CEO USINIVUE MI MCHUMBA WA MTU* * *SEHEMU YA KUMI NA MOJA*
Siku ile ilikuwa ndefu sana kwangu sikuwa najua nafanyaje maaa nilikuwa na mawazo sana yaaani hadi usiku unafika sijui kam ni usiku maaan nilikua nimevurugwa sana, hadi nikawa nalinganisha kati ya CEO na Hussein yupi bora na mwenye upendo wa kwel moyo unaniaambia Hussein akili inaniambia CEO nilikuwa nachanganyikiwa yaani nilikuwa kama kachizi flan ile siku nakumbuka hadi usingizi haukuwa rahisi kupatikana kwangu ilikuwa napata taabu sana kwakweli, ila ule usiku wa mawazo ulipita na
Asubuhi tulijiandaaa, tukaendaa kumalizia vitu vilivyobakia ili kuanza kwenda dukani, kiukweli dada angu alikuwa na furaha sana na hakutaka kuizuiaa kuionesha mbele yangu. yaani ukimuangalia tu unajua anafuraha kiasi gani dada angu mpaka nilikuwa najihisi amani moyoni kwa kumtizama dada angu akifurahi, yaani kana kwamba mtu aliepewa dhahabu ila nilijua kwa upande wake hii ilikuwa hatua kubwa sana kwenye maisha ni haki afurahi ni wazi hakuwahi kufikirila kam atakuja kumiliki dukaa lake, na kila kitu kilikamilika sem yule wa bangoo ndio aliechelewa sana ilichukua siku mbili kumaliza, ila tulimaliza na sasa rasmi dada alikuwa kesho yake ambayo mimi ni siku yangu ya mwisho kubaki nyumbani kwenye ruhusa yangu, ndio dada alikuwa anataka kwenda kukaa kwenye saloon yakee, ila ilikuwa pambeee jamani, maan kulikuwa hadi na sehem ya location kam ushawahi kuona zile saloon mtu ukimaliza kupodolewa unaenda kwenye ile sehemu kupiga picha, ilikuwa pambe balaa
Poa tuliwaambia na wazazi wetu, walifurahi sana na kuzidi kumsifiaa CEO wa kampuni yetu kwamba ni mtu mzuri, ana moyo wa kusaidia watu na anaupendo sana hili lilinipa ushawishi wa kuendeleaa kumuona Ellias ni mtu wa muhimu sana, lakin kila nikiwaz nauona moyo wangu bado upo kwa Hussein
Wakati muda huo huyoo Hussein ninae muwaza. Hata kunijuliaa hali hawezi toka tulivyopishana ile siku hii ilinizid kunifanya mnyongee, kwa sababu muda huu nilitaka aje mwenyew kwasababu nilipitia hata nakala baadhii za ushauri kwnye mahusianoo, zilikuwa zinasema kwamba wapendanao lazima wategemeane kihisia na sio mmoja kuwa anamtegeaa mwenzziee kwamba asipo mtafuta na yeye hamtafutii akikosewa yeye ndio aombe samahani hii ilikuwa ni situation yangu. ndio nikagundua kwamba mimi ndie namtegemea Hussein kihisia na wala sio yeye, yaani mmoja ndio anaempenda mwenzie ila nilikuwa nataka nijithibitishie kitu kimoja tu niimjuee huyoo wa maana kwake na kipaumbele chake na kama ni mimi aniambie kwanini hanipi muda na nafasi ya kuenjoy kwenye mahusiano bali yeye ni wakunigandamiza kila siku
Hii siku ilikuwa imetulia nilikuwa sijiskii kutoka nyumbani, kwahyo dada alienda kufunguaa saloon yake mwenyew, sama nilimshauri tu afungue na dua maan wachawi ni wengi, mimi nikawa nimebaki nyumbani yeye akaenda kufungua saloon. Yake
Nilikuwa nimetulia nipo nachek movie, mara natumiwa sms na namba ngeni inasema "shga me Zakia nimebadili namba, njoo nyumbani mara moja shgaa angu" nikajua huu ni umbeaa na hivi nilikuwa na mistress nikaamua bora nikajue umbea labda nitachangamka maana nilikuwa nina muda pia sijamuona Zakia nikaamua kwenda kumuona pia sasa nimpe ubuyu nimfanyie suprise ya ubuyu, ila nilochokikuta ni zaidi ya suprise nilishangaa sana...
Itaendelea.....
Chapters
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni