
Nakumbuka Joan alisema βachana nao kipenzi. Ni vile wanakuonea wivu. Huna sababu za kujisikia vibaya kwasababu wewe ni bora kuliko wao. Wanatamani kuwa kama wewe ila hawawezi. Vumilia kipenzi ndiyo mambo ya kazini hayo.β
Nilimtazama Joan na kutabasamu. Ingawa hili lilikuwa tabasamu fake. Fake kwasababu mimi binadamu naumia pia. Natamani sehemu ya kazi iwe sehemu yenye utulivu ila badala yake tena mambo ndiyo kama haya. Nilikuwa ninaumia sana. Nilimwambia Joan βwatu wasipokusema, wasipokuonea wivu, wasipokusengenya basi ujue huna unachofanya duniani. Twende kipenzi.β
Tulishikana mikono na taratibu tulielekea chumbani. Chumba ambacho ndiyo tutala hapo mpaka hili suala liishe.
Nilichoka sana kusema kweli, nilichoka na kazi sana. Tulipita sehemu tunabadili mavazi kuna namna tunafanya tu hapa mavazi yanaandaliwa kwaajili kesho na mambo kqma haya. Sikuwasha hata simu. Tulienda mpaka huko chumbani na niliona ni heri nioge kwanza na ndiyo mambo mengine yaendelee.
Ndiyo, nilioga, nikala. Ilikuwa mida ya saa moja moja hivi. Nikajilaza wallahi nijinyooshe mgongo wangu. Ila ndiyo nikalala moja kwa moja. Nilikuwa kushtuka mida ya saa nane usiku. Saa nane usiku ndiyo nimeshtuka.
Mimi kitu cha kwanza nikawa namuwaza baby wangu kwamba nimelala
tu na alivyo itakuwa amenitafuta sana. Hivyo kitu cha kwanza nikiwa nimejilaza nimegeukia upande mwingine nikawasha simu yangu.
Kama nilivyowaza na mnavyomjua baby wangu. Nilikutana na meseji nyingi sana za βbaby upo wapi, washa simu nimekumiss mwenzio , baby nataka kuondoka mimi nitalala vipi sijakuona na vitu kama hivyo.
Majina yote mazuri na mbwembwe zake kafanya mara atume emoji analia aseme ππππMr Tarick kapeperusha njiwa wangu.β Unajua nasoma hata nacheka tu mwenyewe ila ujumbe wa mwisho aliniambia βsitalala mpaka uniambie unanipenda usiku huu.β
NB: πΎπππ ππ ππππππ πππ ππππ ππππππππππππ ππππ?
Soma muendelezo wa season three kwa sh 1000
Njoo WhatsApp 0743433005


Maoni