FROM BANGI TO BABY ππ SEHEMU YA 21
Nikamuuliza "we umejuana vipi na D??"
"Yule D ni mdogo wake na Boss wangu, ni binamu yake kitu kama hicho, mie sijawahi hata kuwa na mazoea nae kabisaaa ila kuna issue ilitokea kati yake na Kaka yake maana kaka yake anaishi Rwanda na ndio Boss wetu, Na mie ndo naangalia Gari nyingi hapa Tz sasa kuna baadhi ya Vifaa viliibiwa ndio Boss akawa anamuhisi Huyu D akaniomba niwe karibu nae ili nijue mwenendo wake, Ndio maana nikaunga ukaribu nae na akawa mshkaji wangu tu"
"MUNGU WANGU!!!" mmh yaani mbona hamu sina tena mie nilijua nimepata bwana mi hela ipo kumbe hana lolote !
"Ndo hivyo, hata ile siku cassino pale ulipo ondoka nilishukuru sana aisee sikutaka kabisa wewe kuwa pale, naa ulipo kuwa unapiga simu sana alikuwa anaziangalia tu ndio nikamwambia anipe nikuulize hata kama umefika salama isije kuwa unapiga labda kuna Tatizo baada ya kunipa simu nikakupigia na ndio siku hizo nilipata nafasi ya kukagua simu yake , nika jua yeye hakuiba ila ndio aliuza Ramani ya Vitu waje kuibaa "
"Eeeh Mungu wangu!!!"
"Usijali Vero, Mie nashukuru tu Yule mjinga amekuepuka"
Nikamkumbatia Veda yaani mpaka naogopa jamani nilikuwa nimedumbukia wapi miee kwa huyu mjinga kila siku alikuwa ananambia ana magari makubwa ya kupeleka mizingo nje ya nchi na mie nikaamini maana ana hela za kutosha, Veda akanikumbatia kwa kunipa amani...
Nikamwambia sasa kuhusu vitu vyangu vile Veda amevizuia pale kwake maana yeye ndio alinipangishia akasema atafatilia kesho pakikucha ..
Basi ule usiku hakuna hata alietamani kulala ulikuwa ni Muda wa kila mtu kutoa lake la moyoni na Ahadi tam tam kibao ..
Kukakucha mwenyewe nikajidamkaaa si unajua ukweni tena japo sijazoea kufanya mi kazi kazi lakini lazima nifanye nikamkuta ma mkwe ndo mkwe tena jamani kafanya kazi haswaa kunizalia jidumee yaani ex mbona abarikiwe mie leo ningeishia kula kwa macho hili limkakaa..
Mama akanambia yaani rudi ukalale kama unaenda kazini jiandae uende sawa mimi sijazeeka kihivyo, halafu nina nguvu mie na hapa hakuna kazi hizoo za kukudamsha, Wakati mama anaongea Veda akatoka maana nilimuacha amelala, hata hajanisemesha akamsalimia mama yake halafu akanivutaa ndani mpaka kitandani
"Yaani wewe badala tumpe joto mtoto unakimbilia kumpigisha baridi nje" nikacheka tu akanisaula hapo akanikula asubuhi asubuhi basi nikabaki tu nacheka mabusu kama yote, nikaenda kuoga wakati natoka kuoga ma Mkwe akaniita Akaniuliza
"Vipii, Amelainika??" Nikachekaa maana aliniuliza kwa sauti ya chinii
"Ndio mamaa tumeyamaliza"
"Aaleleleleeee " alipiga vigele gele huyoo jamani akanipa Hongera kibao akanitakia baraka zote za kuishi na mtoto wake basi mie nikarudi ndani nimechanua meno yote duh yaani nimepata lindo kiwepesiii hata siamini
"Enhee mama amefurahi nini??" Nikacheka tu
"Ya Kike haya bwana" nae akacheka akanambia jiandae vizuri nakupeleka mie mwenyewe kazini, Waooh nikasema sawa Ba mpenzi wangu, Nikavaa chap chap, nikamwambia mie hizi nguo hata sio zangu naomba unisaidie kupata vitu vyangu kwa D akanambia usijali Ma mpenzi hilo zoezi nalifanya leo leo kabla sijasafiri ...jamani nikamuuliza unasafiri tena akanambia tutaongea ukirudi kazini ma mpenzi si unajua ndio kazi yangu na lazima maisha yaendelee daah nilihuzunika et vi machozi vikatoka ...
Akanikumbatia kwa muda mpaka nikawa sawa akanambia haya twende, wee nikapanda mpiki piki wa Ba mpenzi mamaaa aloo, akanipeleka mpaka kazini akanambia unatoka sa ngap nikuijie nikamwambia muda wangu akasema sawa nitakuwa hapa li saa li moja kabla nikacheka ...
Basi nipo nafanya kazi mchana ule muda wa Lunch nashangaa naitwa mapokezi kutoka namkuta Ba mpenzi na mfuko aloo nikabaki nacheka tukaenda sehem ya kupatia chakula akanambia nimekuletea tu matunda kwa ajili ya mtoto, nilicheka huyo mtoto jamani mmh basi tukala wote akaondoka ...
Tinner hizo simu anapiga balaa, nilipo mpa taarifa kwanza tumeyamaliza na hivi sasa penzi moto motoo aah alifurahi huyoo alifurahi hatari ..
Jioni kweli natoka namkuta Ba mpenz getini na Honda yake amependeza huyo waooh jamani mie nina bonge la mkaka hakiamungu Ex wee asante sanaa ..
Nikawa nacheka huku navuta hatua kwenda alipo kabla sijamfikia D huyuu eeh kwanza nikasimama maana walikuwa usawa sawaa
"Vero.. nimekufat huku tuongee naomba twende nyumban" kama kakatika kichwa hata sikumjibu kitu nikapiga zangu hatua mpaka kwa ba mpenzi wangu akani Hug mabusu kama yotee huku amenishika kiuno akaniuliza habar z kazi nikasema nzuri Babaa etu kipenzi akalishika Tumbo huyu nae vipi nikamwambia ananisumbua tu maana anakumiss sanaaa basi akainama akambusu mwanane, akanambia haya twende ile napanda kwenye piki piki nilishangaa nimevutwa kwa nyuma mpaka nikaanguka chini yaani ni kitendo cha sec jamani naiona ngumu inakuja Mungu wangu Veda aliwahi akamsukuma pembeni , Wacha wapigane ngumi nje ya geti la hospitali...
D alipigwa ngumi za haraka haraka ndio Veda akamuacha anavuja tu damu mdomoni mie pale chini kiuno kilikuwa kimekaza hata kuinuka siwezi, Veda akanibeba haraka alikuwa anahasira mpaka anatetemekaa jamani akaniingiza hospitali haraka nikafanyiwa vipimo nilikuwa nalia kiuno, Veda anaomba dua zote mtoto awe sawa akanambia kama mtoto amepata na shida naapa kwa Mungu yule Mjinga namuuwa leo leoo..
Mmh nikamwambia Veda usiseme hivyo bwana, Mie naogopa tuombe mtoto awe sawa"
Huyu Veda kwa ile staili aliyonionesha pale kwake mmh anaweza kuuwa huyu mwenzangu...
Basi nikafanyiwa vipimo wakasema mimba inatishia kutoka nikapewa dawa nikawekwa na Dripu siku enyewe tukalala hapo mpaka asubuhi Veda pembeni ya kitanda, asubuhi nikapimwa tena wakanambia nipo sawa ila nisifanye kazi ngumu wala kubeba vitu vizito nijiepushe pia na msogo wa mawazo nikasema sawa .
Tukaruhusiwa, Zile habar nyumbani mama zilimshtua sana ila akashukuru nipo sawa Tinner pia akaja kunipa pole ..
Nilipewa Ruhusa ya siku tatu kazini, mchana mama akatuita wote na Veda akanambia hizi siku tatu kwanini tusitumie kwenda kwenu ili uchumbiwe usiwe unaishi tu hapa sio vizuri hatujafata misingi yeyote"
Nikamtazama mamaa nikamwambia asante kwa kujali mama yangu asante sana lakini mie unavyo niona sina wazazi wala ndugu huyo Tinner mie ndio ndugu yangu ndio shoga yangu kwa sababu tumekuwa wote kwenye kituo cha watoto yatima sijawahi kuwa na wazazi nimejitambua nikiwa pale mpaka leo nipo mtaani!!"
Veda alishangaa akanambia kwanini hukunambia hilo, nikamwambia tu Hukuniuliza !" Akaniomba sana samahani ni kweli hatukuongelea chochote kuhusu familia zetu basi akaomba sana samahani jamani akanambia sasa nikitaka kutoa mahali naenda wapi nikamwambia nipe tu mwenyewe, tukacheka hapo mpaka basi ..
Jioni akanambia D vitu vyangu ameuza, Gari iliniumaa yaani kauza Gari yangu mjinga yule hata mkopo sijamaliza kulipia daah gari ilinuma ile kuliko chochote, Veda mwenyewe alijua nimeumia kuhusu gari, akanambia nitakununulia gari haitakuwa ya hela nyiiingi lakini nitaangalia uwezo wangu, Nikamwambia usijisumbue bwana, akanambia nitakununulia hiyo ni ahadi yangu
Basi mie nikaanza maisha ndani kwa Ba mpenzi wangu, Vedastus wangu baba wa mwanangu mapenzi yalikuwa moto sanaa akisafiri simu kila sec yaani kila sec aisee ni simu mimba ilikuwa inanisumbua sana nikaacha kazi kwanza nitulie nyumbani ..
Mimba ilikuwa kama na miezi 6 hivi, Ndio tukafunga ndoa ya kanisani kabisaa, Yule mdada aliekuwa mke wake daah alisumbua baada ya ndoa jamani et anataka wagawane mali, mali zenyewe ni ile nyumba aisee tena hakuwa anafanya kazi yeyote ila anavyotaka nyumba hatari, Mie hata kipaumbele changu hakikuwa nyumba kipaumbele changu ni Veda wangu na familia yake maana hawa ni kama familia yangu tena wadogo zake wale mapacha jamani walijua kunipa upendo walinipa thamani zaidi ya shemeji yao, tunakaa nyumba moja na mama mkwe lakini mpaka leoo sijawahi kuona kasoro ya yule mama jamani ananipenda kama bint yake ..
Yaani kanibeba kama bint yake sio mkwe wake kabisa
Basi bwana miezi ikasonga penzi pajaa tena na ba Mpenzi wangu, Nikajifungua mtoto wa kikeee Mashaallah sura ya Baba yakee kabisaa ..
Basi huo ndo ulikuwa mkasa wangu From bangi up to now ndo baby ndo ba mtoto wangu ndio Nyonga mkalia Inni wangu Veda wangu , Mwanangu sasa ana mwaka mmoja jamani kwahiyo bado kijana
Sijawahi kusikia habar za D popote kwanza hata sitakiii kusikia
Huu ndo mwisho wa mkasa wangu asanteni kwakua pamoja na mie mwandishi ni malkia osam na mie ni Veronika au Mama Vivian
MWISHOOO
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi


Maoni