*AAAAAASH BOSS ENZO* *season two* *SEHEMU YA KUMU*
Jambo likawa lelelele, Yaani ni patashika nguo kuchanika, Kwa upande wangu Walahi nilikuwa nikifurahi tu, na amina alikuwa akilia tu nakuomba msamaha.
Enzo wa watu mwaya akachukua muda wake na kumuelezea mama amina baadhi ya mambo kisha akamgeukia pully na kumuuliza.
"Kwanini ulibadili Jina na kuolewa na Mimi?"
Pully alibaki akilia tu, hapo Enzo alichukia sana na kujikuta akimpiga pully mabao matatu mfululizo.
"Nasema nasema
Muda huo huo Antie Asu akadakia kwa hasira,
"Nitazungumza Mimi Mwenyewe "
Kila mtu akamgeukia Antie Asu na kumpatia attention kubwa sana.
"Huyu sio pully wangu, pully wangu Mimi ni Mke wa mtu uko Dubai kwa sasa, hivi madam groly ulifikili nitaruhusu Mtoto wangu aweze kuolewa
na Mtoto wako? Katika vitu sitaki kusikia ni
Mimi kuungana undugu na familia yako, madam groly nakuchukia sana, siwezi kusahau yaliyotokea miaka 25 nyuma"
Aaaah kumbe mpenda umbea sikuwa peke yangu bwna, kila
Mtu alikuwa makini snaa kumsikiliza Antie Asu.
"Madam groly unakumbuka marehemu mume wangu wangu alivyokuwa anaumwa ? Tuliitaji Pesa nyingi sana lakini Ulikataa kutusaidia ingawa tulikuwa partiners kwenye kampuni ya kwanza, bado Kwakuwa ulikuwa ukitudai ukauza Nyumba na gari yetu, tangu siku ile nikasema utalipia haya"
Madam groly akanyanyuka kwa jazba na kuuliza.
"Kulipia kwangu kunahusiana nini na wewe kutuozesha huyu kapuku wako?"
Eeeeeh Leo hii madam groly anamuita mkwe yake pully kapuku? haya kulia kupokezana.
Antie Asu akaCheka kwa SAUTI ya juu na kujibu.
"Najua kabisa ukumbuki sura ya Binti yangu pully na Ndio Maana ulimpokea amina kwa mikono miwili na kumfanya mkwe Yako, amina nilimtuma kazi moja tu kummaliza Enzo ili na wewe upate maumivu niliyoyapata Mimi wakati nimempoteza mume wangu kwa roho mbaya yako"
"Nini wewe?"
Enzo Aliuliza kwa jazba na wasiwasi ya hali ya juu.
"Mimi nahusikaje hapo jamani Kwanini mtake kuniua "
Enzo aliendelea kuuliza na madam Asu akajibu.
"Enzo Mwanangu, uhusiki na chochote kile, na Ndio Maana, sumu ilivyokuwa inakusumbua niliwai hospital na kukuchoma sindano ya kukuokoa kwani ata sumu niliandaa Mwenyewe Nisamehe sana Kijana wangu"
Eeeeh nyie watu wanavisasi Walahi, Yaani watu wanataka kuuwana daaaah.
"Ba Enzo Naomba NAMBA ya Afande Dee aje awachukue hawa mashetani sasa hivi"
Alizungumza madam groly kwa hasira Sana.
"Mama Haina haja haya yote uliyataka wewe kuniozesha kwa mwanamke ambaye sio chaguo langu, na baada ya kusema haya, Naomba kila Mtu aondoke, pully wa mchongo pia utaondoka na mama yako, Mimi na wewe ndoa yetu ni batili
Kiukweli mambo yalikuwa mengi sana, Kwakuwa Jambo langu lilikamilika, sikuwa na sababu ya kuendelea kubaki nikaondoka pasi na kumuaga mtu yeyote Yule.
Siku iliyofuata, nikapokea ugeni NYUMBANI kwangu ambaye ni Suzy na Kwakuwa tayali tulikuwa ni Kama marafiki nikampokea kwa Furaha zote, na siku hiyo Mimi Ka Suzy tulipika
NYUMBANI kwangu na kula kwa pamoja.
"Haya sasa ma mjengo jimbo la kaka yangu liko wazi ni muda wako kujiachia "
Alizungumza Suzy katikati ya story zetu.
Hapo kwanza nikajikuta nikiwa mpole na kwa SAUTI ya utulivu nikajibu.
"Sizani Kama naweza Tena, Suzy siwezi Kuwa Mke wa Enzo, nimechoka drama za kila siku, hatua niliyofikia natamani kwenda mbali kabisa,
mbali na drama Hizi za kila siku"
Muda huo huo Enzo akaingia na kuzungumza.
"Utakapoenda utaenda na Mimi "
Mimi na Suzy tuka........
ITAENDELEA
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni