Simulizi za Maisha,Mafunzo,Mapenzi ,Chombezo Habari za Michezo na Burudani vyote kwa Kiswahili ndani ya โ Gonga94 Semajambo
Gonga94 ยท Stories
15 Jan 2026
132 views
VYOTE NDANI GONGA94
BINAMU WEE UNGEWEZA? SEHEMU 14
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
ENDELEA.......
" Mmmmh!" Manka aliguna baada ya fungua mlango. Hawakumjali wsliingia ndani wote.
Sony baada ya kuwaona wazazi wake alishtuka kidogo.
"Mmefuata nini nyumbani kwangu?" Manka aliwauliza kwa makasiriko baada yabkugundua mtu waliyeongozana nae ni mtumishi wa MUNGU.
"Manka hawa ni wazazi wangu kwanini unawauliza swali kama hilo?" Sony aliongea kwa unyonge.
"Na wewe mbwa kelele mimi siongei na mbwa naongea na mwenye mbwa"
"Ndo huyo kijana wenu?"
Mchungaji aliuliza.
"Ndo yeye baba, tunaomba umsaidie kijana wetu"
"Ni kweli ukimuangalia t hata kwa macho ha kawaida unagundua kuwa hayupo sawa"
"Jamani kuweni wastaarabu majumbani kwa watu, kwanini mnachukua sheria mkononi tu bila ridhaa ya wenyewe" Mama Manka aliongea hayo.
"Vipi kama huyu mwanangu angekuwa mwanao ungefurahia kumuona na hali hiyo. Mchungaji hapa hatujaja kwaajili ya maneno tumekuja kwaajili ya neno la MUNGU na maombi. Naomba tuanze maombi"
Mama sony aliyasema wote kwa pamoja walianza kuomba. Sony alipandwa na mapepo. Maombi yaliendelea mpaka Sony alitulia ishara mapepo yamemuachia. Akili yake ililudi sasa.
Manka na mama yake muda huo walikuwa washakimbilia chumbani.
Baada ya maombi wote kwa pamoja walimshukuru MUNGU.
"Sony aliwaomba msamaha wazazi wake, na wao walimsamehe.
"Vipi msimamo wako kwa sasa kuhusu Manka"
"Kwanza yupo wap?"
"Nadhani wapo chumbani"
"Hakuna ndoa tena na kama mtoto ni wangu basi nitamtunza. Mama ni ujinga wwngu mwenyewe na tamaa ndio zimesababisha kuachana na Nice mwanamke aliyenipenda.
Sidhani kama anaweza kukubali kuludiana na mimi tena na hata hivyo nasikia yupo nje ya nchi. Nimemuuliza sana Nice na sikujali maumivu yale na yote ni kwaajili ya Manka........
Inabidi umuombe msamaha msafishiane nia maana kuna leo na kesho. Mimi ninaenda MUNGU awabariki sana" mchungaji aliaga akaondoka.
Manka na mama yake waliitaa sebleni. Aibu pyuuuuu! Sura zimewashuka kama tumbili.
"Mnaweza kuniambia kwanini mliniloga. Ili niwe zezeta?"
"Hapana baba" mama Manka aliongea.
"Baba. Nani baba ako?. Kuanzia sasa sihitaji kuwaona nyumbani kwangu. Yaani usiku hui huu muondoke.
" lakini Sony kumbuka kuwa nina mimba yako"
"Ondokeni bhana au mpaka niwashikie bastora?"
"Vipi hukusu hii mimba?"
"Fanya utakavyo lakini usije ukajitokeza tena kwenye maisha yangu"
"Kama mimba ni yako kubali kulea mtoto. Si busara kumsusia mtoto asiye na hatia" Baba Sony aliomgea..........ITAENDELEA..........
Maoni
You're not logged in
X
Login
X
signup
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa
+ Endelea kugundua zaidi
SHAMIRA sehemu ya 36&37
Wassap:0742443214 Mwandishi; lissa wa huru media Basi mwanaume akaondoka zake na mimi ndo nikashika simu sasa .nikampig...
Maoni