AAAAASH BOSS ENZO* *SEHEMU YA KUMI NANE*
Nilishtuka na moyo wangu uliumia sana Kana kwamba msumari wenye moto uligongewa
kifuani mwangu
Sikutaka kuleta drama yoyote, nikajikaza na kumuangalia Enzo kwa utulivu sana na kumuuliza.
"Lakini ulisema Kuwa Utazungumza na mama kuhusiana na mahusiano yetu na kunipenda Mimi na kila kitu
Enzo akaniangalia na kunijibu
"I did it ingawa sikumwambia Kuwa mwanamke Mwenyewe ni wewe, Ishani mama yangu.
amegoma kabisa na jana ametishia kujiua, hapa unaponiona Nipo Nipo tu Sijui Hatima ya haya yote, na mama yangu akisema kitu amesema
ujue
"Lakini Enzo wewe ni mtu mzima Una maamuzi. juu ya maisha yako, Una kila haki ya kupanga na kuchagua maisha yako, Kwanini unakuwa hivyo ? Kwanini unakuwa mnyonge kwenye haki.
yako?"
Hapo Enzo hakuwa na majibu yoyote Yale kwa wakati huo, alibaki akiniangalia tu, akili yake. Ilionekana kuchoka sana kutokana na drama.
ambazo zinaendelea kwenye familia yake.
Ila Hizi familia za kitajiri jamani, aaaah zinakela sana kwakweli.
Kikapita kimya kifupi Nikamuangalia Enzo wangu jinsi ambavyo anawaza peke yake, kwa utulivu nikamwambia.
"Enzo, najua iki ni kipindi kigumu sana kwako
lakini pia kwangu, hatujui Mungu ameandika story gani kati yetu, hatujui hatua zetu za Leo Kama zinaweza kufanana na hatua za kesho, lakini Mimi ishani wako nikuaidi tu Kuwa, katika
vita yako, katika kila pito lako Mimi nitakuwa upande wako, kwenye kila hatua yako Mimi Nipo na wewe, nakupenda sana"
Nilizungumza uku nikitamani ata kulia, kuna
Namna nilliona kabisa Enzo awezi Kuwa wangu. Mimi, kwanza sisi ni watu wawili tofauti, ni Kamal nimeenda kujiungiza kwenye maumivu ya milele
tu
Baada ya maongezi, nikaendelea na zoezi la kupika na baada ya muda Nilimaliza na kutenga chakula lakini hakuna ata mmoja ambaye alikuwa Na hamu ya kula chakula.
familia Kwa upande wa NYUMBANI Kwa kina Pully, Walahi mambo yalikuwa hot, ilichangamka Kama Samaki aliyetiwa ndimu na chumvi ya kuzidi
Maandalizi ya send off yalikuwa Makubwa sana kwa wakati huo.
Familia ikiwa bize na mandalizi, muda huo huo, ikafika ndinga moja Kali sana na Madam Groly akashuka akiwa amependeza ana akiwa na
baadhi ya zawadi.
"Arririrririn
Vilisikika vigeregere vya shangwe vikimpokea. mkwe ambaye ni mama mzazi wa Enzo, Yaani madam Groly, nyimbo za Furaha za vilugha ziliimbwa uku na uku.
Pully alimuuliza madam Groly pale tu alipopata wasaa wa kuzungumza nae.
"Mama Mbona ni wewe ndio umeniletea Gauni yangu Enzo yuko wapi?"
"Mmmh!! Pully Binti yangu, aliyekuambia kwamba muda huu unatakiwa kuonana na Enzo ni Nani Kwenye Mila na desturi hiyo kitu haikubaliki kabisa, Enzo utamuona kesho Tena
mwishoni Mwa shughuli ya kukuaga hapa
nyumbani kwenu"
"Kumbe, samahani mama sikuwa nikijua hayo yote
Alijibu Pully kwa unyenyekevu sana.
"Usijali Mwanangu, haya smile"
Aaaah ukiachana na unafiki na Wivu, Kiukweli Pully ni mrembo Tena sana.
Kwa upande wangu Bwana Mimi na Enzo ukimya ulikuwa ni wa hali ya juu sana, Maana hali halisi iko hivi, jumatano Ndio send off, wanapumzika
Ijumaa na alhamisi halafu jumamosi ni ndoa ya kanisani kati ya Pully na Enzo wangu.
"Utalala hapa Leo?"
Nilimuuliza Enzo
"Ndio"
Alijibu Enzo kisha akapanda kitandani na kugeukia upande wa pilli, Kiukweli Furaha ilitoweka kabisa, hakukuwa na amani Wala Furaha siku hiyo ni huzuni na mawazo Ndio
vilitawala.
Kwa siku hiyo Mimi na Enzo tulilala mzungu wanne hakuna ata kugusana
Asubuhi na mapema niliamka kutokana na Kuwa na mawazo mazito sana juu ya hiyo ndoa ya
Enzo ambayo ilikuwa inanukia tu, baada ya
kuamka, nilishtuka sana baada ya kutokumuona Enzo kitandani, niliangalia uku na uku pasi na kumuona, zaidi, nilikutana na karatasi ambayo
ilikuwa na mwandiko wa Enzo na ata hakuwa
ameandika Maneno mengi allandika hivi. "AM SORRY, BYEEH!"
Nyleeeeeh kwell Mimi sina Bahati yaaani Ndio nishaachwa hivyo, Enzo ameamua kumchagua Pully mwanamke aliyechaguliwa na wazazi wake.
Kwa maumivu makali ambayo nilikuwa nayo, nilijikuta nikilia sana Tena kwa sauti, haikuchukua muda mrefu, mashoga zangu wawili wakaja chumbani kwangu wakiwa na
wasiwasi mkubwa sana
"Ishani kuna nini Bwana Mbona unalia hivyo?" "Umepata taarifa ya msiba au? Ishani zungumza kitu
WAliendelea kuniuliza maswali mfululizo lakini kwa upande wangu ni kilio tu Ndio kilitawala.
"Ishani unatuogopesha Bwana"
"Enzo amekupiga ?"
Niliwangalia kwa muda kisha nikajibu kwa sauti ya kulla
"Enzo anaoa jumamosi
"Nini wewe ?"
Mashoga zangu walishtuka kwa Pamoja, ni wazi Kuwa hawakuwa wakiamini Maneno yangu.
"Ishani acha Basi, Unataka kumaanisha Kuwa Enzo ana mwanamke mwingine licha ya mapenzi yote ambayo amekuwa akikuonesha?"
"Aaah wanaume wanaume ni mbwa Kasoro baba yangu tu
Weeeh nilivyosikia Enzo wangu anasakamwa haraka Nikadakia.
"Enzo hausiki na chochote hapa, Ila mama yake Ndio anitaki Mimi
Mashoga zangu wakaona kabisa Kuwa nimekufa nimeoza kwa Enzo, walichofanya ni kunituliza tu nisilie pasi na kunishauri kitu chochote kile
Majila ya jioni nikiwa nimekaa tu Ndani kwangu, muda wote nikiangalia simu uwenda Enzo angenipigia simu, lakini wapi, Enzo akunipigia simu Wala kutuma sms ingawa nilimtumia jumbe nyingi sana.
Majila ya Saa MBILI usiku nikiwa nazunguka zunguka mtandaoni, gafla nikakutana na status ya Enzo, kwa shauku nikaifungua na kukutana na Picha ya Pully akiwa amependeza sana, akiwa
kwenye vazi lake la send off, Ka make up
kalimpendezesha zaidi, Picha hiyo iliongozana na caption iliyosomeka hivi.
"Shining like diamond my future wife Pully"
"Nawachukia"
Nilizungumza kwa maumivu makali sana na kuangua kilio.
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni